Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

UONGOZI WA AZAM WAKANA KUMTEMA BOCCO.

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
KUFUATIA kuzuka kwa tetesi zinazodai kocha wa timu ya Azam FC Zeben Hernandez kutokubali kiwango cha shambuliaji wa timu hiyo John Bocco, uongozi wa timu hiyo ubeibuka na kudai kuwa mwalimu huyo bado hajatoa tathmini yake.

Uongozi huo kupitia kwa Katibu Mkuu wake Saadi Kawemba umasema kuwa kocha huyo anatarajiwa kutoa tathmini ya timu hiyo toka alipoanza kuifunzisha rasmi Jumatatu ya wiki ijayo na anashangazwa na taarifa hizo kwani kama wao kama uongozi hawajapokea taarifa zozote kutoka kwa mwalimu inakuaje watu wa nje wanaongea kitu wasichokijua. 

Azam iliingia kambini mwanzoni mwa mwezi huu kwa ajili ya kujiweka sawa kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ikiwemo kucheza mchezo mmoja wa kirafiki kama majaribio kwa wachezaji wao waliokuja katika majaribio.

Baada ya kuanza na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Ashanti united sasa timu ya Azam FC inatupa karata yake nyingine leo kwa timu ya Friends Rangers.
Mchezo huo utakuwa wa pili wa kifariki kwa ajili ya kuwapima wachezaji wao wapya waliopo kwenye majaribio kabla ya kuanza rasmi kwa mechi zao  za kifariki.

Kuelekea msimu ujao timu hiyo imepanga kuwa na kikosi bora zaidi ili kutimiza adhma yao ya kunyakua ubingwa baada ya Yanga kutwaa taji hilo misimu miwili mfululizo. Afisa habari wa timu hiyo Jaffar Idd Maganga amesema kuwa baada ya kucheza na kupata ushindi dhidi ya Ashanti sasa wanawageukia Friends Rangers na michezo hiyo itaendelea kupima uwezo wa wachezaji wao wapya ambao wamekuja ndani ya Azam kwa ajili ya majaribio.

Amesema kuwa wameamua kufanya hivyo kutokana na wachezaji hao uja kwa nyakati tofauti hivyo wale watakaofuzu majaribio watakuwa nao katika michezo mingine hasa ya kirafiki ya kimataifa, "Mwalimu aliomba mechi za kirafiki za mapema ili kuangalia uwezo wa wachezaji waliokuja katika majaribio huku tukiamua timu yetu icheze na timu za daraja la kwanza kwani zimekuwa kambini kutokana na kushiriki mashindano mbalimbali pia ni nzuri kwani zimekuwa zikitupa wakati mgumu."

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU KUZINDUA RIPOTI YA LISHE DUNIANI KESHO.

$
0
0
Ripoti ya Lishe ya Dunia 2016 kuzinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu (Pichani)kesho (Jumatano) jijini Dar es salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ilitolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Jukwaa la lishe Tanzania (PANITA) Bw. Tumaini Mikindo ambae taasisi yake kwa kushirikiana na UNICE, UN Reach, Feed the Children mashirika mengine wanaoratibu uzinduzi huo, amesema katika uzinduzi huo utakaofanyika hapa jijini, Makamu wa Rais anatarajiwa kuambatana na mawaziri kadhaa ambao wizara zao zinazohusika kwa karibu na maswala ya lishe.

“Uzinduzi wa ripoti hiyo yenye kichwa cha habari “Kutoka ahadi mpaka utekelezaji, tumalize utapiamlo ifikapo 2030’’ (From promise to impact. Ending Malnutrition by 2030) uzinduzi huo hapo kesho ni mwendelezo wa zinduzi ziliyofanyika katika majiji tofati duniani ikiwa ni pamoja na Beijing, Johannesburg, Nairobi, New Delhi, New York, Stockholm na Washington D.C na sasa ni Dar es salaam,’’ alisema Bw Mikindo.

Amesema ripoti hiyo ni zana muhimu katika jitihada za kutokomeza utapiamlo nchini kwa kuwa itatoa hali halisi ya lishe Dunia nzima kwa unahusisha nchi Zaidi ya 129 ulimwenguni. Ripoti hiyo iliyohaririwa na jopo la wataalamu wa lishe duniani wakiongozwa na Bwana Lawrence Haddad ambae ni mtafiti aliebobea kwenye masuala ya lishe na kinara wa lishe Duniani, Tanzania kama sehemu ya ripoti hiyo itapata nafasi ya kujipima na kuchukua hatua stahiki.

Zaidi, akitaja malengo ya ripoti hiyo Bw Mikindo alisema ni pamoja na kupitia na kutathmini maazimio ya kupunguza utapiamlo yaliyowekwa na nchi katika mkutano wa kwanza wa Lishe na uchumi uliofanyika London mwaka 2013, pia kuisihi serikali kuongeza muamko wa kisiasa kwenye masuala ya lishe na kuongeza rasilimali za ndani kwa ajili ya kushughulikia matatizo ya Lishe nchini.

