Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110025 articles
Browse latest View live

ACTIVISTA TANZANIA WAADHIMISHA SIKU YA VIJANA DUNIANI

$
0
0
Mkurugenzi wa DOT Tanzania, Dawson Luogard akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya siku ya vijana leo katika ukumbi FES Oyster Bay jijini Dar es Salaam.
Mtandao wa Vijana wa Activista Tanzania wakishirikiana na Tanzania Youth Vision Association(TYVA) wameadhimisha siku ya Vijana Duniani kwa kuwakutanisha vijana zaidi ya 120 kutoka maeneo mbalimbali na kujadili mada mbalimbali kuhusu Kodi, Kilimo na Maendeleo Endelevu ya malengo ya millenia.(Picha na Geofrey Adroph)
Mwenyekiti wa Activista Tanzania, Hatibu Kilenga akifunga mafunzo kwa vijana yaliyoandaliwa na Mtandao wa Vijana wa Activista Tanzania wakishirikiana na Tanzania Youth Vision Association(TYVA) katika maadhimisho ya siku ya Vijana Duniani.

MASHINDANO YA YA MAJESHI YAPAMBA MOTO NCHINI RWANDA, TIMU YA JWTZ MPIRA WA PETE YA YAANZA

$
0
0
 Mchezaji  Faraja Malaki wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 .
 Mchezaji  Veronica Patrick wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27.
Mchezaji  Veronica Patrick wa Tanzania akiwania mpira mbele ya Wachezaji wa Uganda katika michezo wao wa Kwanza wa mashindano ya Majeshi kwa nchi za  Afrika Mashariki katika Uwanja wa Amahoro Nchini Rwanda Tanzania ilishinda 29-27 .
(Picha na Selemani Semunyu).

Na Selemani Semunyu JWTZ.
TIMU ya Mpira wa Pete (Netball) ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania imerejesha heshima yake baada ya Kuwafunga mabingwa Watezi  wa Michuano hiyo kwa Mpira wa Pete Uganda kwa magoli 29 kwa 27.

Katika Mchezo huo uliokuwa wa Vuta nikuvute  na rabsha za hapa na pale zilizizojitokeza kabla wakati na Baada ya Mchezo huo ambao ulikuwa na Upinzani Mkali kutokana na historia ya Timu hizo.

Katika Robo ya Kwanza Tanzania ilimaliza ikiongoza kwa magoli saba kwa Sita huku Timu zote zikicheza Mchezo wa kuviziana lakini uliojaa nguvu na kukamiana miongoni mwa Wachezaji.

Katika Robo ya Pili Tanzania pia ilimalizai ikiwa mbele kwa mabao 13 kwa 11 kukiwa na tofauti ya magoli mawili tofauti na robo ya kwanza ambayo ilimalizika kwa tofauti ya goli moja.

Robo ya Tatu Uganda walikuja na kusawazisha na kasha kuongeza na hivyo kumaliza kwa ushindi wa magoli 20 kwa 19 ya Tanzania  na kuwafanya Tanzania kwenda kujiuliza.

Hatimaye robo ya Mwisho ikamalizika na Timu ya Tanzania kuibuka na Ushindi na hivyo kuwatisha Mabingwa wa mwaka uliopita pengine utarejea kwa Tanzania Kwa Upande wa Nahodha wa Timu hiyo Dorita Mbunda alisema mechi yao na Uganda wamecheza kama fainali kutoka na historian a kuahidi kujipanga kwa ajili ya kuwakabili Kenya. 

Kwa upande wake Nahodha Uganda Lilian Ajio amelalalimika Waamuzi kutoelewa Sheria Mpya za Mchezo huo hali iliyopelekea wakati mwingine kutokuwa na maamuzi sahihi.

vipaji Airtel Rising Stars vyamvutia RC Makalla, jijini Mbeya

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amefungua rasmi mashindano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Mbeya na kuvitaka vilabu vya soka kutumia vipaji vinavyoibuliwa na programu hiyo ya vijana. Ufunguzi huo ulifanyika kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya leo Agosti 9, 2016.

