Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109570 articles
Browse latest View live

SERIKALI YAKANUSHA TAARIFA ILIYOSAMBAA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII KUWA ITAANZA KUTOA AJIRA


AJALI ZA BARABARANI ZAENDELEA KUUA NA KUACHA MAJERUHI MKOANI MWANZA.

0
0
Na George Binagi-GB Pazzo

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewataka watumiaji wa barabara mkoani Mwanza, kuzingatia sheria za usalama barabarani jambo ambalo litasaidia juhudi za kupambana na ajali kufanikiwa.

Mongella ametoa kauli hiyo hii leo kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani mkoani Mwanza, uliofanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza, ambapo elimu ya usalama barabarani itaendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo kwa juma zima.

Amesema watumiaji wote wa barabara wanao wajibu wa kufuata sheria za usalama barabarani huku akikemea tabia ya baadhi ya abiria wanaowahimiza madereva kuendesha vyombo vyao kwa mwendo kasi.

Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza, Robert Hussein, amebainisha kwamba kwa kipindi cha mwaka jana kati ya mwezi januari na septemba kulikuwa na ajali 161 zilizosababisha vifo 132 na majeruhi 187 na kwamba kwa kipindi kama hicho mwaka huu kulikuwa na ajali 159 zilizosababisha vifo 150 na majeruhi 162 ambapo takwimu hizo zinaonesha kuwepo kwa ongezeko la vifo 18 sawa na asilimia 12 na upungufu wa majeruhi 25 sawa na asilimia 13.3

Baada ya Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kufanyika Kitaifa mkoani Geita kuanzia Septemba 29 hadi Oktoba Mosi Mwaka huu, Maadhimisho kama hayo kwa mkoa wa Mwanza yamezinduliwa hii leo kwenye Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza ambapo imeelezwa kwamba bado juhudi za kila mtumiaji wa barabara zinahitajika ili kutokomeza ajali za barabarani.

Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Mwanza, Robert Hussein, amebainisha kwamba kwa kipindi cha mwaka jana kati ya mwezi januari na septemba kulikuwa na ajali 161 zilizosababisha vifo 132 na majeruhi 187 na kwamba kwa kipindi kama hicho mwaka huu kulikuwa na ajali 159 zilizosababisha vifo 150 na majeruhi 162 ambapo takwimu hizo zinaonesha kuwepo kwa ongezeko la vifo 18 sawa na asilimia 12 na upungufu wa majeruhi 25 sawa na asilimia 13.3

Pichani juu ni maandamano ya bodaboda pamoja na wa watumiaji wengine wa barabara yakiingia Uwanjani kwenye maadhimisho hayo ambayo yamezinduliwa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani mkoani Mwanza
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Ahmed Msangi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani mkoani Mwanza
Wanafunzi wa shule ya Msingi Butimba Jijini Mwanza wakiingia uwanjani kuimba wimbo wa kuhamasisha matumizi sahihi na salama ya barabarani.

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 24.10.2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

INTRODUCIN NEW AUDIO by Mesen Selekta - Kiss & Love

MATUKIO MBALIMBALI UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIUCHUMI WA KOREA NA AFRIKA MJINI SEOUL, KOREA KUSINI

0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa ameshika kibao alichoweka alama ya kiganja chake, kuunga mkono umoja na mshikamano wa nchi za Kiafrika zinazohusiana kiuchumi na Korea Kusini baada ya kufunguliwa kwa mkutano wa Tano wa ushirikiano huo kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC) katika ukumbi wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), (Katikati) (Kulia kwake) na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Akinwumi Adesina, (Kushoto) Baada ya kufunguliwa Rasmi kwa Mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Kiafrika, unaofanyika Mjini Seoul, Korea Kusini
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa na Maafisa kutoka Tanzania, wakitoka kwenye Ukumbi wa Mikutano  wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini, baada ya kufunguliwa rasmi kwa mkutano wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika, mjini Seoul, Korea.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Philip Mpango (Mb), akipokea zawadi ya kitabu kinachoelezea njia zilizotumiwa na nchi ya Korea Kusini, kupiha hatua kubwa ya maendeleo, kutoka kwa Afisa Mikopo wa Benki ya Exim ya Korea Kusini, Park Gil Jong, kabla ya kuhudhuria ufunguzi wa mkutano wa tano wa ushirikiano wa Korea Kusini na nchi za Afrika  (KOAFEC), Mjini Seoul, Korea Kusini. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

VICHWA VYA HABARI YA MAGAZETI YA LEO JUMANNE OCT 25

MFALME WA MOROCCO MOHAMED VI AWASILI IKULU NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS DKT. MAGUFULI

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakipita katika gadi ya mapokezi iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakilakiwa na wafanyakazi pamoja na wageni mbalimbali katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma pamoja na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.


