Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AMFAGILIA RAIS MAGUFULI


MKUTANO WA RAIS MAGUFULI NA WAZEE WA DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick  kuzungumza na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Hemed Mkali wara baada ya  kuwasili kwenye ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Dini mbalimbali waliofika wakati wa mkutano wake na Wazee wa jiji la Dar es Salaam.



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam  kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam  kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Minister for Foreign Affairs, East Africa, Regional and International Cooperation of the United Republic of Tanzania Dr. Augustine Mahiga attends Ministerial Meeting of the ICGLR in Luanda, Angola

$
0
0
Hon. Dr Augustine Mahiga, Minister for Foreign Affairs, East Africa, Regional and International Cooperation of the United Republic of Tanzania, leading the Tanzanian delegation at the Ministerial Meeting of the International Conference of  the Great Lakes Region (ICGLR) held on 11th February 2016 in Luanda, Angola. Sitting behind is Amb. Samuel Shelukindo, Director for Africa and Mr. Mobhare Matinyi. 
The Ministerial meeting considered a number of issues including the status of member states' contributions, the status of the implementation of the Pact on Security, Stability and Development in the Great Lakes Region as well as the security situation in the Region particularly Burundi, South Sudan, Central African Republic and Eastern DRC

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI

YALEEEE YALEEEEE......DEREVA WA BAJAJI APONEA CHUPUCHUPU JIJINI MBEYA

$
0
0
Baadhi ya wananchi wa Eneo la Njiapanda Stereo Mkabala na Kanisa la Roma Jijini Mbeya wakiwa katika Bajaji iliyogongwa na Lori  aina ya Fuso   lililo kuwa likiiovateki Bajaji hiyo na kupelekea pia Lori  hilo kuingia kwenye Mtaro kutokana mwendo  kasi. Hakukuwa na majerui wala kifo..
Bajaji iliyogongwa na Roli ikiwa katika hali ya kusikitisha 
 Baadhi ya Wananchi wa Eneo hilo wakishuhudia Tukio hilo lilotokea leo Jijini Mbeya
Gari aina ya Fuso (Roli) likiwa katika jitihada ya kutolewa kwenye Mtaro.
PICHA NA MR.PENGO MMG MBEYA.

WAZIRI UMMY MWALIMU ATEMBELEA MUHIMBILI KUKAGUA UTEKELEZAJI WA AGIZO LA RAIS MAGUFULI

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu ametembelea hospitali ya Taifa Muhimbili kukagua utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli la kuwataka watumishi wa wizara hiyo waliokuwa wakilitumia jengo la Kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto kuhamisha ofisi zao na kuliacha kwa ajili ya matumizi ya wodi ya wazazi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo katika hospitali hiyo, Waziri Ummy amesema kuwa mpaka kufikia kesho tayari jengo hilo litakuwa limeanza kutumika kwa kuwa watafanya kazi ya kuhamisha makabrasha ya watumishi hao usiku kucha kuhakikisha agizo la Rais John Magufuli linatekelezwa mara moja.
FSA_6533

Picha mbalimbali zinaonesha Waziri Ummy Mwalimu akikagua utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli pamoja na watumishi na vibarua wakihamisha nyaraka na makabrasha mbalimbali kutoka kwenye jengo lililokuwa likitumiwa kama ofisi na watumishi wa wizara hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.