“Hii ndio njia pekee ambayo inaweza kutuletea maendeelo ya soka na kuiwezesha nchi yetu kuondokana na matokeo mabaya katika mashindano mbali mbali ya kimataifa”, alisema. Aliishukuru kampuni ya Airtel Tanzania kwa kubuni programu hii ambayo imekuwa ikiwapa vijana fursa ya kuonyesha na kuviendeleza vipaji vyao.

Makala amewataka vijana kucheza kwa kujituma na kufahamu kwamba hatma ya mchezo wa soka hapa nchini iko mikononi mwao. Alilitaka Shirikisho la soka nchini (TFF) kufanya kazi kwa karibu na wadau wengine ili kuhakikisha kuwa vijana wanaoibuliwa kupitia Airtel Rising Stars wanaendelezwa.

Amewataka viongozi wa chama cha soka mkoa wa Mbeya (MREFA) kuyatumia vizuri mashindano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa na kuchagua vijana nyota watakaounda timu za mkoa kushiriki kwenye fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinazotarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Septemba 6 hadi 11 jijini Dar es Salaam.

Michuano ya Airtel Rising Stars ngazi ya mkoa inaendelea katika mikoa minginge ambapo timu za wavulana za Makongo Sekondari na Kawe United zilitoshana nguvu baada ya kutoka suluhu katika uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Fainali za Taifa zitashirikisha timu za wavulana na wasichana kutoka mikoa ya kisoka ya Ilala, Temeke na Kinondoni. Timu nyingine zitatoka Morogoro, Mwanza, Mbeya, Arusha, Lindi na Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amoss Makalla aliye simama akizungumza na wachezaji kabla ya kuzindua michuano ya Airtel Rising Star kwa Mkoa wa Mbeya iliyo anza kutumia vumba jana katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na kushirikisha timu sita.
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde akifafanua jambo kwa wafanyakazi wa Airtel Mkoani Mbeya wakati wa uzinduzi wa michuano ya Airtel Rising Stars mkoani hapo
Wachezaji kutoka timu sita zinazo shiriki Michuano ya Airtel Rising Star chini ya miaka 17 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amsos Makalla hayupo katika picha kabla ya kuzindua rasmi michuano hiyo kimkoa jana katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

BALOZI MAHIGA AUZUNGUMZIA MGOGORO WA UTURUKI NA UNAVYOHUSISHWA NA SHULE ZA FEZA

BALOZI HAULE AAGWA NAIROBI

$
0
0
Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya jana walitayarisha hafla fupi kumuaga Mhe. Balozi John Michael Haule, ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria. Mhe. Haule aliteuliwa kuwa Balozi mwaka mmoja uliopita baada ya kutumikia Wizara ya Mambo ya Nje kwa miaka minne kama Katibu Mkuu.

Katika risala yao, watumishi wa Ubalozi walimuelezea kama 'mjenzi' aliyeimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Kenya, na kiongozi mtaalamu, mnyenyekevu na mwadilifu.

Mwakilishi wa Watanzania waishio Kenya, Bw. Victor Matemba, alimsifu Mhe. Haule kwa ari na juhudi alizofanya kufufua umoja wao ambao umedorora kwa muda mrefu. Ubalozi unaratibu uandishi wa Katiba mpya ya Umoja huo ambayo iko katika hatua za mwisho.

"Unaondoka wakati ambao ulezi na uongozi wako tunauhitaji zaidi. Tutakumiss sana Mheshimiwa," alisema Bw. Matemba. Akiongea kwenye hafla hiyo, Mhe. Haule alisema uhusiano kati ya Tanzania na Kenya ni imara, kinyume na taarifa za baadhi ya vyombo vya habari zinazodai kuwa kuna msuguano. "Uhusiano wetu ni mzuri sana."

Balozi alielezea wasiwasi kuhusu mtafaruku wa kisiasa nchini Sudan Kusini na kutaka hatua madhubuti zichukuliwe kuepusha mapigano zaidi, ambayo alisema yataathiri pia Watanzania waishio nchini humo.

