Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109992 articles
Browse latest View live

WAZIRI LUKUVI: SERIKALI TUMEDHAMIRIA KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI

$
0
0
Na Sheila Simba- MAELEZO


Waziri wa Aridhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema kuwa Serikali imeanza kazi ya kupima ardhi  nchi nzima kuanzia mkoani Morogoro.

Akizungumza  katika kipindi kipya cha "TUNATEKELEZA" kinachoandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO na TBC1 ,alisema utekelezaji wa zoezi hilo umeanzia mkoani humo ili kupima maeneo ya wakulima na wafugaji na kutatua migogoro ya ardhi Mkoani humo.

“Serikali tumedhamiria kumaliza migogoro ya ardhi, kutimiza ndoto ya Rais Magufuli ya kuondokana na migogoro ya ardhi isiyo na tija inayosababisha watu kupoteza maisha’’Alisema Lukuvi

 Ameongeza kuwa katika upimaji huo wa ardhi serikali inashirikiana na kampuni binafsi zilizosajiliwa ili kumuwezesha mwananchi anayemiliki shamba,kiwanda ,mkulima na mfugaji mwenye eneo  kupimiwa na kuongezewa thamani.

 “Nakuhakikishia katika kipindi cha miaka 10 kila kipande cha ardhi Tanzania kitakuwa kimepangwa na kupimwa utaratibu mzuri utakao mwezesha kila mtumiaji wa ardhi kutumia eneo lake”alifafanua Lukuvi.

Pia ameeleza suala la kuthibiti bei ya kupima ardhi kwa kushirikiana na wapimaji binafsi katika kumfanya kila mtanzania alipe bei halali ya kupima ardhi.Aidha amesme kuwa Serikali itaweka ukomo wa kumiliki ardhi ili kuondoa tabia za watu kumiliki eneo kubwa la ardhi bila ya kuliemdeleza kwa muda mrefu.

“serikali itaweka muda wa mtu kumiliki ardhi, haiwezekani mtu mmoja amiliki eneo hata bila kulitumia, tabia hii itafika mwisho.”Akizungumzia suala la wageni kumiliki ardhi alisema kuwa ni marufuku kwa wageni na wawekezaji kununua ardhi vijijini bila kupitia wizara inayohusika.

“Ni marufuku kwa mgeni au mwekezaji kwenda kijijini kununua ardhi bila kuja kwangu au Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),wakifanya hivyo tutawapa ardhi wawekeze, Pia mtu yeyote anayetaka kujenga kiwanda popote afike ofisini kwangu nitampatia ardhi ndani ya siku saba.”alisema Lukuvi

Ameongeza kuwa  Wizara imetenga viwanja 240 kwa ajili ya Viwanda eneo la Kigamboni ili kutimiza lengo la Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.Mbali na hayo Waziri Lukuvi alisema  wananchi wote waliodhulumiwa viwanja Jijini Dar es Salaam kwa makosa ya watendaji wa Serikali wameanza kupewa  viwanja vingine mbadala.


“Naagiza Halmashauri zote ziwapatie viwanja mbadala wananchi ambao walidhulimiwa viwanja vyao kwa makosa ya watendaji.”

Mwanadiplomasia: Hakuna sababu ya maandamano

$
0
0
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

Dar es salaam

Tofauti za kisiasa zilizopo nchini zisivuruge nuru ya amani iliyojengwa tangu enzi za Serikali ya Awamu ya Kwanza ambapo siasa za nchi zililenga katika umoja, amani na ujenzi wa Taifa imara, anaonyesha mmoja wa walimu wa diplomasia nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia nchini (CFR), Dkt. Bernard Achiula wakati wa mahojiano na Mwandishi wa habari hii kuhusu hali ya siasa nchini kwa sasa na ushiriki wa watanzania kwa ujumla katika kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano katika utatuzi wa changamoto za kimaendeleo badala ya kuanzisha tabia za vurugu na maandamano.

Dkt. Achiula amesema kuwa uwepo wa amani nchini unachangia katika kuvutia wawekezaji  nchini, kukuza utalii wa ndani, kuvutia wahisani kutoa misaada kwa kuchangia katika uanzishaji na uendelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo kila raia nchini bila kujali itikadi yake ya dini wala chama ana budi kuilinda amani iliyopo.

“Tofauti za kisiasa zipo katika kila nchi kulingana na mitazamo tofauti iliyopo ila kinachotakiwa ni kuweka taifa mbele kwa manufaa ya nchi, watanzania tunatakiwa kuwa wazalendo ili kuimarisha umoja na amani iliyopo kwani vitu hivi vinategemeana na hatimaye kuiwezesha Serikali ya awamu ya tano kuwatumikia wananchi kwa kuwaletea maendeleo.