“Malengo mengine ni kuhamasisha uwajibikaji wa pamoja katika ngazi zote za utawala ambazo zitasaidia nchi kumaliza tatizo la utapiamlo na kusisitiza kuzingatiwa kwa malengo ya Baraza la Afya Duniani katika vita dhidi ya utapiamlo,’’ alitaja Bw Mikindo huku akibainisha kuwa ripoti hiyo imekuwa ikitolewa kila mwaka kwa miaka mitatu sasa.

Jukwaa hilo la lishe (PANITA) ni muunganiko wenye lengo la kuwakutanisha Asasi zote za Kiraia zinazohusika na lishe, waadishi wa habari, wanasiasa na makundi mengine kwa lengo la kuhamasisha jamii juu ya masuala ya lishe ilikutokomeza tatizo la utapiamlo katika jamii.

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ILIYOANDIKWA NA GAZETI LA JAMHURI KUHUSU OFISI YA BUNGE.

KATIBU MTENDAJI WA BARAZA LA UWEZESHAJI BENG'I AFUNGA MAHAFALI YA WAJASIRIAMALI WA MRADI WA MKUBWA

$
0
0

atibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akizungumza jambo na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.

Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), wakicheza na kufurahi pamoja wakati wa hafla hiyo ya kuhitimu mafunzo jijini Dar es Salaam leo.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Tanzania Beng'i Issa akisalimiana na mmoja wa Wanawake wajasiriamali walionufaika na mafunzo chini ya Mradi wa Mpango wa Kukuza Biashara kwa Wanawake (MKUBWA), alipokagua bidhaa zao wakati wa mahafali, yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Wajasiriamali 510 walihitimu baada ya kuhudhuria mafunzo, yaliyoandaliwa na asasi ya Tanzania Gastby Trust (TGT). Kushoto ni Mwenyekiti TGT, Epeineto Toroka na Afisa Mtendaji Mkuu wa Asasi hiyo, Olive Luena.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

kampuni ya chemcotex yatimiza miaka 25 tangu kuanzishwa kwake,yawazawadia wateja wake kwa kutoa gari

$
0
0

Gari lililoandaliwa na kampuni ya chem&cotex inayotengeneza na kusambaza dawa ya meno ya whitedent ambayo itashindaniwa na watumiaji wa dawa hiyo kwa kubuni idadi ya dawa zilizondani ya gari hiyo ikiwa ni katika kusherehekea miaka 25 ya dawa ya whitedent. 
 
Katika kusherehekea miaka 25 tangu kuanzishwa kwa dawa ya meno ya whitedent kampuni ya chem&cotex imeamua kuwazawadia wateja wake kwa kutoa gari itakayoshindaniwa kwa wateja hao kujaza idadi ya dawaza meno zilizo ndani ya gari hiyo, kampeni iliyozinduliwa mkoani morogoro.

Mgeni rasmi katibu tarafa wa manispaa ya morogoro Pakalapakala Mlenge akiongea na akiongea na wakazi wa morogoro waliojitokeza katika hafla ya kusherehekea miaka 25 ya dawa ya meno ya whitedent.
Wanyakazi wa kampuni ya chem&cotex inayotengeneza na kusambaza dawa ya meno ya white dent wakiwa katika picha ya pamoja na katibu tarafa manispaa ya morogoro Pakalapakala Mlengekatika hafla ya kusherekea miaka 25 ya dawa hiyo iliyokwenda sambasa na uzinduzi wa bahati na sibu ya kushinda gari kwa wateja kutaja idadi ya dawa zilizo ndani ya gari hiyo. 

Rais Mstaafu Mwai Kibaki atembelea daraja la Mwalimu Nyerere.

$
0
0

Mwakilishi Maalumu wa masuala ya maji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Watu wa Kenya Mwai Kibaki ametembelea mabanda ya maonesho ya sita katika ya wiki ya maji Afrika yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Katika tukio hilo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Emmanuel Kalobelo amimweleza Mwakilishi huyo kuwa Tanzania imejipanga kuhakikisha kuwa hadi ifikapo 2020 iweze kufikisha maji kwa wananchi wote kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

Mhandisi Kalobelo aliongeza kuwa hatua hiyo itaifanya Tanzania kufikisha maji kwa wakazi wa mijini kwa asilimia 95 na kwa wakazi wa vijijini kw asilimia 85.

Aidha, katika hatua nyingine, Mwakilishi huyo alitembelea barabara iliyopewa jina la Mwai Kibaki inayoanzia eneo la Morocco hadi njia panda ya Kawe jijini Dar es salaam pia alitembelea na daraja la Mwalimu Nyerere linalounganisha eneo la Kigamboni kupitia bahari ya Hindi na eneo la katikati ya jiji la Dar es salaam.

Maonesho ya sita katika ya wiki ya maji Afrika mwaka huu yanayoendelea jijini Dar es salaam yanaongozwa na kaulimbiu inayosema “Kufikia lengo la Mendeleo Endelevu (SDGs) juu ya Usalama wa Maji na Usafi wa Mazingira”.

