Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

HALMASHAURI YA IKUNGI YAPATIWA ZAIDI YA SHILINGI MIL. 900 KUJENGA DARAJA LA MINYUGHE

$
0
0
SERIKALI imeipatia Halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida zaidi ya shilingi milioni mia tisa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa daraja la mto Saiwa, uliopo katika Kijiji cha Minyughe, tarafa ya Ihanja,wilayani Ikungi ili kuwanusuru wananchi wa vijiji vya Minyughe, Majengo, Mayaha, Mtavira na Mteva wasipoteze maisha yao kwa kusombwa na maji yanayosafiri kupitia mto huo.

Kukosekana kwa daraja hilo kwa zaidi ya miaka kumi sasa kumechangia watu na mifugo kupoteza maisha, magari kusombwa na maji yanayosafiri kupitia kwenye mto huo.

Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Minyughe na Misake, tarafa ya Ihanja, wilayani hapa, Mbunge wa jimbo la Singida magharibi, Elibariki Kingu aliweka bayana kwamba gari moja la Kampuni ya vinywaji baridi la Pepsi, lilizama na kisha kudidimia kwenye mchanga ambapo mpaka leo halijaweza kutolewa.
Mmoja wa wananchi wanaosafirisha mizigo yao kwa kutumia usafiri wa baiskeli akijaribu kuvuka katika eneo la mto huo ambao kwa sasa umekauka kama alivyonaswa na kamera ya mwandishi wa wetu.

Mbunge huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa daraja hilo iwapo Mkandarasi wake ameanza shughuli za ujenzi wa daraja hilo.

Kwa upande wake Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauri hiyo,Haruna Mbegalo licha ya kukiri Halmashauri ya wilaya hiyo kupokea fedha za ujenzi wa daraja hilo,lakini alitofautiana na Mbunge huyo kwa kudai kuwa Halmashauri hiyo imepokea zaidi ya shilingi milioni mia saba kwa ajili ya shughuli hizo.

“Tatizo la mto Minyughe au mto saiwa tunalishughulikia, Mkandarasi ameshapatikana,ameshaonyeshwa site na ameanza zile taratibu za awali na sasa hivi alikuwa anasubiri maji yapungue au mto ukauke ili aweze kuanza shughuli za ujenzi”alifafanua Mhandisi Mbegalo.
Kwa mujibu wa Mhandisi huyo kiasi hicho cha zaidi ya shilingi milioni mia saba zilitengwa katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita wa 2015/2016 na kwamba shughuli za ujenzi huo zimekwishaanza kwa kufanyika kwa upembuzi yakinifu ambapo mpaka sasa zaidi ya shilingi milioni 103 zimetumika.

Hata hivyo akizungumzia suala la fidia kwa wananchi waliokuwa wakiishi kuzunguka eneo la mto huo wanaotakiwa kuhama kupisha mradi huo,Mhandisi Mbegalo alikiri kuwa hakuna fedha zozote zilizotengwa kwa ajili ya kuwalipa wananchi hao.

Wakizungumzia madhara yaliyopatikana na ambayo endapo daraja hilo halitajengwa yataendelea kutokea,baadhi ya wananchi wa Vijiji hivyo waliyataja kuwa ni pamoja na kukwama kwa magari ya abiria na mizigo pamoja na binadamu na mifugo kupelekwa na maji yanayopita kwenye mto huo.

Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi sasa zaidi ya magari ya mizigo 15,mabasi ya abiria 5,wanyama wafugwao zaidi ya 50 walisombwa na maji huku magari yakizama kwenda chini ya maji na kushindikana kuvutwa.
Muonekano wa sasa ukiwa umekauka mto Saiwa uliopo katika Kijiji cha Minyughe,Tarafa ya Ihanja,wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida ambao ni tishio kwa watu wanaopia katikati ya mto, magari ya mizigo, magari ya abiria pamoja na mifugo inayokwenda kunywa maji.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Minyughe,tarafa ya Ihanja waliokutwa wakinywa maji kwenye mto Saiwa walipokuwa wakirudi kutoka shuleni wakienda nyumbani baada ya masomo yao ya asubuhi.(Picha zote Na.Jumbe Ismailly).