“Tofauti hizo zisiwe chachu ya kuvuruga amani tuliyonayo bali watanzania kwa ujumla tunatakiwa kuitunza amani hii iliyojengwa tangu enzi za Mwalimu Julius Nyerere ili kuweza kuvutia wawekezaji na  utalii katika nchi yetu” alifafanua Dkt Achiula.

Alisema kuwa haoni sababu kwa vyama vya siasa nchini kuandaa maandamano yanayolenga kuvuruga amani iliyopo kwani kikubwa kinachotakiwa kwa wananchi ni misingi mikuu ya maendeleo ikiwemo elimu, afya na huduma bora mbalimbali  ambapo Rais Magufuli ameanza kuvifanyiakazi. 

Akizungumza kuhusu Balozi zetu nje ya nchi Dkt Achiula aliwashauri mabalozi hao kuzidi kuitanganza nchi yetu ya Tanzania ili kuweza kuvutia wawekezaji, utalii na biashara ili kusaidia katika ukuuaji wa sekta ya viwanda ambapo Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuipeleka nchi katika uchumi wa viwanda.

Akizungumzia utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano Dkt Achiula amesema kuwa Rais Dkt. Magufuli amejikita katika kutatua changamoto zinazolikabili taifa kwa muda mrefu ikiwemo kupiga vita rushwa, kuongeza ukusanyaji mapato kwa kuwabana wakwepa kodi, kubana matumizi ikiwa nia ni kuimarisha uchumi wa nchi na kuipeleka nchi kwenye uchumi wa Kati.

TAARIFA YA MSIBA WA HANIFA SEKIBO

$
0
0
 Familia ya Marehemu Mossey Abdulsalim Sekibo,  Wa Motel Villa, Kijitonyama,  Inasikitika kutangaza kifo cha Binti yao Hanifa Sekibo,  Kilichotokea jana katika Hospitali ya Temeke. 

Ratiba ya Leo. 

Saa 4:00-Mwili kuwasili nyumbani  kwa Mama  wa Marehemu, Bi Gile, Mbezi Makabe.
Saa 5:00-Kusomewa Dua
Saa 6:00-Chakula
Saa 7:00- Marehemu ataswaliwa Msikiti wa Mangara Baada ya Swalat Adhuhuri.
Saa 8:00- Msafara kuelekea Bagamoyo.
Saa 10:00-Maziko Makaburi ya Familia ya Sekibo, Kiromo Shule, Bagamoyo.
Saa 11:00- Msafara kurejea kwa Tanga Ndugu.

Marehemu ameacha mtoto mmoja, Grace-Linda Pascal Mayalla na mjukuu mmoja Sarrah-Patricia.
Innalilah Wainnailaih Rajiun.

 Kufika  msibani kutokea Mbezi mwisho Stendi Mpya. Fuata njia ya Makabe Msakuzi mpaka njiapanda ya Makabe.  Ulizia Msikitini kwa Mangara.

Kwa kuanzia Bagamoyo Rd. Njia ya Goba hadi njia panda ya Makabe .
 
Kwa Maelezo zaidi
Contact
1.Kaka wa Marehemu-Haji Sekibo -0713 866 480
2. Dada wa Marehemu -Masha Sekibo 0719226422.

MUNGUA AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI  PEMA PEPONI-AMIN

WATANZANIA WALIOSOMA CHINA kupata uongozi mpya

$
0
0
NA LEAH MUSHI
Chama cha watanzania waliosoma China- CHINA ALLUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (CAAT) hii leo tarehe 27 August, 2016 kinatarajia kufanya uchaguzi mkuu kwa ajili ya kupata viongozi wake wapya.

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Rombo Green views Hotel sinza Dar es salaam kuanzia saa saba kamili mchana nakufuatiwa na sherehe ya kuwapongeza viongozi wapya na kuwaaga viongozi waliomaliza muda wao.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa uchaguzi wa chama hicho GUSTAV SANGA uchaguzi huo utawaweka madarakani viongozi hao miaka mitatu kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

Nafasi zinazogombewa katika uchaguzi huo ni Chairperson, Secretary, Treasurer, Director of Statistics, media and information, director of Art, culture and heritage pamoja na Director of Education, Science and Technology
SANGA pia amewakaribisha watanzania wote waliomaliza China kujiunga katika chama hicho ili kuweza kutimiza malengo mbalimbali waliyojiwekea ikiwemo kuishauri serikali masuala yahusuyo TANZANIA- CHINA.