Mwakilishi Maalumu wa masuala ya maji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Watu wa Kenya Mwai Kibaki (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Wiki ya Maji Afrika (Sylivester Matemu) wakati wa maonesho ya sita katika ya wiki ya maji Afrika yanayoendelea jijini Dar es salaam. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Emmanuel Kalobelo.
Mwakilishi Maalumu wa masuala ya maji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Watu wa Kenya Mwai Kibaki akisalimia na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Emmanuel Kalobelo leo jiji Da es salaam.
Katibu wa Mwakilishi Maalumu wa masuala ya maji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Watu wa Kenya Mwai Kibaki (katikati), Profesa Nick Wanjohi akifafanua jambo kwa mwakilishi huyo alipotembelea na daraja la Mwalimu Nyerere linalounganisha eneo la Kigamboni kupitia bahari ya Hindi na eneo la katikati ya jiji la Dar es salaam. 
Katibu wa Mwakilishi Maalumu wa masuala ya maji kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Watu wa Kenya Mwai Kibaki (katikati), Profesa Nick Wanjohi akifafanua jambo kwa mwakilishi huyo alipotembelea na daraja la Mwalimu Nyerere linalounganisha eneo la Kigamboni kupitia bahari ya Hindi na eneo la katikati ya jiji la Dar es salaam.

NMB yaorodhesha Hati Fungani zake kwenye soko la hisa, DSE

$
0
0

BENKI ya NMB leo imeorodhesha kiasi cha shilingi Bilioni 41.4 ilichokipata kutokana na mauzo ya hati fungani katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE). Tukio hilo limezinduliwa rasmi leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk. Adelhelm Meru kwa ishara ya kupiga kengele kwenye ofisi za DSM. 

Akizungumza katika hafla hiyo Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji - Dk. Meru alipongeza hatua hiyo ya kuorodhesha hati fungani kwenye soko la hisa na kuongeza kuwa ni ya kizalendo na kuwataka wawekezaji katika sekta binafsi kushiriki kikamilifu. “Hati fungani hii inatarajiwa kuleta maendeleo katika soko la mitaji na inafungua njia kwa mashirika mengine binafsi, mashirika ya serikali na mamlaka za manispaa kutafuta njia mpya za kukuza mitaji na uwezeshaji” alisema Dk. Adelhelm.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NMB - Ineke Bussemaker alisema “Hati fungani hii ya miaka mitatu si tu imeleta msisimko chanya kwenye soko la mitaji bali hata katika soko la hisa, NMB inakuwa benki ya kwanza kupata Kiwango zaidi ya mara mbili ya Kiwango tulichoomba awali.” Bi Ineke aliongeza kuwa mwitikio chanya kwenye hati fungani ya NMB unatoa somo kuwa kuna umuhimu wa benki mbalimbali kuchangia kwa Kiwango kikubwa katika kuendeleza masoko ya mitaji na pia kupigania elimu ya fedha kwa jamii. Hati fungani inayoorodheshwa leo ina riba ya asilimia 13 kwa mwaka na iitakomaa baada ya miaka miatatu.

Bi Ineke alisema Kutolewa kwa hati fungani ya NMB ni sehemu ya mkakati wa benki kutafuta njia mbadala za vyanzo vya fedha. Fedha zilizopatikana kwenye hati fungani zitatumika kwaajili ya kutoa mikopo kwa wateja, wateja watakaonufaika ni pamoja na wateja binafsi, wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa pamoja na taasisi za serikali. Akiongea kwenye hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE - Moremi Marwa alisema “mafanikio ya Hati fungani ya NMB yanatuambia kuwa wawekezaji wanajua uwepo wa fursa zilizopo katika masoko ya mitaji na wana uwezo na hamu ya kusaidia wale walio na uhitaji wa kukuza mitaji yao.”

Hati fungani ya NMB ilipata mwitikio chanya kutoka kwa wawekezaji na kupita Kiwango kilichopangwa awali kwa asilimia 107. Benki ilipata maombi 1,811 yenye thamani ya shilingi bilioni 41.4 huku maombi mengi yakirundikana wiki ya mwisho kabla ya kufunga upokeaji wa maombi. Kutokana na kuorodheshwa kwenye soko la hisa, wawekezaji wataweza kuuza hati fungani zao kupitia soko la hisa la Dar es Salaam – DSE. Stanbic Bank Tanzania Ltd. Ndio wawezeshaji wa hati fungani ya NMB huku makampuni ya Orbit Securities Ltd. na EA Capital Ltd wakiwa kama mawakala viongozi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji - Dk. Adelhelm Meru (katikati) akipiga kengele kuashiria kuorosheshwa rasmi hati fungani za Benki ya NMB kiasi cha shilingi Bilioni 41.4 leo katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE). Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NMB, Bi. Ineke Bussemaker pamoja na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Moremi Marwa (Kulia).Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji - Dk. Adelhelm Meru (kulia) akimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker (kushoto) mara baada ya tukio la Benki ya NMB kuoroshesha rasmi hati fungani kiasi cha shilingi bilioni 41.4 katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).Mmoja wa maofisa waandamizi wa DSE (aliyeshika kengele) akiongoza hafla  ya Benki ya NMB kuoroshesha rasmi hati fungani kiasi cha shilingi bilioni 41.4 katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE). Wengine kutoka kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa DSE, Moremi Marwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk. Meru na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ineke Bussemaker wakishuhudia.

SBL yazindua bomba la 470m/- kudhibiti majitaka

$
0
0
 Kampuni ya Bia ya Serengeti leo imezindua bomba la kudhibiti wa majitaka ambalo linalenga kuhakikisha kiwango cha juu kiafya kwa kampuni, mazingira na wakazi wa maeneo yaliyo karibu.