Mhe. Haule, ambaye aliambatana na mkewe Mary kwenye hafla hiyo ya kumuaga iliyofanyika kwenye ofisi za Ubalozi, aliwashukuru watumishi wote kwa ushirikiano mkubwa waliompatia.
Mhe. Haule akiongea wakati wa hafla ya kumuaga jana. Kushoto ni mkewe Mary.
Mhe. Balozi Haule (aliyeketi katikati) katika picha ya pamoja na Maofisa Ubalozi. Kushoto ni Mama Mary Haule na Kulia ni Mkuu wa Utawala Ubalozini, Bi. Talha Waziri.
Mhe. Haule na mkewe katika picha ya pamoja na watumishi wa Ubalozi wanaotoka Kenya (Local staff).
Mwakilishi wa Watanzania waishio Kenya, Bw. Victor Matemba akitoa salamu zao kwa Mhe. Haule.

WADAU WA MAENDELEO WAKUTANA NA SERIKALI KUJADILI NAMNA YA KUBORESHA UHUSIANO

$
0
0

Mwenyekiti wa mkutano wa wadau wa Washirika wa Maendeleo Dkt. Donald Kaberuka akifafanua jambo kwa wajumbe (hawapo pichani) waliohudhuria mkutano wa kutafuta njia bora ya kuhuisha na kuimarisha ushirikiano kati ya wadau hao wa maendeleo na serikali, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa mkutano unaojadili kuhusu namna ya kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Wadau wake wa Maendeleo, aliyewahi kuwa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika-AfDB-Dkt. Donald Kaberuka (kushoto), akifafanua jambo kwenye ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu, Jijini Dar es salaam, kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Servacius Likwelile.

Kaimu Katibu Mkuu wa Tume ya Mipango Bi. Florence Mwanri (kushoto) akisikiliza kwa makini hoja ya mjumbe wa Mkutano kuhusu namna ya kuboresha ushirikiano kati ya Tanzania na Wadau wake wa Maendeleo, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Jijini Dar es salaam

Washirika wa Maendeleo wakiwa katika mkutano wa pamoja kuhusu namna ya kuimarisha uhusiano wa Maendeleo nchini Tanzania, mkutano umefanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Jijini Dar es salaam. 

DC KAKONKO AKABIDHI MAGARI MAWILI YA WAGONJWA KITUO CHA AFYA MGAZA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Kakonko Col. Hosea Maloda Ndagala akikabizi funguo za magari mawili ya kubebea wagonjwa  (hayapo pichani)kwa Mganga Mkuu wa kituo cha afya Mgaza Wilayani Kakonko Dkt Selemani Fadhiri. Wanaoshuhudia wapili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya KakonkoLusubilo Mwakabibi na kushoto ni Diwani wa Kiziguzigu, Renatus Daniel.
 Mkuu wa Wilaya akijaribu moja ya magari hayo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kakonko, Col. Hosea Ndagala akiongea na  Madiwani. Watumishi wa Hospital wakati wa hafla ya kukabidhi magari ya wagonjwa katika kituo cha afya Mgaza Wilayani Kakonko.

RAIS DKT.MAGUFULI ANA NIA NJEMA KWA WATANZANIA,TUMUUNGE MKONO-MBUNGE WA MKURANGA

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga wilayani Pwani Abdallah Ulega amewaondoa hofu wananchi wake na kuwaeleza kuwa wasiwe na wasiwasi kwani Rais Dkt.Magufuli ana nia njema kwa watanzania
 
Mh.Ulega ametoa kauli hiyo wilayani Mkuranga katika mkutano wake wa kuwashukuru wananchi wa kijiji cha Sotele kilichopo kata ya Dondo wilayani humo. Amesema kuwa hakuna haja ya kumchukia Rais kwani anayoyafanya Rais leo yamesababishwa na watu wachache ambao Kazi yao ilikuwa ni kujijali wenyewe tu na si vinginevyo na pia waliwasahau wananchi kuzisikiliza shida na kero zao na kuzifanyia kazi.
 
."Mnajuwa Rais anadhamira ya dhati kabisa na watanzania na katika bajeti ya mwaka huu ndio maana ametenga  fedha nyingi ambazo zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi hivyo kinachotakiwa ni kumuunga mkono na kuzidi kumuombea tu"amesema Ulega.
 
