Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110152 articles
Browse latest View live

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
Ngoma ya 'Bane' ya Oliver Ngoma (RiP) si ya kusahau

Msimamo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Uingereza

$
0
0
No Movement1Man Utd384389
No Movement2Man City383278
No Movement3Chelsea383675
No Movement4Arsenal383573
No Movement5Tottenham382072
No Movement6Everton381563
No Movement7Liverpool382861
No Movement8West Brom38-449
No Movement9Swansea38-446
No Movement10West Ham38-846
No Movement11Norwich38-1744
No Movement12Fulham38-1043
No Movement13Stoke38-1142
No Movement14Southampton38-1141
No Movement15Aston Villa38-2241
No Movement16Newcastle38-2341
No Movement17Sunderland38-1339
No Movement18Wigan38-2636
No Movement19Reading38-3028
No Movement20QPR38-3025

ngoma azipendazo ankal

$
0
0
Miriam Makeba aliirusha bendera ya Tanzaniajuu duniani kwa wimbo huu wa 'Malaika'

sensei Rumadha Fundi ala nondozzz marekani

$
0
0
Mtanzania mtaalamu wa Karate na Yoga Sensei Rumadha Fundi (3rd Dan,Black Belt ) mwenye maskani yake kule marekani juzi Mei 17, 2013 Sensei Rumadha Fundi amekula nondozzz ya "Associate in Applied Science Cardiopulmonary Respiratory Care" katika chuo cha "Collin College, McKinney, Texas, USA. 
Sensei Rumadha sasa amekuwa mtaalam wa hewa na gesi ya kupumua (wa Respiratory Therapist) anayetibu mapafu na moyo chini ya maelekezo ya mganga wa mapafu"pulmonalogist. 
Respiratory therapist ana majukumu mengi kama kuwatibu wagonjwa wa pumu,COPD,Ephysema,Asthma,TB na majonjwa yote yanayohusu mapafu na moyo. Pia ana uwezo wa kutafsiri damu baada ya kupima hali ya mgonjwa kama ana oxygen ya gesi ya kutosha na kama inahitaji tiba yeyote. 
Kwa mengi zaidi kuhusiana na utaalam wa Respiratory Therapist nenda"Who is a Respiratory Therapist? http://en.wikipedia.org/wiki/Respiratory_therapy
 Sensei Rumadha Fundi akielekea kuchukua Nondozzzz zake
 Sensei Rumadha na mkewe Anita pamoja na mdogo wake Rumadha,Kibwana Fundi katika shangwe
 Sensei Rumadha Fundi (mstari wa nyuma) akiwa na wataalamu wenzie wa mapafu
Sensei Rumadha akiwa na ndugu na marafiki.
Sensei Rumadha akiwa na binamu yake Dotto Haruna

mambo ya gado

$
0
0

Good luck to President Jonathan - Against Boco Haram!

mama tunu pinda amjulia hali majeruhi wa bodaboda arusha

$
0
0
Mama Tunu Pinda akimpa pole Mzee Athumani Abdala (76) ambaye amevunjika miguu yake miwili kutokana na kugongwa na pikiki Mzee huyo amelazwa katika Hospitali ya Mkoa  Arusha Maunt Meru Mama pnda alifika hospitalini hapo kuwajulia hali wahanga wa Bomu Picha na Chris Mfinanga

KILELE CHA WIKI WA HIFADHI YA JAMII MJINI DODOMA

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt Jakaya Mrsisho Kikwete akifurahia zawadi aliyopewa na makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi SSRA Bi, Jayne Nyimbo  akimtambia “ kuwa ni championi wa Hifadhi ya Jamii’wakati wa kilele cha wiki ya hifadhi ya Jamii hivi karibuni wakitizama ni waziri wa kazi na ajira Mh. Gaudencia Kabaka na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.