WANAFUNZI WA LONGIDO SEKONDARI MWISHO KULALA MADARASANI

0
0
Nteghenjwa Hosseah – Arusha 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amechangia mabati 136, mifuko ya Saruji 30 pamoja na Fedha taslimu Tsh 500,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa mabweni mawili yaliyoungua moto hivi karibuni katika Shule ya Sekondari Longido.

Rc Gambo ametoa msaada huo wakati wa ziara yake ya Kikazi wilayani hapo ambapo alitembelea Shule hiyo na kukuta wanafunzi wakilala madarasani tangu Mabweni hayo yalipoungua na uongozi wa Shule hiyo kuamua kutumia madarasa hayo katika kipindi hiki cha mpito wakati wakiwa wanaendela na ujenzi wa mabweni hayo ambayo ujenzi wake unagharimu zaidi ya Tsh Mil 45.

Akisaoma taarifa ya ujenzi wa mabweni hayo Afisa Elimu Sekondari Bw.Gerson Mtera alisema endapo wangetumia Mkandarasi ujenzi huo ungegharimu zaidi ya Ths Mil 75 lakin kwa kuwa wanajenga kwa kutumia mafunzi wa jamii pamoja na wataalamu wa Halmashauri mabweni hayo yatagharimu Tsh Mil 45 tu.

Nimeona jitihada za uongozi wa Wilaya pamoja Shule katika kukabiliana na changamoto hii na jitihada zenu hakika sio za kupuuzia na mimi kama Kiongozi wa Mkoa nawiwa kuchangia kazi hii ili iweze kukamilika haraka na wanafunzi warudi katika malazi yaliyo bora na madarasa hayo yaweze kutumika kwa shughuli stahiki alisema Gambo.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa alikutana na walimu pamoja na wafanyakazi wasio Walimu kusikiliza malalamiko na kubaini baadhi wa walimu kutolipwa malimbikizo ya Fedha za Likizo pamoja na watumishi kuajiwa kwa zaidi ya miaka kumi pasipo kuwa na mkataba wala barua ya ajira kutoka kwa Mwajiri wake.

Akiongea katika Kikao hicho Mhe. Gambo alisemani ni muhimu kwa kila Halmashauri kuwajali watumishi wake haswa walimu na wafanyakazi wa kada za chini ili kuwaongezea ari ya kufanya kazi na kuwatia moyo waweze kutumikia Taifa hili kwa uzalendo sio kila siku mnatoa vipaumbele kwa watumishi wa Kada za juu kufanya hivi mnasababisha matabaka yasiyo ya lazima katika utendaji kazi wenu wa kila siku.

Mkuu wa Wilaya ya Longido Mhe. Daniel Chongolo aliahidi mbele ya Mkuu wa Mkoa kuwa atasimamia ipasavyo wote wanaohusika na ujenzi wa mabweni ya Sekondari ya Longido ili kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa na kumhakikishia kwamba mpaka mitihani ya Kidato cha nne itkapoanza wanafunzi hao watakua wameshahamia kwenye Mabweni hayo na madarasa hayo yatatumika kwa ajili ya kazi hiyo na baadae wanafunzi wataendelea kuyatumia katika masomo yao.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo (pili kushoto) akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Longido Daniel Chongolo(kwanza kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido Mhe. Esupat Mulupa wakielekea kukagua ujenzi wa mabweni katika Shule ya Sekondari Longido . 
Afisa Elimu wa Halmashauri ya Longido Ndg. Gerson Mtera(mbele) akisoma taarifa ya ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Longido wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wilayani hapo. 
Ujenzi unaendelea katika mabweni ya Shule ya Sekondari Longido na hivi ndivyo yanavyoonekana kwa sasa. 

