Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110004 articles
Browse latest View live

Article 11

$
0
0
KC GLOBAL LINKS LTD

SEA AND AIR CARGO UPDATES..!

THE NEXT AIR CARGO NO 1001 TO DAR WILL DEPART ON SATURDAY 01/10/2016. CUT OFF FRIDAY 30/09/16

OUR NEXT CONTAINER CARGO NO 1001 TO DAR WILL DEPART ON 15/10/2016  CUT OF 14/10/2016

PLEASE BRING YOUR CARGO NOW TO AVOID DELAYS

AIR CARGO TO DAR £3.50 PER KG INCLUSIVE CLEARANCE  

AIR CARGO TO DAR £1.80 PER KG EXCLUSIVE CLEARANCE

AIR CARGO TO NAIROBI £1.80 EXCLUSIVE CLEARANCE

MZIGO KWA MELI TO DAR £1.80 INCLUSIVE CLEARANCE
(CONTAINER ZINAONDOKA MARA MBILI KWA MWEZI)

YOU CAN BUY ANY ITEMS ON EBAY, AMAZON OR AUTOTRADER AND LET THEM DELIVER TO OUR OFFICE AND WE WILL DELIVER IT TO YOU WITHIN 7 DAYS

CONTACT US ON;
OFFICE; +44 1375 85 85 25
MOBILE; +44 7494 36 41 94
kcgloballinks@yahoo.com
info@kcgloballinks.co.uk

KC GLOBAL LINKS LTD
SUITE 2 CLIPPER HOUSE, TILBURY DOCKS, RM18 7SG
CARGO COLLECTION ANYWHERE IN LONDON IS FREE

NEWS ALERT: WAZIRI MKUU KUHAMIA RASMI DODOMA KESHO IJUMAA

MALAIKA ATOA SIRI ZAKE NA CHEGE CHIGUNDA NA MAMBO MENGINE KIBAO

$
0
0
Hit Maker wa Rarua, Malaika amefunguka Mambo kibao kwenye Sehemu ya kwanza ya Exclusive Interview na DJHAZUU kupitia VMG Africa TV. Kwenye Interview hii Malaika anazungumzia Mahusiano yake ya awali na Chege Chigunda Kabla na baada ya Kufanya naye wimbo wa USWAZI TAKE AWAY.Hata hivyo pia amezungumzia Sababu ya yeye Kufeli Masomo yake na  kushindwa kuendelea na shule. TAZAMA EXCLUSIVE INTERVIEW YAKE HAPA CHINI

WAFANYAKAZI WA CATS-NET LTD WAMPONGEZA MFANYAKAZI MWENZAO MISS GABRIELLA (A.K.A Miss CATS-NET) KWA KUADHIMISHA SIKU YAKE YA KUZALIWA

$
0
0
Miss Gabriella Faith  A.K.A Miss Cats-net akikata keki leo mbele ya wafanyakazi wenzake (hawapo pichani) kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa leo maarufu kama Birthday. 
Birthday Lady Miss Gabriella akimlisha mmoja wa wafanyakazi wenzake Bwana Spenser katika kusherehekea siku hiyo ya kuzaliwa kwake ambayo ameiadhimisha siku ya leo.
Miss Gabriella akimlisha kwa madaha mmoja wa wafanyakazi wenzake Mr. Abbas wakati wa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa leo.

Wafanyakazi wa CATS-NET LTD Wanapenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Miss Gabriella kwa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa leo na wanamtakia maisha marefu na yenye baraka nyingi. 
"HAPPY BIRTHDAY GABRIELLA"

14 year old Nigerian girl Zuriel demands action to address climate change

TAARIFA KUTOKA TFF

$
0
0
TAIFA STARS WATAKAOIVAA ETHIOPIA HAWA HAPA
 Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa ametaja majina ya nyota 24 watakaounda kikosi ambacho kitasafiri mwishoni mwa wiki ijayo kwenda Addis Ababa, Ethiopia kucheza na wenyeji wetu kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika Oktoba 8, mwaka huu. 
Mkwasa maarufu kwa jina la Master amesema wachezaji aliowaita wataingia kambini Oktoba 2, 2016 kabla ya kuanza kukiandaa kuanzia Oktoba 3, 2016 ikiwa mara baada ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ya mwishoni mwa wiki hii ambako Mwadui itacheza na Azam huku Mbao ikishindina na JKT Ruvu Oktoba 2, mwaka huu.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