 Mh Waziri wa  Kazi na  Ajira  Mhe. Gaudencia Kabaka akifurahia zawadi aliyopewa na makamu mwenyekiti wa bodi ya SSRA  Bi. Jayne Nyimbo akimtambua jitihada zake katika kuendeleza sekta  ya hifadhi ya Jamii nchini

 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa SSRA waliosimama kuanzia  safu ya nyuma kuanzia kushoto Bw. Mchafu Chakoma na Bw. Jonathan Peles. Mstari wa pili ni  wakuu wa mifuko ya hifadhi ya Jamii Tanzania Bara  wakiwa tuzo  kutoka  SSRA. Walioketi kuanzia kulia ni Mkurugenzi mkuu wa SSRA  BI. Irene Isaka , Makamu mwenyekiti wa Bodi Bi, Jayne Nyimbo, Raisi   wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt Jakaya Kikwete, waziri wa kazi na ajira mh. Gaudencia Kabaka na mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi  
 Picha ya Pamoja ya kamati ya maandalizi na Wanamaonesho wa wiki ya hifadhi ya Jamii chini ya uenyekiti  wa Bi, Sarah Kibonde Msika – Mkuu wa   Mahusiano na Uhamasishaji SSRA
Picha ya  Mgeni rasmi  akiwa pamoja na baadhi ya wajumbe wa  menejimenti ya SSRA  wakati wa kilele cha maonesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii mjini Dodoma.

MTWARA WAPOKEA TUZO ZA SAFARI LAGER

$
0
0

 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami (wa pili kushoto) akipokea moja ya tuzo za Bia Bora Afrika ilizoshinda bia ya Safari Lager kutoka kwa Mwakilishi wa TBL mikoa ya Lindi na Mtwara, Bariki Massawe(kushoto)  Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa ziara maalum ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuonesha Tuzo ilizoshinda Bia yake ya Safari Lager ambapo jana walikuwa Mkoani Mtwara. Kulia ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami (kushoto), Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (wapili kushoto),Meya wa Maspaa ya Mtwara Mikindani, Shilingi Mtalika (wapili kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Smythes Pangisa wakiwa wameshikilia tuzo za Ubingwa wa Bia Bora Afrika ambayo ilitwaliwa na Bia ya Safari Lager inayozaliwa na Kampuni ya Bia Tanzania mara baada ya Tuzo hizo kupokelewa na Viongozi hao Mkoani Mtwara jana.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami akionge BD Y kupokea moja ya tuzo za Bia Bora Afrika ilizoshinda bia ya Safari Lager katika shindano la Bia Bora Afrika lililofanyioka nchini Ghana.

SUMAYE AENDESHA HARAMBEE CHUO CHA TUMAINI MJINI IRINGA ASUBUHI HII

$
0
0

 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye akizungumza na  wasomi  wa chuo  cha Tumaini hivi  sasa 
 
 Na Francis Godwin
Waziri Mkuu mstaafu, Mhe Frederick Sumaye amewafunda  wasomi  wa  chuo  kikuu Iringa  zamani Tumaini  kuwa  watumie  kanisa  hilo litakalojengwa kwa ajili ya kueneza amani  zaidi  huku  akiwataka kuachana na malalamiko  yasiyokwisha yanayotokana na  baadhi yao  kutojituma katika  kazi. 
Mhe Sumaye  ametoa kauli  hiyo  leo katika  hotuba  yake kwa wasomi  wa chuo   kikuu cha Iringa cha Tumaini kabla ya kuanza kuendesha harambee kwa ajili ya ujenzi  wa kanisa  la  chuo hicho. 
Amesema  kuwa katika  Bibilia  rushwa na ufisadi ni  dhambi kubwa katika Taifa na  kuwa  vitu  hivyo  tunavilea wenyewe japo kuna tatizo  kubwa  na kuwa kaburi  pekee la mambo machafu ni  ujenzi  wa kanisa  hilo na matumizi yake  kutumika kwa malengo ya  kuhubiri amani na kukemea ufisadi. 
" Mfano  ni nani kati yenu amepata  kutozwa  rushwa na mkulima ila rushwa  inatozwa na  wenye nafasi na hivyo lazima  vijana  wasomi  mkumaliza hapa lazima  kwenda  kubadilisha Taifa....ndio maana  nilipoitwa na baba  askofu kwa ajili ya changizo la kanisa nikasema nitafika kwani ni jambo jema" Mhe. 
Sumaye  alisema na kuongezea  kuwa kumshangilia  mtu anayeendesha gari la kifahari alilolipata  kwa njia ya wizi ni hatari na kuendelea kuliangamiza Kanisa.
 Alisema  kuwa  hivi  leo  watu  wanajenga  chuki kati ya  wanyonge na matajiri na  kuwa   limezuka jambo baya  zaidi kwa  watu kuchukiana kwa misingi ya  dini  zao na kuwa  nchi  yeyote  itakayoingia katika machafuko ya imani ni hatari  zaidi.
 Mhe Sumaye  alisema  kuwa vita  ya kiimani ni mbaya  zaidi na siku  zote  vita  hiyo huwa haina mshindi  hivyo ni vema kila dini kuanza utaratibu  wa kuwafundisha  vijana  wake  ili  kuwa na uzalendo katika Taifa   hili.  
Aidha  alisema  kuwa  malumbano ya  kidini yanayoendelea  mbali ya kutokuwa na mshindi ila  bado  vita  hiyo haitakuwa na mshindi na  hivyo ni  vyema  kila mmoja kuachwa akiendelea  kuamini kile ambacho ana amini  hata kama ni chini ya mti  asisumbuliwe. 
Alisema  vita  ya  udini inayoendelea kwa   sasa  ni mbaya  zaidi  na  kuwa  watanzania  tusiruhusu vita   hiyo kupandikizwa .



