Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110167 articles
Browse latest View live

KAIMU MKURUGENZI WA IDARA YA UTAMADUNI AZINDUA KITABU CHA KAMUSI YA UKRISTO

$
0
0
 Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utamaduni, Lily Beleko kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akizungumza jambo kabla ya Uzinduzi wa Kitabu cha Ukristo katika Ukumbi wa Baraza la Maaskofu Dar es Salaam
 Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Publishers, Walter Bgoya akizungumza jambo kabla ya uzinduzi wa kitabu cha Ukristo
 Katibu Mtendaji Baraza la Kiswahili  la Taifa (BAKITA), Dk. Selemani Sewangi akionesha kitabu hicho kwa wadau na kwa waandishi wa habari wakati wa hafla fupi ya Uzinduzi huo wa kitabu cha Kamusi ya Ukristo kilicho zinduliwa na  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utamaduni, Lily Beleko kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
 Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utamaduni, Lily Beleko (katikati) kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akizindua Kitabu cha Kamusi ya Ukristo katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam. kulia ni Mhadhiri Chuo Kikuu Katoliki (WEA) Nairobi na Mhariri Mkuu wa Kampuni ya Uchapishaji ya Gaba Publications , Padri, Dk.Jordan Nyenyembe  ambaye ndie mtunzi wa kitabu hicho na Padri Ubaldus Kidavuri  
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

SERIKALI inawashauri viongozi wa dini nchini  kuendelea kutafsiri maneno magumu ya kidini  ili kuepusha chuki, vurugu, ghasia na mapigano  katika jamii.
Kauli hiyo ya  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ililisomwa na Kaimu Mkurungezi wa Maendeleo ya Utamaduni, Lilly Beleko katika uzinduzi wa ‘Kamusi ya Ukristo’ jijini Dar es Salaam .
Alisema kuzinduliwa kwa kamusi itahamasisha na kurahisisha uelewa wa vitabu na maandiko kwa usahihi na ufasaha kwa jamii na kuleta upendo, Utulivu na Amani.
“Lugha yetu ya Kiswahili ni chombo muhimu cha mawasiliano ambachokimekuwa kiungo cha kuimarisha umoja, Amani na uzalendo, hivyo lazima tukiendeleze,” alisema.
Alisema serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za  za kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili na kuthamini  wanataaluma na wadau wa harakati za kutetea hadhi ya Kiswahili.
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) Padre Abadius Kidavule alisema ni mara ya kwanza Tanzania ndani ya Kanisa Katoliki kuzinduliwa Kamusi ya Ukristo.
“Ni jambo la  kujivuni  kuzindua kamusi, hivyo watanzania wanapaswa kukinunua ili wajisomee,” alisema.
Mwandishi wa Kanusi hiyo, Dk.Jordani N Yenyembe alisema watanzania tumefanya makosa kutopenda kusoma vitatu, hali imesabisha kupatikana waandishi wachache wa vitatu.
“Wengi hawapendi kukosomewa  na wakikosolewa kutokana na uandishi wao, hususa kuandika  mimi naendelea kuandika nahitaji kukolewa kwenye kamusi hii,” alisema


WILAYA YA KINONDONI YABAINI WANAFUNZI HEWA.

AZAM FC WATWAA NGAO YA JAMII, WAITANDIKA YANGA BAO 4-1 (PENATI)