PROF. MBARAWA AITAKA BODI MPYA YA TAA KUSITISHA AJIRA ZA UPENDELEO

0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, ameitaka Bodi mpya ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kusimamia Menejimenti ya Mamlaka hiyo katika Idara ya Utawala na Rasilimali watu ili kuhakikisha ajira zote zinazotolewa zinazingatia sifa na vigezo vya kuajiri.

Akizungumza katika uzinduzi wa Bodi hiyo mpya jijini Dar es salaam pamoja na mambo mengine, Profesa Mbarawa ameisisitiza bodi hiyo kuifanyia kazi Ripoti ya Uchunguzi wa uendeshaji wa Viwanja hivyo nchini na kufanya mabadiliko mara moja.

“Nataka muipitie ripoti niliyomkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mkuu na mufanyie maamuzi, suala la kuajiri watu kiholela, ninataka wote waliandikwa kwenye ripoti hiyo kuwa hawana sifa watolewe wapishwe watu wenye sifa ili waweze kufanya kazi”, amesema Waziri Mbarawa.

Aidha, Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kusimamia kwa uadilifu miundombinu yote ya viwanja vya ndege nchini na kuhakikisha mashine za ukaguzi zinafanya kazi masaa 24 ili kudhibiti mianya yote ya rushwa.Ameitaka Bodi hiyo kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato katika viwanja vyote ili kuweza kufikia lengo lililowekwa na kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Profesa Mbarawa ameitaka Bodi hiyo kushirikiana na wafanyakazi wa Viwanja hivyo katika mambo mbalimbali ili kuboresha utendaji na kuweka uwazi katika utoaji wa huduma katika viwanja hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Ninatubu Lema amemhakikishia Waziri huyo kuwa ataongeza ushirikiano na wafanyakazi wote na kusimamia maagizo yote yaliyotolewa.Ameahidi kuboresha huduma katika viwanja vyote nchini na kusema kuwa umuhimu wake utaongeza mapato katika viwanja hivyo na nchi kwa ujumla.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Ninatubu Lema.
Wajumbe wa Bodi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa(hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Prof. Ninatubu Lema (kulia) wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Prof. Ninatubu Lema, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (kushoto), wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo. Kulia kwake ni MKurugenzi wa Miundombinu ya Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Hussein Mativila.

MASAUNI AFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI WA UNHCR NCHINI

0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimfafanulia jambo Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (kulia) wakati Mwakilishi huyo alipomtembelea Naibu Waziri ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya kuwahudumia Wakimbizi nchini. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya wakimbizi wa Wizara hiyo, Harrison Mseke. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati alipokuwa anamfafanulia jambo kuhusu masuala ya wakimbizi nchini. Mwakilishi huyo alipomtembelea Naibu Waziri ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Wadau waishauri Taasisi ya Tanzania Christian Deliberation Burea (TCDB) kuandaa upya mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kwa Wasanii.

0
0

Na: Genofeva Matemu – WHUSM,

Wadau wa Tasnia ya Filamu na Muziki wameishauri Taasisi ya Tanzania Christian Deliberation Burea (TCDB) kuandaa upya mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kwa kuwa na takwimu kutoka kwa Taasisi zote zinasimamia sekta ya Filamu na Muziki nchini.

Rai hiyo imetolewa na wadau mbalimbali wa tasnia hizo walioshiriki katika kikao kilichoandaliwa kwa ajili ya kuwasilisha mwongozo huo kwa wadau leo Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kikao hicho Rais wa Shirikisho la Filamu Bw. Simon Mwakifwamba amesema kuwa ni vyema mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kutoka TCDB kuzingatia takwimu na taarifa sahihi kutoka kwa wadau ili kuweza kuendana na hali halisi ya tasnia hizo.

“Katika kutekeleza azma ya Taasisi ya TCDB ni vyema mkaandaa mchakato wa kufikia na kushirikisha vyombo vya wadau kuanziia ngazi ya chini kwa kupitia shirikisho la filamu pamoja na Taasisi za Serikali ambao watachangia katika kuandaa mwongozo ulio bora” amesema Bw. Mwakifwamba.

