Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109591 articles
Browse latest View live

Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Songwe akutana na wajumbe wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa CCM Wilaya ya Songwe

0
0
Na Mwandishi Wetu, Songwe. 

Mbunge Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza amesema wanawake wa mkoa huo ni nguvu kuu, wazalishaji mali wakubwa na wenye ushawishi katika familia, hivyo amewataka kukaa na vijana wao kuwaeleza maadili mema na umuhimu wa kudumisha amani iliyopo na kufanya kazi kwa bidii ili kuondokana na utegemezi usiokuwa na tija.

Shonza alitoa rai hiyo, jana wakati akizungumza na wajumbe wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (Uwt) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songwe, alipokutana nao kujadili na kupeana mikakati ya wanawake hao kuanzisha na kujiunga kwenye vikundi vya ujasariamali kwa kila kata kuweza kuanzisha miradi mbalimbali ya kuwaingizia kipato katika familia.
Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza (CCM) akilakiwa na wajumbe wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (Uwt) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songwe, jana alipokutana nao mji mdogo wa Mkwajuni.Shonza alikutana na wanawake hao ili kujadili na kupenana mikakati ya kuuunda na kuimarimasha vikundi vya ujasiriamali.

Alisema wanawake na watoto ndio waathirika wa kwanza endapo amani itatoweka eneo husika, lakini pia ndio wenye ushawishi mkubwa kuhakikisha wanawaweka sawa vijana wao, kutambua umuhimu wa kuipigania amani isivurugwe.

“Mtoto wenu leo nimekuja kuwashukuru kwa kunichagua kuwa mwakilishi wenu bungeni. Na nimekuja na mkakati wa kutaka nyinyi mjiunge kwenye vikundi vya ujasiriamali kwenye kata zenu. Lakini niseme ni lazima tukumbuke kuilinda amani iliyopo. Wanawake tuhakikishe tunakaa na vijana wetu tuwaeleze maadili mema, tusiache wakavurugwa akili na mwisho wa siku wanakuja kuvuruga amani.
Mbunge Viti Maalumu, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza, akizungumza na wanawake wa Baraza la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songwe, jana alipokutana nao mji mdogo wa Mkwajuni. Shonza alikutana na wanawake hao ili kujadili na kupenana mikakati ya kuuunda na kuimarimasha vikundi vya ujasiriamali.

Kwani hata amani ikitoweka hata hii mipango tunayopanga leo ya kuanzia miradi kwenye kata zetu haitafanikiwa kwakuwa kila mmoja atakuwa mafichoni. Hivyo niwaombe tujikite kwenye ujasiriamali huku tukidumisha amani yetu,” alisema Mbunge Shonza.

Kuhusu uanzishwaji wa vikundi vya ujasiriamali, Shonza alisema tayari ametoa Sh30,000 kwa kila Kata kwa ajili ya kusajilia vikundi watakavyounda lakini pia alitoa mtaji wa Sh200,000 kwa kila kata husika za kuanishishia miradi watakayokuwa wameibuni na baada ya kukamilisha zoezi hilo sasa atarajia kuanza kupeleka elimu ya ujasriamali kwa wanawake hao ambapo atawatafutia wataalamu wa masuala ya elimu.
Mbunge Viti Maalumu, Mkoa wa Songwe, Songwe Juliana Shonza, akiwa amepiga magoti akiwasalimia wanawake wa Umoja wa Wanawake Tanzania (Uwt), wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Songwe jana alipokutana nao mji mdogo wa Mkwajuni.Shonza alikutana na wanawake hao ili kujadili na kupenana mikakati ya kuuunda na kuimarimasha vikundi vya ujasiriamali.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Songwe, Samuel Opulukwa na Mbunge wa Jimbo la Songwe, Philip Mulugo walisema kina mama ndio wenye ushawishi mkubwa katika mambo mbalimbali ya kijamii hivyo waliwaahidi kuhakikisha vikundi watakavyounda kwa kushirikiana na Shonza vinakuwa endelevu na vyenye tija.