$
0
0
 Wachezaji wa Timu ya Azam pamoja na viongozi wao wakishangilia baada ya kutwaa Ngao ya Jamii, kwa kuifunga Yanga kwa mikwaju ya penati 4-1, kufuatia mchezo wao kumalizika kwa sare ya bao 2-2.
Mgeni Rasmi katika Mtanganye wa kuwania Ngao ya Jamii uliozikutanisha Timu ya Azam na Yanga, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akikabidhi Ngao hiyo kwa Nahodha wa Timu ya Azam, John Boko 'Adebayour', baada ya kuifunga Yanga kwa mikwaju ya penati 4-1, kufuatia mchezo wao kumalizika kwa sare ya bao 2-2.
 Beki wa Timu ya Azam FC, David Mwantika akizua mpira kwa umaridadi mkubwa huku akimdhibiti Mshambuliaji machachari wa Yanga, Donald Ngoma katika mchezo wa Ngao ya Jamii ikiwa ni sehemu ya ufunguzi wa Ligi kuu Tanzania bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Dakika 90 zilimalizika kwa timu hizo kulingana 2-2, na kupelekea kuamuliwa kupigwa mikwaju ya penati iliyoipa ushindi timu ya Azam kwa mabao 4-1.
 Mshambuliaji wa Yanga, Amisi Tambwe akitaka kuzuia shuti la Beki wa Azam, Shomari Kapombe.
 Kipa wa Azam akiwa chini huku mpira ukiwa wavuni, baada ya kupelekwa markiti na Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma kwa mkwaju wa penati.
 Beki wa Yanga, Hassan Kessy akiutuliza mpira kwa ustadi mbele ya Benchi la Wapinzani wake.



KISOMO CHA KHITMA NA DUA YA HAYATI MZEE ABOUD JUMBE

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) pamoja na Viongozi na waumini wa Dini ya kiislamuwakisoma Khitma ya kumuombea Dua Marehemu Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi katika msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Mjini Unguja leo jioni
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) pamoja na Viongozi na waumini wa Dini ya kiislamu wakisoma Khitma ya kumuombea Dua Marehemu Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi katika msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Mjini Unguja leo jioni
 Viongozi mbali mbali waliojumuika katika Kisomo cha Dua ya Khitma ya kumuombea Dua Marehemu Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi katika msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Mjini Unguja leo jioni
 Miongoni mwa Waumini wa Dini ya Kiislamu walioshiriki katika msikiti wa Mushwawal Mwembe Shauri Mjini Unguja wakisoma dua ya Khitma leo ya kumuonbea Dua Marehemu Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Mzee Aboud Jumbe Mwinyi aliyezikwa juzi nyumbani kwake Migombani
Mustafa Aboud Jumbe Mwinyi  akitoa shukurani kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein  pamoja na Viongozi na Wananchi na waislamu walioshiriki katika Khitmaya Dua ya kumuombea  Rais mstaafu wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi,Iliyosomwa leo katika Msikiti wa Mushawala Mwembe shauri Mjini Unguja. Picha na Ikulu Zanzibar

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA UJUMBE WA SHIRIKA LA GLOBAL COMMUNITIES NA UJUMBE WA MER GROUP JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja wa ujumbe wa Shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali la Global Communities uliomtembelea leo ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam wengine pichani ni kutoka kushoto ni Meneja wa Biashara Ndugu Lucas Mazige,Meneja wa Shirika hilo Ndugu Mwita Mchuni , kulia ni Meneja wa Mikopo wa Shirika hilo Ndugu Victor Anthony .

..........................................
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameutaka uongozi wa Shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali la Global Communities uhakikishe unaweka utaratibu bora wa kupata taarifa muhimu kuhusu masuala ya kilimo kutoka kwa wakulima wenyewe hatua ambayo itasaidia serikali, wafadhili na wadau wengine wa maendeleo kukipa msukumo wa kipekee kilimo ili kiweze kuwa na tija nchini.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo 17-Aug-16 alipokutana na ujumbe wa watu watatu wa shirika hilo ukiongozwa na Programu Meneja Mwita Mchumi ambao ulimtembelea ofisini kwake Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha na kuelezea shughuli zinazofanywa shirika hilo nchini.

Makamu wa Rais amesisitiza kuwa kama wakulima wakipata taarifa sahihi kuhusu masuala ya kilimo na masoko wataweza kuongeza uzalishaji wa mazao na hivyo kuleta mapinduzi makubwa ya kilimo kwa kujiongezea kipato na la taifa kwa ujumla.