Rais wa Tanzania Christian Deliberation Burea (TCDB) Bw. Carolous Bujimu (kushoto) akielezea mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kwa wasanii wakati wa kikao na wadau wa tasnia ya Filamu na Muziki leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo 
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo (katikati) akizungumza na  wadau walioshiriki katika kikao cha uwasilishaji wa mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kwa wasanii kutoka TCDB leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais wa Tanzania Christian Deliberation Burea (TCDB) Bw. Carolous Bujimu. 
Mjumbe kutoka COSOTA Bw. Paul Makula akichangia mada wakati wa kikao cha uwasilishaji wa mwongozo wa programu ya kusimamia na kukuza vipaji kwa wasanii kutoka TCDB leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais wa Shirikisho la Filamu Bw. Simon Mwakifwamba.

KAMPUNI YA YARA TANZANIA YAZINDUA RASMI USAFIRISHAJI WA MBOLEA KWA NJIA YA TRENI

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya YARA Tanzania Ltd, Alexandre Macedo, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Usafirishaji wa mbolea kwa njia ya Reli TRL, Uzinduzi huo umefanyika leo kwenye Ofisi za YARA Tanzania zilizopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa TRL, Focus Makoye Sahani.
Azungumzia uzinduzi huo Mkurugenzi huyo alisema kuwa YARA kwa kushirikiana na TRL na SAGCOT, wameamua kuzindua njia hiyo ya usafirishaji ili kupunguza gharama za usafirishaji kwa kutumia barabara na maji ili kuwafikia walengwa kwa wakati na kwa gharama nafuu, ambapo awali kusafirisha Tani moja kutoka Viwandani Ulaya hadi jijini Dar es Salaam, ilikuwa ni Dola za Kimarekani 40, kwa Tani moja na Dar es Salaam hadi Tabora ni Dola za Kimarekani 100 kwa Tani moja kwa njia ya barabara. Aidha Macedo, alisema kuwa kuamua kutumia usafiri wa Treni sasa usafiri utashuka kwa asilimia 35.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya YARA Tanzania Ltd, Alexandre Macedo (katikati) Naibu Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa TRL, Focus Makoye Sahani (kushoto) na Mratibu wa Program ya SAGCOT Centre, Emmanuely Lyimo, kwa pamoja wakionyesha ushirikiano kwa kushikana mikono kuashiria uzinduzi rasmi wa Usafirishaji wa mbolea kwa njia ya Reli TRL uliofanyika leo kwenye Ofisi za YARA Tanzania zilizopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

WAZIRI WA BIASHARA VIWANDA NA MASOKO BALOZI AMINA SALUM ALI AZINDUA BARAZA JIPYA LA KUSIMAMIA MFUMO WA UTOWAJI LESENI

0
0
Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar 

Baraza jipya la Kusimamia Mfumo wa Utoaji Leseni (BLRC) limeagizwa kusimamia mfumo huo kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2013 ili kuondosha kasoro zilizojitokeza katika mfumo wa zamani na kurahisisha ufannyaji wa biashara Zanzibar.

Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali ametoa maagizo hayo Ofisini kwake Migombani alipokuwa akizindua Baraza hilo lenye wajumbe 13 kutoka Taasisi za Serikali na watu binafsi likiongozwa na Mwenyekiti wake Vuai Mussa Vuai.

Amesema mfumo uliokuwa ukitumika wa utoaji leseni za biashara ulikuwa sio rafiki kwa wadau, ni wenye unaurasimu na unachukua muda na pia unagharama kubwa katika upatikanaji wa baadhi ya leseni.

Ametaja kasoro nyengine za mfumo wa zamani wa utoaji leseni kuwa ni kuwepo kwa sheria na vyombo vingi vya utaji leseni, kutokuwepo msimamizi wa vyombo hivyo na kuwepo kwa aina tofauti za leseni, vibali au ruhusa ya kuendesha biashara ambazo zote zina lengo moja.