MATARUMA YA KIWANDA CHA KONGOLO CHA TAZARA-MBEYA KUJENGA RELI YA KISASA.

$
0
0
Serikali imesema itatumia kiwanda cha Kongolo cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kilichopo Mbeya kuzalisha mataruma yatakayotumika kwenye ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) inayotarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni ili kupunguza gharama.

Hayo ameyasema Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alipotembelea kiwanda hicho kuona utendaji kazi na  uzalishaji unaopatikana na kuiagiza kamati maalumu ya ujenzi wa reli hiyo kutembelea kiwandani hapo kuangalia uwezo wa uzalishaji wa kiwanda hicho.

Profesa Mbarawa amesema Serikali ina dhamira ya kufufua viwanda hapa nchini ili kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania na kuifikisha nchi katika uchumi wa kati kupitia mapinduzi ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

"Nitahakikisha mkandarasi atakeyejenga reli hii anatumia mataruma yatakayozalishwa katika  kiwanda hiki, badala ya kuagiza vifaa vya ujenzi kutoka nchi za nje", amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa kwa kutumia kiwanda hicho Serikali itaokoa pesa ambazo zitaisaidia TAZARA kujiongezea mapato yatakayotokana na matengenezo ya mataruma na kupanua wigo wa kibiashara kwa wateja wa ndani na nje ya nchi.

Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amekagua maabara ya kupima viwango na ubora wa kokoto na nondo kilichopo kiwandani hapo na kutoa mwezi mmoja  kwa TAZARA kupata cheti cha ukaguzi kutoka Shirika La Viwango (TBS), ili iweze kurasimishwa rasmi.

Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa kuzalisha mataruma katika Kiwanda Cha Kongolo cha TAZARA-Mbeya Eng. Boniface Phiri amesema kuwa fursa ya kuwa sehemu ya mradi wa ujenzi wa reli ya Kisasa itaongeza uzalishaji wa kiwanda na kukuza pato la Mamlaka. "Kwa kushirikiana na wenzetu tutaongeza vifaa ili tuweze kuzalisha kwa wingi na ubora unaotakiwa katika mradi huu", amesema Eng. Phiri.

Kiwanda cha Kongolo ni kiwanda pekee katika nchi za Afrika na kati kinachozalisha mataruma kwa ajili ya reli na kina uwezo wa kuzalisha mataruma elfu ishirini na  nne kwa mwaka. Waziri Prof. Mbarawa yupo katika ziara ya kukagua miundombinu ya reli, barabara na mawasiliano mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa(Kushoto) akitoa maelekezo kwa Afisa Mfawidhi Kutoka Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) Bw.Denis Daudi, wakati alipokagua huduma za mabasi katika kituo cha nane nane Mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili Kushoto), akikagua moja ya kifaa kinachotumika kwenye Reli wakati alipotembelea kiwanda cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia(TAZARA), Kongoro Qwarre kilichopo Mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kushoto) akikata moja ya kifaa kinachotumika kujengea reli wakati alipotembelea kiwanda cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia, Kongoro Qwarre kilichopo Mkoani Mbeya.

KATIBU MKUU MALIASILI NA UTALII AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA HIYO KUMUAGA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU, SAID MSAMBACHI

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA RASMI KESHO NCHINI RWANDA, JWTZ WAWASILI SALAMA MJINI KIGALI

$
0
0
Na Selemani Semunyu, JWTZ

Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho.

Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.

“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.

Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo

Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.

Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.

“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali Nyamvumba.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika.
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Leo Jumatatu Agosti 8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ.
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ akifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).
Baadhi ya Viongozi na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho (Leo) katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).

