Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110016 articles
Browse latest View live

MWANDISHI WA HABARI MARY LYIMO KUZIKWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
Mwandishi wa Habari,Mary Jovian Lyimo amefariki dunia Agosti 23 baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa Kansa ya Ini, kwa mujibu wa Dada wa marehemu, Liliani Jovian Lyimo amesema kuwa marehemu enzi za uhai wake aliwahi kufanya kazi katika Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASCO), kama Ofisa habari wa shirika hilo, pia alifanya kazi katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).


Marehemu atazikwa leo Agosti 27 saa nane katika makaburi ya Kondo Kunduchi jijini Dar es Salaam. Mungu ailaze roho ya marehemu  mahali pema peponi amani.
 

Walimu Wilayani Serengeti wapewa mafunzo kupitia vishkwambi

$
0
0
Walimu wakuu 109 kutoka shule za msingi Wilayani Serengeti wamewezeshwa mafunzo ya utumiaji wa mfumo wa taarifa za shule (School Information System - S.I.S) kwa kutumia vishikwambi (Tablet).

Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofadhiliwa kupitia programu ya EQUIP Tanzania yalianza tarehe 25 Agosti na kukamilika 26 Agosti 2016 katika shule ya Msingi Kambarage iliyopo katika Mji wa Mugumu yamewawezesha walimu hao pia kupatiwa kishikwambi kwa kila mmoja.

Akizungumza kuhusu mafunzo hayo, Mwezeshaji kitaifa wa Mfumo wa School Information System Bw. Victor Mkama alisema "Mafunzo hayo ni muhimu kwa walimu ili kuweza kutumia vishikwambi hivyo bila matatizo na kuwajengea uelewa wa umuhimu wa kutuma taarifa kwa kutumia njia ya mtandao".

Mwezeshaji aliendelea kwa kusema kuwa "wametoa vishikwambi 109 kwa walimu wakuu wote wa shule za msingi wilayani serengeti vyenye thamani ya Milioni 38.1 ili kuweza kutuma taarifa muhimu zinazohusu shule waliyopo moja kwa moja TAMISEMI".

Vishikwambi hivyo vitatumika katika ukusanyaji wa taarifa muhimu zikiwemo idadi ya walimu, wanafunzi, madarasa, madawati, matundu ya vyoo pamoja na nyumba za walimu na rasilimali zinazopatina katika maeneo ya shule na kutumwa moja kwa moja TAMISEMI hivyo kupunguza usumbufu wa upatikanaji wa taarifa uliokuwa ukiipata Serikali.
Mwezeshaji Kitaifa wa Mfuno wa SIS (School Information System), Deusdedit Martin akiwaelekeza baadhi ya Walimu shule za msingi Wilayani Serengeti namna ya kutumia Mfumo huo, kwa kutumia tablet.
Baadhi ya Walimu hao wakiendelea kujifunza Mfumo wa SIS.
Walimu wakielekezana namna ya kuutumia mfumo huo.

WAZIRI MKUU,MAJALIWA AKUTANA NA OFISA MTENDAJI MKUU WA GLOBAL FUND.

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Global Fund, Mark Dybul  (kulia  kwake)  kwenye hoteli ya Windsor Agosti 26,2016.Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mathias Chikawe.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Global Fund, Mark Dybul    kwenye hoteli ya Windsor Agosti 26,2016.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Global Fund, Mark Dybul   kabla ya mazungumzo yao kwenye hoteli ya Windsor jijini Nairobi, Agosti 26,2016.
 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

TANZANIA IPO TAYARI KUJIFUNZA KWA NCHI NYINGINE-MAJALIWA.

$
0
0



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko tayari kujifunza kutoka kwa nchi nyingine ambazo ni wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) ili iweze kuboresha hatua ilizofikia kwenye mpango huo.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Ijumaa, Agosti 26, 2016) wakati akichangia mada katika Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM Forum) uliofanyika kwenye hoteli ya InterContinental jijini Nairobi, Kenya.

“Nitumie fursa hii kukiarifu kikao chako kwamba Tanzania imeshaanza kutekeleza mpango kazi wa Kitaifa ambao umejikita kutatua changamoto katika sekta za maji, elimu, kilimo, nishati na miundombinu kama zilivyoainishwa kwenye kikao cha APRM,” alisema.

“Ili kuhakikisha kuwa zinafanyiwa kazi haraka, changamoto hizi za kisekta zimepewa kipaumbele kwenye Mpango wetu wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano wa 2016-2021 ambao umejikita zaidi kwenye viwanda,” aliongeza.

Tanzania ilifanyiwa tathmini yake Januari, 2013 kwenye kikao cha Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa, Ethiopia.

Mapema, akifungua mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema viongozi wa Afrika hawana budi kukubaliana na kuungana kutafuta suluhisho katika ushindani wa kibiashara.

Alisema nchi wanachama wa mpango huo hawana budi kujenga umoja kama njia ya muafaka ya kufikia makubaliano hayo.

Wakati huohuo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema bara la Afrika linakabiliwa na changamoto 11 (strategic bottlenecks) ambazo zinakwamisha maendeleo ya bara hilo na akataka zitafutiwe ufumbuzi ili kuzisaidia nchi nyingi barani humo.  