Balozi Amina amelitaka Baraza hilo katika kutekeleza majukumu yake kuondosha urasimu na kupunguza muda katika utaratibu wa kuomba na utoaji leseni, kusimamia utaratibu rahisi na wa kupunguza gharama katika upatikanaji wa leseni na kuwepo masharti ya kusimamia biashara.
 Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Balozi Amina Salum Ali akizindua Baraza jipya la Kusimamia Mfumo wa utoaji leseni Ofisini kwake Migombani, Mjini Zanzibar.
 Katibu Mtendaji wa BLRC Rashid Ali akitoa maelezo mafupi ya shughuli za Baraza hilo wakati wa uzinduzi rasmi uliofanywa na Waziri Amina Salum Ali Ofisini kwake Migombani.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

ASILIMIA 70 YA WATANZANIA KUSHIRIKI KATIKA SHUGHULI ZA KIUCHUMI.

0
0
Na Ally Daud-MAELEZO.

WATANZANIA zaidi ya asilimia 70 wamepewa kipaumbele kushiriki katika shughuli za kujenga uchumi wa nchi kufikia uchumi wa kati katika kutekeleza sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi mpaka kufikia mwaka 2020.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi(NEEC) Bi. Beng’i Issa wakati wa ufunguzi wa ripoti ya Tathimini ya Sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ambao umefanyika leo jijini Dar es salaam.

“Tunataka kufikia 2020 watanzania asilimia zaidi ya 70 waweze kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kufikia katika uchumi wa kati ili kutekeleza sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi nchini” amesema Bi. Issa.

Aidha Bi.Issa amesema kuwa watanzania wanatakiwa washiriki katika shughuli za kiuchumi na wasitegemee zaidi wawekezaji kutoka nje ili kuifanya Tanzania iendelee kiuchumi kutoka ngazi ya mmojammoja hadi kufikia maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Kwa upande wa Meneja wa Utafiti na ufatiliaji wa Sera hiyo kutoka NEEC Bi. Frola Kajela amesema kuwa Serikali imeandaa sera hiyo ili kuwezesha watanzania kutumia rasilimiali zilizopo katika kuinua uchumi wa nchi na kuweza kumilikiwa na watanzania wenyewe.

“Sera hii inalenga zaidi kwa watanzania kumiliki uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo nchini ili kujishughulisha katika kuleta maendeleo ya nchi kwa jamii na taifa kwa ujumla mpaka kufikia 2020” alisema Bi. Kajela.

Aidha Bi. Kajela amesema kuwa sera hiyo inafanyiwa maboresho ili kuweza kuwafikia watanzania wote katika kuelewa na kumiliki uchumi kwa kiasi kikubwa katika kutekeleza mpango wa serikali uliyowekwa kuhakikisha watanzania wanajiinua kiuchumi.

WAZIRI MAKAMBA ATAKA KUFANYIKA KWA TATHMINI YA ATHARI KWA MAZINGIRA YA MTO KATUMA

0
0
Na Lulu Mussa, Katavi 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesema kuwa uharibifu wa Mazingira katika Mto Katuma ni tishio kubwa kwa uhai wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi na wakazi wa Mkoa huo. 
Akiwa katika mwendelezo wa ziara yake ya siku 16 kutembelea Mikoa mbalimbali hapa nchini, Waziri Makamba amesema kuwa Mto Kasuma uko hatarini kutoweka kutokana na ongezeko la shughuli za binadamu, wingi wa mifugo,  Uchimbaji wa madini, ukataji wa miti na uchepushaji wa maji kunakopelekea kupoteza mtiririko wa maji yenyewe. 
Waziri Makamba amesema ni vema kuwa na mikakati na hatua za haraka na zile za muda mrefu ikiwa ni pamoja na kufanya sensa ya mifugo ili kuweza kujua Mkoa una mifugo kiasi gani na kuainisha maeneo ya malisho. "Zoezi hili si hiari, ni lazima na takwa la kisheria' Makamba alisisitiza.

 Imependekezwa pia kufanyika kwa Ubomoaji wa mabanio yanayokinga maji kama hatua ya haraka ili maji yaweze kutiririka kwa wingi katika kipindi hiki cha kiangazi, na kuagiza kufanyika kwa doria za mara kwa mara ili kubaini watu wanaokiuka taratibu hizo. 
Waziri Makamba pia amezitaka Mamlaka za bonde kutimiza wajibu wao kwa kutoa vibali stahiki kulingana na ujazo wa maji uliopo katika maeneo yao ili kujenga usawa wa matumizi sahihi ya rasilimali maji. ' Mamlaka za bonde zisitoe vibali ofisini na operesheni ifanyike kwa wote wasio na vibali" Alisema Waziri Makamba. 
Pia, Waziri Makamba ameagiza kufanyika kwa Tathimini ya athari kwa mazingira kwa Mto Kasuma na kuuagiza uongozi wa Mkoa wa Katavi kuainisha baadhi ya maeneo ambayo yatatangazwa kama maeneo nyeti ili kunusuru mazingira ya Katavi na ustawi wa Mto Katuma.