FSA_6416FSA_6443


MKUU WA WILAYA YA IRINGA MHE RICHARD KASESELA AONGOZA ZOEZI LA UOKOAJI WAATHIRIKA WA MAFURIKO KIJIJI CHA PAWAGA

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Iringa 
Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Iringa zimesomba mashamba na nyumba na kuwaacha wananchi wengi wakiwa hawana mahali pa kukaa. 
Vitongoji vilivyo athirika sana ni Kisanga, Nyallu, Makoka na Mbughani. Mpaka sasa bado idadi isiyo rasmi inakadiliwa watu zaidi ya 200 bado wamezingirwa na maji siku ya 4. 
Juhudi za uokoaji zikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela zimefanikiwa kuokoa watu 399 kitongoji cha Kisinga, watu 38 kutoka kitongoji cha Makoka, na watu 23 kutoka kitongoji cha Nyalu. Jeshi la polisi lilitoa helicopter kusaidia uokoaji na pia kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kilikuwa mstari wa mbele kwenye zoezi hilo. 
Maeneo mengi yalihitaji waogoleaji mahiri ili kuwafikia wananchi. Zoezi linaendelea hado sasa. shule 2 zimetengwa kwa ajili ya kupokea wahanga wa mafuriko shule ya msingi Itunundu na shule ya msingi Kisanga.
kitongoji cha Nyalu wamezingirwa na maji


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akiongoza uokoaji wa wananchi walioathirika na mafuriko kijiji cha Pawaga
Eneo lililoathirika
Njia haipitiki kwa vyombo vya moto
Familia zikiwa imezingirwa na maji.
Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA

Bingwa wa Olimpiki katika kuogelea kuwafunda makocha, waogeleaji wa Dar Swim Club

$
0
0
Muogelaji nyota wa zamani wa dunia na mshindi wa medali ya dhahabu ya michezo ya Olimpiki kwa upande wa wanawake, Penelope “Penny” Heyns wa Afrika Kusini ataendesha mafunzo ya siku mbili ya kuogelea kwa makocha wa klabu maarufu ya mchezo huo hapa nchini, Dar Swim Club. 

Penny ambaye ni bingwa wa kihistoria wa michezo ya Olimpiki kwa staili ya ‘Breastroke’ atawasili nchini Alhamis akitokea  Afrika Kusini tayari kuendesha mafunzo hayo kwa makocha watano wa klabu hiyo. 
Katibu Mkuu wa Dar Swim Club, Inviolata Itatiro alisema jana kuwa maandalizi yamekamilika na klabu yao itagharimia mafunzo hayo kwa lengo la kuboresha viwango vya wachezaji wao na makocha kwa ujumla. 
Inviolata alisema kuwa makocha wao watakaoshiriki katika kozi hiyo kuwa ni Michael Livingstone, Ferick Kalengela, Radhia Gereza, Kanisi Mabena, Adam Kitururu, Simon Ngoya na Salum Mapunda. Alisema kuwa makocha wao wanasifa za ngazi ya juu ya ufundishaji wa mchezo huo, kutokana na kukua kwa kasi kwa mchezo huo, wameona bora wapate mbinu za kisasa ili kwenda na wakati. 
“Makocha wetu wote watano ni bora katika ufundishaji, waliwahi kupata mafunzo Dubai, Marekani na nchi mbalimbali, lakini klabu imeona kuendelea kuwapa mbinu zaidi ili kufikia malengo yetu ya miaka 10,”
 “Tunataka kuona kila mtoto anacheza mchezo wa kuogelea, tulianza na watoto wadogo ambao kwa sasa ni mastaa katika mchezo huo na kuweza kushinda medali mbalimbali nje ya nchi,” alisema Inviolata. 
Alisema kuwa wao wameamua kupromoti mchezo wa kuogelea kwa vitendo ili kuona siku moja watanzania wanafuzu kushindana michezo ya Olimpiki, Jumuiya ya madola na mashindano ya dunia siyo kupata nafasi za upendeleo kama ilivyo sasa. 
Alifafanua kuwa Penny alitwaa medali za dhahabu katika mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika mjini Atlanta 1996 kwa mita 100 na 200 na wanaamini kuwa ujio wake utapandisha morali wachezaji wao na makocha. 
Wakati huo huo; klabu hiyo imeendesha zoezi la ukusanyaji fedha kwa ajili ya kufanikisha semina hiyo na kufikia lengo lake. Inviolata alisema kuwa zoezi hilo limefanikiwa kutokana na msaada wa wadhamini mbalimbali ambao ni Best Western (Coral Beach Hotel), Euopcar, Butcher Shop Dar es Salaam, CapeTown Fish Market, Warere, Lemon Spa,Pyramid Consumers, Instyle Hair and beauty salon, Coca Cola, Zen Spa, Karambezi Cafe, The Water Front na Southern Sun Dar es Salaam. “Nawapongeza watu waliochangia na kufanikisha zoezi hili, makocha na waogeaji wetu watapata mafunzo bure na si kwa kuwabana wazazi au walezi wao kama ilivyokuwa awali,” alisema Inviolata.