Akiwasilisha mada binafsi katika mkutano huo, Rais Museveni alisema kwa zaidi ya miaka 50, amekuwa kiongozi katika sehemu kadhaa na kwamba amebaini kuwa changamoto hizo zimezuia ukuaji wa uchumi barani Afrika pamoja na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
Alisema asilimia kubwa ya changamoto hizo haikupata ufumbuzi hata wakati malengo ya maendeleo ya milenia (MDGs) yalipokuwa yanatekelezwa.

Alizitaja changamoto hizo kuwa ni mikanganyiko ya kiitikadi ambayo huzaa ubinafsi na maslahi binafsi; kuwepo kwa mataifa dhaifu (weak states); nguvukazi duni (kitaaluma na kiafya), uduni wa miundombinu (barabara, maji, umeme, tehama) ambao unashindwa kuvutia uwekezaji; uhaba wa viwanda unaolazimisha nchi kusafirisha mali ghafi na uhaba wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa barani Afrika.

Changamoto nyingine ni uduni wa huduma za kijamii unaosababisha huduma mbovu kwenye maeneo ya utalii, mabenki na mahoteli; kilimo duni kisichotumia mbolea, dawa za kuua wadudu, mbegu za kisasa au njia za umwagiliaji; makosa ya kisera kama vile ubinafishaji au utaifishaji mali zinazomilikiwa na sekta binafsi; ukandamijazi wa demokrasia na ukosefu wa maadili miongoni mwa watumishi wa umma.

Naye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alisema kwa vile changamoto hizo zinagusa nchi nyingi za Afrika, ni vema iundwe timu ya wataalamu watakazipitia zote na kuainisha zipi zinafaa kufanyiwa kazi na kisha taarifa yao iwasilishwe kwenye kikao kijacho cha Wakuu wa Nchi wanachama.

Akifunga mkutano huo, Rais Kenyatta aliitaka sekretarieti ya APRM ipitie changaoto hizo na kuziwakilisha kwenye kikao chao kijacho ambacho alisema kitafanyika Januari 2017, mjini Addis Ababa, Ethiopia katika tarehe itakayopangwa baadaye. 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, AGOSTI 27, 2016.

WAFANYAKAZI WA NMB TAWI LA NELSON MANDELA WASHIRIKI ZOEZI LA USAFI MJINI MOSHI LEO

$
0
0
Wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi wakiwa wamebeba vifaa kwa ajili ya kufanya usafi katika eneo la njia mbili maarufu kama Double Road mjini Moshi leo.
Meneja wa NMB tawi la Neslon Mandela Emanuel Kishosha akiwa amebeba taka mara baada ya kumaliza kuzikusanya wakati wa zoezi hilo la usafi.

MKUTANO WA MAWAZIRI WA TICAD WAFANYIKA JIJINI NAIROBI.

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye kikao cha Mawaziri wa Mkutano wa Sita wa Kimataifa kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo kati ya Japan na Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD VI) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) tarehe 26 Agosti, 2016. Kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Khalid Salum Mohammed na kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Amina Mohammed akizungumza wakati wa Mkutano huo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Fumio Kishida nae akizungumza wakati wa mkutano wa Mawaziri
Sehemu ya Wajumbe waliohudhuria mkutano huo.
Picha ya pamoja ya meza kuu.

Kikao cha Mawaziri kuandaa Mkutano wa Kilele wa Sita wa Kimataifa kuhusu Ushirikiano wa Maendeleo kati ya Japan na Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD VI) kimemalizika Jijini Nairobi leo ambapo Mawaziri hao wameikubali kwa kauli moja Rasimu ya Azimio la Nairobi na Mpango Kazi wake tayari kwa kuwasilishwa kwa Wakuu wa Nchi na Serikali kwa ajili ya kupitishwa.


                                                KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

MSAADA TUTANI WADAU

$
0
0
I wish to become a Doctor…Can You walk with me please ?
Dar es Salaam, 26th August 2016
His name is Festus, 12-year old and in class six, coming from Kilombero District in Morogoro, Tanzania. He came to Muhimbili Referral Hospital in Dar es Salaam for treatment and was diagnosed with a hip cancer which necessitated an amputation. On the operation day, he lost his father of stroke as he was preparing to go and be with his son before he goes to the theatre.

“He is healing very well”, a caring nurse Sussane who has been with him since his arrival commented this morning. His mother said that he performs very well in school, first and second position tops since grade one. She fears that the passing of his father and his amputation may impede him for continuing with school.

I asked Festus “what would you like to be when you finish studies?” He answered, “a doctor”. I was surprised of his answer considering a painful journey at a young age he had just gone through. All I could then say to him was “Festus, you will finish your studies, you will become a doctor. You do not have a leg but I know some people out there will walk with you”

I lost my sister 16 years ago this day of cancer, memories of her still very fresh in my mind and heart. I don’t wish to see this young boy lose his dream because of this misfortune. He needs TZS 250,000/- for a wheel chair. Let us be his parent and his leg and see this boy pursue his dream. It is not the end of his life and so should not be the end of his dream. Who knows, maybe as a doctor he could find a cure for Cancer!!