"Kuwe na tozo ya uharibifu wa Mazingira na tozo hiyo iendane na kiwango cha uharibifu atakachofonya muhusika" 
Akiongea na Wadau wa Mazingira katika Ukumbi wa Maji Mkoani Katavi Waziri Makamba amekumbusha watumishi wa Umma Nchini kuwa na nidhamu na uwajibikaji wa dhati na kusisitiza kuwa hakuna muda wa kubembelezana. "Fanyeni kazi kwa weledi, nidhamu na uadilifu" alisema Makamba. 
Katika hatua nyingine Waziri Makamba ametembelea eneo ulipokuwa mradi wa uchenjuaji wa dhahabu wa Jema Sitalike Project ambao ulikua ukifanya shughuli zake bila kibali cha Wizara ya Nishati na Madini na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). 
Waziri Makamba ameagiza kusimamishwa kwa shughuli za Mradi wa Jema ambao kwa sasa wamehamishia shughuli zao Mkoani Mwanza na kuwataka kuchukua hatua za haraka kufunika mashimo yaliyopo Sitalike - Katavi ili kunusuru uhai wa viumbe vinavyozunguka maeneo ya Sitalike. 
Waziri Makamba yuko Mkoani Katavi kwa ziara ya kikazi na hii leo amekutana na Viongozi wa Vikundi vya Mazingira, katembelea eneo lilikokuwa na shughuli za Uchimbaji wa Madini na  chanzo cha Mto Katuma.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba akiangalia eneo lililokuwa likitumiwa na Jema Sitalike Project ambao walizuiwa kuendelea na shughuli za uchenjuaji wa dhahabu kutokana na kutokuwa na vibali. Wengine katika picha ni pamoja Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga

 Mashimo yaliyokuwa yakitumiwa na Jema Sitalike Project ambao walizuiwa kuendelea na shughuli za uchenjuaji wa dhahabu kutokana na kutokuwa na vibali, yakiwa yameachwa wazi hali inayotishia usalama wa wananchi wanaozuka maeneo hayo. Waziri Makamba ameagiza kusimamishwa kwa shughuli za Mradi wa Jema ambao kwa sasa wamehamishia shughuli zao Mkoani Mwanza na kuwataka kuchukua hatua za haraka kufunika mashimo yaliyopo Sitalike - Katavi

Viboko Katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi wakiwa wanaathirika kutokana na upungufu wa maji katika Mto Katuma. Waziri Makamba ametangaza hatua za haraka na za muda mrefu za kurejesha mto huo katika hali yake ya awali.

BUJUMBURA READIES FOR REGIONAL PETROLEUM TALKS

0
0

The 8th East African Petroleum Conference and Exhibition 2017 (EAPCE’17) will be held from 8th to 10th March, 2017 at the Le Panoramique Hotel in Bujumbura, Burundi. The conference organized by the East African Community (EAC) is expected to attract more than 600 participants. 

The 2017 edition of the biennial conference under the theme, East Africa - An Emerging Hotspot for Oil and Gas Exploration, Infrastructure Development and Commercialization, aims at promoting the region’s petroleum potential and investment opportunities. The last five Conferences have proven a valuable forum for governments and petroleum industry players from around the world to dialogue.

According to the EAC Secretary General, Amb. Liberat Mfumukeko, the conference is expected to provide a forum for dialogue for all players in the Petroleum industry regionally and internationally. 

“It will provide unique networking opportunities with government, private sector, regional organizations, academia, technology developers, investors and civil society,” added the Secretary General.Held since 2003, the East African Petroleum Conferences have provided increasing awareness of the potential for petroleum development in the region and other important developments in the petroleum sector including technological advancements in exploration, development and production. 