Chama hicho cha watanzania waliosoma China kina miaka sita tangu kuanzishwa kwake na kina wanachama tangu waliosoma china miaka ya1980 kwa ngazi ya shahada , astashahada na shahada ya uzamivu. 

BANDA LA MAONESHO LA TANZANIA LANG'ARA KWENYE MKUTANO WA TICAD VI

$
0
0
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka mara baada ya kuwasili kwenye Banda la Maonesho la Tanzania yanayofanyika wakati wa Mkutano wa TICAD VI Jijini, Nairobi. Makampuni na Taasisi mbalimbali kutoka nchi za Afrika ikiwemo Tanzania na Japan yanashiriki maonesho hayo yanayolenga kuvutia wawekezaji na wafanyabishara. 
Mhe. Naibu Waziri akipata maelezo kuhusu bidhaa mbalimbali zinazozalishwa Tanzania zilizokuwepo kwenye Banda hilo. Bidhaa hizo ni pamoja na Kahawa, Majani ya Chai na Viungo vya chakula.
Mhe. Naibu Waziri akikaribishwa na Bi. Latifa Kigoda, Afisa Mwandamizi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) alipotembelea banda la Tanzania.

DC MTATURU AWATAKA WANANCHI WALIOVAMIA ENEO LA HIFADHI KUHAMA NDANI YA MWEZI MMOJA

$
0
0
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kaugere Beatus Kapatya akitoa ufafanuzi mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu.

Na Mathias Canal, Singida

Serikali ilitangaza eneo la Hifadhi ya msitu wa wananchi waliomo ndani mwaka 2003 ambao kutangazwa huko kuliashiria wananchi kuhama katika maeneo hayo ili kutoa fursa kwa serikali kusimamia kwa karibu eneo hilo lakini wananchi hao mpaka sasa hawajahama kwa kukaidi agizo hilo.

Jambo hili limemsukuma Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kufanya ziara na kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo kwa lengo la kuwaelemisha juu ya uvunjaji sheria za nchi kwa kuendelea kusalia katika maeneo ambao wametakiwa kuhama jambo ambalo kama watashindwa kulitekeleza serikali itawatoa kwa nguvu kwani kwa kiasi kikubwa wanaharibu mazingira.

Akizungumza na Wananchi hao katika Kijiji cha Kaugeri Kata ya Mwaru Wilayani hapa Dc Mtaturu ametoa mwezi mmoja kwa wananchi hao kuhama haraka iwezekanavyo ili kupisha eneo hilo la Hifadhi ya msitu kufanya Kazi iliyokusudiwa kwa zaidi ya miaka kumi sasa.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisikiliza Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kaugere Beatus Kapatya akitoa taarifa juu ya kusimama kwa ujenzi wa Zahanati hiyo.

Mtaturu amesema kuwa Kwa mujibu wa sheria Kijiji kinapaswa kutoa Ardhi hekari zisizozidi hamsini kwa mwekezaji lakini uongozi wa Kijiji hicho umegawa kwa mwekezaji hekta 150 hadi 200 kinyume kabisa na taratibu za kiutendaji ukiwa ni pamoja na kuingia mikataba ya kinyonyaji.

Pamoja na hayo pia viongozi hao wametoa Ardhi hiyo bila kushirikisha wananchi jambo ambalo limeibua hisia Kali kwa wananchi ambao wanatambua uporwaji huo wa maeneo yao.

Kufuatia kadhia hiyo ya viongozi hao kugawaji Ardhi kinyume na taratibu Dc Mtaturu amewaweka lumande Mwenyekiti wa Kijiji cha Kaugeri Mange Nkuba, Aliyekuwa Kaimu Afisa Mtendaji Laurent Bomba, na mjumbe wa serikali ya Kijiji Paul Kilo huku Amani Clement ambaye alitoweka kabla Ya mkutano kumalizika anaendelea kutafutwa mpaka apatikane.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Kijiji cha Kaugeri wakati akitoa maelezo wakati wa kikao cha serikali ya kijiji.

Katika hatua nyingine Dc Mtaturu ameagiza mkandarasi Samwel John kukamatwa na kuhojiwa kwa kushindwa kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji tangu Mwaka 2013 ambapo tayari alishapewa kitita cha shilingi milioni 19 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo.

Hata hivyo pamoja na mkandarasi kukabidhiwa fedha hizo alianza ujenzi lakini jengo hilo halijafika hata kwenye Renta huku likiwa limejengwa chini kiwango.