"Changamoto kubwa katika kilimo ni hii ya kukosekana kwa taarifa kutoka kwa wakulima wenyewe. Nyinyi kama shirika wekeni kama mradi hivi, mnaenda mfano Singida mnaongea na wakulima wenyewe aina ya mazao ya biashara yanayolimwa pale, pembejeo wanapata kwa wakati na inakidhi haja vitu kama hivyo. Taarifa hizo zitaisadia serikali, wafadhili kukiwezesha kilimo kuwa na tija," alisema Mheshimiwa Samia.

Katika mazungumzo hayo Mwita Mchumi aliiomba serikali iangalie uwezekano wa kupunguza riba ili kuwawezesha wafanyabiashara na wakulima kukopa kwenye mabenki jambo ambalo Makamu wa Rais alisema serikali inalifanyia kazi.

Shirika la Global Communities lenye makao yake makuu Washington, Marekani tangu lilipoanza kazi rasmi hapa nchini mwezi Februari mwaka huu limeweza kuwaunganisha wauzaji na wanunuzi wadogo na wa kati wa biashara za kilimo ambao wameweza kufanya biashara ya takribani Dola za Kimarekani milioni 150.

Shirika hilo limeweza pia kufundisha mabenki umuhimu wa mfumo wa kuuza mazao kupitia stakabadhi ghalani na kuifanya Benki ya Afrika (BOA) kutenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuwakopesha wakulima wadogo wadogo wanaojishughulisha kuuza mazao kupitia stakadhi ghalani katika mkoa wa mbeya

Kwa mujibu wa Mwita Mchumi hivi sasa kuna mafunzo yanaendelea ngazi ya cheti katika kuwajengea uwezo wataalam wa benki katika biashara za kilimo ili waweze kutoa huduma stahiki katika sekta ya kilimo.

Mwita Mchumi amesema shirika hilo ambalo limeanzishwa mwaka jana linajishughulisha zaidi na masuala ya kilimo hasa biashara za kilimo katika minyororo ya thamani ya mazao ya nafaka, jamii ya mikunde, bustani, mifugo na mazao ya mafuta kama alizeti na ufuta.

Shirika hilo pia linatumia njia za tehama katika kupata taarifa za masoko na kuwakutanisha wauzaji kwa ajili ya kuingia biashara na kujenga uwezo kwa wafanyabiashara wa kati na wadogo pamoja na wakopeshaji ambao ni taasisi za kifedha kama mabenki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe kutoka kampuni ya MER GROUP,wa kwanza kushoto ni Meneja wa Kampuni hiyo Bw. Dov Aronovich, wengine ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo Bw. Omer Leviv na Meneja wa Biashara Bw. Mohammed Magori, Ujumbe huu ulimtembelea Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam na kutambulisha shughuli wanazofanya nchini.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KIONGOZI MKUU WA MADHEHEBU YA BOHORA DUNIANI MTUKUFU DKT. SYEDNA MUFADDAL SAIFUDDIN (TUS) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin wakwanza kushoto.(Katikati ni mkalimani)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 17 Agosti, 2016 amekutana na kufanya mazungumzo na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb(TUS) Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ali na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga ambapo Rais Magufuli ameipongeza Jumuiya ya Dawoodi Bohra kwa juhudi kubwa inazofanya katika kutoa huduma za kiroho na pia kushiriki katika maendeleo.
Dkt. Magufuli amewakaribisha wana Jumuiya hiyo kuwekeza hapa nchini hususani katika sekta ya viwanda na pia amewakaribisha katika Maadhimisho ya Jumuiya ya Dawoodi Bohra duniani yanayotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam Mwezi Oktoba 2016.
"Tanzania ni nchi nzuri, tumekuwa na ushirikiano mzuri sana na wenzetu wa Jumuiya ya Bohra, hivyo njooni mfanye biashara na Tanzania,  tumepanga katika kipindi cha mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021 Tanzania iwe nchi ya viwanda, kwa hiyo tunawakaribisha kuja kuanzisha viwanda vya kutosha" Amesema Rais Magufuli.
Kwa upande wake Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb amempongeza Rais Magufuli kwa kazi nzuri inayofanywa na Serikali yake ya awamu ya Tano, na pia ameahidi kuwa Jumuiya ya Dawoodi Bohra ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika maendeleo.
Aidha, Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb amemkabidhi Rais Magufuli hundi ya Dola la Marekani Elfu Hamsini na Tatu (USD-53,000) sawa na Shilingi Milioni 116 za Kitanzania kwa ajili ya kuchangia utengenezaji wa madawati ya wanafunzi kwa shule mbalimbali hapa nchini na pia amekabidhi hundi ya Dola za Marekani Elfu Ishirini na Moja (USD-21,000) sawa na Shilingi Milioni 46 kwa ajili ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA).
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amepokea barua kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Saharawi Mhe. Brahim Ghali iliyowasilishwa na Mjumbe Maalum wa Rais huyo ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Bachir Moustapha Sayed.Pamoja na kupokea barua hiyo Rais Magufuli amesema Serikali yake ya Awamu ya Tano itaendeleza na kuimarisha zaidi ushirikiano wake na Jamhuri ya Kiarabu ya Saharawi na pia itaendelea kuunga mkono juhudi za wananchi wa Saharawi kupata haki ya kuamua hatma yao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
17 Agosti, 2016.
 Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin akimuombea dua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na  Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin wengine katika picha ni Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir,  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga pamoja na viongozi wengine wa BAKWATA na wa madhehebu ya Bohora.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na  Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin wengine katika picha ni Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir pamoja na viongozi wengine wa Madhehebu ya Bohora.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeir Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuagana na  mgeni wake Kiongozi Mkuu wa Madhehebu ya Bohora Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin.
PICHA NA IKULU.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