Delegates can expect high quality technical presentations, exhibitions from a wide spectrum of players from the petroleum sector. The conference programme integrates field excursions to selected sites in each Partner State for delegates to see the rich geological variety that the region possesses as well as the touristic attractions that the region is well known for. 

EAPCE’17 is taking place at the peak of EAC's transforming into a Common Market. This transformation is geared towards providing great opportunities for business and investment in all sectors as the single market provides for free movement of goods, capital and services within the region.

For more information on EAPCE’17, visit the conference website: www.eapce17.eac.int 

MELI YA MV MAPINDUZI II YAREJEA ZANZIBAR

0
0
Na Kijakazi Abdalla, 
Maelezo - ZANZIBAR
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetumia kiasi ya dola 90 elfu kuifanyia matengenezo ya kawaida Meli ya MV Mapinduzi ll iliyopelekwa Chelezoni Mombasa.
Akizungumza na waandishi wa Habari Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji  Mustafa Aboud Jumbe mara baada ya kuwasili Bandarini Malindi amesema itaanza safari zake za kawaida za Pemba kuanzia kesho ili kupunguza usumbufu wa usafiri uliojitokeza baada ya kuondoaka meli hiyo. 
Alisema kuwa meli hiyo imefanyiwa matengenezo ya kawaida  na hakuna kitu kilicho badilishwa na baada ya  matengenezo hayo itakuwa  chini ya Mamlaka ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoka kwa udhamini wa mtengenezaji.
Hata hivyo Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji  amesema hivi sasa Serikali imo katika mchakato wa kununua meli nyengine mbili mpya, moja  kwa ajili ya abiria na mizigo na nyengine itakuwa ya mafuta.
Mapema Nahodha wa Meli hiyo Abdulrahman  Mzee amesema matengenezo ya meli yaliyofanyika yamekwenda sambamba na muda uliopangwa na  yamefanywa kwa hali ya ubora kabisa.
Amesema kuwa kufanyika kwa matengenezo ya meli hiyo ni jambo la kawaida kwa chombo chochote cha usafiri jambo linalokipa ubora chombo husika.
Meli ya MV Mapinduzi ll iliondoka Zanzibar  wiki mbili zilizopita kwenda chelezoni  Mombasa na imerejea  Zanzibar leo kupitia  Pemba ikiwa imechukua  abiria 1200 pamoja na mizigo.

NYOTA WA KANDANDA WA BRAZIL CARLOS ALBERTO AFARIKI DUNIA

0
0

Beki wa kulia na nahodha wa timu ya Taifa ya Brazil kwenye Kombe la Dunia Mwaka 1970  Carlos Alberto amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 72,  klabu yake ya zamani Santos imetangaza leo.
Beki huyo amechezea Brazil mara 53 na kufunga goli linalotajwa kuwa bora zaidi katika historia ya Kombe la Dunia kwa kupiga shuti kali lililomaliozia ushidni wa bao 4-1 dhidi ya Italy kwenye fainali hizo za mwaka 1970 (angalia video hapo juu).
Kwa mujibu wa habari kutoka Brazil Carlos Alberto alifariki kwa ugonjwa wa moyo. Alipata kuchezea vilabu vya  Fluminense, Santos, Flamengo na New York Cosmos kati ya miaka 1962 hadi  1982 kabla ya kuwa kocha.Taarifa ya klabu ya Santos imesema: "Carlos amecheza jumla ya mechi 445  na kufunga magoli 40 goals toka 1965-1975, na anasifika kuwa beki wa kulia bora kabisa katika Brazil". Klabu hiyo imetangaza siku tatu za maombolezo.


KAMPUNI YA MAXCOM AFRICA - MAXMALIPO WAZINDUA MFUMO WA KULIPA BIMA KIELEKTRONIKI

0
0
Mkurugenzi  Uendeshaji wa Maxcom Africa Kanda ya Africa, Jameson Kassati (wa nne kulia) akiwa  katika picha ya pamaoja na wafanyakazi wa kampuni hiyo pamoja na baadhi ya wadau wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfumo huo.  Kwa taarifa kamili na picha zaidi BOFYA HAPA
Viewing all 109570 articles
Browse latest View live




Latest Images