Sambamba na hayo pia Mkuu huyo wa Wilaya ya Ikungi amemuagiza mkurugenzi wa Halamashauri ya Wilaya hiyo kupitia idara ya ujenzi kutoa taarifa kwanini hawakushiriki kutoa huduma za kiutaalamu katika kusimamia jengo hilo la umma kabla na wakati ujenzi unaanza.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Taasisi ya Dr. Amon Mkoga yazinduliwa rasmi jijini Dar

$
0
0
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Habibu Msammy (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Dr. Amon Mkoga yenye lengo la kupunguza uhaba wa madawati mashuleni, Amon Mkoga, kwa pamoja wakionyesha bango la Taasisi hiyo kwa wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uzinduzi wake ikiwa ni ishara ya uzinduzi wake, uliofanyika kwenye Hoteli ya Southen Sun, Jijini Dar es salaam.Kushoto ni Meneja wa shirika la Ndege la Qatar nchini Tanzania ambao ni wadhamini wa kuu wa mradi wa madawati uitwao Simama kaa desk campaign ambao unaendeshwa na Taasisi hiyo, Basel Haydar.

mabadiliko ya mifumo ya ujenzi wa uchumi wa viwanda hayawezi kuletwa na Serikali pekee - Waziri Mkuu

$
0
0
Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu wa Tanzania
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mabadiliko ya mifumo ya ujenzi wa uchumi wa viwanda hayawezi kuletwa na Serikali peke yake bali ni lazima yahusishe pia wadau kutoka sekta binafsi.

“Tunahitaji kushirikiana na sekta binafsi ili tuweze kufanikisha ajenda zetu za maendeleo ziwe za kitaifa, kikanda au za bara zima la Afrika. Ushirikiano huu utasaidia kuleta mabadiliko dhahiri ya kiuchumi na kukuza ustawi wa jamii zetu,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Agosti 27, 2016) wakati akichangia mjadala kuhusu TICAD na umuhimu wake kwa maendeleo ya Afrika mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Sita wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Bara la Afrika (TICAD VI) uliofanyika katika kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Jomo Kenyatta (JICC) jijini Nairobi, Kenya.

“Wakati Serikali zinaweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara na uwekezaji, jukumu kubwa la sekta binafsi ni kuleta mageuzi ya kiuchumi na kujenga uchumi wa viwanda ambao ndio tunakusudia kuufikia,” alisema.

Waziri Mkuu ambaye anahudhuria mkutano huo wa siku mbili kwa niaba ya Rais, Dk. John Pombe Magufuli, alisema Tanzania inawakaribisha wawekezaji wa sekta binafsi kutoka Japan waje kujenga viwanda vya kusindika gesi asilia, kutengeneza mbolea na kemikali mbalimbali, vyuma, nguo, bidhaa za ngozi na usindikaji wa mazao.

Alisema ili kufikia uchumi wa viwanda na maendeleo endelevu, ni lazima nchi za Afrika na wabia wa TICAD wawekeze kwa pamoja na washirikiane kujenga uwezo wa rasilimali watu, kwa kuwa ndio nguzo muhimu ya kuleta ushindani wenye tija katika sekta ya viwanda.

Akizungumzia mpango wa mafunzo kwa vijana wa Kiafrika katika masuala ya biashara (African Business Education Initiative for Youth–ABE), Waziri Mkuu alisema: “Huwezi kuzungumzia mabadiliko ya mfumo wa uchumi wa viwanda bila kujenga uwezo wa watu wetu ambao hasa ndiyo watekelezaji wa mabadiliko hayo. Ni lazima pia tuangalie vipaumbele vya kidemografia kama kweli tunataka kukuza uchumi kwa kujenga tabaka la watu wenye ujuzi.”

Mapema, Waziri Mkuu wa Japan, Bw. Shinzo Abe aliwaahidi viongozi wa nchi za Afrika kwamba nchi yake itatoa kiasi cha dola za marekani bilioni 10 katika kipindi cha miaka mitatu kwa ajili ya kuendeleza miundombinu barani humo na kwamba sehemu ya fedha hizo itatolewa kwa kushirikiana na Benki ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB).

“Ahadi hii ina nia ya kuendeleza miundombinu ya barabara, bandari na nishati jadidifu hasa ya nishati ya jotoardhi kwani bara hili lina uwezo mkubwa wa kuzalisha nishati hiyo kwa wingi,” alisema.