KAULI NZITO YA MAKOCHA SERENGETI BOYS 
Makocha wa timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wa Tanzania ‘Serengeti Boys’, Bakari Nyundo Shime na Muharami Mohammed anayewanoa makipa watatu wa timu hii, wamesema kwa pamoja: “Tuko tayari kwa vita.” 
Shime maarufu kama Mchawi Mweusi, amezungumza hayo wakati anaendelea kufanya maandalizi ya mwisho ya mchezo dhidi ya Jamhuri ya Congo utakaofanyika Jumapili Oktoba 2, kwenye Uwanja wa Alphonse Massamba-Débat ulioko kwenye Makutano ya Barabara za Nkolo na Boko, hapa jijini Brazzaville. 
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

Article 5

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 29.09.2016


Africa 2016 Photo Competition: Agility Announces Winners of Africa 2016 Photo Competition

$
0
0
 Technology category and grand prize winner: Stephen Simiyu, Kenya. 
JUNA, UGANDA (Source of the Nile River): For more than 20 years. Mr. Atika’s fishing business on Lake Victoria has helped him provide his family with a comfortable life. Now they have joined the global digital world.
 Industry category winner: Esdore Hakizimana, Rwanda.
This solar power industry, situated in the 20 miles east Kigali, Rwanda, has a capacity of 10 megawatts. The energy it produces powers nearly 1500 homes. The solar farm has had a large impact on the people of Rwanda.

Cities category winner: Henry Oliver Hakulandaba, Zimbabwe
Western side of Harare CBD, just after rush hour.

UN TO WORK CLOSELY WITH EAC TO PROMOTE PEACE IN EAST AFRICA

$
0
0
The United Nations Office in Nairobi (UNON) will work closely with the East African Community to promote peace and security within the East African region. 
The Director General of the UNON, H.E. Sahle-Work Zewde, said that the UN was keen on collaborating with the EAC and other Regional Economic Communities (RECs) in conflict prevention and conflict management. 

Ms. Zewde said the UN’s priority was preventive diplomacy in preventing conflicts, adding that it would cooperate with the EAC addressing the conflict in South Sudan, radical extremism in East Africa and supporting Burundi peace process. 
Ms. Zewde said the UN mission in Burundi had been through several stages including peacekeeping and a political mission. The UN official emphasized the importance of homegrown solutions and mediation in addressing national conflicts, adding that electoral disputes were the cause of political instability in Africa. 
Ms. Zewde was speaking when she paid a courtesy call on the EAC Secretary General, Amb. Liberat Mfumukeko, at the EAC Headquarters in Arusha, Tanzania.  
In his remarks, Amb. Mfumukeko briefed the Director General on the progress of the Inter-Burundi Dialogue and the efforts being made by the EAC Secretariat to facilitate the peace talks.   
On the entry of the Republic of South Sudan into the Community, the SG said that the EAC Secretariat was working on a roadmap to integrate the world’s youngest country into the EAC. 
The two leaders agreed on the development on a joint EAC-UN Framework on Collaboration in various sectors under which the EAC would identify priorities it would like to be addressed in cooperation with the UN.
 EAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko in talks with H.E. Sahle-Work Zewde, the Director General of the UN Office in Nairobi, who paid him a courtesy call at the EAC Headquarters in Arusha, Tanzania today. 
 Director General of the UN Office in Nairobi, H.E. Sahle-Work Zewde, with EAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko outside the EAC Headquarters. On the left is Ms. Ruphina Mbua Manono, the Political Adviser to the Director General. 
 EAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko with H.E. Sahle-Work Zewde, the Director General of the UN Office in Nairobi outside the EAC Headquarters in Arusha, Tanzania today. 
EAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko with H.E. Sahle-Work Zewde, the Director General of the UN Office in Nairobi outside the EAC Headquarters in Arusha, Tanzania.

WAZIRI MKUU MAJALIWA APOKEA MISAADA ZAIDI YA WAATHIRIKA WA TETEMEKO KAGERA

$
0
0




 Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea mchango wa shilingi milioni 10 kutoka kwa Mstahiki Meya wa Dar es salaam Mhe. Isaya Mwita ukiwa ni mchango wa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 29, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na UwekezajiCharles Mwijage.
 Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea mchango wa shilingi milioni tano kutoka kwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Shyrose Bhanji ukiwa ni mchango kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 29, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na UwekezajiCharles Mwijage.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea moja kati ya mabati 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka kwa Eric Shigongo Mkurugenzi Mtendaji wa  Global Publishers  (kushoto)  ukiwa ni mchango wa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisni kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 29, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
 Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea mchango wa shilingi milioni 20 kutoka kwa watendaji wa kampuni ya Trans Ocean Supplies Limited ukiwa ni mchango wa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 29, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na UwekezajiCharles Mwijage.
Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akipokea mchango wa shilingi milioni 50 kutoka kwa watendaji wa kampuni ya Pepsi ukiwa ni mchango wa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 29, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na UwekezajiCharles Mwijage.