Mashindano ya MPINGA CUP 2016 kuanza kutimua vumbi Agosti 12

BWAWA LA MAINI LILIVYOITANDIKA BILA HURUMA TIMU YA DUNIA MABAO 4-0 KATIKA DIMBA LA WEMBLEY

$
0
0
Ulikuwa usiku mujarabu kwa vijana wa Jurgen Klopp, Liverpool ndani ya dimba la Taifa la Ungereza,Wembley baada ya kuisambaratisha bila huruma bingwa wa Laliga Barcelona kwa mabao 4-0 na kuwaacha mashabiki wengi wa soka Ulimwenguni wasiamini walichokiona na kukisikia.

Wakicheza kwa kujituma huku wakifahamu wazi kuwa wanacheza na timu bora kabisa duniani, wachezaji wa Liverpool walihakikisha hawawapi nafasi wapinzani wao kumiliki mpira kwa kuingilia pasi zao,dakika ya 14, Lalana anamnyang'anya mpira Alex Vidal na kumpa pasi Firmino ambaye anamrudishia Lalana naye anampa tena Sadio Mane na bila ajizi anaukwamisha mpira huo wavuni,1-0.

Goli hilo linadumu hadi mapumziko, kipinndi cha pili kilipoanza inachukuwa dakika moja tu Liverpool wanaandika bao la pili kwa beki Mascherano kujifunga akiwa katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Sadio Mane. 

Dakika moja baadaye yaani dakika ya 47, Stewart anampokonya mpira Busquets na kumpenyezea pasi murua Diovick Origi anayewazidi mbio Gerard Pique na Mascherano nakupiga shuti linalopita katikati ya miguu (tobo) ya kipa wa Barcelona Terstegen. 3-0.

Katika kipindi hiki timu zote zilifanya mabadiliko ya wachezaji zaidi ya 6 kwa kila timu, na hapo Barcelona walitawala zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Liverpool lakini ngome ya Liverpool ambayo iliongozwa na Lovren ilicheza kwa nidhamu ya hali ya juu na kufanikiwa kuzuia hatari zote.

Watu wakiamini kuwa mchezo unamalizika kwa hayo mabao matatu, Dakika ya 92 yaani dakika moja kabla ya mpira kumalizika kwa zile dakika za nyongeza Liverpool wanapora mpira katikati ya uwanja na kufanya shambulizi la kushitukiza, ambapo mpira wa krosi unapigwa na Markovic unatua kichwani kwa Grujic na kuupiga pembeni juu ya kona ya goli, waswahili hupenda kuita "anapotagia ndege" na mpira huo kutinga wavuni na kuandika bao la nne, hivyo kuhitimisha karamu hiyo ya mabao.4-0.

WAKAZI WA MBEYA WANUFAIKA NA GULIO LA SIMU LA BEI CHEE ZA VODACOM TANZANIA

$
0
0
Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania, Lawreny Vimenty(kulia) akimkabidhi John Mwalusako simu aliyonunua jana katika Gulio la simu linaendeshwa na kampuni hiyo, katika kituo cha mabasi cha nane nane wakati wa maadhimisho ya wakulima Nane nane yanayoendelea katika uwanja John Mwakangale jijini Mbeya.
Wacheza shoo wakiendelea kutoa burudani kwa wateja waliofika kwenye Gulio la simu lililoendeshwa na Vodacom Tanzania,katika kituo cha mabasi cha nane nane wakati wa maadhimisho ya wakulima Nane nane yanayoendelea katika uwanja John Mwakangale jijini Mbeya.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania(wenye flana nyeusi) wakitoa huduma mbalimbali kwa wateja waliofurika katika Gulio la simu liloandaliwa na kampuni hiyo,katika kituo cha mabasi cha Nane nane nje ya viwanja vya maonyesho ya wakulima Nane nane maarufu John Mwakangale.

