Waendesha bodaboda wakikokota pikipiki zao wakati wa kuvuka katika njia ya mabasi ya mwendokasi eneo la Magomeni Mwembechai jijini Dar es salaam leo, ikiwa ni ushahidi tosha kwamba utii bila shuruti katika jamii ni jambo linalowezekana kabisa endapo kama sheria zilizopo zitasimiwa na kuonekana zinasimamiwa na hatua kuchukuliwa kwa wakosaji bila simile. Yaani, baada ya mamlaka husika kuanza kuchukua sheria kwa wananchi wabishi na wakorofi na kuwafikisha mahakamani mara moja, watumiaji wengi wa barabara, hasa wenye vyombo vya moto vya magari na pikipiki wameshika adabu zao. Kila wafikapo katika njia za mwendo kasi aidha hawapiti kwenye barabara hizo, ama hushuka kwenye pikipiki zao na kukatisha huku wakiwa wakizikokota. Ufuatiliaji wa Globu ya Jamii umeshuhudia haya yakifanyika bila kuwa na usimamizi ama ulinzi. Tunatarajia hali hii itashamiri katika kila nyanja ya maisha yetu.
Mdau akikatisha barabara ya mwendo kasi maeneo ya Magomeni Usalama akiwa anakokota pikipiki yake. Sheria ni kwamba ukatisha ukiwa umepanda hiyo pikipiki ni kosa na ni kupelekwa rumande na kesho mahakamani. Hakuna mjadala wala faini....
Hata waendesha baiskeli nao wamekuwa wapole. Kabla ya sheria kuchukua mkondo wake hapo angepita akiwa ameipanda hiyo baiskeli na kuvuka. Sheria ya njia ya mwendo kasi ya UDART inasema endapo kama utagongwa na basi ni wewe utayekuwa umefanya kosa....
Huyu mdau alikuwa akikokota pikipiki yake iliyosheheni mzigo mkubwa. Pikipiki ikamshinda maeneo ya Magomeni Kagera. Utii wa sheria bila shuruti oyeeee...!!!