MICHANGO YA ZAIDI YA SH. MILIONI 760 YAPOKEWA LEO
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea zaidi ya sh. milioni 760 zikiwa ni misaada kwa wananchi walioathirika na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Septemba 10, mwaka huu.
Amepokea misaada hiyo kutoka kwa taasisi na wadau mbalimbali likiwemo kundi la wanawake New Millennium linaloundwa na wake wa viongozi wa Serikali walio madarakani na waliostaafu.
Makabidhiano ya michango hiyo, yamefanyika leo jioni (Alhamis, Septemba 29, 2016) kwa nyakati tofauti kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam pamoja na makazi ya Waziri.
Miongoni mwa waliokabidhi misaada hiyo ni pamoja Meya wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Isaya Mwita sh. milioni 10, Kampuni ya mabati ya ALFA imekabidhi mabati yenye thamani ya sh. milioni 50 na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) sh.milioni 100. 
Wengine ni Ofisa Mtendaji Mkuu kampuni ya vinywani baridi ya Pepsi Cola, Bw. Avinash Jha amekabidhi sh.milioni 50, kampuni ya Round Table pamoja na wadau wao sh. milioni 57, kampuni ya Wool Worth  sh.milioni 20 na Jumuiya ya Waislam (FIRDAUS) imetoa viti 15 vya walemavu.

Aidha, kampuni ya Trans Ocean Supplies LTD imetoa sh. milioni 20, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza amekabidhi sh. milioni 18.681,Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Shy-Rose Bhanji amekabishi sh. milioni tano. 

Pia Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta Tanzania kimekabidhi sh. milioni 415.8, kundi la mtanzao wa kijamii la Whatsapp la Papaso, D’jaro Arungu limekabidhi sh.520,000 na kampuni ya mafuta ya Camel iliyokabidhi mifuko 1,000 ya saruji.

Jumuia ya Wanataaluma ya Vyuo Vikuu vya Umma Tanzania (ASAs) imekabidhi sh. milioni 7.5, Umoja wa Wamiliki wa Maduka ya Dawa Muhimu Tanzania umekabidhi dawa zenye thamani ya sh. milioni tano pamoja na Eric Shigongo wa Global Publisher amekabidhi mabati 500 yenye thamani ya sh. milioni 10.

Waziri Mkuu amewashukuru wadau wote kwa misaada hiyo na kuahidi kuwa Serikali itahakikisha michango hiyo inafikishwa Kagera kwa walengwa.
“Tunashukuru sana kwa michango yote. Michango hii ni muhimu na inaonyesha mshikamano wa dhati uliopo. Michango hii inaonyesha kuguswa na mapenzi ya dhati kwa waliopatwa na maafa. Amesema.
Akaunti ya maafa imefunguliwa katika Benki ya CRDB yenye Namba. 015 222 561 7300 kwa jina la KAMATI MAAFA KAGERA – Swiftcode: CORUtztz na namba za simu za mkononi zinazotumika kupokea michango hiyo ni 0768-196-669(M-Pesa), au 0682-950-009 (Airtel Money) au 0718-069-616(Tigo Pesa).
Tetemeko hilo lililotokea Jumamosi, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17 na wengine 440 walijeruhiwa kati yao watu 253 walifikishwa Hospitali ya Mkoa, 153 walilazwa, 113 walitibiwa na kuruhusiwa na wengine 38 wanaendelea na matibabu ambapo kati yao watu 23 wamefanyiwa upasuaji mkubwa na wanaendelea vizuri.
Pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 2,063 kuanguka huku nyingine 14,081 zikiwa katika hali hatarishi baada ya kupata nyufa na 9,471 zimepata uharibifu mdogo huku wananchi 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
ALHAMIS, SEPTEMBA  29, 2016  





RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kabla ya kuanza kwa Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongoza Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 29, 2016.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa taarifa juu ya  maamuzi ya Baraza la Mawaziri kuhusu Serikali kuridhia rasmi utekelezaji wa mradi ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Kabaale katika Wilaya ya Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania. 