Opulukwa alisema ‘Kina mama mimi ni mgeni kabisa hapa Songwe, na mipango yangu ni kupiga vita umasikini Songwe, hivyo nimefajirika sana kuona Mnbunge Shonza amekuja na mikakati ambayo ndio kipaumbele change na katika hili ninawaahidi kuwapa ushirikiano kwa hatua mnayofanya, mkikwama sio lazima mmpigie simu Shonza, njoo kwangu kwanza’.
Mbunge Viti Maalumu, Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza (CCM) akiserebuka muziki na Wajumbe wa Umoja wa Wanawake Tanzania (Uwt) wa Chama cha Mapinduzi 9CCM) Wilaya ya Songwe, jana alipokutana nao mji mdogo wa Mkwajuni.Shonza alikutana na wanawake hao ili kujadili na kupenana mikakati ya kuuunda na kuimarimasha vikundi vya ujasiriamali.

Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Songwe na Chunya, Mboka Konzo alisema Mbunge Shonza amekuja na ukombozi wa kiuchumi kwa mwanamke wa Songwe na mkoa kwa ujumla katika muda mwafaka na wao kama viongozi watahakikisha wanamtumia Shonza kwenye mipango ya kimaendeleo na si vinginevyo.

Aliwataka madiwani wa viti maalumu kwa kila kata kuhakikisha wanakuwa walezi wa karibu kwenye vikundi hivyo na kuwasaidia wanakikundi pindi wanapokwama kwa kufanya mawasiliano na viongozi wa ngazi juu kwa tatizo lolote ili mradi usiweze kukwama.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA RAIS WA BENKI YA EXIM YA CHINA IKULU NDOGO YA CHAMWINO MKOANI DODOMA.

0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Benki ya Exim ya China Liu Liang katika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais wa Benki ya Exim ya China Liu Liang  wa kwanza kulia katika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma. Wakwanza kushoto ni Balozi wa China hapa nchini Lu Youqing.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha pamoja na ujumbe wa Rais wa Benki ya Exim ya China Liu Liang katika Ikulu ndogo ya Chamwino mkoani Dodoma.
PICHA NA IKULU.

WAZIRI MWAKYEMBE AKUTANA NA WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA MSAADA WA KISHERIA.

0
0
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria, Dkt. Harrison Mwakyembe ( wanne toka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Sekretarieti ya Msaada wa Kisheria (LAS) baada ya kumaliza mazungumzo nao ofisini kwake jijini Dar Es Salaam 19/7/16.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza katika kikao na watumishi wa Sekretarieti ya Msaada wa Kisheria (LAS) kilichofanyika ofisini kwake jijini Dar Es Salaam, 19/7/16.

MWIGULU NCHEMBA ASHIRIKI KONGAMANO LA VIONGOZI WA DINI, AWATAKA WASHIRIKIANE NA SERIKALI KUPAMBANA NA UHALIFU NCHINI

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (wapili kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Baraza la Kuu la Waislamu (BAKWATA), Suleman Said Lolila wakati Waziri huyo alipokuwa anawasili katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, kwa ajili ya kushiriki Kongamano la Viongozi wa Dini lililojadili masuala ya ugaidi. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara hiyo, Marlin Komba, na wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Dk Leonard Mtaita.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba akizungumza na viongozi wa dini kuhusu masuala mbalimbali ya amani nchini katika Kongamano la Viongozi wa Dini lililofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam. Katika hotuba yake, Waziri Mwigulu aliwataka viongozi hao kutokuhusisha kosa lifanyalo na mtu au watu fulani kulifananisha na dini yake, amewaomba viongozi hao watoe ushirikiano kwa kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu nchini. Kutoka kulia ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora, Paul Ruzoka, Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakary Zubeiry Bin Ally na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Dk Leonard Mtaita.
Sehemu ya viongozi wa dini walihudhuria katika Kongamano la Viongozi wa Dini nchini lililofanyika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (hayupo pichani), lilijadili masuala mbalimbali ya ugaidi pamoja na ushirikiano wa dini mbalimbali nchini. Hata hivyo Waziri Mwigulu aliwataka viongozi hao kutokuhusisha kosa lifanyalo na mtu au watu fulani kulifananisha na dini yake, amewaomba viongozi hao watoe ushirikiano kwa kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu nchini.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (watatu kulia) akiandika maelezo ya hotuba ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Dk Leonard Mtaita (kushoto) katika kongamano la viongozi wa dini lililofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo lilijadili kuhusu ugaidi na ushirikiano wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini. Kulia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT Mstaafu, Alex Malasusa. Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakary Zubeiry Bin Ally (wapili kushoto), Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora, Paul Ruzoka (watatu kushoto) na Mufti wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba akizungumza na viongozi wa dini kuhusu masuala mbalimbali ya amani nchini katika Kongamano la Viongozi wa Dini lililofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam. Katika hotuba yake, Waziri Mwigulu aliwataka viongozi hao kutokuhusisha kosa lifanyalo na mtu au watu fulani kulifananisha na dini yake, amewaomba viongozi hao watoe ushirikiano kwa kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu nchini.
Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba akimfafanulia jambo Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakary Zubeiry Bin Ally (kushoto) mara baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu M.L Nchemba (hayupo pichani) kuzungumza na viongozi wa dini kuhusu masuala mbalimbali ya amani nchini katika Kongamano la Viongozi wa Dini lililofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Sheria wa Wizara hiyo, Berious Nyasebwa. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