Akizungumzia maendeleo ya jimbo la Mkuranga alisema amejipanga kikamilifu kuwaletea maendeleo wananchi wake na ndio.maana anapita kuwashukuru na kuhimiza maendeleo. 

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kibewa kilichopo kata ya Dondo mkoani Pwani ,ambapo katika mkutano huo Mh.Ulega aliwashukuru wananchi hao kwa kumchagua kuwa Mbunge wao na kisha akatumia fursa hiyo kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi .

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya mkuranga Juma Abed akizungumza jambo mbele ya wananchi wa Kijiji cha kibewa ambao aliwataka kumtumia mbunge wao Ulega na kwamba ni muda wao sasa kumbebesha majukumu yao kwani ndio kazi waliyompa,na zaidi kuacha siasa na kujikita kufanya kazi.

Badhi ya Wananchi wakifuatilia mkutano wa Mbunge wa jimbo la MKuranga,Mh Ulega alipofanya ziara fupi katika kijiji cha Kibewa Kata ya Dondo katika ziara ya kushukuru kwa wananchi wake baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Mzee aliyejitambulisha kwa jina la Jumbe Kazenga wa kijiji cha Kibewa Kata  ya Dondo akitoa ya moyoni kwake kwa mbunge wa Jimbo la mkuranga Abdallah ulega ambapo pamoja na mambo mengine alimpongeza kwa kazi nzuri aliyoianza,ulega yupo katika ziara ya kushukuru kwa wananchi wake baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Mbunge Abdallah Ulega wa Jimbo la mkuranga akiwa sambamba na watendaji na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo akikagua mradi wa ufugaji wa samaki unaondeshwa na kikundi cha ufugaji samaki katika kijiji cha kibewa.Mh Ulega anaendelea na ziara zake za kushukuru wananchi wake.

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah Ulega akimsikiliza Mganga wa Zahaniti ya Kijiji cha Sotele,Emily Bugingo kilichopo kata ya Dondo bara baada ya kutembelea Zahanati hiyo leo Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka,Globuya jamii)

Suluhu ya magwangala yapatikana Mkoani Geita

$
0
0
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akifafanua jambo katika eneo la Lwenge, Nyamikoma ambalo ni moja ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuhifadhi magwangala.

Na Greyson Mwase, Geita

Mgogoro uliodumu kwa muda mrefu katika mkoa wa Geita kuhusu upatikanaji wa magwangala na eneo la kuhifadhi magwangala hayo, umepatiwa ufumbuzi baada ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kukutana na mkuu wa mkoa wa Geita, uongozi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM), watendaji wa halmashauri ya mkoa huo na wawakilishi kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

Profesa Muhongo alifanya ziara katika mkoa huo ikiwa ni utekelezaji wa agizo lililotolewa na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania John Magufuli lililotolewa Julai 31 mwaka huu la wachimbaji wadogo kupatiwa magwangala pamoja na maeneo ya kuhifadhi magwangala hayo ili kuchenjua na kupata dhahabu.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita. Kulia ni mkuu wa mkoa huo, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga.

Akizungumza katika kikao kilichokutanisha watendaji kutoka Mkoa wa Geita, Wizara ya Nishati na Madini, Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) na Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Profesa Muhongo alisema maeneo ya awali yaliyopatikana kwa ajilli ya kuhifadhi magwangala hayo ni pamoja na Lwenge- Nyamikoma, Kasota B na Samina B yaliyopo mkoani Geita.

Aliagiza Ofisi ya Madini Mkoani Geita kutoa leseni za uchenjuaji madini mara moja kwa vikundi vyote vya wachimbaji madini ili waanze kazi mara moja ya uchenjuaji madini kwa kutumia magwangala hayo.

“Ninaagiza Ofisi ya Madini Mkoani Geita kutoa leseni za uchenjuaji madini kwa vikundi vilivyoundwa kupitia halmashauri mara moja bila vikwanzo vyovyote ili waanze na shughuli za uchenjuaji madini mara moja,’ alisema Profesa Muhongo. Akizungumzia suala la usafirishaji wa magwangala katika maeneo hayo Profesa Muhongo alisema ni jukumu la vikundi vilivyopewa magwangala hayo kusafirisha kutoka kwenye mgodi hadi kwenye maeneo yaliyoainishwa.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga (mbele) akisoma taarifa ya utekelezaji wa mpango wa kubaini maeneo kwa ajili ya kuhifadhia magwangala mbele ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Halmashauri ya Geita.