THANKING YOU FOR YOUR KINDNESS:

Mother’s Number:+255 (0) 788 886399
Nurse Sussane’s Number: +255 (0) 713 405068
Nurse Sussane is collecting for the wheelchair. By austin m. makani

OFFICAL LAUNCH AND WORLD PREMIERE SCREENING OF MUSIC VIDEOS at NAFASI ART SPACE


WANAFUNZI 20 KUSOMEA MAFUTA NA GESI A.SILIA CHINA

$
0
0
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa tano kulia), Naibu Balozi wa China Gou Haodong (wa sita kulia) pamoja na wanafunzi waliopata ufadhili kwa ajili ya kusomea fani ya mafuta na gesi asilia katika chuo cha GeoScience (Wuhan).
 Naibu Balozi wa China Gou Haodong (anayezungumza), Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mbele), wakiwa pomoja na wanafunzi waliopata ufadhili pamoja na waandishi wa habari katika kikao hicho kilichofanyika katika ofisi ya Wizara makao makuu jijini Dar es salaam cha kuwaaga wanafunzi hao.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na mwanafunzi aliyewakilisha wezake, Mkini Raphael Iddphonce akiwapongeza wanafunzi waliopata fursa hiyo ya kusomea mafuta na gesi asilia nchini china.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na mwanafunzi aliyewakilisha wezake kwa upande wa wanawake, Salmin Yusra akiongea kwa niaba ya wezake na kuishukuru serikali kwa fursa ya kusomea mafuta na gesi asilia nchini china.


Na Rhoda James

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliwakabidhi Nyaraka za masomo na kuwaaga wanafunzi 18 kati ya wanafunzi 20 mwishoni mwa wiki wanaotarajia kwenda kusomea Shahada ya Uzamivu na ya Uzamili ya Mafuta na Gesi Asilia nchini China.


Profesa Muhongo alisema kuwa, Udhamini huo umetolewa na Serikali ya China na Tanzania, na kuongeza kuwa udhamini huo umekuwa ukitolewa kwa miaka mingi kwa upande wa fani ya Mafuta na Gesi Asilia.


“Udhamini ulianza mwaka 2013-2014 ambapo wanafunzi 10 walipata udhamini huo, mwaka 2014-2015 wanafunzi 10 walipata udhamini, mwaka 2015-2016 wanafunzi 22 walipata na mwaka huu 2016-2017 wanafunzi 20 wamepata udhamini kati ya hao wanafunzi 2 tayari wapo China, ambapo kwa ujumla wanafunzi 62 wameshapata udhamini huo,” alisema Profesa Muhongo.


Profesa Muhongo alisema kuwa wanafunzi hao wameteuliwa kwenda kusoma katika chuo cha China Univesity of Geoscience (Wuhan) na wanatoka mikoa mbalimbali nchini.


“Wanafunzi tunaowachukua sio wa upande wa Mafuta na Gesi asilia tu bali ni wa nyanja mbali mbali ikiwa ni pamoja na Sheria na Fedha,” amesema Profesa Muhongo.


Aidha, alieleza kuwa, Serikali imekuwa ikitoa kipaumbele kwa wanafunzi wa kike kusoma masuala ya mafuta na gesi asilia na mwaka huu, wanafunzi 10 wa kwanza, wa kike waliopata ufadhili kusomea mafuta na Gesi asilia watasomea Shahada ya Uzamili katika chuo cha ‘Geoscience (Wuhan).’


“Nendeni msome kwa bidii bila kujishughulisha na biashara yoyote, kwa kuwa nchi ya Tanzania bado inahitaji wataalamu wa fani ya Mafuta na Gesi asilia,” alisisitiza Profesa Muhongo.


Kwa upande wake Naibu Balozi wa China, Gou Haodong alimshukuru Profesa Muhongo kwa kujali na kuifanya kazi yake kwa ufanisi na kusaidia upatikanaji wa nafasi kwa ajili ya wanafunzi wa Tanzania kwenda kusomea masuala ya Mafuta na Gesi Asilia nje ya nchi.


“Profesa Muhongo amekuwa katika mstari wa mbele katika kutafuta vyuo na ufadhili kwa ajili ya wanafunzi wa Tanzania, hii inaonesha anaipenda kazi yake na anaifanya kwa ufanisi mkubwa,” alisema Naibu Balozi wa China Gou Haodong

Mafundi wa TEMESA washauriwa kutumia mafunzo waliyoyapata kuendana na mabadiliko ya teknolojia

$
0
0
Mafundi wa TEMESA wameshauriwa kutumia mafunzo waliyoyapata kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika utengenezaji magari na vifaa vya umeme.

Ushauri huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mjumbe wa Bodi ya Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi Wakala hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).

Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri amesema kuwa Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA imedhamiria na kuhakikisha kuwa magari na mitambo yote ya Serikali inatengenezwa kitaalam ili kuleta tija na thamani halisi ya fedha iliyokusudiwa pamoja na kukidhi kiu na matarajio ya wateja.

”Napenda kuwakumbusha kwamba mnayo dhamana kubwa ya kutengeneza magari ya Serikali hivyo kwa mafunzo mliyoyapata ninaamini mmejenga uwezo wa kutosha wa kuhudumia magari na vifaa vya umeme kwa kutumia mfumo wa kisasa” alisema Mhandisi Mashauri.

Ameongeza kuwa ni fursa pekee kwa mafundi waliopata mafunzo hayo kwenda kuwafundisha wenzao ambao hawakuweza kupata mafunzo hayo ili kuongeza kasi ya kutengenza magari na vifaa vya umeme na kupunguza changamoto zilizopo katika utengenezaji magari kwa kutumia mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Aidha Kaimu Mtendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mhandisi Manase Ole Kujan amewashukuru washirika wa TEMESA wakiwemo Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na kampuni ya Superdoll kwa kuwezesha kufanyika kwa mafunzo hayo ambayo yataleta chachu ya utendaji kazi wa mafundi na karakana za TEMESA zilizopo nchini nzima.

Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA kwa kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) na kampuni ya Superdoll waliandaa mafunzo ya siku 14  yaliyoanza Agosti 9 na kumalizika Agosti 26, 2016 yaliyoshirikisha jumla ya mafundi 25 kutoka mikoa mbalimbali ili kuwapa uwezo wa kutengeneza magari kwa kutumia mifumo ya kisasa.
Kaimu Mtendaji TEMESA Mhandisi Manase Ole Kujan(kulia) akitoa neno kwa mafundi wa TEMESA wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016 kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri .
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akionesha moja ya vifaa vilivyokabidhiwa na mafundi wa TEMESA kwa ajili ya karakana zao wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016.
Mjumbe wa Bodi ya TEMESA Brigedia Jenerali Msataafu Mhandisi Mabula Mashauri akikabidhi cheti kwa mmoja wa mafundi Bw.Saidi Waziri kutoka Arusha wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo kwa mafundi hao iliyofanyika katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Agosti 26,2016. 

TANZANIA IKO TAYARI KUJIFUNZA KUTOKA NCHI NYINGINE.

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko tayari kujifunza kutoka kwa nchi nyingine ambazo ni wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) ili iweze kuboresha hatua ilizofikia kwenye mpango huo.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Ijumaa, Agosti 26, 2016) wakati akichangia mada katika Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM Forum) uliofanyika kwenye hoteli ya InterContinental jijini Nairobi, Kenya.

“Nitumie fursa hii kukiarifu kikao chako kwamba Tanzania imeshaanza kutekeleza mpango kazi wa Kitaifa ambao umejikita kutatua changamoto katika sekta za maji, elimu, kilimo, nishati na miundombinu kama zilivyoainishwa kwenye kikao cha APRM,” alisema.

“Ili kuhakikisha kuwa zinafanyiwa kazi haraka, changamoto hizi za kisekta zimepewa kipaumbele kwenye Mpango wetu wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano wa 2016-2021 ambao umejikita zaidi kwenye viwanda,” aliongeza.

Tanzania ilifanyiwa tathmini yake Januari, 2013 kwenye kikao cha Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa, Ethiopia.

Mapema, akifungua mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema viongozi wa Afrika hawana budi kukubaliana na kuungana kutafuta suluhisho katika ushindani wa kibiashara.

Alisema nchi wanachama wa mpango huo hawana budi kujenga umoja kama njia ya muafaka ya kufikia makubaliano hayo.

Wakati huohuo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema bara la Afrika linakabiliwa na changamoto 11 (strategic bottlenecks) ambazo zinakwamisha maendeleo ya bara hilo na akataka zitafutiwe ufumbuzi ili kuzisaidia nchi nyingi barani humo.  

Akiwasilisha mada binafsi katika mkutano huo, Rais Museveni alisema kwa zaidi ya miaka 50, amekuwa kiongozi katika sehemu kadhaa na kwamba amebaini kuwa changamoto hizo zimezuia ukuaji wa uchumi barani Afrika pamoja na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
Alisema asilimia kubwa ya changamoto hizo haikupata ufumbuzi hata wakati malengo ya maendeleo ya milenia (MDGs) yalipokuwa yanatekelezwa.

Alizitaja changamoto hizo kuwa ni mikanganyiko ya kiitikadi ambayo huzaa ubinafsi na maslahi binafsi; kuwepo kwa mataifa dhaifu (weak states); nguvukazi duni (kitaaluma na kiafya), uduni wa miundombinu (barabara, maji, umeme, tehama) ambao unashindwa kuvutia uwekezaji; uhaba wa viwanda unaolazimisha nchi kusafirisha mali ghafi na uhaba wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa barani Afrika.

Changamoto nyingine ni uduni wa huduma za kijamii unaosababisha huduma mbovu kwenye maeneo ya utalii, mabenki na mahoteli; kilimo duni kisichotumia mbolea, dawa za kuua wadudu, mbegu za kisasa au njia za umwagiliaji; makosa ya kisera kama vile ubinafishaji au utaifishaji mali zinazomilikiwa na sekta binafsi; ukandamijazi wa demokrasia na ukosefu wa maadili miongoni mwa watumishi wa umma.

Naye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alisema kwa vile changamoto hizo zinagusa nchi nyingi za Afrika, ni vema iundwe timu ya wataalamu watakazipitia zote na kuainisha zipi zinafaa kufanyiwa kazi na kisha taarifa yao iwasilishwe kwenye kikao kijacho cha Wakuu wa Nchi wanachama.

Akifunga mkutano huo, Rais Kenyatta aliitaka sekretarieti ya APRM ipitie changaoto hizo na kuziwakilisha kwenye kikao chao kijacho ambacho alisema kitafanyika Januari 2017, mjini Addis Ababa, Ethiopia katika tarehe itakayopangwa baadaye.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ASHIKIRI MKUTANO WA APRM NAIROBI

$
0
0



  Waziri Mkuu wa Japan ,Shinzo Abe akizungumza katika mkutano wa Sita wa TICAD kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa  cha Jomo Kenyatta jijini Nairobi  Agosti  27, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Sita wa TICAD wakishiriki katika mkutano huo kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa  cha Jomo Kenyatta jijini Nairobi Agosti  27, 2016.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiw katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wakuu wa Nchi na serikali kwenye Kituo cha Mikutano cha  Mikutano cha Jomo Kenyatta jijini  Nairobi  Agosti  27, 2016.