KOZI ZA WAAMUZI KUANZA JUNI 23.

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KAMATI ya Waamuzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, imeandaa kozi mbalimbali ikiwa ni maandalizi ya kwa waamuzi katika michuano ya kimataifa sambamba na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017.

Kozi hiyo MA (Members Associations) itaanza kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) ambao kwa sasa wako 18 hapa Tanzania na wengine 12 wa ‘Elite’ ikiwa na maana ya waamuzi wanaotarajiwa kuveshwa Beji za FIFA. Darasa la waamuzi hao litakuwa na waamuzi 30.

Waamuzi hao wenye Beji ya FIFA na wale wanaotarajiwa kuveshwa beji hiyo, wanatakiwa kuripoti Dar es Salaam Julai 23, 2016 ambako kwa mujibu wa ratiba wataanza program ya kozi hiyo kwa kupima kasi ya kukimbia siku inayofuata Julai 24, 2016 wakisimamiwa na wakufunzi kutoka FIFA.

Mara baada ya programu hiyo, kozi itaendelea kwa waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo kwa msimu wa 2016/2017 na kwamba wahusika wote watajigharamia gharama zote.

Waamuzi hao wa ligi ya ndani wataripoti na kujisajili Kituo cha Dar es Salaam Julai 29 na siku inayofuata Julai 30, 2016 na Julai 31, 2016 watakuwa na kozi ya kitathmini kasi kwa kukimbia kabla ya Agosti 1 na 2, 2016 kuwa na semina darasani na mitihani wakati Agosti 3, 2016 kutakuwa na semina na mitihani kwa makamishna mbalimbali wa michezo ya mpira wa miguu.

WAKAZI WA TABATA BIMA JIJINI DAR WASOGEZEWA KARIBU HUDUMA ZA VODACOM TANZANIA

0
0
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Domician Mkama (katikati) akikata utepe kuzindua duka jipya la kampuni hiyo lililoko Tabata Bima jijini Dar es Salaam jana.Wengine ni Meneja wa duka hilo,Emmanuel Mekaki (kushoto) na Brigita Stephen ambaye ni Mkuu wa maduka ya Rejareja wa kampuni hiyo.
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Domician Mkama (kushoto) akizungumza na wateja wakati wa Uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo lililoko Tabata Bima jijini Dar es Salaam jana
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Domician Mkama (kulia) akikata keki kuashiria Uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo lililoko Tabata Bima jijini Dar es Salaam jana.Wanaoshuhudia ni Meneja wa duka hilo,Emmanuel Mekaki (katikati) na Brigita Stephen ambaye ni Mkuu wa maduka ya Rejareja wa kampuni hiyo.
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Domician Mkama( wa pili kulia) akimlisha keki mteja wa kwanza katika duka jipya la kampuni hiyo lililoko Tabata Bima jijini Dar es Salaam jana, Fligona Maswi (kulia) Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mauzo ya Simu wa kampuni hiyo,Samson Mwangela (katikati), Meneja wa duka hilo,Emmanuel Mekaki (wa pili kushoto) na Brigita Stephen ambaye ni Mkuu wa maduka ya Rejareja wa kampuni hiyo.
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Domician Mkama (kulia) na Mkuu wa Mauzo ya Simu wa kampuni hiyo,Samson Mwangela (wa pili kulia), wakifungua mvinyo kuashiria ufunguzi wa duka jipya la kampuni hiyo lililoko Tabata Bima jijini Dar es Salaam jana.Wanaoshuhudia ni Meneja wa duka hilo,Emmanuel Mekaki (wa pili kushoto) na Brigita Stephen ambaye ni Mkuu wa maduka ya Rejareja wa kampuni hiyo ya simu ya mkononi ya Vodacom Tanzania.