Aliongeza kuwa iwapo vikundi vitakosa uwezo wa kusafirisha magwangala hayo, halmashauri inaweza kufanya mazungumzo na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) kwa ajili ya gharama ya kusafirisha magwangala hayo.

WANAOSAFIRI NJE YA NCHI WATAHADHARISHWA KUHUSU UPATAJI WA KADI ZA CHANJO HOMA YA MANJANO

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imewatahadharisha wananchi wanaopanga kusafiri kwenda nje ya nchi kuhakikisha kuwa wanafika katika vituo vya afya na kuchanjwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya Homa ya Manjano badala ya kuwalipa fedha baadhi ya watumishi wa afya wasio waaminifu ili watengenezewe kadi hizo kinyume cha sheria.

Mkurugenzi wa Huduma za Kinga wa Wizara hiyo Dk. Neema Rusimabayila akitoa ufafanuzi kuhusu suala hilo leo jijini Dar es salaam amesema baadhi ya wasafiri wamekuwa wakishirikiana na watumishi wa afya wasiowaaminifu kwa kuwalipa fedha ili waweze kuwatengenezea kadi hizo na kisha kuzitumia nje ya nchi jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa Afya zao.

“Kumekuwa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu ambao hupokea fedha na kisha kutengenezesha kadi za wasafiri zinazoonesha kuwa wamepatiwa chanjo, Jambo hili ni hatari kwa afya ya msafiri, sasa tunaona mlipuko wa ugonjwa huu ukitokea katika nchi za karibu ni muhimu mtu kuchanja ili kuepuka kuwa chanzo cha kuleta ugonjwa huu” Amesisitiza Dk.Neema.

Amesema ni jambo lisilokubalika kwa msafiri kuwa na kadi ya chanjo ya Kinga ya Homa ya Manjano akijua kabisa hajapatiwa chanjo hiyo na kuongeza kuwa jambo hilo linamuweka muhusika katika hatari ya kupata maambukizi akisafiri kwenye nchi zenye mlipuko wa ugonjwa huo.

“Napenda kusisitiza kuwa ni muhimu sana msafiri akachanjwa chanjo hii kwa ajili ya kinga ya afya yake mwenyewe, kupata kadi bila kuchanjwa na kwenda mahali ambapo kuna ugonjwa huu ni kujidanganya, epuka kuwa chanzo cha kusambaza ugonjwa huu” Amesisitiza Dk. Neema.

Kuhusu gharama za chanjo hiyo amesema kuwa msafiri anayetaka kupata chanjo hiyo anatakiwa kulipia gharama ya Elfu Ishirini (20,000/=) ikiwa ni malipo halali ya Serikali na mlipaji hupatiwa stakabadhi halali.

Aidha, amesema mbali na hatua zinazochukuliwa kudhibiti hali hiyo, Wizara inakamilisha utaratibu wa kuwa na kadi maalum ambazo zitakuwa tofauti, zenye nembo maalum ambazo mtu hataweza kughushi wala kufanya udanganyifu wa aina yoyote.
Mkurugenzi wa Huduma za Kinga wa Wizara hiyo Dk. Neema Rusimabayila akitoa ufafanuzi kuhusu Chanjo ya Homa ya Manjano na vitendo vya baadhi ya watumishi wa afya wasiowaaminifu ambao hulipwa fedha ili waweze kuwatengenezea wasafiri kadi za Chanjo ya Homa ya Manjano na kisha kuzitumia nje ya nchi jambo ambalo kinyume cha sheria na hatari kwa usalama wa Afya zao. Picha/Habari na Aron Msigwa – MAELEZO. 