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko tayari kujifunza kutoka kwa nchi nyingine ambazo ni wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) ili iweze kuboresha hatua ilizofikia kwenye mpango huo.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Ijumaa, Agosti 26, 2016) wakati akichangia mada katika Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM Forum) uliofanyika kwenye hoteli ya InterContinental jijini Nairobi, Kenya.

“Nitumie fursa hii kukiarifu kikao chako kwamba Tanzania imeshaanza kutekeleza mpango kazi wa Kitaifa ambao umejikita kutatua changamoto katika sekta za maji, elimu, kilimo, nishati na miundombinu kama zilivyoainishwa kwenye kikao cha APRM,” alisema.

“Ili kuhakikisha kuwa zinafanyiwa kazi haraka, changamoto hizi za kisekta zimepewa kipaumbele kwenye Mpango wetu wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano wa 2016-2021 ambao umejikita zaidi kwenye viwanda,” aliongeza. 

Tanzania ilifanyiwa tathmini yake Januari, 2013 kwenye kikao cha Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa, Ethiopia.Mapema, akifungua mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema viongozi wa Afrika hawana budi kukubaliana na kuungana kutafuta suluhisho katika ushindani wa kibiashara.

Alisema nchi wanachama wa mpango huo hawana budi kujenga umoja kama njia ya muafaka ya kufikia makubaliano hayo.Wakati huohuo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema bara la Afrika linakabiliwa na changamoto 11 (strategic bottlenecks) ambazo zinakwamisha maendeleo ya bara hilo na akataka zitafutiwe ufumbuzi ili kuzisaidia nchi nyingi barani humo. 

Akiwasilisha mada binafsi katika mkutano huo, Rais Museveni alisema kwa zaidi ya miaka 50, amekuwa kiongozi katika sehemu kadhaa na kwamba amebaini kuwa changamoto hizo zimezuia ukuaji wa uchumi barani Afrika pamoja na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.Alisema asilimia kubwa ya changamoto hizo haikupata ufumbuzi hata wakati malengo ya maendeleo ya milenia (MDGs) yalipokuwa yanatekelezwa.

Alizitaja changamoto hizo kuwa ni mikanganyiko ya kiitikadi ambayo huzaa ubinafsi na maslahi binafsi; kuwepo kwa mataifa dhaifu (weak states); nguvukazi duni (kitaaluma na kiafya), uduni wa miundombinu (barabara, maji, umeme, tehama) ambao unashindwa kuvutia uwekezaji; uhaba wa viwanda unaolazimisha nchi kusafirisha mali ghafi na uhaba wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa barani Afrika.

Changamoto nyingine ni uduni wa huduma za kijamii unaosababisha huduma mbovu kwenye maeneo ya utalii, mabenki na mahoteli; kilimo duni kisichotumia mbolea, dawa za kuua wadudu, mbegu za kisasa au njia za umwagiliaji; makosa ya kisera kama vile ubinafishaji au utaifishaji mali zinazomilikiwa na sekta binafsi; ukandamijazi wa demokrasia na ukosefu wa maadili miongoni mwa watumishi wa umma. 

Naye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alisema kwa vile changamoto hizo zinagusa nchi nyingi za Afrika, ni vema iundwe timu ya wataalamu watakazipitia zote na kuainisha zipi zinafaa kufanyiwa kazi na kisha taarifa yao iwasilishwe kwenye kikao kijacho cha Wakuu wa Nchi wanachama.

Akifunga mkutano huo, Rais Kenyatta aliitaka sekretarieti ya APRM ipitie changaoto hizo na kuziwakilisha kwenye kikao chao kijacho ambacho alisema kitafanyika Januari 2017, mjini Addis Ababa, Ethiopia katika tarehe itakayopangwa baadaye.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, AGOSTI 27, 2016.

MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA AMSIMAMISHA KAZI AFISA MAENDELEO YA JAMII WA JIJI KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE

$
0
0

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Ndg. Athumani J. Kihamia amempuzisha kutekeleza majukumu yake Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji Bi. Mwantumu Dosi kwa tuhuma za kushindwa kutekeleza majukumu yake hivyo kukiuka kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003.

Mkurugenzi Kihamia ametoa taarifa hiyo leo tarehe 27.08.2016 baada ya kukamilisha mbio za Mwenge wa Uhuru na kufanya tathmini ya miradi iliyopitiwa na Mwenge na kugundulika kwa dosari zilizojitokeza katika moja ya mradi ambao uko chini ya Idara hii.

Mradi huo ni kikundi cha vijana wanaojishughulisha na Uselemara pamoja na Uchomeleaji kinachojulikana kama Mbeshere Umoja Group kilichopo Kata ya Olorieni kiligundulika kuwa na wananchama waliovuka umri wa miaka 35 ambao hawastahili kunufaika  na Mikopo ya Vijana kwa mujibu wa Sera.