MAKALLA ATOA RATIBA YA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI WA MKOA WA MBEYA

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh.Amos Makalla atoa Ratiba kamili ya kuzungumza na kutatuwa Kero za Wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambapo,
Alhamisi Ya wiki ya Mwisho Mwezi July, Tarehe 28 Saa Nne Asubuhi mpaka Saa Kumi Jioni katika Ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya.
Ratiba ya mwezi wa Nane pia Atasikiliza Kero Tarehe 4/8/2016 na Wiki ya Mwisho ni Tarehe 28/8/2016.
Mikutano yote itafanyika Ukumbi wa Mkapa wote mnakaribishwa.

CHUO KIKUU HURIA CHAWAKARIBISHA KWENYE MAONYESHO YA ELIMU YA JUU (TCU), KARIMJEE JIJINI DAR


EACJ TO HEAR WITNESS EVIDENCE IN HON. MARGARET ZZIWA’S CASE NEXT WEEK

0
0
The East African Court of Justice, Arusha, Tanzania, 20th July 2016. The First Instance Division of the East African Court of Justice will hold an extraordinary session from 25th to 29th July, 2016 to hear oral evidence in a case filed on 10th December 2014 by Hon. Margaret Zziwa against the Secretary General of the East African Community complaining against certain actions and decisions of the East African Legislative Assembly and its Committee on Legal Rules and Privileges which pertained to investigations against her and consequential impeachment motion. Hon. Zziwa was the then elected Speaker of the EALA.

Hearing of the case could not take off in September 2015 because of a preliminary objection raised by the secretary General on grounds that the applicant and her witnesses could not give oral evidence without special leave of the Assembly under section 20(1) of the Privileges Act. The First Instance Division of the Court by its ruling of 6th November, 2015 overruled the Preliminary objection on ground that it was not open to it to find that the evidence that Honourable Zziwa and her witnesses would adduce would be an affront to Section 20 of the Privileges Act, without first hearing them. 

The Secretary General being dissatisfied by the said ruling appealed to the Appellate Division of the Court which by its ruling of 27th May, 2016 dismissed the Appeal and found that the First Instance Division did not commit any error of law in arriving at its conclusion.

On 24th June, 2016 the First Instance Division dismissed Hon. Margaret Zziwa's application to have the Court issue her and her witnesses Witness Summons to attend court and give evidence and/or produce documents. The court held that the applicant and her witnesses had voluntarily chosen to give evidence in support of the case and therefore do not require summons to attend Court. 

On whether the Applicant and her witnesses can lawfully be compelled to produce documents within the purview of Section 20 of the EALA (Powers and Privileges) Act 2003 the Court held that even if it could issue summons to voluntary witnesses, the summons cannot be used to circumvent, defeat or act as an appeal or review of the Assembly's decision made under Section 20 rejecting her application to have the witnesses testify and produce certain documents. The court refused to grant the applicant's request.

The Court fixed the matter for four days hearing of oral evidence from 26th to 29th July 2016. The Applicant is expected to give evidence herself and call five witnesses while the Secretary General is expected to call five witnesses.

KARIBU MJUMBE: MAKAMU WENYEVITI WA CCM BARA NA ZANZIBAR WAMKARIBISHA MJUMBE WA KAMATI KUU YA CCM, RAIS DKT. MAGUFULI LEO

0
0
Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Zanzibar, Rais Dk. Ali Mohammed Shein, wakimuonyesha kiti cha kukaa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais Dk. John Magufuli, walipoingia ukumbini, kabla ya kuanza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM, kilichoongozwa  na Mwenyekiti wa CCM, Dk Jakaya Kikwete,  katika ukumbi  wa Sekretarieti, katika jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, leo.Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano.

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA WIZARA YA ELIMU

Vijana wajisajili Airtel Rising Stars

0
0
Usajili wa wachezaji kwa ajili ya mashindano ya vijana chini ya umri 17 ya Airtel Rising Stars 2016 umeanza leo katika mikoa inayoshirikia michuano hiyo mwaka huu ambapo mashindano katika ngazi ya mkoa yamepangwa kuanza wiki ijayo Julai 30.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa miguu nchi TFF, michuano hiyo ngazo ya mkoa inatarajiwa kumalizka Agosti 28 na kufuatiwa na mashindano ya taifa yatakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 6 hadi 11.