“Uzalishaji wa umeme barani Afrika, unatarajiwa kuongezeka kwa kiwango cha megawati 2,000. Nishati ya jotoardhi itaboreshwa kwa kutumia yeknolojia za Kiajapan. Na kutokana na mradi huo, utazalishwa umeme wa kutosha kuhudumia nyumba zaidi ya milioni tatu ifikapo mwaka 2022,” alisema.

Hii ni mara ya kwanza kwa mkutano wa TICAD kufanyika barani Afrika tangu mikutano hii ianze mwaka 1993. Mkutano huo, unahudhuriwa na washiriki zaidi ya 6,000 kutoka bara la Afrika na Japan.

Mkutano huo uliofunguliwa kwa pamoja na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, umehudhuriwa na marais 34 kutoka nchi za Afrika, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Ban Ki-Moon na Marais wa Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB).

PEACOCK HOTEL YAZINDUA RASMI MTANDAO WAKE WA KIJAMII UNAOLENGA KUTANGAZA CHAKULA CHA ASILI CHA MTANZANIA.

$
0
0

Mmoja kati ya Wakurugenzi wa Peacock Hotel,Daniel Mfugale akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya uzinduazi wa mtanao wa kijaamii unaolenga kutangaza chakula cha asili cha Mtanzania leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wafanyakazi wa hotel hiyo waliofika kwenye uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).

Uongozi wa Peacock Hotel umezindua rasmi mtandao wake wa kijaamii unaolenga kutangaza chakula cha asili cha Mtanzania.

Mmoja kati ya Wakurugenzi wa Hotel hiyo Daniel Mfugale alisema kuwa uamuzi huo umefanyika baada ya kuona mitandao ya kijamii sasa inasambaza taarifa haraka na kuwafikia watu wengi nje na nchi hivyo itasaidia kuongeza utalii Nchini.

“Kwa sasa mitandao ya kijamii ndiyo imeshika hatamu kwa usambazaji wa taarifa hivyo huduma yetu iitwayo Usiku wa Mtanzania ambayo ni maalumu kwa chakula cha asili cha makabila yote nchini itakua inatangazwa katika kurasa zetu za facebook na Instagram tulizozifungua leo”, alisema Mfugale. 

KIFAHAMU KIPINDI KIPYA CHA 'CHUKUA HATUA' KINACHOHUSU VIJANA MKOANI DODOMA

$
0
0
Chukua Hatua ni kipindi kipya cha radio kitakachowashirikisha vijana, wakizungumza na kujadili kwa pamoja masuala yanayowahusu hasa ya kujikwamua na maendeleo mkoani Dodoma na maeneo jirani.

Hiki ni kipindi ambacho kinatarajiwa kujadili kwa kina changamoto za ajira kwa vijana kupata mwelekeo wa maendeleo kwa vijana wa kike na kiume.

Lengo kuu la kipindi hiki ni kutoa taarifa muhimu ambazo zitasaidia vijana kuondokana na ukosefu wa ajira na changamoto wanazokutana nazo katika mihangaiko yao, kipindi kitapaza sauti za vijana ambazo hazikupata nafasi ya kusikika hapo kabla.

Si kipindi tu, bali pia ni jukwaa kwa ajili ya kubadilishana ujuzi, mawazo, uzoefu na pia kujifunza kutoka kwa wengine, ni mahala pekee ambapo kijana atayaona matarajio na uzoefu kutoka fani na taaluma mbalimbali.

Kipindi pia kinatarajiwa kuimarisha ujuzi na kuelekeza upya akili za vijana kufanya kazi na kuchangamkia fursa za ajira kwa ujasiriamali, kujiajiri na kuukwepa umaskini uliokithiri miongoni mwao.

Kipindi kitaanza kuruka hewani siku ya Alhamisi ya tarehe 01/09/2016 kupitia kituo cha RASI FM RADIO inayopatika masafa ya 103.7 Dodoma.

Pia kipindi kitakuwa kinapatikana kupitia mtandao wa Youtube ukurasa wa CHUKUA HATUA, pia mijadala itakuwa inaendelea kupitia ukurasa wetu wa facebook ambao ni CHUKUA HATUA, Instagram ni KIJANA CHUKUA HATUA, na Twitter ni CHUKUA HATUA1

Kipindi hiki kimewezeshwa na mpango wa pamoja wa ajira kwa vijana wa Umoja wa Mataifa kupitia shirika la kazi Duniani (ILO) kwa udhamini wa SIDA.
Watangazaji wa kipindi kipya cha CHUKUA HATUA Happy Balisidya na Mohammed Hammie, siku ya kwanza walipokutana wakati wa maandalizi ya kutengeneza kipindi hicho.