Mwenge wa Uhuru katika Jiji la Arusha ulikimbizwa tarehe 24.08.2016 na Kikundi hicho kilikua ni miongoni mwa miradi iliyokua inapitiwa na Mwenge wa Uhuru ambapo wanachama wake hawakizi vigezo. Wanachama hao walikua wameandaliwa kupewa Hundi ya TSH Milioni tano kama ishara ya kuunga mkono jitihada zao zakuboresha maisha.  Mkimbiza Mbio za Mwenge Kitaifa Ndg. George Jackson Mbijima alisitisha zoezi hilo baada ya kugundua dosari za umri kwa baadhi ya wanachama.

Kupumzishwa kutekeleza majukumu ya Mkuu wa Idara hii kunafuatana na masharti ya kukabidhi Ofisi kwa Mratibu wa Tasaf Bi. Tajiel Mahega ambaye kwa sasa atakua Kaimu Mkuu  wa Idara  hii mpaka pale uchunguzi utakapokamilika.

Nteghenjwa Hosseah
Afisa Habari, Halmashauri ya Jiji
Arusha.
27  Agosti,2016 


SIMBA YAVUTWA SHATI NA JKT RUVU TAIFA LEO, ZATOKA SARE YA BILA KUFUNGANA

$
0
0
KOCHA msaidizi wa Simba Jackson Mayanja amesema kuwa kikosi chake kilicheza vizuri sema mapungufu katika safu ya ushambuliaji yameinyima ushindi timu yake.

Simba imelazimishwa suluhu ya kutokufungana na JKT Ruvu katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mayanja amesema kuwa bado wanajipanga kuweza kuhakikisha wanashinda kwenye michezo yao inayofuata.

Katika mchezo wa awali Simba walitoka na ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Ndanda na baada ya matokeo haya wanasalia na alama nne huku kwenye michezo mingine Azam amefanikiwa kushinda 3-0 dhidi ya Majimaji ya Songea mchezo ulipigwa uwanja wa Chamazi.

Mtibwa Sugar nayo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Ndanda huku Mwadui Fc wakitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0, huko Mkoani Mbeya Tanzania Prisons imetoka sare ya bao 1-1 na Ruvu Shooting, wakati huko Kaitaba Mjini Bukoba, Kagera naye kashindwa kutamba uwanja wa Nyumbani kwa kutoka suluhu ya bila kufungana na Stand United.

Mtibwa Sugar nayo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 2-1 dhidi ya Ndanda huku Mwadui Fc wakitoka kifua mbele kwa ushindi wa goli 1-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Jamal Mnyate akitafuta mbinu ya kumtoka Beki wa timu ya JKT RUVU, Rahim Juma, ikiwa ni muendelezo michezo ya Ligi kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam. hadi mwamuzi wa mchezo huo, Selemani Kinugani anapiliza kipenga cha kuashiria kumalizika kwa mchezo huo, hakuna timu hata moja iliyoliona lango la mwenzake (0-0) na kuzifanya timu hizo kugawana point moja moja.

Mshambuliaji wa Timu ya Simba, Fredrick Blagnon akiondoka na mpira mbele ya kiungo wa Timu ya JKT RUVU, Michael Aidan, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.Mchezo huo umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana.
Mshambuliaji wa Timu ya JKT RUVU, Saady Kipanga akiruka juubaada ya Mlinda mlango wa Timu ya Simba, Vincent Angban alipoutokea mpira huo.

WAKURUGENZI WATANO TPDC WASIMAMISHWA KAZI KUPISHA UCHUNGUZI


WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA YAELEKEZA NGUVU YA UFUNDISHAJI MTAALA WA KKK.

$
0
0


Na Chalila Kibuda. Globu ya Jamii.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imewajengea uwezo wathibiti ubora wa shule 1,469 ili wapate umahiri wa kusimamia kwa ufanisi ufundishaji na ujifunzaji bora unaozingatia umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK).

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya uthibiti ubora wa shule nchini, Marystella Wasena alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mikakati ya Idara hiyo katika kukagua na kusimamia utekelezaji wa ufundishaji wa kusoma , kuandika na kuhesabu katika shule za awali na msingi nchini.

“Kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016 Idara ilifanya tathmini ya mafanikio ya utekelezaji wa mtaala ambapo shule za Msingi 6,831 zilikaguliwa na ilibainika kuwepo kwa wanafunzi 10,273 (wakiume 5,010 na wakike 5,263) wasiojua kusoma wala kuandika katika shule za Msingi 515,” alifafanua Wasena.

Marystella amesema tathmini hiyo imebainisha sababu zinazotokana na wanafunzi wenyewe kushindwa kumudu kujifunza kwa umahiri husika na sababu zinazotokana na utekelezaji wa mtaala ikiwemo ukosefu wa walimu wa kufundisha KKK.

Amesema ili kuondokana na tatizo la wanafunzi kutojua kusoma na kuandika, kila kanda na kila wilaya zimeteua shule mbili za mfano zikiwemo za Serikali na Binafsi ili kuhakikisha wathibiti ubora wa shule wanafanya ufuatiliaji wa KKK katika shule hizo kwa kutoa msaada wa kitaalamu kwa walimu kuhusiana na changamoto za ufundishaji na ujifunzaji mahiri wa KKK.

Aidha Marystella amefafanua kuwa, Idara kupitia mpango wa LANES imeongeza idadi ya magari katika wilaya 38 yatakayotumika kwa ajili ya ukaguzi wa shule za awali, Msingi na Sekondari ambapo idara hiyo imepanga kukagua shule 8426 za awali na Msingi na Sekondari shule 2392 ili kuona utekelezaji wa KKK pamoja na kutoa msaada kwa walimu kufundisha kwa ufasaha kulingana na malengo ya Mtaala husika.