 Penny mara baada ya kushinda medali katika mashindano ya Olimpiki
 Meneja wa hotel ya Coral Beach, Glynis Markus (katikati) akimpa zawadi maalum Katibu Mkuu wa klabu ya Dar Swim Club, Inviolata Itatiro (kulia) baada ya klabu hiyo kuwa mabingwa wa jumla wa mashindano ya Taliss 2016. Kushoto ni mratibu wa shighuli hiyo, Deidre De Wet.

Meneja wa hotel ya Coral Beach, Glynis Markus (kulia) akimpa zawadi maalum  kocha mkongwe wa mchezo wa mchezo wa kuogelea wa klabu ya Dar Swim Club, Ferick Kalengela wakati wa hafla ya kutunisha mfuko wa timu hiyo ili kuendesha semina ya makocha na wachezaji wao iliyopangwa kuanza Ijumaa ijayo. Wengine katika picha ni makocha na waogeaji wa timu hiyo.

MGODI WA BULYAHULU WAIPATIA MSALALA ZAIDI YA MILIONI 700 KWA AJILI YA USHURU WA HUDUMA

$
0
0
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi hundi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Patrick Karangwa,ikishuhudiwa na Mkuu wa wilaya ya Kahama Vita Kawawa(katikati)
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kahama wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutembelea mgodi wa Bulyanhulu
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Vita Kawawa akizungumza wakati wa ziara yake katika mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu ambapo amesisitiza kuwa kodi ya ushuru wa huduma iliyotolewa na Mgodi wa Bulyanhulu itumike vizuri kujenga miundombinu ambayo wananchi wataiona kwa macho
Afisa Maendeleo na Mahusiano wa mgodi wa Bulyahulu ,Sara Teri akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Vita Kawawa,kushoto kwake ni Mshauri wa Mahusiano ya Kampuni ya Acacia na Serikali , Alex Lugendo.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe Vita Kawawa (Kushoto) akielekea katika eneo la mgodi wa chini ya ardhi Bulyanhulu.

INTRODUCING "EH MAMA" VIDEO by Aethan from Uganda

$
0
0
Today TMMG/Klear Kut Entertainment release the second music video for the single “EH MAMA”. Eh Mama is the official single from Mr. So UG’s sophomore album, Destination AFRICA and it features the “RnB Kyabazinga” Maro. 

The song is produced by one of the most sought after UG Hip-Hop/Urban music producers in Uganda Aethan and it’s a remake of an old Ugandan folk song which attributed it to being a fan favorite in clubs and on radio.
“Eh mama for me brings back many childhood memories driving around with my father, as he played the original version.” Mith explained. “I decided to do this remake for it, so this generation can have their moment with the song whether in clubs, bars, cars, or just chilling back at home”


The video was shot in various locations of Kampala and it was shoot iViZUALZ. The video comprises of vibrant, different sceneries of Kampala with The Mith and Maro performing in different locations that keep the video true to the song and rich in concept while driving the message to the viewer. 
“The video had to be shot like so it stays authentic to the song,” Mith reflecting on the concept of the video. “We didn’t want to stray unnecessarily far from what we were saying on the in the song and the general feel of the song. That’s why it was done like that.”


In this video people will connect and engage with the storyline since the concept is something they can relate to. The video conveys and communicates a feeling in addition to its implicit story through its storyline.
The album is available on iTunes and all other digital platforms. (iTunes link: http://apple.co/1PkhHUj)

WAKAZI WA KAHAMA,GEITA NA MWANZA WAKAE MKAO WA KULA TAMASHA LA PASAKA.