Bomba hilo limejengwa chini ya usimamizi wa Kampuni ya Maji Safi na Taka ya Dar es Salaam (Dawasco), Mamlaka ya Barabara (Tanroads) na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke likihusisha takribani kilometa mbili kuanzia katika kiwanda cha bia cha Serengeti kilichpo Temeke hadi Kurasini ambako ndip ulipo mfumo wa majitaka wa Dawasco.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, huo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie, alisema kwamba mradi huo wa aina yake na wa kwanza nchini unadhihirisha juhudi zisizo na ukomo za kampuni hiyo katika kuhifadhi mazingira.

“Ubora wa maji ni jambo lililo mstari wa mbele katika utengenezaji wa bia lakini suala la usafi kutokana na kuzalishwa kwa majitaka ni sehemu kubwa inayotujengea hisia za kimazingira katika shughuli za kutengeneza bia. Kwa hiyo uzinduzi wa bomba hili ni moja ya hatua ya kusonga mbele katika kuhakikisha yanakuwepo mazingira safi kiafya,” alisema Weesie.

Mkurugenzi Mtendaji huyo alibainisha kwamba majitaka yanayotolewa na bomba hilo yatakuwa yanafanyiwa tiba kwanza ili kuondoa aina yoyote ya sumu kabla ya kuachiwa ili kuingia katika mfumo wa majitaka wa Dawasco.

Alisema kuwa uzinduzi huyo uko katika mkondo mmoja na sera ya Kampuni ya Serengeti ya kujikita katika ustawi wa jamii ambayo imeainishwa katika maeneo manne ya vipaumbele ambavyo vinajumuisha, Utoaji wa Stadi za Maisha, Uendelevu wa Mazingira na Kuboresha Unywaji wa Kistaarabu.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Masuala ya Muungano na Mazingira, Mh. Luhanga Mpina aliipongeza Serengeti kwa kuzindua bomba hilo akibainisha kwamba ujenzi unaendana na ajenda ya serikali ya uhifadhi wa mazingira.

Mpina alibainisha kwamba uchafuzi wa mazingira katika miji na maeneo ya pembezoni unaathiri afya za watu wengi na kupunguza tija inayotokana na mazingira na kutoa wito kwa makampuni mengine kuiga kazi nzuri.  
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina akiwasha mtambo wa kusafirisha majitaka kiwandani hapo mara baada ya kuzindua rasmi katika hafla iliyofanyika katika kiwanda hicho Temeke Jijini Dar es salaam. 
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina akiongea na wafanyakazi wa kiwanda cha bia ya serengeti mara baada ya uzinduzi wa bomba la kudhibiti majitaka katika kiwanda hicho Jijini Dar es salaam. 
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina , Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie na waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini jinsi mtambo wa kusafirisha majitaka unavyofanya kazi kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa mradi huo. 
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina (katikati) akifurahi jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie mara baada ya kukata utepe katika mtambo kusafirisha majitaka katika hafla iliyofanyika mapema leo kiwandani hapo.


MAHAKAMA YA TANZANIA YAKUSUDIA KUBADILISHA MUONEKANO WAKE

$
0
0
Na Lydia Churi- Mahakama ya Tanzania 

Mahakama ya Tanzania imeamua kuchukua juhudi za makusudi ili kubadilisha muonekano wake na kuwa chombo kitakachojibu maswali na kuondoa kiu ya watanzania katika kupata haki kwa wakati.

Akifungua Mkutano wa Mahakama ya Tanzania na wadau wake wa kujadili utekelezaji wa Mpango Mkakati wa mhimili huo leo mjini Dodoma, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Dodoma Mheshimiwa Mwanaisha Kwariko amesema Mahakama ya Tanzania inakusudia kukibadilisha chombo hicho ili kiweze kutoa haki kwa wakati kwa mujibu wa jukumu ililopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Alisema katika kufanikisha azma hiyo, Mahakama ya Tanzania inaendelea na mafunzo ya wiki mbili kwa watumishi wake yanayolenga kuuboresha Mpango Mkakati wake kwa kushirikiana na wadau ili kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati na taswira ya mahakama inakuwa chanya wakati wote.

Jaji Kwariko amesema Mahakama imeamua kuwashirikisha wadau kwenye Mpango Mkakati wake kwa kuwa umuhimu na nguvu waliyonayo Sitasaidia kufanikisha utendaji wa Mahakama katika kuyafikia malengo ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aidha, Jaji Kwariko aliwataka watumishi wa Mahakama ya Tanzania kufanya kazi kwa bidii katika kuutekeleza Mpango Mkakati kwa kuwa utendaji kazi wao utapimwa kwa jinsi watakavyotekeleza majukumu yao kulingana na Mpango Mkakati huo. Aliongeza kuwa Mahakama ya Tanzania itaelekeza rasilimali zake zote kama vile watu, fedha na muda katika kuleta matokeo makubwa yanayotarajiwa.

Alisema endapo watumishi hao watajikita katika kufanikisha uimara wa nguzo zote tatu za Mpango Mkakati huo, upatikanaji wa haki kwa wakati na uhusishwaji wa wadau na imani ya wananchi vitakifanya chombo hicho kutimiza ndoto yake na kuifikia dira yake. Nguzo tatu za Mpango Mkakati huo ni Utawala bora, Uwajibikaji na Usimamizi wa rasilimali.