WAZIRI MKUU MAJALIWA USO KWA USO NA ASKOFU GWAJIMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Uzima na Ufufuo katika hafla ya harusi ya Naibu Katibu Mkuu wa Sheria na Katiba, Amon Mpanju na mkewe Analises iliyofanyiak kwenye ukumbi wa jeshi wa Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Amon Mpanju akilishwa keki na mkewe , Analises katika tafrija ya harusi yao iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary walihudhuria katika tafrija hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Amon Mpanju akimlisha keki mkewe , Analises katika tafrija ya harusi yao iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary Walihudhuria katika tafrija hiyo.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWASILI MKOANI LINDI TAYARI KWA MAADHIMISHO YA KILELE CHA SIKU YA WAKULIMA NANENANE KESHO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Lindi mchana huu akitokea mkoa wa Dar es Salaam kwa njia ya barabara ambapo hapo kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha   Sikukuu ya Wakulima Nanenane kitaifa kwenye viwanja wa Ngongo katika Manispaa ya Lindi.


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufunga maonyesho hayo ya Nane nane hapo kesho kwa  niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Pombe Magufuli.


Alipowasili ikulu ndogo mjini Lindi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan  amepokelewa na Mkuu wa mkoa wa LINDI Godfrey Zambi pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na wa vyama vya siasa.


Katika Msafara wake, Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Kilimo, Maliasili na Uvuvi wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mstahiki Meya wa Lindi mjini Ndugu Mohamed Liumbwe mara baada ya kuwasili mkoani Lindi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivishwa skafu wakati wa mapokezi na Vijana wa mkoa wa Lindi .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Wakina Mama wa mkoa wa Lindi wakimuimbia nyimbo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa mapokezi mkoani hapo.
 Wakina Mama wa mkoa wa Lindi wakimuimbia nyimbo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa mapokezi mkoani hapo.

PROF MUHONGO AANDAA MASHINDANO YA NYIMBO ZA KWAYA JIMBO LA MUSOMA

$
0
0

Vikombe Vya washindi wa Nyimbo na Kwaya katika Jimbo la Musoma Vijijini. Mashindano hayo yameandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo Kwa ajili ya kusheherekea sherehe za NANE NANE katika Jimbo hilo. Mashindano hayo yanezinduliwa Leo Tarehe 7/8 kwa Nyimbo za Kwaya na Kumalizika Kesho Kwa Ngoma za utamaduni. Washindi wa kwanza hadi 3 watapewa Kombe na Fedha Taslimu (Mshindi wa kwanza 1,000,000, wa Pili 600,000 na wa tatu 400,000).

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASILI MBEYA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya Agosti 7, 2016 ambako Agosti 8, 2016 atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane
   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakipokea heshima kutoka kwa Skauti wa Mbeya baada ya kuwasili kwenye uwanja wa  Songwe Agosti 7, 2016 ambako Agosti nane atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakifurahia ngoma baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya Agosti 7, 2016 ambako  Agosti 8, 2016 Mheshimiwa Majaliwa atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makla. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

ZANZIBAR YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya Arusi Said Suleiman wa kwanza (kulia) akizungumza na akinamama waliohudhuria maadhimisho ya kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani katika kijiji cha Mwera Wilaya ya Kati Unguja.

Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar  

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) limesisitiza umuhimu kwa Tanzania kuongeza juhudi katika kuweka mikakati ya kuboresha unyonyeshaji wa watoto mara tu baada ya kuzaliwa hadi kufikia miaka miwili.

Akitoa salamau za kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani iliyoadhimishwa katika kijiji cha Mwera Wilaya ya kati Unguja,  Afisa Lishe kutoka  UNICEF  Dar es Salam, Elizabeth Macha  alisema utafiti wa 2014 unaonyesha  ni mtoto mmoja kati ya wawili wenye umri hadi kufiki miezi 23 wanaonyonyeshwa mara baada ya kuzaliwa kwa Tanzania.  
       
Alisema kwa Zanzibar ni asilimia 61 tu ya watoto wenye umri kati ya miaka 0-23 wanaonyonyeshwa katika muda wa nusu saa baada ya kuzaliwa na Mkoa wa Kusini Pemba upo nyuma  zaidi ukiwa na asilimia 52.