$
0
0
Mkurugenzi wa Msama Promotions Ltd,ambao ndio waandaji wa tamasha la Pasaka,Bwa Alex Msama akizungumza na Waandishi wa habari mapema leo Ofisini kwake kuhusiana na tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika Kahama,Geita na Mwanza.Msama amewataka wapenzi wa tamasha hilo wajitokeze kwa wingi na kupokea neno la Mungu kupitia waimbaji hao.Tamasha hilo mwaka huu linatimiza miaka 16 tangu lianzishwe hivyo linatarajia kuwa tofauti na miaka ya nyuma.

WAIMBAJI nyota wa nyimbo za Injili Faustine Munishi anayeshi Nairobi, Kenya na Jesca Honore ‘BM’ wamethibitisha kupamba jukwaa la tamasha la paska litakaloanza kufanyika Machi 26 Mkoa wa Geita.

Akizungumza jana Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo Alex Msama, alisema kuwa waimbaji hao wametihitisha kuimba siku hiyo, ambako bado kamati hiyo itaendelea kutaja waimbaji wengine wakubwa kwani bado iko kwenye mazungumzo nao.
Msama alisema kamati yake inaendelea kuchagua waimbaji watakaoimba katika mikoa wa Mwanza Machi 28, wilaya ya Kahama Machi 27 na Geita kwakuwa waimbaji ni wengi wanaomba kuimba katika tamasha hilo la kimataifa.

Msama ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Msama promotions, amesema kwakuwa kamati hiyo kwa mwaka huu inatoa nafasi kubwa kwa waimbaji wa ndani amboa ndio wengi walioomba wanaangalia namna ya kukubaliana hivyo huenda kukawa na waimbaji wengi zaidi katika tamasha hili la kuliko yaliyowahi kufanyika mikoani.

Amesema Munishi ni mwimbaji wa kwanza aliethibitisha kutoka nje ya Tanzania huku akisistiza kuwa huenda wakamalizia na wengine kutoka Afrika kusini na nchi nyinginezo za Afrika. Msama ilieleza kuwa kamati yake imeamua kumleta Munishi kutokana na maombi ya wadau mbalimbali wa muziki wa injili hapa nchini .

“Naomba niwafahamishe mashabiki wa muziki wa Injili kwamba tumekubali maoni yao, sasa wajipange kumpokea Munishi na atatumbuiza Mwanza, Kahama na Geita wakae mkao wa kupokea neno la mungu kupitia mtumishi wa Mungu” amesema Msama'“Kama mnavyojua mwaka huu tunatimiza miaka 16 tangu tuanze Tamasha la Pasaka, hivyo tunaleta kitu tofauti kabisa,” alisema Msama na kuongeza kuwa hivi sasa Munishi pia ni mhubiri wa neno la mungu..

Baadhi ya nyimbo zilizompa umaarufu Munishi ni pamoja na Malebo, Siasa na Injili, Paka Kulia Usiku, Kuhubiri ni Taalum, Jirani, Jirani Mchokozi, Fasheni ni Yesu, Nimeamua Mwenyewe na Maji Yana Mdudu.Kwa mujibu wa Msama hilo litakuwa tamasha kubwa la nyimbo za kumsifu Mungu na litakuwa na tofauti kubwa ukilinganisha na matamasha mengine yaliyowahi kuandaliwa na kampuni yake.
Msama alimalizia kusema licha ya kuja mwimbaji wa ndani Jesca BM ambaye anatamba na baadhi ya nyimbo kama ‘Napokea’, Nakuabudu na Nimezima Ukimya,’ waimbaji wengine waliothibitisha ni pamoja na Rose Muhando na Bonny Mwaitege.

INTERNSHIP OPPORTUNITIES AT ESRF

$
0
0
esrfMore details on the documents below;-

SHUKRANI KWA WALIOTUFARIJI WAKATI WA MSIBA WA MAMA YETU LYDIA BANZI

$
0
0


Familia ya PCP (Rtd) Nicas Pius Banzi wa Ukonga Dar es Salaam inayoheshima kutoa shukrani za dhati kabisa kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walishiriki kwa namna moja ama nyingine kufanikisha msiba, mazishi na hatimaye matanga ya mama yetu mpendwa LYDIA JACOB BANZI aliyefariki dunia January 21, 2016 katika hospitali ya Rabininsia na Kuzikwa katika Makaburi ya Pugu Dar es Salaam January 24, 2016.