HIVI HAPA VIKOSI VYA YANGA NA AFRICAN LYON WANAOKIPIGA LEO TAIFA

JAFO AFANYA ZIARA YA SIKU MBILI MKOA WA SHINYANGA NA GEITA

$
0
0
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo amefanya ziara ya Siku mbili katika mikoa ya Shinyanga na Geita na kukagua miradi mbalimbali. 

Akiwa Mkoani Shinyanga, Jafo alitembelea Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambapo alijionea changamoto mbali mbali ikiwepo ya Jengo dogo linalotumiwa na kinamama wakati wakujifungua kutokana na hospitali hiyo kuzidiwa uwezo.

Kufuatia hali hiyo, Jafo amemuagiza Injinia wa Wilaya kuhakikisha wanaharakisha ujenzi wa Jengo kubwa la kisasa la kinamama kwani fedha zipo za Ujenzi huo ili wagonjwa wasiendelee kupata mateso kwa michakato ya Ujenzi mirefu isiyo na tija.

Kadhalika, akiwa wilayani Kahama, Naibu Waziri Jafo ametembelea Mradi wa Soko na kumuagiza Mkurugenzi wa Wilaya, Andason Msumba, kuhakikisha anakaa na timu yake ya Wataalamu ili kutatua mgogoro wa Soko hilo kwa Maslahi mapana ya wananchi wa Mji wa Kahama.

Amehitimisha Ziara yake mkoani Shinyanga kwa kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama na Halmashauri ya Msalala ambapo amewataka Watumishi kufanya kazi kwa kujituma huku wakiepuka Uzembe kazini,upendeleo, kupigana majungu, na kuchukiana.

Katika mkoa wa Geita, Jafo amekagua mradi wa Maji na Kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti wilayani Chato huku akimuagiza Mhandisi wa Maji wa Wilaya hiyo kuhakikisha mradi unakamilika mapema kabla ya Mwezi wa 10 ili kuweza kusaidia kutatua changamoto ya Maji.

Amesema wananchi hawawezi kuwa na Upungufu wa Maji wakati kuna maji mengi ya Ziwa Victoria. Akikagua Mradi wa kiwanda cha kukamua Mafuta ya Alizeti, Jafo alimwagiza Mkurugenzi kuhakikisha anashirikiana na Sido ili kuweza kuukamilisha mradi huo haraka.

Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akizungumza na wananchi nje ya kiwanda cha kukamulia alizeti mjini Chato.
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mashine za kukamulia mafuta ya alizeti mjini Chato.
Mkurugenzi wa mji wa Kahama, Andason Msumba akitoa maelezo kwa Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo kuhusu mgogoro wa soko  wanalolitaka wananchi kutumika kwa maslahi ya wananchi wa mji huo. 
Naibu waziri Ofisi ya rais, Tamisemi, Selemani Jafo, akikagua mradi wa maji  kijiji cha Chankorongo wilayani Geita uliohujumiwa na watendaji na kumuagiza Katibu tawala wa mkoa wa Geita kuunda timu ya uchunguzi.

MKUU WA MKOA WA MWANZA ATEMBELEA MFUKO WA PENSHENI WA PPF KANDA YA ZIWA

$
0
0
Mkuu wa Mwanza, John Mongella akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, wakati alipofanya ziara yake ya kwanza ya kutembelea ofisi za taasisi mbalimbali za umma jijini humo.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, namna Mfuko huo unavyofanya kazi, ambapo alisema kuwa mfuko huo sasa unawalipa mafao wanachama wake kwa wakati ambapo umevuka lengo kwa kukusanya michango ya shilingi bilioni 17.03  kati ya shilingi bilioni 17.6 za lengo kwa mwaka jana ulioishia juni 2016. Bandawe alimweleza mkuu huyo wa mkoa kuwa mfuko wa PPF umefanikiwa kusajili wanachama wapya 13,028 kwa Kanda ya Ziwa pekee ikiwa ni sawa na asilimia 105 ya lengo la kusajili wanachama 12,350 kwa kipindi cha mpaka juni 2016.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella akiangalia Kadi yake ya Uanachama wa PPF aliyokabidhiwa na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe.
Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe akimkabidhi Kadi ya Uanachama wa PPF, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akipatiwa maelezo na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Kanda ya Ziwa, Meshach Bandawe (shati jeupe) wakati alipotembelea moja ya Idara ya Mfuko huo, Jijini Mwanza.