MUSEUM ART EXPLOSION

death announcement and condolences

$
0
0
Dear friends, it is with extreme sadness that I am contacting you to inform you of the passing of our beloved mother Nargis Bhimji on August 10 at 6:10pm in White Rock, BC. 
We are in the process of arranging the funeral.  At the moment it is unlikely to occur on Thursday.  It will likely be on the afternoon of August 13. 
We ask that you say a prayer to remember a wonderful soul who is now back in heaven with our father, whom we lost in 2011.
Fazal, Arif, Iffat, Joy (Farhat), Jeff (Najaf)

604-644-7773
------------------------------------------------------
Salaam Alaikum – Dear Bhimji family,
 Our whole Alidina Family expresses our deepest condolences to you all for passing on of our beloved Cha Chi. 
We remember her fondly and as our school teacher lives with us forever. Her kindness, courtesies and thoughtfulness will never be forgotten.
 Our earnest prayer that her soul rest in eternal peace. We also pray for the family for strength and fortitude during this difficult period. Ameen.
 At any time, if we can be of any assistance, please do not hesitate to contact us and please let’s keep in touch.

With warm regards,
Alidina Family.
------------------------------------------
Salaam Alaikum.
 We just received word that the funeral will not be possible today.  
 The namaaz will be on Friday morning at 9am followed by procession to Forest Lawn Cemetery in Burnaby.  The estimated burial time will be 10am.  
 Please pass the word.
 Thank you.
 Bhimji Family

  

NMB YAZINDUA TAWI KATIKA JENGO LA ROCK CITY JIJINI MWANZA

$
0
0
Benki ya NMB imeendelea kutanua mtandao wa matawi yake nchini ili kuwa karibu zaidi na wateja wake. Mwishoni mwa wiki iliyopita, NMB ilizindua tawi jipya la NMB Rock City lililopo ndani ya jengo jipya la kibiashara la Rock City jijini Mwanza.

Tawi hili linafanya jumla ya matawi ya NMB kwa Mwanza mjini kufikia matano na 28 kwa kanda nzima ya ziwa ni imani ya NMB zinduzi huu unaleta tumaini jipya kwa wateja wa NMB jijini Mwanza na kanda ya ziwa kwa ujumla. Huduma zinazotolewa na tawi hili jipya ni pamoja na kufungua akaunti, mikopo, huduma ya fedha za kigeni, huduma za kuweka na kutoa fedha.

Katika kuhakikisha kuwa NMB inahudumia makundi mbalimbali ya wateja wake kulingana na mahitaji yao ya kifedha, wiki iliyopita, benki iliendesha mkutano wa Klabu ya Biashara uliowakutanisha pamoja zaidi ya wateja 300 wanaohudumiwa na matawi ya NMB ya jijini Mwanza. Baadhi ya faida zilizopatikana katika mkutano huo ni pamoja na mafunzo ya jinsi ya kukuza biashara, elimu ya mlipa kodi, jinsi ya kutunza daftari la biashara na njia mbalimbali za kuboresha biashara.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela (katikati) akikata utepe kuzindua tawi la Rock City Mall la benki ya NMB jijini Mwanza, wa tatu kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa NMB Bi Magreth Ikongo na wa tano kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Ineke Bussemaker.
Meneja wa NMB kanda ya ziwa- Abraham Augustino akiongea katika mkutano wa klabu ya biashara uliofanyika jijini Mwanza wiki iliyopita. Zaidi ya wateja 300 walihudhuria mkutano huo ambapo pamija na mambo mengine walipata mafunzo ya jinisi ya kukuza biashara, elimu ya mlipa kodi na njia mbalimbali za kuboresha biashara.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurungezi ya NMB- Margaret Ikongo akizungumza katika mkutano wa Klabu ya Biashara jijini Mwanza.