SERIKALI YARIDHIA UTEKELEZAJI WA 
UJENZI WA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA
SERIKALI ya Tanzania imeridhia rasmi utekelezaji wa mradi ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Kabaale katika Wilaya ya Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania. 
Uamuzi huo umefikiwa katika Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika leo (tarehe 29 Septemba, 2016) Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. 
Taarifa ya kuridhiwa rasmi kwa mradi huo imetolewa naWaziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambaye amesema ujenzi wa mradi huo utakaoanza wakati wowote kuanzia sasa unatarajiwa kukamilika mwaka 2020. 
Amesema ujenzi wa bomba hilo unatarajiwa kugharimu dola za Marekani Bilioni 3.5 ambapo kati yake Dola Bilioni 3 zitatumika kujenga bomba upande wa Tanzania. 
Mradi huom kubwa utatekelezwa kwa ubia wa ujenzi na uendeshaji kwa kushirikishaka mpuni za Total ya Ufaransa, CNOOC ya China, Tullow ya Uingereza na Serikaliza Tanzania na Uganda. 
Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilometa 1,443 linatarajiwa kusafirisha mapipa 200,000 kwa siku ambapo kila pipa litaliingizia taifa Dola za Marekani 12.2. 
Amebainisha kuwa pamoja na kusafirisha mafuta ya kutoka nchini Uganda bomba hilo pia linatarajiwa kusafirisha mafutakutoka nchi nyingine zaJ amhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudani Kusini ambazo zimeonesha nia ya  kusafirisha mafuta yao kupitia bandari ya Tanga. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaja faida nyingine ambazo Tanzania itazipata kutoka na namradi huo kuwa ni kupatika na kwa ajira zaidi ya 15,000 wakati wa ujenzi na ajira 2,000 baadaya ujenzi kukamilika, kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia, kukuza biashara katika ukanda wa kaskazini mwa Tanzania, kampuni za ujenziza Tanzania kupata kazi za ujenzi. 
Aidha, amesema Tanzania inatarajia kunufaika zaidi kwa kutumia bomba hilo kupitisha mafuta yanayotarajiwa kupatikana katika maeneo ya ziwa Tanganyika na Ziwa Eyasi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMATANO, SEPTEMBA  28, 2016  



BENKI KUU YA TANZANIA YASEMA PATO LA TAIFA LIMEONGEZEKA KWA ASILIMIA 7.9

$
0
0

Na Dotto Mwaibale

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imesema ukuaji wa pato la Taifa umeongezeka kwa asilimia 7.9 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 5.8 kwa kipindi kama hicho mwaka 2015.

Hayo yamebainishwa na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu Dar es Salaam leo asubuhi wakati akizungumza na wanahabari kuhusu ukuaji wa pato la Taifa kwa robo na nusu mwaka 2016.

Profesa Ndulu alisema shughuli za kiuchumi zilizokua kwa kasi ya juu zaidi katika kipindi hicho ni usafirishaji na uhifadhi wa mizigo ikiwa ni asilimia 30.6, uchimbaji wa madini kwa asilimia 20.5, mawasiliano na habari asilimia 12.6 na sekta ya fedha na bima kwa asilimia 12.5.

Alisema ukuaji wa sekta ya uchukuzi na uhifadhi wa mizigo umetokana na kuongezekea kwa usafirishaji wa abiria kwa njia ya barabara na gesi asilia ambao umekua kwa zaidi ya nusu ukilinganisha na robo ya pili ya mwaka 2015 kwa asilimia 9.4.

"Kwa upande mwingine, ukuaji wa sekta ya uchimbaji wa madini na gesi umechangiwa zaidi na kuongezeka kwa uzalishaji wa gesi ambao umekua kutoka mmSFt3.7,793 kwa mwaka 2015 mpaka mmSFt3 11,267 kwa mwaka 2016" alisema Ndulu

Profesa Ndulu alitaja sekta nyingine ambayo imefanya vizuri ililinganishwa na kipindi kama hicho kwa mwaka 2015 kuwa ni sekta ya kilimo ambayo imekua kwa asilimia 3.2 kwa robo ya pili ya mwaka 2016 wakati mwaka jana ilishuka kwa asilimia 1.9.

Aidha sekta ya fedha na bima imekua kwa asilimia 12.5 kwa robo ya pili ya mwaka 2016 ikilinganishwa na asilimia 10.0 kwa robo ya pili ya mwaka 2015.