Akiongea wakati wa usajili katika mkoa wa kisoka wa Temeke, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mpira Temeke Kassim Mustafa alisema mkoa wake wamejiandaa vema kwa ajili ya kutetea ubingwa walioshinda mwaka jana. “Leo tumeanza usajili wa wachezaji kwa ajili ya michuano ya Airtel Rising Stars 2016. Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru Airtel kwa mradi wake huu wa kusaka na kukuza vipaji vya soka kwa vijana wetu. Temeke tunao vipaji vyingi na ndio sababu mkoa wetu uliweza kushinda taji la ARS 2015,” alisema Mustafa.

Naye kocha mkuu wa Twalipo Youth Academy Neville Kanza alisema anafurahi ujio wa Airtel Rising Stars 2016 huku akisema vipaji vipo vingi na kutamba kuendelea kutoa vijana wengi kwenye kombaini timu ya mkoa. Mwaka jana Twalipo academy ilitoa wachezaji watano ambao waliunga timu ya taifa ya Airtel Rising Stars Dream Team.

Kwa wake Ofisa Uhusiano Airtel Tanzania Jane Matinde alisema wanayo furaha kuona vijana wameweza kufanikisha ndoto zao kwa kupitia michuano ya Airtel Rising Stars. “Ni furaha kuona timu zetu za taifa zikiwa na wachezaji ambao wametoka na program hii ya Airtel Rising Stars,” alisema na kuongeza kuwa hii ni fursa nyingine kwa vijana kujitokeza kwenye usajili ambao utawawezesha kushiriki michuano hii na kuonyesha vipaji vyao.

Alisema Airtel Rising Stars mwaka inafanyika chini ya mwanvuli wa kampeni ya Airtel RURSA iliyozinduliwa mwaka jana kwa lengo la kuwahamasisha vijana kutumia fursa mbalimbali walizonazo ili kujiendeleza kiuchumi. “Airtel Rising Stars yenyewe ni Airtel FURSA kwa kuwa inawawezesha vijana kutumia vipaji vyao kujikwamua kimaisha kupitia mpira. Mpira ni chano cha kipato cha kuaminika”, alisema.

Mikoa inayoshirikia mwaka huu ni Ilala, Temeke, Kinondoni, Mwanza, Mbeya na Morogoro (wavulana) na Ilala, Kinondoni, Temeke, Arusha, Lindi na Zanzibar zikishirikisha wasichana.
Hamza Hemed kutoka Twalipo Youth Academy akijaza fomu ya usajili kwa ajili ya michuano ya Airtel Rising Stars 2016 huku akishuhudiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa miguu wa mkoa wa soka wa Temeke Kassim Ally.
Farid Ally kutoka Mbangala Youth Academy FC akijaza fomu ya usajili kwa ajili ya michuano ya Airtel Rising Stars 2016 huku akishuhudiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa miguu wa mkoa wa soka wa Temeke Kassim Ally.
Hamisi Nassoro kutoka Carpet FC akijaza fomu ya usajili kwa ajili ya michuano ya Airtel Rising Stars 2016 huku akishuhudiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa miguu wa mkoa wa soka wa Temeke Kassim Ally

“NAVY KENZO KUMSINDIKIZA MISS TANGA 2016”.

0
0

NA MWANDISHI WETU TANGA.
MSANII wa Mziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania Navy Kenzo anatarajiwa kutumbuiza kwenye shindano la kumtafuta malkia wa Mkoa wa Tanga Miss Tanga 2016 litakalofanyika Julai 29 mwaka huu kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Resort.

Licha ya Navy Kenzo wasanii wengine ambao watasindikiza onyesho hilo kwa kutoa burudani ni kundi la mziki wa kizazi kipya mkoani Tanga,Wazenji Classic pamoja na Dances.

Akizungumza jana,Mratibu wa Onyesho hilo, alisema kuwa maandalizi ya kuelekea shindano hilo yanaendelea vizuri ambapo tayari warembo watakaoshiriki wameanza kuingia kambini .

Shindano hilo ambalo limeandaliwa na kituo cha Radio cha TK FM 88.5 kilichopo mjini Tanga kwa kushirikiana na Hotel ya Tanga Beach Resort wameelezea namna walivyo jipanga kuhakikisha onyesho hilo linakuwa na ushindani mkubwa kutokana na aina ya warembo waliopo.