VIDEO: HII NDIO MIKWAJU YA PENATI ILIYOWAPA USHINDI TIMU YA AZAM DHIDI YA YANGA LEO

$
0
0
Kipa wa Azam, Aishi Manula akiruka kuwania mpira uliopigwa na Mchezaji wa Yanga, Haruna Niyonzima ambao ulikwenda nje wakati wa changamoto ya mikwaju ya penati kuamua nani wa kunyangua Ngao ya Jamii, ambayo imekwenda wa Timu ya Azam, baada ya kuichabanga Yanga mabao 4-1 kufuatia mchezo wao kumalizika kwa sare ya bao 2-2.
Kipa wa Yanga, Deogratius Munish akiwa kapelekwa markiti kwa Mkwaju wa penati ulioimaliza Yanga, uliopigwa na Mchezaji wa Azam, Bolou Kipre.
Wachezaji wa Timu ya Azam, wakishangilia Ushindi wao kwa kumrusha juu juu Kocha wao.

MAGAZETINI LEO ALHAMISI AGOSTI 18


Article 14

RAIS DKT MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKUU WA MKOA ARUSHA FELIX NTIBENDA,AMTEUA MRISHO GAMBO KUWA MKUU WA MKOA

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha,Mrisho Gambo aliyeteuliwa na Rais,kuapishwa kesho ijumaa Ikulu jijini Dar
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya uongozi na kumteua Bw. Mrisho Gambo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuanzia leo (Alhamisi, Agosti 18,2016).

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Bw. Gambo anachukua nafasi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Felix Kijiko Ntibenda ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Amesema Bw. Ntibenda anahamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu ambako atapangiwa majukumu mengine.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Gambo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha. Ataapishwa kesho (Ijumaa, Agosti 19, 2016) saa 3 asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM.
ALHAMISI, AGOSTI 18, 2016.

BALOZI WA ISRAEL NCHINI AMTEMBELEA WAZIRI MAKAMBA.

$
0
0
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akiongea jambo na Balozi wa Israel Nchini Tanzania Mh. Yahel Vilan alimpomtembelea Waziri Makamba  Ofisini kwake barabara ya Luthuli jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January Makamba wakijadiliana jambo na Balozi wa Israel Nchini Tanzania Mh Yahel Vilan alimpomtembelea Waziri Makamba  Ofisini kwake barabara ya Luthuli jijini Dar es Salaam. Wengine ni Maafisa toka Wizara ya mambo ya nje waliongozana na Balozi huyo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akisoma Nakala za machapisho  alizopatiwa na Balozi wa Israel Nchini Tanzania Mh . Yahel Vilan. 