 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwa katika harambee ya ujenzi  wa kanisa chuo  cha Tumaini ambako mgeni rasimi  ni waziri mkuu mstaafu  Mhe Frederick Sumaye 


Mbunge Msigwa akisalimia katika  harambee  hiyo

Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt Mdegella ,waziri mkuu mstaafu Mhe  Frederick Sumaye na mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dkt Ishengoma  wakiwa katika harambee  hiyo. Picha na Francis Godwin. 

news alert: PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-

$
0
0

Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

 Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania 
(TFF)

Jaji Mkuu wa Tanzania ziarani mkoa wa katavi leo

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman, akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Tanzania mkoani humo walikokuja kumpokea leo asubuhi Katika Ofisi ya Ikulu ndogo ya Mkoa wa Katavi kuanza ziara yake ya kikazi ya kutembelea Mahakama na kujionea hali ya utoaji haki mkoani humo. Picha na Mary Gwera wa Mahakama ya Tanzania

Miss Tabata kutembelea hifadhi ya wanyama ya Mikumi Mei 26, 2013

$
0
0
Washiriki wa Miss Tabata 2013  (pichani) watatembelea mbuga ya wanyama ya Mikumi wikiendi ijayo. Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga anasema lengo la ziara hiyo ni kukuza utalii wa ndani, na kwamba  warembo hao pia watapata fursa ya kujua vivutio vilivyomo kwenye mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.
 “Hii siyo mara yetu ya kwanza kuwapeleka warembo wetu mbugani. Tumekuwa tukifanya kila mwaka,” alisema Kalinga. Kapinga alisema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na CXC Africa. 
 Shindano la kumsaka Miss Tabata litafanyika Mei 31 katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata. Wadhamini wa shindano hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, CXC Africa, Brake Point, Michuzi Blog  na Saluti5. 
Warembo watakaoshiriki kwenye shindano hilo  (pichani) linaloandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19), Rehema Kihinja (20), Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na Suzan Daniel (18). 
 Warembo watano watachaguliwa kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania. Anayeshikilia taji la Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.

majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote yamalizika Visiwani Zanzibar

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (tnbc) Bw. Raymond Mbilinyi, akizungumza na washiriki mbalimbali mjini Unguja Visiwani Zanzibar wakati wa kuhitimisha majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (smart partnership dialogue) katika ngazi ya kanda ikiwa ni hatua ya kuelekea katika ngazi ya kitaifa, (katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dk. Idrisa Hija na mwisho (Kulia) nia Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Zanzibar Bw. Ali Vuai.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (tnbc) Bw. Raymond Mbilinyi, (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Zanzibar Bw. Ali Vuai, wakati wa kuhitimisha majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (smart partnership dialogue) katika ngazi ya kanda ikiwa ni hatua ya kuelekea katika ngazi ya kitaifa. Majadiliano hayo yalifanyika huko Unguja Visiwani Zanzibar.