ATOWEKA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA

$
0
0
MKAZI wa kijiji cha Kabare kata ya Uwarama wilaya ya Kakonke, Robent Laurent (35) ametoweka nyumbani kwake Dodoma Makulu katika mazingira ya kutatanisha.
Kwa mujibu wa Shemeji yake, Mchungaji Philip Kayanda, amesema kuwa Laurent alikuwa ametokea Zanzibar na kuelekea Kahama lakini alipofika hapa Dodoma aliteremka na kuelekea nyumbani kwao eneo la Dodoma makulu ambako alitoweka kusikojulikana. Pia  alisema kuwa shemeji yake huyo ana matatizo ya akili.
Laurent ambaye rangi yake ni maji ya kunde amesema kabla ya kujachanganyikiwa akili, alikuwa anafanya kazi ya uchungaji katika kanisa la FPCT huko kijijini kwao Kabare mkoa wa Kigoma ikiwemo na Zanzibar.

Amesema jitihada za kumtafuta kwa ndugu, jamaa na marafiki zimefanyika bila mafanikio na tayari wametoa taarifa kituo cha polisi kati cha Dodoma na kufungua jalada namba RB/DOM/8409/2016.
Ameomba kwa yeyote atakayemuona atoe taarifa katika kituo chochote cha polisi kilichopo karibu ama apige simu namba 0688 - 688229,0788 – 669300 au 0655 – 090820

Serikali kubadili mtaala wa elimu wa darasa la tatu na la nne

$
0
0
Mmoja wa wanafunzi wahitimu wa darasa la saba katika Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, akimuonesha mgeni rasmi wa mahafali ya tano ya shule hiyo, Kaimu Afisa Elimu Wilaya ya Ilala Asha Mapunda (wa pili kushoto) darubini na jinsi inavyofanya kazi. Wanafunzi 65 wa shule hiyo wanatarajiwa kuihtimu elimu ya msingi mwaka huu.
Mkurigenzi Mtendaji wa Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, Machage Kisyeri akiingiza kijiti kilichowashwa moto ndani ya ‘test tube’ kuzalisha hewa ya oksijeni ikiwa ni sehemu ya maonesho ya wahitimu wa shule hiyo wakionesha jinsi ya.Kulia ni mgeni rasmi wa mahafali ya tano ya shule hiyo, Kaimu Afisa Elimu Wilaya ya Ilala Asha Mapunda, akishuhudia.
Kikundi cha kwaya cha Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, wakiimba wimbo kwenye mahafali ya tano ya wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha Skauti cha Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam,kikionesha umahiri katika mchezo wa Karate kwenye mahafali ya tano ya wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


YANGA YAANZA LIGI KWA USHINDI MNONO, YAICHAPA AFRICAN LYON BAO 3-0 LEO

$
0
0
TIMU ya African Lyon leo imeweza kupoteza mchezo wao baada ya kukubali kipigo cha goli 3-0 kutoka kwa Yanga. Huku Kocha mkuu wa Yanga, Mholanzi Hans Van De Pluijm amesema kuwa wachezaji wake wametumia nafasi walizozipata ila mabadiliko ya kipindi cha pili yameweza kubadilisha mfumo wa ushambuliaji.
Pluijm amesifia wachezaji wake kwa kupambana katika dakika zote 90 na kuhakikisha wanapata alama tatu muhimu.
Akitoa tathmini ya mchezo mzima, Pluijm amesema kuwa African Lyon ni moja ya timu nzuri na ina wachezaji wazuri sema kama wataendelea hivyo watakuwa na ushindani wa hali ya juu msimu huu.
Kwa upande wa Kocha mkuu wa African Lyon, Bernado Tevares amesema kuwa wachezaji wake walionesha kujiamini ila walishindwa kuzitumia nafasi walizozipata.
Katika mchezo wa mwanzo dhidi ya Azam, African Lyon  waliweza kutoka sare ya 1-1 huku wakionesha kandanda safi, na amewapongeza pia wachezaji wa Yanga kwa nafasi walizozipata na kuzitumia vizuri.
Katika mchezo mwingine Timu ya Mbeya City imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Toto Africa mechi iliyopigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.
Magoli ya Yanga yamefungwa na Deus Kaseke dakika ya 18, Saimon Msuva dakika ya 60 na Juma Mahadhi dakika ya 90.
 Mshambuliaji wa Timu ya Yanga, Simon Msuva, akiipatia timu yake bao la pili dhidi ya Timu ya African Lyon, katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Yanga imeanza ligi hiyo kwa ushindi mnono wa Mabao 3-0.
 Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma akitafuta namna ya kuwatoka Mabeki wa timy ya African Lyon, katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Yanga imeanza ligi hiyo kwa ushindi mnono wa Mabao 3-0.
 Deus Kaseke wa Yanga, akishangilia baada ya kuipatia timu yake Bao la awali dhidi ya African Lyon, katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Yanga imeanza ligi hiyo kwa ushindi mnono wa Mabao 3-0.
Mshambuliaji wa Timu ya African Lyon, Tito Okello akijaribu kutana kumtoka Kiungo wa Yanga, Thaban Kamusoko, katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. Yanga imeanza ligi hiyo kwa ushindi mnono wa Mabao 3-0.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA RAIS UHURU KENYATTA JIJINI NAIROBI

