Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho amesema kuwa kasoro ambazo zimejitokeza katika mtambo wa kupima mafuta Bandarini (Flow Meter) zinapatiwa ufumbuzi na mkandasi wa vifaa vya mitambo hiyo.
Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Chamuriho amesema kuwa mtambo huo lazima uangaliwe kwa umakini kutokana na serikali ndipo inapata kodi yake halisi ya mafuta yanayoshuwa na meli.
Amesema kuwa mkandarasi msambazaji vifaa kutokana na mkataba ni lazima ahakikishe kwa vitu viliyopata kasoro kutatua kabla ya tatizo halijawa kubwa au kutojirudia.
Aidha amesema kuwa suala la kamera ambazo zimepata hitilafu baada ya kupigwa na radi zitengenezwe mara moja na tatizo lisijirudie wakati mwingine kutokana na umhimu wa kamera katika eneo hilo.
Amesema kutokana hali hiyo amemtaka Kaimu Meneja wa Bandari kupeleka taarifa jumatatu ikiwa na ina vitu vyote ambavyo vipo katika mradi wa mtambo huo.
Kwa upande wa Meneja Mradi Mtambo wa kupima mafuta, Mhandisi Mary Mhayaya amesema kuwa jana kumetokea changamoto katika mtambo iliyotokana na mafuta kukwama kutokana na uchafu ambapo wameweza kusafisha.
Aidha amesema katika majaribio wa mtambo huo umeweza kuwa na mafanikio baada ya meli tatu kushusha mafuta bila matatizo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho akipata maelekezo kutoka kwa Meneja Mradi wa Mtambo wa Kupima Mafuta wa TPA, Mhandisi Mary Mhayaya leo wakati ziara kushtukiza na katibu Mkuu huyo Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano –Uchukuzi, Mhandisi Dk. Leonard Chamuriho akiwa juu ya mtambo akiangalia miundombinu yake wakati wa ziara ya kushtukiza katika mtambo wa kupima mafuta Kigamboni, jijini Dar es Salaam.
Mtambo wa Kupima Mafuta wa TPA,uliopo Kigamboni, jijini Dar es Salaam.