SHULE ZA FEZA HAZITAFUNGWA

$
0
0

UONGOZI wa  Shule za Feza nchini umeibuka na kukanusha taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii,  kuwa wao  hawana uhusiano na  Fethullah Gulen wala serikali ya Uturuki  kwa vile   hawajawahi kupokea misaada toka pande hizo mbili za uendeshaji na kuwa shule hizo hazitafungwa.
Kauli hiyo imetolewa baada ya hivi karibuni kuenea kwa uvumi kuwa shule za Feza  zipo hatarini kufungwa kwa madai kuwa  mmiliki wake ni yule aliyejihusisha na jaribio la kuipindua serikani nchini Uturuki.
Mwenyekiti wa Bodi wa Shule hizo, Habibu Miradji amesema Watanzania wanapaswa kufahamu kuwa Shule za Feza ni kama asasi  zingine zilizosajiliwa kishera na serikali, hivyo ni mali ya watanzania.
“Shule za Feza zitabaki kuwa kiwanda  cha kuzalisha wazalendo wa kitanzania  na raia bora wa duniani, hivyo wazazi wanapaswa kuondoa hofu,” alisema.
Alisema toka mwaka 1995 shule hiyo imepata mafanikio ya kujenga shule za awali tatu, shule za msingi mbili, sekondari tatu na shule ya kimataifa moja.
Aliongeza kuwa  huo ni uwekezaji  wenye mchango katika kukuza pato la taifa, kutoka awamu ya pili, tatu, nne hadi awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli.
\Alisema shule ya Feza ni hazina kwa Tanzania kwani shule zake zimekuwa zikishika nafasi ya 10 bora toka mwaka 2004 hadi leo.
Alisema  wanatoa  wito kwa wazazi  kuwasiliana na uongozi wa shule hiyo  kujua kinachoendelea kwenye shule husika kwa manufaa ya wanafunzi wetu na taifa bila kusikiliza uvumi huo unaoenezwa na watu wasiopenda maendeleo ya shule hizo.

LGBT VOICE TANZANIA MATATANI


SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

$
0
0
SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ametangaza kua waalimu wote wanatarajia kusafiri bure kwenye usafiri wa treni ya abiri jijini Dar es salaam.https://youtu.be/uuHgPBv1-cU

SIMU.TV: Taasisi ya sayansi na teknolojia ya Nelson Mandela inatarajia kuanza mradi wa kusafisha maji ya bwawa la Nadosaito wilayani Monduli ili wananchi wapate maji safi.https://youtu.be/jiqNgrflcxw

SIMU.TV: Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imetengua uamuzi uliotolewa na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu wa kufuta kosa la utakatishaji wa fedha kwenye kesi ya Hary Kitilya na wenzake. https://youtu.be/zB2tU_YAJbs

SIMU.TV: Baadhi ya shule mkoani Manyara zinaelezwa kukabiliwa na upungufu wa vyumba vya madarasa hali inayowafanya wanafunzi kusomea kwenye bweni katika shule ya  sekondari Engeno wilayani Simanjiro. https://youtu.be/-QEutPcpC84

SIMU.TV: Moto umeteketeza baa maarufu ya Carebean iliopo eneo la Sinza jijini Dar es Salaam na kusababisha uharibifu mkubwa. https://youtu.be/mLm4JR740zA

SIMU.TV: Shule ya msingi Msufini iliopo Mbagala jijini Dar es Salaam inakabiliwa na upungufu mkubwa wa madarasa kutokana na kuwa na wanafunzi wengi.https://youtu.be/qxC_K5GadzM

SIMU.TV: Uongozi wa bodi ya utalii nchini TTB umetembelea kampuni ya habari ya Africa Media Group ili kuangalia namna ya kushirikiana katika kukuza utalii wa ndani.https://youtu.be/maeWbvvau0s

SIMU.TV: Shirika la viwango nchini TBS limeanza mazungumzo ya uboreshaji wa matakwa ya viwango na wadau ili kuwa na bidhaa zenye viwango vinavyokubalika.https://youtu.be/mqf7_v5hyz0

SIMU.TV: TBS imekifunga kiwanda cha uzalishaji wa mikate cha Herry Bakery kutokana na kuzalisha bidhaa bila kuwa na nembo ya ubora. https://youtu.be/4D3lL1jx-jY

SIMU.TV: Ligi ya taifa ya mpira wa wavu inatarajiwa kuanza tarehe kumi na nane mwezi huu wilayani Kibaha mkoani  Pwani na itashirikisha timu kutoka mikoa mbalimbali.https://youtu.be/jb61SteedIE

SIMU.TV: Mashindano ya michezo mbalimbali yaliyoandaliwa na mbunge wa jimbo la Songea mjini yamehitimishwa kwa washindi kukabidhiwa zawadi zao.https://youtu.be/rYO_tKZOXF8

SIMU.TV: Meneja wa klabu ya Arsenal amesema hatma yake ya kuendelea kuifundisha klabu hiyo itategemea matokeo ya klabu hiyo msimu huu wa ligi kuu Uingereza.https://youtu.be/d6DNxIjl74w

CHEMSHA BONGO: HII TASWIRA INAPATIKANA WAPI???