VOA: Trump awakera waislamu na viongozi wa chama chake

WILAYA YA PANGANI KUFANYWA YA MFANO KWA KUUNGANISHIWA UMEME YOTE

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mkaramo kilichopo wilayani Pangani mkoani Tanga. Waziri Muhongo yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kukagua miradi ya kusambaza umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na kuzungumza na wananchi.

Na Greyson Mwase, Pangani

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa Serikali ina mpango wa kusambaza nishati ya umeme katika wilaya nzima ya Pangani na kuifanya kuwa wilaya ya mfano ndani ya kipindi cha miaka miwili.

Profesa Muhongo aliyasema hayo alipokuwa akihutubia katika kijiji cha Mkaramo kilichopo wilayani Pangani mkoani Tanga. Profesa Muhongo yupo mkoani Tanga kwa ajili ya kukagua miradi ya usambazaji wa umeme vijijini inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Kabla ya kuwasili katika kijiji hicho msafara wa Profesa Muhongo ulisimamishwa na wananchi wa kijiji cha Sakura kilichopo wilayani Pangani mkoani Tanga waliokuwa na mabango wakiomba kupatiwa umeme katika kijiji chao.

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisisitiza jambo wakati alipokuwa akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Mkaramo kilichopo wilayani Pangani mkoani Tanga (hawapo pichani).


Akizugumza kwa niaba ya wanakijiji wenzake, Boga Mbega alisema kuwa kijiji hicho kimekuwa gizani kwa muda wa miaka mingi hali inayopelekea uchumi katika kijiji hicho kudumaa.

Aliongeza kuwa kutokana na ukosefu wa umeme katika kijiji hicho wamekuwa wakifuata huduma za jamii kama vile matibabu na maji katika vijiji vya mbali na hivyo kuhisi kama wako kwenye kisiwa cha giza.

Mara baada ya Waziri Muhongo kuwasili katika kijiji cha Mkaramo na kuanza kuhutubia alisema kuwa kutokana na wilaya ya Pangani kuwa nyuma kimaendeleo kuliko wilaya nyingine nchini, Serikali imepanga mikakati ya kuhakikisha kuwa wilaya nzima ya Pangani pamoja na vijiji vyake vyote inapata nishati ya umeme ndani ya kipindi cha miaka miwili.
Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Zainab Abdallah Issa (kushoto) akiwasilisha mahitaji ya umeme katika wilaya ya Pangani.

Akielezea malengo ya kuipa kipaumbele wilaya ya Pangani kwenye mpango wa usambazaji wa umeme vijijini chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Profesa Muhongo alieleza kuwa ni kufuta umasikini kupitia uboreshaji wa huduma za jamii kama shule, zahanati, pamoja na kuzalisha ajira na kupunguza wimbi la vijana kukimbilia mjini kutafuta ajira.

Alisema katika utekelezaji wa mradi wa REA Awamu ya tatu katika wilaya ya Pangani, maeneo yatakayopewa kipaumbele cha kwanza ni pamoja na shule, zahanati, vyuo, makanisani na misikitini. Aliwataka wananchi wa wilaya ya Pangani kujiandaa na mradi huo kwa kubuni fursa mbalimbali kama vile kuanzisha vikundi vidogo vidogo kwa ajili ya kuanzisha viwanda, ukulima na ufugaji wa kisasa ili kujipatia maendeleo.
Waziri wa Nishati na Madini (kulia) akipokea kero mbalimbali kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Mkaramo.

Alifafanua kuwa ni wakati wa wakinamama wa wilaya ya Pangani kuachana na matumizi ya kuni na kutumia majiko ya umeme na gesi. Profesa Muhongo aliendelea kusema kuwa miradi ya umeme haihitaji siasa na kuwataka wananchi kuweka nguvu zaidi kwenye uchumi kwa kutumia nishati ya umeme badala ya kupoteza muda kwenye siasa.