Naye Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mheshimiwa Katarina Revokati alisema baada ya Mpango Mkakati wa Mahakama kukamilika, watumishi watasaini kadi itakayokuwa ikionyesha namna ya utekelezaji wa Mpango Mkakati na kadi hiyo itaweka alama za kuonyesha ufaulu katika utekelezaji, endapo mtumishi atapata alama ndogo atachukuliwa hatua.

Akizungumzia namna Mahakama inavyopambana na rushwa, Msajili huyo alisema Mahakama imeweka mazingira ya uwazi katika utoaji wa huduma zake pamoja na kuweka mifumo ya kielekitroniki na kuhusisha wadau wake katika utendaji kazi wake. 

Mahakama ya Tanzania inaendelea na Mafunzo ya wiki mbili kwa watumishi wake kuhusu uandaaji na utekelezaji wa Mpango Mkakati wake ambapo leo ilikutana na wadau wake ili kujadili namna ya utekelezaji wa Mpango huo. 

Wadau waliohudhuria, mafunzo hayo leo ni Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Polisi Makao Makuu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa-TAKUKURU na Wakala wa Majengo Tanzania-TBA.

Wengine ni pamoja na Baraza la Habari Tanzania-MCT, Tume ya Kurekebisha Sheria, Tume ya Usuluhishi wa Migogoro, Ofisi ya Nyaraka za Taifa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI.

MUSEUM ART EXPLOSION 2016

TASWIRA MBALIMBALI KATIKA UFUNGUZI WA TAMASHA LA MZANZIBAR, MJINI UNGUJA

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe,Mohammed Aboud Mohmamed akiangali bidhaa za wajasiriamali wakati alipotembelea mabanda ya maonesho kabla ya ufunguzi wa Tamasha la Mzanzibari kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika viwanja vya Mnara wa kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi Michenzani Mjini Unguja
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe,Mohammed Aboud Mohmamed akitoa hotuba ya ufunguzi wa Tamasha la Mzanzibari kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika viwanja vya Mnara wa kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi Michenzani Mjini Unguja
Akina mama waliovalia vazi la asili ya Mzanzibari wakati wa sherehe za ufunguzi wa Tamasha la Mzanzibari lililofanyika leo katika viwanja vya Mnara wa kumbukumbu ya miaka 50ya Mapinduzi ambapo mgeni rasmi akiwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe,Mohammed Aboud Mohmamed kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
Wasanii wa Jeshi la mafunzo Zanzibar wakicheza ngoma ya Mkurungu yenye asili yake kjijiji cha Nungwi Wilaya Kaskazini A.Unguja wakati wa ufunguzi wa Tamasha la mzanzibari lililofunguliwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe,Mohammed Aboud Mohmamed kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika viwanja vya mnara wa kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi,Michenzani Mjini Zanzibar

TWINNING OF TOWNS AND CITIES’ THE WAY TO GO IN EAC, EALA SPEAKER SAYS AT LAUNCH OF GREENING CEREMONY IN LIRA MUNICIPALITY

$
0
0
EALA Speaker, Rt Hon Daniel F. Kidega has reiterated the need for cities and towns in the EAC to embrace the twinning principle to spur best practices in their management, enhance investments, security and cleanliness. At the same time, the Speaker says Partner States should indeed enhance common environmental policies that would sustain the eco-systems of Partner States beyond this current generation. 

Rt Hon Kidega, made the remarks over the weekend at the inaugural Lira Waa (Our Lira) Annual Prayer Breakfast, themed ‘Making Lira City Green and Clean’ held in Lira Municipality, in Uganda.

“In Kigali for example, the Umuganda initiative (Community work) has gone a long way in ensuring cleanliness and this is attributable to good leadership, a thing which must be celebrated”, he said. 

“I am happy that a number of cities are today concerned about becoming clean- but the city authorities cannot do it alone without support. Successful collaboration will lead us to achieve what we want; clean, and well planned towns and cities”, he added.
A section of the participants who attended the Lira Waa Breakfast

The Speaker offered to be the bridge in assisting the authorities in Lira Municipality to twin with a City of their choice in the Partner States saying it was aimed at exchange of information and comparing notes.

The guest preacher at the function attended by over 100 persons was Bishop Alfred Acur of West Lango Diocese. Bishop Acur said the church was also committed to ensuring the face of Lira Municipality is changed.

“Planting trees and making the environment clean and pure is good.  Trees make life nicer and reduce stress”, he said as citing several verses in the Bible that attach importance to cleanliness.
Speaking at the occasion, the Regional District Commissioner (RDC), Lira, Mwaka Emmanuel, Lutukumoi, the brainchild of the initiative, said the cause would make Lira clean and strengthen its quest for elevation to a city.