Akizungumzia ukuaji wa pato la Taifa alisema katika nusu ya mwaka 2016 yaani Januari hadi Juni 2o16 kasi ya ukuaji wa pato la taifa imeongezeka na kufikia asilimia 6.7 ikilinganishwa na asilimia 5.7 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2015.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandshi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa taarifa ya ukuaji wa pato la taifa kwa robo na nusu ya mwaka 2016. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mabenki, Kenedy Nyoni.
Kaimu Meneja Kitengo cha Mahusiano kwa Umma wa BoT, Victoria Msima, akimkaribisha Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Beno Ndulu  (wa pili kushoto), kuzungumza na wanahabari kuhusu ukuaji wa pato la taifa kwa robo na nusu mwaka 2015 Dar es Salaam leo.
Taswira ya meza kuu katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Kaimu Meneja Kitengo cha Mahusiano kwa Umma, Victoria Msima,Mkurugenzi wa Idara ya  Usimamizi wa Mabenki, Kenedy Nyoni, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Beno Ndulu na Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti wa Sera za Kiuchumi, David Kwimbere.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

KUNDI LA VITIMBI TOKA KENYA LANOGESHA TAMASHA LA 35 LA SANAA BAGAMOYO

$
0
0
 Waigizaji wa Kundi la sanaa la Vitimbi toka nchini Kenya, wakizungumza mara baada ya kutoa moja maigizo yao katika Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, linaloendelea kufanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Sanaa (TaSuBa), Bagamoyo Mkoani Pwani. Wakizungumza na waigizaji hao walisema kuwa wanafuraha sana kushiriki kwenye Tamasha hilo, kwani ni kubwa na la kuvutia sana, pia wametoa wito kwa Waigizaji wa Kitanzania kuungana na wale wa Kenya na kufanya kazi kwa pamoja kwani wanaamini wakiungana wanaweza kufanya kazi nzuri sana.
 Waigizaji wa Sanaa ya Vichekesho kutoka nchini Kenya, Mama Kayaii na Mama wa Mahakama, wakitoa burudani ya moja ya maigizo yao ya jukwaani kwa watazamaji waliojitokeza kwenye Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, linaloendelea kufanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Sanaa (TaSuBa), Bagamoyo Mkoani Pwani.
 Waigizaji wa Kundi la Vitimbi kutoka nchini Kenya, Ondieki, Profesa na Sukuma Wiki wakiigiza jukwaani katika Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, linaloendelea kufanyika kwenye Ukumbi wa Chuo cha Sanaa (TaSuBa), Bagamoyo Mkoani Pwani.
Igizo likiendelea.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamadini Bagamoyo (TaSuBa), Dkt. Herbert Makoye (kushoto) akizungumza na baadhi ya Waigizaji wa Kundi la sanaa la Vitimbi toka nchini Kenya, mara baada ya kutoa burudani ya kuvutia kwa WanaBagamoyo, waliofurika kwa wingi kwenye Ukumbi wa Chuo cha Sanaa (TaSuBa), Bagamoyo Mkoani Pwani.

NAIBU KAMISHNA AKUTANA NA WAKUU WA USALAMA BARABARANI NCHINI (ZTO)

$
0
0
 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Naibu Kamishna wa Polisi Mohamedi Mpinga wa pili kulia, akimsikiliza  ZTO kanda maalum ya Dar Es Salaam ACP Awadhi J. Haji aliesimama akizungumza katika kikao cha utendaji kazi kilichowahusisha ZTO nchi nzima, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Alphendo Mkoani Geita kabla ya kuendelea na shughuli za uelimishaji juu ya Usalaam Barabarani wiki ambayo kitaifa inaadhimishwa  Mkoani Humo.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Naibu Kamishna wa Polisi Mohamedi Mpinga wa pili kulia, akimsikiliza  ZTO kanda maalum ya Dar Es Salaam ACP Awadhi J. Haji aliesimama akizungumza katika kikao cha utendaji kazi kilichowahusisha ZTO nchi nzima, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Alphendo Mkoani Geita kabla ya kuendelea na shughuli za uelimishaji juu ya Usalaam Barabarani wiki ambayo kitaifa inaadhimishwa  Mkoani Humo.
(Picha na Trafiki kuu)

TFS YASAIDIA MADAWATI 12,000 MKOANI MWANZA.

$
0
0
 Naibu  Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii , Eng.  Ramo Makani( kushoto)  akimkabidhi  madawati  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela ( kulia) ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa bungeni mwanzoni mwa mwaka huu na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe ya kutengeneza madawati 20,000,  wa  pili kushoto  ni Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo.
 Baadhi ya madawati yaliyokabidhiwa  jana  na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela  ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa bungeni mwanzoni mwa mwaka huu na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe ya kutengeneza madawati 20,000.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa wamekaa kwenye madawati mara baada ya makabidhiano yaliyofanyika Mkoani Mwanzan jana  na Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani  kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongela  ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa bungeni mwanzoni mwa mwaka huu na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe.

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imekabidhi madawati 12,115 mkoani Mwanza ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa bungeni mwanzoni mwa mwaka huu na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe ya kutengeneza madawati 20,000.