“Nisema tu tumejiandaa vizuri kuhakikisha shindano hilo linafanyika kwa umakini mkubwa ili kuwawezesha wadau wa tasnia ya urembo mkoani hapa kuweza kupata ladha halisi ya onyesho hilo kwani licha ya kuwaona warembo wakali wakini pia mzee wa kamatia chini atakuwepo kuwapagawisha “Alisema.

Hata hivyo alisema kuwa mazoezi ya warembo watanaoshiriki onyesho hilo yanaendelea kwenye ukumbi wa New Hotel uliopo mjini hapa kuanzia saa kumi jioni.

Aidha alisema kuwa kabla ya kufanyika shindano hilo warembo hao watapata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii mkoani hapa ikiwemo Mapango ya Amboni na Hifadhi ya Taifa ya Saadani.

Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

TANZANIA NA POLAND ZASAINI MAKUBALIANO KATIKA SEKTA YA UWEKEZAJI.

0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Dkt Adelhelm James Meru akizungumza na Wawekezaji mbalimbali wa Tanzania na Poland kuhusu uwekezaji baina ya nchi hizo mbili.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji(TIC),Clifford Tandari(kulia) pamoja na  Mtendaji Mkuu wa Uwekezaji nchini Poland, Bartlomies Pawlak(kushoto) wakitia saini ya Makubaliano baina ya nchi mbili hususan katika Sekta ya Kilimo na kusaidia katika kuendeleza Uchumi wa Viwanda pamoja na Elimu hapa nchini.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini, Gedfrey Simbeye akizungumza na Wadau wa Sekta ya Uwekezaji wa Tanzania na Poland juu fursa ya Uwekezaji iliyopo hapa nchini.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji(TIC),Clifford Tandari akiwasilisha mada katika mkutano huo uliowahusisha wadau wa Sekta ya uwekezaji wa Tanzania na Poland.
Wadau mbalimbali wa Sekta ya Uwekezaji wakisikiliza baadhi ya mada zilizokuwa zinawasilishwa katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii).

NAIBU WAZIRI WA HABARI,UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO AFANYA MAZUNGUMZO NA KATIBU MKUU WA SHIRIKISHO LA MZIKI TANZANIA.

0
0
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura akizungumza na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime mara baada ya kupokea taarifa ya mapendekezo ya kuboresha tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime akizungumza na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura ofisini kwa Naibu Waziri wakati aki wasilisha taarifa ya mapendekezo ya kuboresha tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.
Afisa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Habibu Msammy akichangia mada wakati wa majadaliano kati ya na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki Tanzania Bw.John Kitime kuhusu maboresho ya tasnia ya Muziki hapa nchini leo Julai 21 Jijini Dar es Salaam.

JK AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MJINI DODOMA LEO.

0
0
Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akifungua Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, kuliani ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. 
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete kwa ajili ya kufungua Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016 pamoja na wajumbe wa mkutano huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais Dkt John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, kuliani ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt John Pombe Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano unaotarajiwa kufanyika Julai 23,2016.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kuanza kwa kikao chao kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana kabla ya kuanza kwa kikao chao kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimpokea Mwenyekiti Mtarajiwa wa CCM,Rais Dkt John Pombe Magufuli walipokuwa wakiwasili kwenye ukumbi wa Sekretarieti, katika jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, leo.Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KALA JEREMIAH, SUPER NYAMWELA KUPAMBA MSIMU MPYA WA JUKWAA LA SANAA LA BASATA

0
0
Wasanii Kala Jeremiah na Super Nyamwela wanatarajiwa kupamba msimu mpya wa programu ya Jukwaa la Sanaa ambayo imekuwa ikiendeshwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na chama cha waandishi wa habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) kwa miaka mitano sasa tangu mwaka 2011.

Msimu mpya wa Jukwaa la Sanaa unatazamiwa kuzinduliwa rasmi Jumatatu ya tarehe 25/07/2015 kwenye Ukumbi wa BASATA ulioko Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam kuanzia saa saa 4:00 Asubuhi – 6:30 Mchana.

Wasanii hawa wanatarajiwa kuupamba uzinduzi huo kwa kutoa burudani mbalimbali sambamba na kuongea na wasanii wachanga katika kuwahamasisha na kuwajengea uwezo juu ya namna wanaweza kutumia fursa mbalimbali za mashindano ya kukuza vipaji katika kujijenga kisanaa.


BASATA linatambua kwamba kumekuwa na tatizo la wasanii katika kutambua na kuchangamkia fursa mbalimbali zilizoko katika sekta ya Sanaa hasa zile zilizomo kwenye mashindano mbalimbali ya kutafuta vipaji ambayo wasanii Kala Jeremiah na Super Nyamwela wamekuwa wakishiriki kikamilifu.