Nyuzzzz bin Nyuzzzz katika Magazeti ya leo

EU yaipiga tafu Tume ya Taifa ya Takimu, yaipa Bil. 25 kusaidia kuboresha tasnia ya takwimu nchini

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji akionyesha Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa Tanzania mbele ya wadau mbalimbali wa takwimu hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa taarifa hiyo jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji akiongea mbele ya wadau mbalimbali wa takwimu hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa Tanzania jijini Dar es salaam.
Wadau mbalimbali wa takwimu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa Tanzania jijini Dar es salaam.

Na Ally Daud-Maelezo

Tume ya Taifa ya Takimu (NBS) imepokea msaada wa shilingi bilioni 25 kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kusaidia kuboresha tasnia ya takwimu kuhusu haki za watoto nchini.

Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Umaskini wa Watoto wa Tanzania Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Ashatu Kijaji amesema kuwa amepokea msaada huo kwa nia ya kuendeleza tasnia ya takwimu nchini na kusaidia malengo ya nchi ya miaka mitano.

“Tumepokea msaada huu kwa furaha na hamasa kubwa katika kufikia lengo letu la kuboresha na kukuza tasnia ya takwimu nchini ili kuweza kupata taarifa muhimu kwa ajili ya maendeleo ya miaka mitano ya nchi yetu”. Alisema Mhe. Kijaji.

Aidha Mhe. Kijaji amesema kuwa Wizara yake imewapa kipaumbele watoto kwa kutenga shilingi. Bilioni 18 kila mwezi ili kuwasaidia katika mambo muhimu ya kila siku hususani elimu bora, makazi na malazi.

Mbali na hayo Mhe. Kijaji ameshukuru na kuwapongeza Umoja wa ulaya kwa msaada huo na kuwataka wasichoke kuwa nao pamoja katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu ya mwaka 2030.

Kwa upande wa Mwakilishi wa Balozi wa Umoja wa Ulaya Bw. Eric Beaume Amesema kuwa msaada huo sio mwisho wao kwani wanapenda kazi ya NBS na matokeo yake hivyo wapo tayari kutoa kiasi kikubwa zaidi ili kuwezesha tume hiyo kutoa takwimu zenye uhakika kwa maendeleo ya Tanzania.

Bw.Beaume amesema kuwa Umoja wao utakua bega kwa bega na Tanzania katika kutoa misaada ili kusaidia haki zote za watoto ili kujenga taifa lenye tija na muamko wa kimaendeleo kutokana na takwimu zitokanazo na tume hiyo.

Aidha Bw. Beaume ameongeza kuwa Umoja wao upo tayari kusaidia Nyanja za kilimo, Nishati katika maeneo ya vijijini ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu kwa miaka mitano ijayo.

Mbali na hayo Mkurugenzi Mkuu wa NBS Dkt. Albina Chuwa amesema kutokana na msaada huo wamepata hamasa kubwa kwa tume hiyo kuweza kupambana na kupata takwimu yakinifu zitazopelekea kuleta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali yahusuyo jamii nchini na kufikia malengo ya miaka mitano.

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI DARAJA WA WAENDA KWA MIGUU LA FURAHISHA PAMOJA NA UPANUZI WA BARABARA YA MWANZA AIRPORT

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katikati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha pamoja na upanuzi wa barabara ya Mwanza-airport.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani, Mbunge wa Sumve Richard Ndassa wakipiga makofi mara baada ya tukio la uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha pamoja na Upanuzi wa barabara ya Mwanza-airport.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale akitoa maelezo ya namna daraja la Furahisha litakavyokuwa mara baada ya kukamilika.

Viewing all 110025 articles
Browse latest View live




Latest Images