Makabidhiano hayo baina ya TFS na Serikali yalifanyika kitaifa kwenye Uwanja wa chuo cha Mafunzo ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi.

Naibu wa Waziri wa Wizara hiyo , Ramo Makani alitoa mwezi mmoja kwa uongozi wa TFS kuhakikisha unakamilisha kutengenenza madawati 7,885 yaliyosalia kabla ya novemba mwezi huu

‘’ Pamoja na kufikia asilimia 61 ya lengo, nawaomba TFS muhakikishe idadi iliyobaki ya madawati inakamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao’’ Alisema Makani.
Akizungumza kabla ya kukabidhi madawati hayo, Mtendaji Mkuu wa TFS, Prof. Dos Santos Silayo bila kutaja gharama iliyotumika alisema ofisi yake imechelewa kufikia asilimia 100 ya kutengeneza madawati 20,000 kutokana na kuwa na changamoto ya ucheleweshwaji wa taratibu za uvunaji mbao katika baadhi  ya misitu.

TFS tumetekeleza agizo hili kwa kulenga ngazi za chini kabisa za mfumo wa utendaji wa Wakala  ambao ni wilaya. Hivyo katika kugawa idadi ya utengenezaji madawati wa kanda ilizingatia idadi ya wilaya kwa kila kanda’’ alisema Prof. Silayo.

Waziri Makani alisema madawati hayo yatagawiwa katika mikoa ya Simiyu., Kagera, Mara,Geita na Mwanza ambayo itapokea madwati 2,580 yaliyokwisha tengenezwa.

Akizungumz kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa ya Tanzania Bara, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela aliwapongeza TFS na kuahidi kuyatunza madwati hayo ili yatumike kwa muda mrefu kwa manufaa ya wanafunzi.
                ( Picha na Lusungu Helela- Wizara ya Maliasili na Utalii)

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI KUADHIMISHWA KESHO.

$
0
0
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA WAZEE DUNIANI TAREHE 1/10/2016

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto, inatoa taarifa kuwa, tarehe 1 Oktoba ya kila mwaka, ni kilele cha  Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani. Katika siku hii, Tanzania inaungana na nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha Siku hii kwa mujibu wa Azimio la Umoja wa Mataifa Na. 49 la mwaka 1991.  

Maadhimisho ya siku ya wazee duniani ni moja kati ya jitihada za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN) katika kutambua na  kuhamasisha jamii kuweza kulinda na kutetea haki za wazee duniani kote.  Umoja wa Mataifa umetenga siku hii kwa lengo la kutafakari hali ya maisha ya wazee na changamoto zinazowakabili wazee; na hivyo kuweka mipango thabiti ya kuboresha maisha yao na kuwafanya waishi maisha ya heshima, hadhi, na kuthaminiwa utu wao.  

Kila mwaka, Maadhimisho haya huwa yanabeba Kauli Mbiu yenye ujumbe mahsusi. Kwa mwaka 2016 Kaulimbiu inasema “Zuia Unyanyasaji dhidi ya Wazee”. Kaulimbiu hii inahimiza Serikali, jamii, na wadau wengine kutafakari na kuweka mikakati ya kukabiliana na vitendo vya ukatili, mauaji, ubaguzi na dhuluma dhidi ya wazee; vitendo ambayo ni kinyume dhidi ya haki za binadamu. 
Maadhimisho haya kwa mwaka 2016 yanafanyika Kitaifa katika wilaya ya Mbalali, mkoani Mbeya. Kilele cha maadhimisho haya kitajumuisha shughuli mbalimbali ikiwemo huduma ya upimaji wa hiari wa afya na ushauri kwa wazee, michezo na maonesho ya bidhaa na kazi mbalimbali zinazofanywa na wazee. 
Katika kipindi hiki cha Maadhimisho hatuna budi kuenzi na kudumisha mila na desturi nzuri za kuwaenzi wazee kwa kutambua kuwa wazee ndiyo chanzo cha urithi wa historia ya nchi, washauri wa familia na jamii, watu wenye hekima, na walezi katika jamii. Hivyo jamii inaowajibu wa kuwaondolea vikwazo wazee katika kupata huduma za kijamii ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua pale ambapo mzee ananyanyashwa au kutendewa isivyostahili.  

Erasto T. Ching’oro
Msemaji wa Wizara
30/9/2016.

TAASISI 10 ZA SERIKALI ZIMEFANYA CHINI YA KIWANGO YA SHERIA YA MANUNUZI YA PPRA.

$
0
0
  Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga akizungumza na waandishi wa habari juu ya ukaguzi waliofanya katika taasisi za serikali katika kufuata sheria ya manunuzi leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga jijini Dar es Salaam leo.