Hata hivyo Idara hiyo ina mkakati wa kufanya tafiti mbalimbali katika shule za Awali, Msingi na Sekondari kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuona utekelezaji wa Mtaala wa KKK na kutoa mapendekezo sahihi ya kuondoa changamoto na kutoa ushauri kwa Walimu, Wakuu wa Shule, Maafisa Elimu, wamiliki wa Shule, Kamishna wa Elimu na Wadau wa Elimu.

Warembo wanaowania taji la Miss Ilala 2016 wachuana vikali katika kutafuta mrembo mwenye kipaji

$
0
0
 Warembo 15 wanaowania taji la Miss Ilala 2016, usiku wa kuamkia leo walichuana vikali katika kutafuta mrembo mwenye kipaji ambapo warembo wote walishindana kwa kuonesha vipaji vyao vya ubunifu, uchezaji muziki na uimbaji wa nyimbo mbalimbali.
 Washiriki mbalimbali wakionesha ujuzi wao kulingana na vipaji walivyo jaaliwa.
 Washiriki mbalimbali wakionesha ujuzi wao kulingana na vipaji walivyo jaaliwa.
 mashabiki wakishangilia

 Hii ndio tano bora ya Warembo wenye Vijapaji kutoka Miss Ilala 2016.

RAIS DKT MAGUFULI AHUDHURIA MISA YA JUBILEI YA DHAHABU (MIAKA 50) YA NDOA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA NA ANNA MKAPA

$
0
0
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa leo tarehe 27 Agosti, 2016 ameadhimisha Jubilei ya Dhahabu ya Miaka 50 ya Ndoa yake na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya Jubilei hiyo imefanyika nyakati za mchana katika ukumbi wa Kardinali Rugambwa uliopo kando ya kanisa la Mtakatifu Petro-Oysterbay na imetanguliwa na Misa ya shukrani iliyofanyika katika kanisa hilo majira ya asubuhi.

Jubilei hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Sita wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume, Mke wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere, Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Cleopa Msuya, Dkt. Salim Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba na Mhe. Edward Lowassa.

Misa Takatifu ya Shukrani imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha Mhashamu Askofu Josephat Lebulu na kuhudhuriwa na Maaskofu na Maaskofu Wakuu saba akiwemo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.


Akizungumza baada ya kumalizika kwa Misa Takatifu Rais Magufuli amempongeza Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kwa kutimiza miaka 50 ya ndoa na ameeleza kuwa ndoa hiyo iliyowaunganisha wanandoa wanaotoka katika madhehebu tofauti ya Kikristo imetoa fundisho kubwa kuwa binadamu wanapaswa kuwa wamoja hata kama wana tofauti mbalimbali zikiwemo za kimadhehebu ya dini, siasa na kanda.


Rais Magufuli amesema miaka 50 ya ndoa ya Mhe. Benjamin William Mkapa ambaye ni Muumini wa Kanisa Katoliki na Mkewe Mama Anna Mkapa ambaye ni Muumini wa Kanisa la Kilutheri inawafundisha watanzania wote hususani wanasiasa kuishi kwa upendo na kuilinda amani waliyonayo na ametoa wito kwa viongozi dini kuendeleza juhudi zao za kuliombea taifa na kuwaunganisha wananchi licha ya tofauti walizo nazo.

Kwa upande wake Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa pamoja na kuwashukuru Viongozi wote, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria Misa ya Shukrani na Jubilei hiyo ya miaka 50 ya ndoa yake amemshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuijaalia ndoa yake umri mrefu.

Rais Mstaafu Mkapa pia ametoa wito kwa watanzania kupenda na kushirikiana huku akibainisha mafunzo aliyoyapata kutoka kwa viongozi wa dini kuwa "Kila mmoja ni zawadi kwa mwenzake"

Nae Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amempongeza Rais Mstaafu Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa kwa kuadhimisha miaka 50 ya ndoa na amewasihi watanzania kuiga mfano mwema uliooneshwa na wana ndoa hao ambao wamedumu katika imani bila kuyumba.


Kardinali Pengo amesema ndoa ya Rais Mstaafu Mkapa anaifundisha jamii kuwa tunaweza kuishi kwa imani zetu bila kubadili dini.

LO3
Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro  Fr. Stephano Kaombwe akiongoza Ibada ya ukumbusho wa ahadi za ndoa wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
LO4
Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa wakipokea hati maalumu kutoka kwa Baba Mtakatifu  Francis  toka kwa   Askofu  Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo  wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
LO5
Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa akitoa shukurani  wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu ya ndoa yake na  na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
LO6
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akitoa salamu zake za pongezi  wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
LO7
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja viongozi wa dini na viongozi wastaafu na wake zao  wakati wa Misa ya Jubilei ya Dhahabu ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016
LO8
LO9
Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakikata keki  katika hafla ya chakula cha mchana waliyoandaa baada ya Misa ya Jubilei ya Dhahabu ya ndoa yao  katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016. 
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