$
0
0
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta katika Mkutano wa TICAD 6  kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyatta (KICC) jijini Nairobi Agosti 28, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wakuu wa nchi mbalimbali wanaoshiriki katika Mkutano wa TICAD 6 kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Kenyeatta (KICC) jijini Nairobi Agosti 28, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

HEPI BESDEI YA KUZALIWA ANKAL LEO

$
0
0
Ankal akiwa na keki yake aliyozawadiwa na familia yake katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa leo. Anamshukuru Mola kwa kumwezesha kufikisha siku hii adhimu na anaendelea kumuomba amjalie afya njema na baraka tele. Pia anaishukuru familia yake, ndugu, jamaa, marafiki, majirani na wafanyakazi wenzake pamoja na makamanda wa tasnia ya habari kwa salamu za heri walizomtumia.
Wote anawaambia amezipokea salamu hizo kwa kuguswa moyoni na kuwaahidi kuendelea kuwa "mtoto mzuri" na kuendeleza libeneke la Globu ya Jamii ambayo mwezi Ujao Septemba 8 itatimiza miaka 11.
Keki imetengenezwa SWEET HANDS DELIGHT  ya Kawe karibu na Kanisa Katoliki. Namba zao 0713 925071/0714 590165

Ngoma Africa Band yawatia kiwewe wapenzi wa muziki jijini Frankfurt, Ujerumani

$
0
0
Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band maarufu kama FFU-Ughaibuni inayoongozwa na mwanamuziki nguli Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja juzi kati ya jumamosi ya 13 Septemba 2016 ilifanikiwa tena kulitingisha jiji la Frankfurt nchini ujerumani katika maonyesho ya Afrika-Karibik Festival yaliyo fanyika katika viwanja vya Rebstock Park,ambapo bendi hiyo iliwatia kiwewe waudhuriaji wa onyesho hilo.
Bendi hiyo maarufu na mdundo wake "Bongo Dansi" inatajwa kuwa ndio bendi imara ya kiafrika kudumu kwa muda mrefu na kuteka soko la muziki barani ulaya.
 Ngoma Africa band wakishambulia jukwaa jijini Frankfurt
 Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja akiongoza gwaride la FFU Ughaibuni
 Mashabiki wa kila rika na rangi walipata kiwewe kila dakika ngoma zikipigwa
 Palikuwa hapatoshi
Kiongozi wa Ngoma Africa Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja akizongwa na mashabiki baada ya gwaride kali la FFU Ughaibuni jijini Frankfurt 

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI NCHINI SWAZILAND,KUMUWAKILISHA RAIS MKUTANO WA 36 WA SADC

$
0
0

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye ardhi ya mji wa Mbabane nchini Swaziland tayari kuhudhuria mkutano wa 36 wa SADC wa Wakuu wa nchi  na Serikali ambao utafanyika tarehe 29 Agosti mjini hapo.
 Sehemu ya Mabinti wa Swaziland wakiimba na kucheza wakati wa mapokezi ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na ngoma mbali mbali mjini Mbabane nchini Swaziland.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akizungumza na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Phiwayinkhosi Mabuza wa Swaziland ambaye pia ni Kaimu Waziri wa Fedha mara baada ya kuwasili kwenye kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mfalme Mswati III.
                              -------------------------------------------------------
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Mbabane - Swaziland leo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 36 wa Wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika- SADC.  
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano huo ambao utafanyika tarehe 29 Agosti  2016 ambapo Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya hiyo.
Mkutano huo wa 36 wa SADC ni maalum kwa wakuu wa nchi na serikali wanaounda Kamati ya siasa,ulinzi na usalama ambao watajadili kwa kina hali ya siasa na usalama, demokrasia na maombi ya Burundi na Comoro kwa ajili ya kujiunga na SADC.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika  msafara wake amefuatana na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa Augustine Mahiga, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Amina Salum Ali.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI 
Viewing all 109992 articles
Browse latest View live




Latest Images