Na  Yassir Adamu, Globu ya Jamii.
RIPOTI ya Ukaguzi kwenye manunuzi ya umma ya mwaka wa fedha 2015/2016 uliofanywa na mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) unaonyesha taasisi  10  nunuzi  zimefanya  manunuzi chini ya kiwango kisichoridhisha chini ya asimia 60.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga amesema taasisi hizo zimefanya chini ya kiwango katika kufanya manunuzi  yake  kwa  mujibu wa sharia ya manunuzi.

Amesema jumla ya PPRA imefanya  jumla ya mikataba 21,313 ya manunuzi yenye thamani ya sh.Trioni 1.05 katika ujenzi ,vifaa, huduma ushauri wa kitaalam .huduma zilizohitaji mikatba ya ushauri wenye thamani ndogo  pamoja na mikataba yenye makubaliano maalum.

Balozi Lumbanga amezitaja taasisi zilizofanya chini ya kiwango ambazo ni Taasisi ya Uzalishajin (NIP), Dar es Salaam Rapid Transist (DART), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Makumbusho ya Taifa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), Taasisi ya Mifupa (MOI), Halmashauri ya Manispaa ya Msoma pamoja na Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Bukoba (Buwasa).  

Amesema mikataba 122 ya ukusanyaji wa mapato iliyokaguliwa kwenye mamlaka tisa ya serikali za mitaa kwa mujibu wa mikataba iliyokaguliwa imebainika kuwa na mapungufu kadhaa katika usimamizi wa mikataba hiyo na kufanya halmashauri kushindwa kukusanya kiasi cha sh. Milioni 761.54.

Aidha Balozi Lumbanga amesema kuwa kushindwa kukusanya mapato hayo Halmashauri zimesababisha hasara halmashauri hizo zimeshindwa kuchukua hatua zozote dhidi ya wazabuni waliopewa miradi kutokana mikataba walioingia.

TANESCO YAFANYA KIKAO CHA UJIRANI MWEMA NA VIONGOZI WA JAMII INAYOZUNGUKA VITUO VYA KUFUA UMEME WA GESI VYA KINYEREZI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme nchini TANESCO na viongozi wa dini, vyombo vya dola na viongozi wa Serikali za Mitaa sita inayozungu vituo vya kufua umeme wa Gesi asili vya Kinyerezi jijini Dar es Salaam, wamekubaliana kuweka mikakati ya pamoja kuhakikisha jamii inashiriki katika ulinzi wa miundombinu ya umeme.

Makubaliano hayo yamefikiwa leo Septemba 30, 2016, kwenye kikao cha ujirani mwema kati ya TANESCO, TPDC, viongozi wa dini, viongozi wa serikali za mitaa na vyombo vya dola ili kujadili namna bora ya kulinda miundombinu ya umeme kwenye vituo hivyo.

“Umeme wa Gesi ni umeme salama kabisa, hata hivyo ni wajibu wetu kushirikiana pamoja kuhakikisha miundombinu ya umeme huu wa Gesi inatunzwa na kulindwa,”, Meneja wa Kituo cha Umeme Kinyerezi I, Mhandisi Lucas Busunge alianza kwa kusema wakati akiwakaribisha wajumbe kwenye kikao hicho.

Tumeona tuitane hapa leo ili tujadiliane pamoja namna bora ya kuhakikisha umeme huu utokanao na Gesi ambao Serikali imeiingia gharama kubwa, miundombinu yake inalindwa na nyinyi viongozi mnao wajibu mkubwa wa kuwafikishia ujumbe wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka mitambo hii. Alisema Mhandisi Busunge.

Akitoa mada juu ya Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu ya umeme wa Gesi na hasara inayoweza kulikumba taifa na jamii kwa ujumla, Mkuu wa Usalama wa TANESCO makao makuu, Misana Gamba alisema, “Lazima tutambue kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa vituo hivi na fedha hizi ni za walipa kodi wa Tanzania, kwa hivyo ni wajibu wetu sote na sio TANESCO pekee kuhakikisha tunalinda miundombinu hii kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo,” alisema Gamba

Akifafanua zaidi, Mkuu huyo wa usalama alibainisha mambo ambayo jamii inapaswa kuelewa kuwa ni hatari dhidi ya miundombinu ya umeme ambayo ni pamoja na kuwasha moto, kulima au kuchimba mchanga, mmomonyoko wa udongo, wezi wa vyuma, uvuvi haramu, kujenga, kufanya biashara au kuendesha magari makubwa sehemu ambayo miundombinu hiyo ya umeme wa Gesi inapita.