SIKINDE NGOMA YA UKAE, COCODO NA THE SPIRITS BAND WATOA BURUDANI SAFI KATIKA TAMASHA LA WAZI LA MUZIKI JIJINI DAR

$
0
0
 Wanamuziki wa Bendi ya Sikinde Ngoma ya Ukae, wakiyarudi magoma katika Tamasha la wazi la Muziki lililofanyika kwenye Viwanja vya NAFASI, Mikocheni jijini Dar es salaam Agosti 27, 2016. Tamasha hilo ni muendelezo wa matamasha ya kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi katika eneo hilo, huku hilo likiwa na upekee, kwani lilihusisha uzinduzi wa Nyimbo mpya mbali mbali za Bendi tatu tofauti ambazo ni Sikinde wenyewe, Cocodo pamoja na The Spirits kutoka Bagamoyo Mkoani Pwani. Ilikuwa ni burudani ya aina yake yenye kuvutia wengi waliofika kwenye eneo hilo maarufu kwa kazi mbali mbali za Sanaa.

 Mdomo wa Bata ukipulizwa kwa ustadi wa hali ya juu na Mkongwe huyu wa Bendi ya Sikinde.
Wanamuziki wa Bendi ya The Spirits kutoka Bagamoyo Mkoani Pwani wakifanya yao jukwaani.

JWTZ YAKABIDHI VIKOMBE KWA MKUU WA MAJESHI

$
0
0
Na Luteni Selemani Semunyu JWTZ .

Timu teule za Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania zilizowakilisha nchi katika mashindano ya majeshi kwa nchi za Afrika Mashariki zimekabidhi kwa bendera na Vikombe ilivyonyakua wakati wa mashindano yaliyofanyika Kigali nchini Rwanda.

Akipokea Bendera na Vikombe kwa Niaba ya Mkuu wa majeshi ya ulinzi Brigedia Jenerali Alfred Kapinga alisema ushindi uliopatika ni faraja kwa watanazania na jeshi hivyo ni vyema kwa wanamichezo kujipongeza hasa ukizingatia ushindani mkubwa .

“Ushindi ni Ushindi hivyo hakuna budi kujipongeza kwa kuwa washindi kwani vikombe vitat u vilivyopatika ni faraja na hasa kikombe cha Mpira wa pete ambacho tulikipoteza mwaka jana na kuchukuliwa na Uganda”,Alisema Brigedia kapinga. Pia alizitaka Timu kuanza maandalizi kwa ajili ya mashindano yajayo lakini pia kujiweka sawa kwa mashindano yatakayoshirikisha vyombo vya ulinzi na usalama ili kuibuka na ushindi zaidi ya ilivyokuwa sasa.

Aliongeza kuwa hakika jeshi limeamua kurejesha heshima yake kama ambavyo mkuu wa majeshi aliagiza katika michuano hiyo. Pia aliwapongeza waandishi wa habari wa kushirikiana na JWTZ na kuwataka kuendeleza ushirikiano huo kwani JWTZ ni timu ya Ushindi hivyo nao ni washindi na vivyo hivyo kwa wadhamini ambao amewaomba kuendeleza ushirikiano wao katika kuchangia mafanikio ya michezo kwa jeshi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa michezo kutoka makao makuu ya JWTZ Brigedia Jenerali martin Busungu ameshukuru kwa ushirikiano na kuwapongeza wote waliofanikisha ushiriki wa JWTZ katika mashindano hayo na kuahidi kufanya vizuri zaidi katika mashindano yajayo.

Alisema katika mashindano hayo waliyoshiriki michezo mitano ambAYO NI Riadha mpira wa Miguu, mpira wa pete ,mpira wa mikono na mpira wa kikapu ambapo katika mpiwa wa miguu JWTZ imeshika nafasi ya tatu, Riadha Wanawwake nafasi ya tatu na Mpira wa pete nafasi ya kwanza na mchezaji Bora ambaye alikuwa na Nasra Suleiman.

Mbali na zoezi la kukabidhi vikombe pia bendera iliyokabidhiwa kwa wanamichezo hao imerejeshwa kuashiriia mwisho wa jukumu hilo walilokabidhiwa la kupeperusha vyema bendera ya taifa .

Brigedia Jenerali Alfred kapinga kwa niaba ya Mkuuu wa majeshi Akipokea bendera toka kwa mkurugenzi wa michezo kutoka makao makuu ya JWTZ ikiwa ni ishara ya kurejea baada ya kumalizika Mashindano ya majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yaliyofanyika Rwanda Hivi karibuni, zoezi la kukabidhi vikombe na bendera ilifanyika katika ukumbi wa Twalipo Mgulani Jijini Dar es Salaam.

Brigedia Jenerali Alfred kapinga akipokea kikombe kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi toka kwa Nahodha wa Timu ya Soka Koplo Stanslaus Mwakitosi walichoshinda katika Mashindano ya majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yaliyofanyika Rwanda Hivi karibuni, zoezi la kukabidhi vikombe na bendera ilifanyika katika ukumbi wa Twalipo Mgulani Jijini Dar es Salaam.
Brigedia Jenerali Alfred kapinga akiongea na wanamichezo wakati wa hafla ya kukabidhi vikombe na bendera mara baada ya kumalizika Mashindano ya majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yaliyofanyika Rwanda Hivi karibuni, zoezi la kukabidhi vikombe na bendera ilifanyika katika ukumbi wa Twalipo Mgulani Jijini Dar es Salaam.
 

Viewing all 110016 articles
Browse latest View live


Latest Images