“By embracing Lira Waa Campaign, we are showing Government our hunger for a city status.  There will be two model streets that we shall all concentrate on to make them clean, painted and with waste bins”, he added.
The EALA Speaker, Rt Hon Daniel F. Kidega plants a tree as other officials watch. the Annual Lira Waa Campaign hopes to keep the environment clean and green

The campaign seeks to rally people to plant trees, flowers and greens and to create reliable waste management systems which is beneficial to all. Lira Waa (Our Lira) campaign is a model that was developed by the Regional District Commissioner and is a model that seeks to unite the Community to own the district, brand it and be proud of it. It envisages the transformation of the Municipality into one of the cleanest in modern day Uganda, and a destination everyone would want to associate with as it hosts sub-national, national, regional and international events.

Lira Municipality currently hosts an ultra-modern market estimated at UGX 28 Billion and an irrigation scheme, one which the RDC says will turn the municipality into a bread basket for the region. Stakeholders in the campaign include the private sector, civil servants, civil sector organisations and cultural leaders.   Corporate companies and the entire Community have also been roped in the initiative.

Under Article 112 of the Treaty for the East African Community, Partner States undertake to develop common environmental management policy that would sustain the eco-systems, prevent, arrest and reverse the effects of environmental degradation.

TRANSFORMING THE LIVES OF PEOPLE WITH DISABILITIES IN TANZANIA, THROUGH HANDICRAFTS, TRAINING & EMPLOYMENT

$
0
0
Iring District Commssioner visited Neema Crafts Centre which has been helping people with Disabilities .The Centre was founded in 2003 by the Diocese of Ruaha, to provide training and employment opportunities for people with disabilities in the Iringa region of Tanzania.

It also aims to change negative attitudes towards people with disabilities in the local society. There’s a great stigma attached to having a disability in Tanzania, and the centre provides dignity and hope for many people who previously relied on street begging or were hidden away at home.

The centre has eight craft workshop areas, a therapy unit for disabled children, an award winning cafe, a conference centre entirely staffed by deaf people and a welcoming guesthouse jointly run by the local Mother’s Union.
All products are made by PWD, from the proceeds they get their daily bread and get away from begging.

Hon Kasesela thanked the centre for the support and promised to find a land for construction of houses as well as improve their lives. He also ask people to buy products from Neema Crafts which will make the centre grow.


WAKUU WA IDARA NDANI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MKURANGA WAMEUNGANA NA MBUNGE WA JIMBO LA MKURANGA ABDALLAH ULEGA KUFANYA ZIARA YA KUKAGUA NA KUANGALI KERO WANAZOKUTANA NAZO WANANCHI.

$
0
0
 Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kibesa katika ziara ya kusikiliza kero na changamoto mbalimbali za wananchi akiwa ameambatana na wakuu wa idara mbalimbali  ndani  ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga  leo Julai 19, 2016 katika Kijiji cha Kibesa wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
 Wananchi wa kijiji cha Kibesa wakimsikilza Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega leo Julai 19, 2016 katika Kijiji cha Kibesa wilaya Mkuranga mkoani Pwani. 
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akimbetembelea shule ya msingi Mbezi   kushoto  kwake anayempa maelezo ni Mwenyekiti wa  serikali ya kijiji cha Mbezi   Muungwana, Hassan Abdalla  
(Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii).

PROFESA MUHONGO AAGIZA MAJI YA NYAMONGO KUPIMWA TENA.

$
0
0
Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (kushoto),  akizungumza na wananchi katika kijiji cha Matongo wilayani Tarime) wakati  Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mwenye koti la Bluu) alipofika kijijini hapo ili kuwaeleza wananchi, maamuzi ya Serikali yanayotokana na Mapendekezo ya  Kamati iliyoundwa mwezi Februari mwaka huu ili kutathmini migogoro kati mgodi wa Acacia NorthMara na wananchi wanaozunguka mgodi huo.
  Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mwenye koti la Bluu) akizungumza na wananchi katika kijiji cha Matongo wilayani Tarime. Profesa Muhongo alifika kijijini hapo ili kuwaeleza wananchi, maamuzi ya Serikali yanayotokana na mapendekezo  ya Kamati iliyoundwa mwezi Februari mwaka huu ili kutathmini migogoro kati mgodi wa Acacia NorthMara na wananchi wanaozunguka mgodi huo.

Na Teresia Mhagama.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ametoa agizo   la kupimwa tena kwa maji yanayotoka katika vyanzo vinavyozunguka mgodi wa dhahabu wa Acacia North Mara ili kujiridhisha kuwa hayana athari kwa binadamu, mifugo na mazingira.

Agizo hilo alilitoa wilayani Tarime wakati  akizungumza na wananchi katika vijiji vya Matongo, Nyabichune, Mrwambe na Nyakungulu ambavyo vinazunguka mgodi huo wa dhahabu.

Profesa Muhongo alitoa agizo hilo baada ya Kamati iliyokuwa ikitathmini migogoro kati ya Mgodi huo na wananchi kueleza kuwa matokeo ya vipimo vya  maabara vinaonyesha kuwa maji hayo yana viwango vinavyokubalika kwa matumizi ya binadamu, mifugo na mazingira na kupendekeza kuwa wataalam wa afya na mifugo wafanye utafiti zaidi ya suala hilo ili kujiridhisha zaidi.