Naye Mbunge wa Pangani Jumaa Hamidu Aweso (CCM) aliishukuru serikali kwa kuipa kipaumbele wilaya ya Pangani na kusisitiza kuwa wataanza kufanya uhamasishaji kwa wananchi wote wa Pangani . Aliwataka wananchi kuachana na maandamano ya siasa na badala yake waweke nguvu kwenye shughuli za kiuchumi zitakazowapatia maendeleo.

Alisema kuwa mara baada ya umeme katika wilaya nzima ya Pangani kupatikana, wawekezaji watajitokeza kuwekeza kwenye viwanda vya korosho na kuongezeka mapato katika halmashauri ya Pangani.

Wananchi wa kijiji cha Sakula kilichopo wilayani Pangani mkoani Tanga wakionyesha mabango yenye jumbe tofauti mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) walipomsimamisha njiani kwa lengo la kuwasilisha kero mbalimbali wakati akielekea katika kijiji cha Mkaramo kwa ajili ya kuhutubia wananchi.

INTRODUCING: ICE BOY X MULLA -TUMBUA MAJIPU

KUTOKA MAKTABA YA GLOBU YA JAMII: HAWA NDIO WAZEE WALIOANZISHA VUGUVUGU LA KUSAKA UHURU WA NCHI YETU

$
0
0
Kutoka kulia waliosimama. 1. Abdallah Shomari (Tandamti no. 3 )2. Nassoro kalumbanya (simba str.) 3. Said Chamwenyewe (Aggrey/Congo str.) 4. Mtoro Ally (Muhonda str.) 5. John Rupia (Misheni kota) 6. Julius Nyerere( Pugu Sekondari ) 7. Said Chaurembo (Congo/ Mkunguni str.) 8. Jumbe Tambaza( Upanga ) 9. Sheikh Suleiman Takadir (Mafia /Swahili) 10. Dossa Aziz ( Mbaruku /Somali kipande ) 11. Mshume Kiyate (Tandamti) 12. Juma Sultan (Kitchwele karibu na kanisa dogo ) 13. Maalim Shubeti (Masasi/ Likoma) 14. Rajab Simba ( kiungani str.) 15. Waziri Mtonga (Kilosa no. 18 , Ilala) 16. Mwinjuma Mwinyikambi ( Mwananyamala) 17. Maxi Mbwana ( Aggrey /Kongo ) 18. Usia Omari (Sungwi ,Kisarawe) 19. Sheh Issa Nasir ( Bagamoyo)

WANAFUNZI HEWA 2331 KATIKA SHULE ZA SEKONDARI MKOANI SIMIYU WABAINIKA

$
0
0
Baada ya kufanya uhakiki wa Wanafunzi Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umebaini uwepo wa wanafunzi hewa 2331  katika shule za Sekondari za Mkoa huo.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka wakati alipozungumza na Walimu Wakuu na Waratibu Elimu Kata mara  baada ya kuwakabidhi Vishikwambi (Tablets) vilivyotolewa na Shirika lisilokuwa la Kiserikali la EQUIP Tanzania kwa ajili ya utunzaji wa Takwimu muhimu za Sekta ya Elimu,.

Mtaka amesema kati ya Halmashauri sita za Mkoa huo, Ni Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi  tu ambayo haina wanafunzi hewa wakati Halmashauri ya Wilaya ya Busega ikiwa na wanafunzi hewa  110, Itilima  2137, Maswa 14, Meatu 125 na Halmashauri ya Mji wa Bariadi 439.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka akizungmza na Walimu wakuu na Waratibu wa Elimu wa Kata baada ya kuwakabidhi Vishikwambi vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la EQUIP Tanzania, kwa ajili ya kutunza kumbukumbu na tawimu sahihi za masuala ya elimu.