Ushiriki wa wasanii hawa katika kuwajengea hamasa na kuwapa changamoto wasanii wachanga utasadia katika kuwajengea uwezo wa kutumia fursa hizo.

Mbali na burudani na elimu hiyo, uzinduzi huu wa msimu wa mpya wa Jukwaa la Sanaa unaotarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya mia moja (100) utahusisha pia kongamano maalum ambalo litajikita katika kutoa elimu mbalimbali kuhusu sekta ya Sanaa kwa wadau watakaohudhuria. 

Jukwaa la Sanaa ni programu iliyobuniwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa lengo la kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo sekta ya Sanaa lakini pia kusaidia waandishi wa habari kupata habari zihusuzo sekta ya Sanaa kutoka vyanzo mahsusi.

MISS TABATA KUFANYIKA LEO DA WEST PARK.

0
0


Na Mwandishi Wetu.
SHINDANO la kumsaka mrembo wa kitongoji cha Tabata mwaka huu Miss Tabata 2016 linafanyika leo  Ijumaa kwenye Ukumbi wa Da West Park, Tabata jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa shindano hilo Joseph Kapinga alisema jana kuwa jumla ya warembo 16 wanatarajia kupanda jukwaani kuwania taji hilo linaloshikiliwa na Ambasia Mallya, ambaye alishinda taji hilo mwaka 2014.

Mratibu huyo aliwataja warembo watakaoshiriki kuwa ni pamoja na Happiness Paul (21), Neema Makwaia (21), Rose Lucas (22), Mariam Maabadi 23), Sabrina Khalifa (20), Catherine Alex (22) na Grace Malikita (21).

Warembo wengine ni Rachel George (21), Nasra Munna (23), Jackline Evarest (21), Flora Msigwa (21),  Noela Pastory (21), Neema Zablon (24) na Jesca Jackson (22).

Aliongeza kuwa warembo watano watakaofanya vizuri katika shindano hilo, watapata tiketi ya kuiwakilisha Tabata katika shindano la Kanda ya Ilala baadaye mwaka huu.

Alisema kuwa warembo watakaoingia tano bora kila moja atazawadiwa kusoma nafasi ya kusoma kozi yoyote katika Chuo cha DataStar Training College. Kila kozi itagharimu 1.8m/-
Mshindi wa kwanza pia atapata fedha  taslimu Sh. 300,000 wakati mshindi wa pili ataondoka na Sh. 200,000 huku mrembo atakayeshika nafasi ya tatu atajinyakulia Sh. 150,000.

 Mshindi wan ne na watano kila mmoja atapata Sh. 100,000 huku kifuta jasho cha Sh. 50,000 kila m Wengine ni Rachel George (21), Nasra Munna (23), Jackline Evarest (21), Flora Msigwa (21),  Noela Pastory (21), Neema Zablon (24),  Narcisa Wilbert (19) na Jesca Jackson (22).
moja kitatolewa kwa waliobakia.

Bendi ya Twanga Pepeta itatumbuiza kwenye shindano hilo linaloandaliwa na Keen Arts na Bob Entertainment.
Nae Mkurugenzi wa Miss Tabata ambae pia ni mkuu wa kambi Godfrey Kalinga alisema jana kuwa maandalizi ya shindano limekamilika.

Miss Tabata inadhaminiwa na Lete Raha, DataStar College, Global Publishers, CXC Africa, Fredito Entertainment, Yono Auction Mart, Saluti5, Kitwe General Traders na Bob Entertainment.

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA KUWAIT NA CONGO JIJINI DAR ES SALAAM.

0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati) akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al Najem (kulia) masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Kuwait na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo.  Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni, kushoto ni Katibu Mkuu, Meja Jenerali Projest Rwegasira na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo nchini, Jean-Pierre Mutamba (kushoto) masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Kongo na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati) akimsikiliza na Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al Najem (kulia) wakati alipokuwa akizungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Kuwait na Tanzania. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ofisi ya Waziri Mwigulu, jijini Dar es Salaam leo.  Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni, kushoto ni Katibu Mkuu, Meja Jenerali Projest Rwegasira na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Simba Yahya.

MTU NA MBWA WAKE.

Viewing all 109591 articles
Browse latest View live




Latest Images