Aliongeza kusema kuwa watoto wakicheleweshwa kunyonyeshwa kwa masaa 2 hadi 23 baada ya kuzaliwa inaongeza hatari ya kufa katika siku 28 za kwanza za maisha ya mtoto kwa asilimia 40.

Watoto wamiminika kambi tiba ya vichwa vikubwa ya GSM na MOI Songea

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,
Zaidi ya watoto 50 leo wamehudhuria kambi tiba ya GSM Foundation inayoendeshwa kwa ushirikiano na Taasisi ya Mifupa na upasuaji ya MOI, yenye lengo la kupunguza vifo na mtindio wa ubongo kwa watoto wanaozaliwa na vichwa vikubwa na mgongo wazi, ambayo leo imeingia katika mkoa wa pili katika msimu wake wa pili pia, wenye lengo la kuwafanyia upasuaji watoto 100.

Kaimu Mkuu wa kambi hiyo iliyoanzia mkoani Mtwara Jumanne ya tarehe 2 mwezi huu, DK Shaaban Hamis, amesema, muiyikio walioupata katika mkoa huu ni muitikio mkubwa zaidi ukilinganisha na mkoa wa Mtwara, ambako ndio kunakosadikika kuwa na wagonjwa wengi zaidi, kutokana na rekodi waliyonayo, baada ya tafiti mbali mbali.

"Inawezekana hapa tukafanyia upasuaji wagonjwa hata 50 kwa siku hizi tatu tutakazokuwepo, na labda tukavuka lengo katika mikoa iliyobaki ya Iringa na Mbeya ambayo ndio ya mwisho katika msimu huu wa pili", alisema Dk Shaaban.

Kwa upande wake Afisa uhusiano wa Taasisi ya GSM ambayo kwa mwaka huu imewekeza zaidi kusaidia sekta ya Afya na Elimu amesema wanafarijika kuona wagonjwa wanakwenda kutibiwa kama walivyodhamiria, maana ndio lengo haswa, kusaidia kupunguza vifo vya watoto ambao wanasadikika kuzaliwa 4000, kwa mwaka lakini kati yao, ni asilimia 25 tu hurudi hospitalini kwa matibabu huku asilimia 75 wakishindwa kutokana na sababu za kiuchumi.

Tiba pekee kwa mtoto mwenye kichwa kikubwa, ama mgongo wazi ni upasuaji, tiba ambayo gharama zake ni kuanzia shilingi laki tatu za kitanzania, mpaka milioni moja, kulingana na ubora wa vifaa ama hospitali anayotibiwa mgonjwa.

Tanzania ina madaktari Bingwa tisa tu wenye uwezo wa kufanya upasuaji wa namna hii ambapo nane wanafanya kazi MOI na mmoja anafanya kazi katika Hospitali ya Bugando jijini Mwanza huku mikoa mingine yote ikiwa haina madaktari wa namna hii.
Wagonjwa wakisajiliwa katika chumba maalum cha kuwapokea katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma 
 ...kazi ya upasuaji ikiendelea maabara
Dk Shaaban Hamis, Naibu Mkuu wa Msafara akiwa kazini

WANANCHI WANATAKIWA KUFUGA KUKU NA SIO KUISHI NA KUKU

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akikagua kuku waliofungwa kisasa ambapo jogoo mmoja aliyefikisha umri wa mwaka mmoja anauzwa shilingi 20,000.

Na Mathias Canal

Wananchi wametakiwa kujihusisha na ufugaji wa kuku kwa njia za kisasa ili waweze kujipatia kipato kupitia mayai ama kuuza kuku mwenyewe ili kuondokana na dhana ya kuishi na kuku ilihali wanajigamba kama wafugaji wazuri.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida Miraji Jumanne Mtaturu alipotembelea banda la Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi katika maonesho ya Nane nane yanayofanyika katika Uwanja wa Nzuguni Kanda ya Kati Dodoma ambayo yanataraji kufikia kilele hapo kesho.