Kufuatia kuwepo kwa wanafunzi hewa Mkuu wa Mkoa huo amesema, Serikali Mkoani humo imepanga kufanya mabadiliko ya Wakuu wa Shule za Sekondari katika Mkoa mzima, wakati taratibu za kinidhamu zikiendelea kwa wakuu wa shule  waliotoa takwimu za uongo za wanafunzi katika shule zao, wakati kwa upande wa shule za Msingi, mabadiliko yatafanyika baada ya kumaliza mtihani wa darasa la saba.

Mtaka amesema kabla ya uteuzi wa wakuu wa shule na walimu wakuu utafanyika upekuzi (vetting) kwa wale watakaopendekezwa ili kujiridhisha kama wahusika wana sifa na uwezo wa kuendesha shule na kusimamia fedha za Serikali zinazopelekwa shuleni kwa ajili ya kugharama elimu ya bila malipo. 
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini (kushoto) akizungumza na Walimu wakuu na Waratibu wa Elimu wa Kata baada ya kukabidhiwa Vishikwambi na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (katikati)vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la EQUIP Tanzania, kwa ajili ya kutunza kumbukumbu na tawimu sahihi za masuala ya elimu(kulia)ni Afisa Elimu Mkoa, Julius Nestory.

“ Serikali inaendelea kupelekea fedha moja kwa moja katika akaunti za shule, kwa hiyo mkuu wa shule au mwalimu mkuu ni afisa masuuli katika shule yake. Ipo haja kwa sisi kujiridhisha kama Serikali kuwa anayeteuliwa kushika nafasi ya kuongoza shule ana uwezo na sifa  ya uadilifu. Sitakuwa tayari kuona katika mkoa huu kuna walimu wakuu wazoefu wa kula fedha za Serikali na wakaendelea kuongoza shule” alisema Mtaka.

Akitoa shukrani kwa Shirika la EQUIP Tanzania, Mkuu wa Mkoa amesema Shirika hilo limekuwa msaada katika kutatua baadhi ya changamoto za Watendaji katika Sekta ya Elimu mkoani Simiyu ikwa ni pamoja na  kuwawezesha Waratibu Elimu Kata kwa kuwapa pikipiki na kuwapa fedha za mafuta shilingi 206,000 kwa kila mwezi pamoja na kutoa mafunzo kwa walimu wakuu na walimu wakuu wasaidizi.
Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa (kushoto) akipokea Vishikwambi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka(kulia) kwa ajili ya Walimu Wakuu na Waratibu Elimu Kata wa Halmashauri hiyo.

Aidha, Mtaka amesema analishukuru shirika hilo kuona umuhimu wa kutoa vishikwambi kwa Walimu wakuu na Waratibu Elimu Kata ambavyo ameelekeza vitumike kutunza takwimu sahihi za kieleimu ikiwemo idadi ya walimu na wanafunzi.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini amewataka Walimu Wakuu na Waratibu Elimu Kata kuvitunza vishikwambi hivyo na kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.
Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Nelasi Mulungu(kushoto) akipokea Vishikwambi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka(kulia) kwa ajili ya Walimu Wakuu na Waratibu Elimu Kata wa Halmasahuri hiyo.

Naye Mkuu wa EQUIP Tanzania Mkoa wa Simiyu, Phoebe Okeyo amesema Vishikwambi hivyo  vitawasaidia Viongozi wa Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya na kata kupata taarifa za masuala mbalimbali yanayofanyika shuleni.

“Sasa hivi mtegemee kupata taarifa sahihi katika sekta ya Elimu kwa sababu ya hivi vifaa tulivyovitoa leo, tumeanza kama pilot study kwa Mikoa ya  Simiyu, Shinyanga, Mara, Tabora, Dodoma,Lindi na Kigoma. Tunatarajia kuongeza mikoa ya Katavi na Singida Januari, 2017” alisema Okeyo.

Jumla ya Vishikwambi(tablets) 637 vimetolewa  kwa Walimu wakuu 516  na Waratibu Elimu Kata 121 kutoka Halmashauri zote sita za Mkoa wa Simiyu, ambapo  kila kimoja kina thamani ya shilingi 315,000/=.
Baadhi ya Walimu wakuu na Waratibu Elimu Kata wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (hayupo pichani) mara baada ya kukabidhiwa Vishikwambi vilivyotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la EQUIP Tanzania, kwa ajili ya kutunza kumbukumbu na tawimu sahihi za masuala ya elimu.