Mkuu huyo wa usalama wa TANESCO alisema, hatari inayoweza kutokea endapo mambo hayo yatafanywa ni pamoja na kurudisha nyuma jiyihada za Serikali katika kuwaletea umeme wananchi, lakini pia hatari ya kulipuka kwa mitambo hiyo ambapo madhama makubwa yanaweza kuwakumba wananchi.

Meneja wa Kituo cha kufua umeme kinyerezi I, Mhandisi Lucas Busunge, akifungua kikao cha ujirani mwema kati ya TANESCO, TPDC na viongozi wa jamii inayozunguka Vituo vya kufua umeme wa Gesi vya Kineterezi jijini Dar es Salaam Septemba 30, 2016.
Mkuu wa Kitengo cha Usalama, TANESCO Makao makuu, Misana Gamba


Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji (aliyesimama), akizungumzia umuhimu wa viongozi wa mitaa kushirikiana na TANESCO katika kuelimisha umma, kutunza miundombinu ya umeme.

Afisa Usalama wa TANESCO makao makuu, Fidelis Almasi, akielezea namna viongozi wanavyoweza kushiriki katika kuelimisha wananchi umuhimu wa kutunza miundombinu ya umeme na athari za zitokanazo na uharibifu wa miundombinu hiyo kwa jamii na serikali.

WAZIRI MKUU APOKEA MICHANGO YA SH. MILIONI 190.

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akipokea hundi ya shilingi milioni 80 kutoka kwa Balozi wa Pakistan nchini, Amir Khan  (wapili kushoto ukiwa ni mchango  kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani  Kagera. 
Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye hoteli ya Kyatt Regency jijini Dar es salaam Septemba 30, 2016. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Augustine Mahiga na  kulia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea hundi ya Shilingi milioni 50 kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Tasisi ya Aga khan nchini, Amin Kurji (kulia) ukiwa ni mchango kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera. Makabidhiano hayo yalifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Septemba 30, 2016. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Augustine Mahiga na wapili kulia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako. 
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea jumla ya sh. milioni 190 kutoka kwa balozi wa Pakistan nchini Mhe. Amir Khan, Kaimu Balozi wa China Mhe. Gou Haodong na Taasisi ya Aga Khan.

Fedha hizo zimetolewa ili kusaidiia  wananchi walioathirika na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Jumamosi, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17 na wengine 440 walijeruhiwa.

Pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 2,063 kuanguka huku nyingine 14,081 zikiwa katika hali hatarishi baada ya kupata nyufa na 9,471 zimepata uharibifu mdogo huku wananchi 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.

Makabidhiano ya michango hiyo, yamefanyika leo (Ijumaa, Septemba 30, 2016) kwenye Hotel ya Hyatt Regency jijini Dar Es Salaam ambapo Waziri Mkuu aliwashukuru kwa michango hiyo na alitumia fursa hiyo kuwaomba wale walioahidi kutoa michango wakamilishe ahadi zao.

“Ninawaomba wale walioahidi kutoa michango wakamilishe ahadi kwa kuzileta ofisini kwangu au kutuma kupitia akaunti ya maafa iliyofunguliwa katika Benki ya CRDB yenye Namba. 015 222 561 7300 kwa jina la KAMATI MAAFA KAGERA – Swiftcode: CORUtztz,” amesema.

Amesema watu walio mbali na benki watumie namba za simu zilizotolewa mahsusi kwa ajili ya kupokea michango ya maafa hayo ambazo ni 0768-196-669 (M-Pesa), au 0682-950-009 (Airtel Money) au 0718-069-616 (Tigo Pesa).

Akikabidhi hundi kwa Waziri Mkuu, Balozi wa Pakistan, Mhe. Amir alisema wanaamini mchango huo wa sh. milioni 80 walioutoa utasaidia kuwapunguzia uchungu wananchi wa Kagera kutokana na athari zilizosababishwa na tetemeko la ardhi.

Kwa upande wake Kaimu Balozi wa China Mhe. Haodong alimweleza Waziri Mkuu kwamba wameshtushwa na tukio hilo na tayari walishawapeleka madaktari na wataalamu wengine mkoani Kagera na leo walikuwa wanakamilisha ahadi yao ya kutoa mchango wa sh. milioni 60.
Naye Muwakilishi Mkazi wa Taasisi za Aga Khan nchini, Amin Kurji  alimkabidhi Waziri Mkuu hundi ya sh. milioni 50.                               
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
IJUMAA, SEPTEMBA  30, 2016.
Viewing all 110004 articles
Browse latest View live




Latest Images