NEWS ALERT: MZEE ALLY KLEIST SYKES AFARIKI DUNIA LEO JIJINI NAIROBI

$
0
0

FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA  MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES  (PICHANI) KILICHOTOKEA LEO MEI 19, 2013  KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA,  ALIKOKUWA AMELAZWA.

MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. MWILI WA MAREHEMU UNATARAJIWA KUWASILI JIJINI USIKU HUU.

MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA KESHO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.

HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ
Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return.



DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE

$
0
0
Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.

DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar.


BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Rais Kikwete afungua na kuongoza semina ya Wabunge wa CCM Dodoma leo

$
0
0
Mwenyekiti Wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua semina maalum ya wabunge wa CCM ilkiyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Spika wa bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM Jenista Mhagama, Waziri mkuu Mizengo Pinda,Makamu wa CCM Bara Ndugu Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Baadhi ya wabunge wa CCM waliohudhuria semina maalum iliyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.(picha na Freddy Maro)

Mkuu wa Mkoa wa Geita atangaza kujitolea kuwa balozi wa kampeni ya Fistula kumaliza tatizo hilo ifikapo 2016

$
0
0
Muuguzi na Mnasihi wa CCBRT Theodola Millinga akielimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na namna ya kupata matibabu yake bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kupitia ufadhili wa Vodacom na Vodafone ya Uingereza. Zoezi hilo ni sehemu ya kampeni ya kusambaza ujumbe wa "Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ya malipo inayondelea mikoani kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ikishirikiana na CCBRT.
Mkuu wa Mkoa wa Geira Said Magalula(katikati), Balozi wa Chapa Vodacom Mwana FA na Meneja Uhusiano wa Mambo ya nje wa Vodacom Salum Mwalim wakifurahia moja ya tukio wakati wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na kufikisha ujumbe wa "Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bilaya malipo" liliondeshwa mjini Geita ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuelekea siku ya fistula duniani Mei 23. Vodacom na Vodafone hufadhili matibabu kwa wanawake wenye fistula kwenye hospitali ya CCBRT.
Shuhuda wa fistula akitoa ushuhuda wa jinsi alivyoteseka na fistula kwa mika mine kabla ya Vodacom kufadhili matibabu yake kwenye hospitali ya CCBRT. Ushuhuda huo ulitolewa wakti wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhus fistula na kufikisha ujumbe wa "Fistula inatibika jitokeza upate matibabu bila ya malipo.
Balozi wa Chapa Vodacom Mwana FA akiwahamasisha wakazi wa Geita kuunga mkono kampeni ya kumaliza tatizo la fistula ifikapo mwaka 2016 inayofadhiliwa na Vodacom an Vodafone ya Uingereza kupitia hospitali ya CCBRT.
Balozi wa Chapa Vodacom Msanii Mwana FA akichana mistari mbele ya wakazi wa Mji wa Geita waliofika katika kampeni ya uelimishaji umma kuhusu fistula na kusambaza ujumbe wa "fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ua malipo". Mwana FA yupo kwenye msafara wa kueneza ujumbe huo kw amikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Singida, Dodoma, Morogoro na Pwani kwa ufadhili wa Vodacom.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Bw. Said Mgalula akimakbidhi kipaza sauti Balozi wa Vodacom Msanii Mwana FA ili awashushie mistari wakazi wa mji huo waliojitokeze kwenye kampeni ya uelimishaji jamii kuhusu fistula na kwamba matibabu yake yanapatikana bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kwa gharama za Vodacom na Vodafone ya Uingereza.
Meneja wa Vodacom Mwanza Victoria na mwenzake wa Misungwi Gift wakihifadhi nambari maalum ya kupiga bure 0800752227 kwa masuala yoyote yanayohusu fistula baada ya kutangazwa kwenye kampeni ya kuwaelimsisha wakazi wa mji wa Geita kuelekea kilele cha siku ya fistula duniani Mei 23. Nambari hiyo ni kwa wateja wa Vodacom pekee.Vodacom na Vodafone ya Uingereza hugharamia matibabu bila malipo kwa wagonjwa wote wa fistula wanaoitibiwa katika hospitali ya CCBRT.