JWTZ YANYAKUA VIKOMBE VITATU MASHINDANO YA MAJESHI MJINI KIGALI

$
0
0
Mnadhimu mkuu wa Jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania Luteni Generali Venance mabeyo akisalimiana na wachezaji wa timu ya Soka ya Tanzania wakati wa mchezo wa mwisho dhidi ya Rwanda Tanzania ilifungwa bao 1-0 na kushika nafasi ya tatu
Mwanariadha Siata Kalinga akipokea kikombe cha mshindi wa tatu kwa riadha wanawake kutoka kwa Naibu Mkuu wa Majeshi wa Uganda Luteni Jenerali Charles Angina.
Viongozi waandamizi wa majeshi waliowakilisha wakati wa sherehe za kufungwa mashindano ya   Majeshi kwa nchi za Afrika Mashariki, yaliyokuwa yakifanyika Mjini Kigali nchini Rwanda kutoka kulia ni mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba, akifuatiwa na Mkuu wa majeshi wa Kenya Jenerali Samson Mwathethe, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Naibu Mkuu wa Majeshi wa Uganda Luteni Jenerali Charles Angina. (picha na Selemani Semunyu)

WAZIRI MKUU AWAWEKA SAWA WATUMISHI WA OFISI YAKE, TAYARI KWA SAFARI YA DODOMA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema safari ya kuhamia Dodoma imeiva na amewataka watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wajipange kisaikolojia.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumatano, Agosti 18, 2016) alipokutana na kuzungumza na watumishi wa ofisi yake kutoka taasisi, idara na vitengo mbalimbali waliopo Dar es Salaam.

Waziri Mkuu aliwataka watumishi hao watambue kuwa uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao chimbuko lake ni agizo lililotolewa Oktoba Mosi, 1973 kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa chama cha TANU.

“Tangu wakati huo kumekuwa na juhudi mbalimbali zilizofanyika ili kuandaa miundombinu na hata awamu ya nne ilisimamia kwa kiwango kikubwa uwekaji wa miundombinu hiyo,” alisema.

“Pia tukumbuke kauli ya Mheshimiwa Rais aliyotoa kwenye hotuba yake ya Julai 23, 2016 alipochaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM, na akairudia tena Julai 25, kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa na mimi siku hiyo hiyo nikaweka msisitizo,” alisema.

“Napenda kuwatoa hofu, mambo yanaenda vizuri ila mtambue kuwa safari imeiva sasa. Kikubwa ni kwamba tutakwenda kwa awamu kama ambavyo imepangwa,” alisema.

Aliwataka watumishi hao wazidishe mshikamano miongoni mwao huku wakitambua kuwa wana dhamana ya kuwatumikia Watanzania kwa uadilifu na uaminifu. “Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu tunapaswa tutambue dhamana tuliyonayo. Tufanye kazi kwa bidii. Tuhakikishe kila kilichopangwa kinafanyika kwa ufanisi na kinafanikiwa,” alisema.

IGP MANGU AWAAGA ASKARI 14 WA KIKOSI MAALUM CHA POLISI (S.F.U)

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akimuuaga PC Prosper Yenda yenda wa kikosi maalum cha Jeshi la Polisi ( S.F.U) ambaye ni miongoni mwa askari 14 wanaokwenda nchini Jordan kwa kozi maalum ya kupambana na uhalifu na wahalifu.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akiwa katika picha ya pamoja na askari 14 wa kikosi maalum cha Jeshi la Polisi (S.F.U) ambao wanaokwenda nchini Jordan kwa kozi maalum ya kupambana na uhalifu na wahalifu. (Picha na Tamimu Adam- Jeshi la Polisi).

UCHAMBUZI WA HABARI ZA MAGAZETI YA LEO

Viewing all 110167 articles
Browse latest View live




Latest Images