Mtaturu amesema kuwa asilimia kubwa ya wananchi Wilayani humo na Taifa kwa ujumla wanajihusisha na shughuli za Kilimo na ufugaji lakini aina ya ufugaji wanayoitumia ni ile iliyopitwa na wakati ya kuishi na mifugo ndani badala ya kuijengea eneo la banda ambalo ni pana na maalumu kwa ajili ya ufugaji.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akipata maelekezo ya ufugaji wa kisasa wa kuku  kutoka kwa mfugaji aliyefanikiwa katika ufugaji Madai Njou anayetokea Kijiji cha Nyangwe, Kata ya Iseke baada ya kupatiwa mafunzo kutoka Idara ya Kilimo na ufugaji ya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.

Dc Mtaturu amewataka wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi katika idara ya kilimo kutoa elimu kwa wananchi juu ya mazao makuu ya biashara yanayostahimili mvua ili kupata mazao ya kutosha na kuyauza kwa wakati tofauti na mazao mengine ambayo yanalimwa kila maeneo hivyo kupunguza gharama halisi ya bei.

Amewataka pia wataalamu hao kuhakikisha elimu wanayoitoa kwa wananchi inakuwa sambamba na kuwashauri wananchi kulima zao la mtama wa muda mfupi aina ya Hakina na Macia.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akikagua Tomato Saurce inayotengenezwa na mjasiriamali Rehema F. Maliwa na nyanya aina ya Tanya.

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayoub Yusuph amesema kuwa ofisi yake itatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na mkuu wa Wilaya hiyo ili kuwainua zaidi wananchi ambao wanalima na kufuga lakini sio kilimo na ufugaji wa kisasa jambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo.

Yusuph alisema kuwa katika maonesho hayo wamewaalika wakulima na wafugaji ambao wamefanikiwa katika kilimo na ufugaji wao baada ya kupata mafunzo kutoka katika ofisi yake ili kushuhudia na kuelezea mbinu walizopatiwa na namna zilivyowasaidia.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILI JIJINI MBEYA LEO

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya Agosti 7, 2016 ambako Agosti 8, 2016 atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakipokea heshima kutoka kwa Skauti wa Mbeya baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Songwe Agosti 7, 2016 ambako Agosti nane atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkewe Mary wakifurahia ngoma baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya Agosti 7, 2016 ambako Agosti 8, 2016 Mheshimiwa Majaliwa atahitimisha maonyesho ya wakulima Nanenane. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makla. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

NAIBU WAZIRI WA MAJI ATEMBELEA BANDA LA AICC KWENYE MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MKOANI LINDI

$
0
0
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) kilipata fursa ya kutembelewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe kwenye maonesho yanayoendelea ya wakulima NaneNane Kitaifa katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

Akiwa kwenye banda la AICC Mhe.Mhandisi Kamwelwe aliweza kupata taarifa juu ya shughuli na huduma zinazotolewa na Shirika hili la Umma ambalo limesimama imara toka kuanzishwa kwake mwaka 1978. Pamoja na kupongeza utendaji mzuri wa Kituo katika shughuli za utalii wa mikutano, alisisitiza umuhimu wa AICC kuendelea kutangaza vivutio vilivyopo Tanzania.

Mbali na kushiriki kwenye maonesho ya NaneNane, AICC pia ilipata mualiko wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi, Bw.Jomaary M. Saturi kwenye hafla fupi ya kuelezea fursa za uwekezaji zinazotarajiwa kufanyika Mkoa wa Lindi kutokana na ugunduzi wa gesi na viwanda vinavyotarajia kujengwa.