Jaji Mkuu ziarani Mkoani Katavi

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman, akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Tanzania mkoani humo walikokuja kumpokea jana Katika Ofisi ya Ikulu ndogo ya Mkoa wa Katavi kuanza ziara yake ya kikazi ya kutembelea Mahakama na kujionea hali ya utoaji haki mkoani humo, mbele ya Mhe. Jaji Mkuu ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mhe. Paza Mwamlima ( picha na Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania).

Na Mary Gwera, Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman amewataka Majaji na Mahakimu nchini kusikiliza kesi na kuzitolea maamuzi kwa wakati ili kuondokana na mlundikano wa mashauri ambao pia unasababisha pia mlundikano wa Mahabusu gerezani.

Wito huo umetolewa na Jaji Mkuu wa Tanzania, akiwa Katika ziara yake ya kikazi ya kutembelea na kukagua Mahakama katika Mikoa ya Mbeya, Rukwa na Katavi hivi karibuni.

"Mahakama imejipanga Katika kuhakikisha kuwa kila kesi inayoingia Mahakamani isizidi zaidi ya miaka miwili, hii ni Katika kuhakikisha kuwa tunaondokana na mlundikano wa mashauri katika Mahakama zetu nchini," alibainisha.

Aliongeza kuwa, hivi karibuni Maafisa mbalimbali wa Mahakama walitembelea Mahakama nchi nzima ili kupata takwimu za kesi za muda mrefu, lengo ni kuwa kumaliza mashauri yote ya nyuma ndani ya miaka miwili ijayo.

Hata hivyo, Mhe. Jaji Mkuu aliongeza kuwa suala la kumaliza mashauri kwa wakati ni jambo ambalo linahitaji ushirikiano wa karibu baina ya wadau wote wa sheria kuanzia Ofisi ya upelelezi, DPP na kadhalika.

Aliainisha juu ya maeneo muhimu ambayo yanaweza kutatua tatizo la mlundikano wa mashauri ikiwa ni pamoja na kuboresha Masjala za Mahakama jambo ambalo linaenda samba samba na utunzaji bora wa Mafaili ya kesi, kuboresha maslahi ya Majaji na Mahakimu pamoja na Watumishi wote wa Mahakama kwa ujumla.

Pamoja na hayo, Mhe. Jaji Mkuu aliainisha madhumuni ya ziara yake kuwa ni kutathmini kazi ya utoaji haki kwa ngazi zote za Mahakama, kuongea na Watumishi ili kuainisha changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika utendaji kazi wa kila siku.

Miongoni mwa changamoto zilizoibuliwa Katika ziara hiyo ni pamoja na uchakavu wa majengo ya Mahakama, maslahi duni kwa watumishi wa Mahakama na mengineyo.

Katika ziara yake Katika Mikoa hiyo Mhe. Jaji Mkuu aliambatana na Naibu Mkurugenzi wa Mahakama za Wilaya hadi Rufaa, Mkurugenzi wa Mahakama za Mwanzo, Afisa Tawala ili kujionea maeneo hayo na hatimaye kuhaidi kufanyia kazi changamoto zilizoainishwa.

NEWS ALERT: MZEE ALLY KLEIST SYKES AFARIKI DUNIA JIJINI NAIROBI LEO

$
0
0
FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA  MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES  (PICHANI) KILICHOTOKEA LEO MEI 19, 2013  KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA,  ALIKOKUWA AMELAZWA.

MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. MWILI WA MAREHEMU UNATARAJIWA KUWASILI JIJINI USIKU HUU.

MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA KESHO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.

HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ
Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return.



Redds Miss Kibaha 2013 ni Nzera Kitano

$
0
0
ALIYEKUWA mshiriki namba 6 katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013 katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer Kibaha Maili Moja mkoani Pwani.

Nzera ambae alionekana kuwa mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa wakishindana kuwania taji hilo.

Aidha kwa ushindi huo Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.

Mshindi wa pili ni Ester Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye vyombo vya habari.

Mshindi wa tatu ni Rachel John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.

Kwa ushindi huo warembo wote watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na Redds Miss Kibaha ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday Resort na Amazon Night Club.

Bendi ya Muziki wa dansi ya Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.
Viewing all 110152 articles
Browse latest View live




Latest Images