“Viwango vinavyopaswa kutumika katika upimaji wa maji haya lazima viwe vya Shirika la Afya Duniani (WHO) hivyo zichukuliwe tena sampuli za maji wakati wa kiangazi na wakati wa mvua na zipimwe tena. Sampuli hizo zigaiwe kwa makundi mbalimbali ikiwemo wananchi, Mkuu wa wilaya, Kamati iliyofanya tathmini na mimi mwenyewe ili kila kundi lipeleke katika maabara inayoaminika na baadaye kuwasilisha majibu ya uchunguzi,” alisema Profesa Muhongo.

Aidha alisema kuwa sampuli za maji atakazopatiwa yeye  atazipeleka katika nchi  mbalimbali duniani ikiwemo Ujerumani na Ubelgiji ambako kuna maabara za kisasa na zinazoaminika duniani.
Aliongeza kuwa, vyanzo vya maji katika sehemu nyingi zenye uchimbaji mkubwa na mdogo duniani vimekuwa vikiathiriwa na shughuli za  migodi na kueleza kuwa atawasiliana na Mamlaka zinazosimamia Sekta ya Maji pamoja Mgodi ili kupata chanzo mbadala cha maji na hivyo kuondoa malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi huo.

Aidha aliagiza wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini kuhakikisha kuwa kila baada ya miezi mitatu wanachukua sampuli za maji  katika vyanzo vinavyozunguka mgodi huo na kuzipima ili kujiridhisha kuwa maji hayo hayana madhara kwa binadamu, mifugo na mazingira.
Naye Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche alimshukuru Waziri wa Nishati na Madini kwa kuamua kuishughulikia changamoto hiyo ya maji kwa kutoa agizo kuwa upimaji wa maji hayo uwe endelevu na  kutafuta chanzo mbadala cha maji.

Aidha Profesa Muhongo alitumia fursa hiyo kuwaasa Wachimbaji  wadogo kujiunga katika makundi ambayo yatawawezesha kufaidika na masuala mbalimbali  ikiwemo Ruzuku  inayotolewa na Serikali ambapo kwa mwaka huu, takribani Dola za Marekani milioni 400 zinatumika kuwaendeleza wachimbaji wadogo kupitia Ruzuku hiyo. 

NSSF YACHANGIA MILIONI 50 HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI LINDI

$
0
0
SHIRIKA la Hifadhi ya Taifa ya Jamii NSSF Makao Makuu ikishirikiana na Ofisi ya Mkoa wa Lindi Imechanga Jumla ya Shilingi Milioni 50 Kwa Ajili ya Kuchangia Harambee ya Kusaidia Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Lindi Iliyoungua Moto Wiki iliyopita.

Kwa Kutambua Umuhimu wa Elimu kwa Watoto Shirika Hilo Kupitia Mkurugenzi Mkuu Wake ,Aliewakilishwa na Meneja wa Mkoa Bi Nour Aziz Limetoa ahadi hiyo kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kasim Majaliwa Alieongoza Harambee Hiyo Ambayo Ilihudhuriwa na Wadau Mbali mbali Akiwemo Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne,Mama Salma Kikwete.

Katika Harambee Hiyo Jumla ya Shilingi Milioni 80 Taslimu zilichangwa Huku Ahadi na Vifaa vya Ujenzi zikifikia Shilingi Milioni 640 Ambapo Katika Ujenzi Mpya Waziri Mkuu Ameagiza Kujengwa Jengo la Ghorofa litakalokuwa na Ofisi na Madarasa.

Katika Tukio Hilo la Moto,Jumla Ya Madarasa 9 na viti na Meza zaidi ya 300,Ofisi 4 na Vyoo Matundu 24 Viliteketea na Moto Uliotokana na hitilafu ya Umeme. (Picha na Abdulaziz Video, Lindi)

Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Lindi, Bi Nour Aziz (kulia) akiwasilisha ahadi ya shirika hilo ya kuchangia milion 50 katika harambee hiyo iliyoongozwa na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Lindi, Bi Nour Aziz akipeana mkono na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimshukuru Mkuu wa Kitengo cha Mafao NSSF, Bw Juma Namuna, baada ya shirika hilo kuahidi kuchangia Milioni 50.

GGM Kilimanjaro Challenge Against HIV & AIDS 15th Anniversary’s Marks a Special Flag Off, 57 Climber 30 Cyclis up to the top.

$
0
0
GGM Kili Challenge 2016 - Heroes Faces Day IV.
Former President of the United Republic of Tanzania HE. Dr Jakaya Mrisho Kikwete has flagged off the 2016 Kili Challenge at Machame Gate in Moshi marking its 15th year historical event!!. Government authorities and institution, United Nations Development Programme representatives in Tanzania, the general public and Strong 57 Kili climbers and 30 Cyclists were all there ready to mark the historical event.

Speaking during the ceremony to start a 7 days double routes, President Kikwete commended GGM and its partnering stakeholders for the continued commitment to support government initiative in the fight against HIV and AIDS.
Today’s images….What a positive sight despite the tiredness!!!!

“The initiative is now approaching to 1,000 people from all across the world participating in the Kilimanjaro Challenge and combined with  joint effort with other initiatives, the reduction of HIV infections has been reduced from a double digits to 5.1% nationalwide…this is commendable effort”.

He added that Tanzania at that percentage, people must be proud of the hard work done by the government through TACAIDS and its associate partners such as GGM and this has been possible through these kind of innovative approaches.