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo ambapo alitoa wito kwa AICC kuwekeza katika sekta ya utalii wa mikutano kwa kujenga Kituo cha Mikutano cha kisasa Mkoa wa Lindi kwa kuwa hakuna kabisa kumbi za kisasa zitakazoweza kukidhi mahitaji yatokanayo na uwekezaji mkubwa unaotarajiwa.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mh. Isack Kamwelwe akisisitiza jambo wakati alipotembelea banda la AICC, Maafisa wa AICC na JNICC wakimsikiliza kwa makini.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Mhandisi Isack Kamwelwe akiweka saini kitabu cha wageni alipotembelea banda la AICC kwenye maonesho ya NaneNane Lindi.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe.Godfrey Zambi akizungumza wakati wa kikao na wadau mbalimbali kwenye wa hafla ya uwekezaji iliyofanyika ukumbi wa Andrew Kagwa, Lindi.
Maafisa kutoka AICC wakisikiliza kwa makini wakati wa hafla ya uwasilishaji wa fursa za uwekezaji zinazopatikana Mkoa wa Lindi. Kutoka kulia ni Afisa Mkuu Masoko na Utafiti wa AICC Bi.Linda Nyanda na Afisa Itifaki na Uhusiano wa JNICC Bi.Beatha Hyera.

MAANDALIZI SIMBA DAY YAKAMILIKA, VIINGILIO VYATAJWA

$
0
0
 Klabu ya Simba inayo furaha kubwa sana kuwaarifu kuwa imeshakamilisha maandalizi yote ya mechi ya kesho dhidi ya timu ya AFC Leopards ya nchini Kenya, Mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Taifa uliopo Dar es salaam

Mechi hiyo ya kimataifa itatanguliwa na burudani mbali mbali za muziki zitakazoongozwa na bendi ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta pamoja na wasanii wa muziki wa kizazi kipya.

Mbali ya burudani hizo.pia kutakuwa na shamra shamra nyingine.zitakazonegesha kilele cha wiki ya sherehe zetu zinazojulikana kwa umaarufu wa Simba Day.

Klabu pia itatumia mechi ya kesho kuwatambulisha wachezaji wote watakaotumika kwenye msimu ujao wa ligi 2016|17.wakiwemo wale wapya waliosajiliwa msimu huu.

Sanjari na hayo kesho tutazindua rasmi jezi mpya za msimu na pia zitaanza kuuzwa pale uwanjani Taifa kwa thamani ya shilingi elfu ishirini kwa jezi moja.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda ataongoza viongozi mbali mbali wa kitaifa kwenye sherehe hizo muhimu ambazo pia ni maadhimisho ya miaka themanini toka kuanzishwa kwa klabu yetu.

Kiingilio kwenye mechi hiyo ni shilingi 5,000 kwa mzunguko.10,000 kwa viti vya orange.15, 000 kwa VIP C. 20, 000 kwa viti vya VIP B na shilingi 25, 000 kwa VIP A.

Tunawaomba sana watu watakaokuja uwanjani kesho wajihadhari na matukio yote yatakayoashiria uvunjifu wa amani.ili kutoa fursa kwa watu kupata burudani na kuona kwa raha mchezo huu muhimu ambao ni sehemu ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom na kombe la Shirikisho.

Imetolewa na 
HAJI S.MANARA
MKUU WA HABARI
SIMBA SC

SIMBA NGUVU MOJA

HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI

RAIS DKT. MAGUFULI ASALI KATIKA KANISA LA BIKIRA MARIA PAROKIA YA CHATO, PIA ATEMBELEA KANISA LA ANGLIKANA, AIC PAMOJA NA MSIKITI WA OMAR BIN-L-KHATTAB CHATO MKOANI GEITA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakisali katika ibada ya Jumapili katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waamini wa kanisa Katoliki wa Parokia ya Chato mara baada ya Ibada katika kanisa hilo Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihamasisha mchango wa ujenzi wa Kanisa jipya la la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.

Shekhe wa Bakwata Wilaya ya Chato Hassan Issa Mnubi akiongoza dua ya Kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli nje ya Msikiti wa Omar Bin-L-Khattab Chato Mkoani Geita. 
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI


Sura za Magazeti ya Leo

Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images