“I sincerely thank GGM and its partners for this noble undertaking. This is a positive corporate responsibility. I therefore ask other companies and even individuals to contribute to this course. Let us all rise up to join the fight against HIV & AIDS in order to make our Country the first in the world to get to 3 Zeros: Zero New Infections, Zero Stigma and Zero AIDS related deaths. "He said.
 the hungry Cycling team was enjoying a video clip while waiting for the lunch to be set on the “Road table”. 

MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA CCM YAPAMBA MOYO MKOANI DODOMA

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana akielekeza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Bara, Ndg. Rajab Luhwavi (mwenye koti) pamoja na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM,Ndg. Nape Nnauye (kushoto), wakati wa maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016 kwenye Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, Mjini Dodoma leo. Alie nyuma ya Katibu Mkuu, ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Zanzibar, Ndg. Vuai Ali Vuai
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM - Bara, Ndg. Rajab Luhwavi wakiweka sawa moja ya Vibao vitakavyotambulisha Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kutoka Mikoa yote nchini, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016 kwenye Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, Mjini Dodoma leo. 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Abdulrahman Kinana akikagua Ukumbi wa CCM Dodoma Convention Centre, kutakakofanyikia Mkutano Mkuu wa CCM, unaotarajiwa kufanyika Julai 23, 2016.
Maandalizi yakiendelea.

IBADA NA MAZISHI YA MWANAHABARI CHARLES SOKORO WA BARMEDAS TV YAFANYIKA JIJINI MWANZA

$
0
0

Ibada ya Mazishi ya aliekuwa Mkuu wa Vipindi na Afisa Mahusiano katika kituo cha runinga cha Barmedas Tv cha Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro, imefanyika jana katika Kanisa la AICT Makongoro na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika katika Makaburi ya Kitangiri.

Mwalimu Sokoro ambae pia alikuwa mwalimu wa muziki wa Injili na Mwenyekiti wa Kwaya ya AICT Makongoro, alifariki jumamosi Julai 16,2016 majira ya saa mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa miezi kadhaa.

Alizaliwa mwaka julai mosi mwaka 1965 katika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza na hadi mauti yanamkuta alikuwa na umri wa 51 ambapo ameacha watoto wanne, alikuwa mgane.
Na BMG
Kwaya ya AICT Makongoro ikiimba katika ibada ya mazishi ya Sokoro
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la AICT Makongoro akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Viongozi mbalimbali wa dini mkoani Mwanza, pamoja na waombolezaji wakiwa katika ibada ya marehemu Sokoro.
Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Mwanza, na mwanachama wa BMG Tanzania, Edwin Soko, pamoja na waombolezaji wakitoa wakiuaga mwili wa marehemu Sokoro.

SERIKALI KUWEKA UTASHI WA KISIASA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UTAPIAMLO- MAKAM WA RAIS.

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SERIKALI imesema kuwa itaweka utashi wa kisiasa katika kupambana dhidi ya utapiamlo kwa kuongeza elimu hususani katika maeneo ya vijijini.

Hayo ameyasema leo Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Dunia iliyoandaliwa na Jukwa la Lishe Nchini (PANITA) , amesema kuwa suala la lishe likiwekewa utashi wa kisiasa litaweza kufanikiwa kutokana na jitihada ambazo zimeanza kuonekana kwa wadau.

Amesema serikali inatambua kuwa mojawapo ya malengo ya Baraza la Afya Duniani ni kutokomeza utapiamlo ifikapo mwaka 2025 na lengo hilo linaweza lisifikiwe kama tutaendelea kutekeleza mipango yetu kwa mazoea.

Makamu wa Rais Samia amesema kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau wote kwa pamoja tuweze katika kutokomeza utapiamlo katika kufikia malengo ya Tanzania isiyo na Utapiamlo, Tanzania ya viwanda na yenye uchumi wa kati.

Amesema malengo kupambana na utapiamlo yatawezekana kwa kuendeleza jitihada za kuongeza bajeti za lishe,kuongeza virutubishi katika vyakula , kutumia vyema wataalam wa lishe na kuhakikisha utekelezwaji wa afua za lishe kwa ufanisi zaidi.

Makam wa Rais, Samia amesema kuwa ripoti imetilia mkazo suala la lishe kama msingi wa maendeleo hivyo kuzungumzia maendeleo inamaanisha afya,elimu ,ajira ,kuondoa umasikini na kuleta usawa.

Amesema suala la usawa limewaangalia kuwajengea uwezo wakina mama kutokana na akina mama kuwa walezi wa jamii ,wazalishaji wakubwa katika sekta ya kilimo lakini wanaume wanawajibu wa kushiriki katika suala hilo.

Nae Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto , Ummy Mwalimu amesema kama wizara inatambua tatizo la lishe na kusema kwa kiwango tulichofikia lazima kipungue.
Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu, Mkurugenzi wa Jukwaa la Lishe Tanzania (Panita), Tumaini Mikindo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy  Mwalimu wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa uzinduzi wa ripoti ya Dunia iliyoandaliwa na Jukwa la Lishe Nchini (PANITA) iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam leo. 
Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu akizungumza na wadau wa lishe katika uzinduzi wa ripoti ya lishe ya dunia katika uzinduzi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Jukwaa la Lishe Tanzania (Panita), Tumaini Mikindo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kuzindua ripoti ya lishe ya Dunia.
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images