Kwa vile waliotuunga mkono na kutufariji wakati wa kipindi hiki kigumu  cha msiba ni wengi na ni vigumu kuwataja kwa majina. Familia, inapenda kwa heshima na taadhima nyingi kutoa shukrani za Jumla ikiwa omba kuzipokea shukrani hizo kwa moyo ule ule kama milivyo tuunga mkono.

Hata hivyo tunapenda kutoa shukrani za pekee kwa madaktari na wauguzi wote wa Muhimbili (MOI) hospitali waliomuhudumia marehemu katika kipindi cha ugonjwa wake na mpaka umauti ulipomkuta. Tunashukuru Uongozi wa Jeshi la Magereza Tanzania, Parokia ya Mtakatifu Agustino Ukonga ikiongozwa na Baba Paroko Steven Nyilawila, Jumuiya ya Mtakatifu Anna, Baba Askofu Antony Banzi wa Jimbo katoliki la Tanga, Viongozi waandamizi na wastaafu wa serikali waliofika kutufariji wakiongozwa na waziri mkuu mstaafu Mizengo Pinda. 

Tunawashukuru Sana. Mungu Awabariki.

KAMPUNI YA RAM NUCLEAR KUTOKA SENNINGERBERG YAONESHA NIA YA KUWEKEZA KWENYE UMEME WA URANIUM

$
0
0
Meneja Mkuu kutoka Kampuni ya Ram Nuclear yenye makazi yake Senningerberg, Bastian Ringsdorf (mbele wa kwanza kulia) akielezea uzoefu wa kampuni hiyo katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia madini ya urani katika kikao chake na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa akifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Meneja Mkuu kutoka Kampuni ya Ram Nuclear yenye makazi yake Senningerberg, Bastian Ringsdorf (hayupo pichani) katika kikao chake na kampuni hiyo pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake.
Meneja Mkuu kutoka Kampuni ya Ram Nuclear yenye makazi yake Senningerberg, Bastian Ringsdorf akifafanua jambo katika kikao hicho.
Baadhi ya watendaji kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Nishati na Madini wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Meneja Mkuu kutoka Kampuni ya Ram Nuclear yenye makazi yake Senningerberg, Bastian Ringsdorf (hayupo pichani)

WAZIRI MKUU MAJALIWA AAGANA NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI KUWAIT, DKT. MAHADHI JUMA MAALIM

$
0
0
 Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe Mahadhi Juma Maalim  ambaye alikwenda  ofisini kwa  Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuaga Februari 15, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Mahadhi Juma Maalim ambaye alikwenda Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam kuaga Februari 15, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Airtel yainua kikundi cha vijana wajasiriamali kupitia Airtel Fursa jijini Dar es Salaam.

$
0
0
Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (Kulia), akikabidhi funguo ya pikipiki aina ya guta kwa mmoja wa wakilishi wa kikundi cha Akilimali Fatuma Rashidi, ikiwa ni sehemu ya msaada wa vifaa vya kutengenezea sabuni, walivyowakabidhi kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, waliopo kigamboni jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Wanaoshuhudia (kutoka kushoto) ni wanakikundi wa Akilimali wapatao vijana 12.
Mwakili wa kikundi cha Akilimali Fatuma Rashidi kilichopo kigamboni jijini Dar Es Salaam wanaojishughulisha na kutengeneza sabuni, akiwa mwenye furaha baada ya kukabidhiwa na Airtel Tanzania, msaada wa pikipiki ya magurudumu matatu aina ya Toyo, malighafi na vifaa mbali mbali vya shughuli hiyo, kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla fupi iliyofanyika katika eneo lao la biashara kigamboni jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki hii.
 Mwakili wa kikundi cha Akilimali Fatuma Rashidi kilichopo kigamboni jijini Dar Es Salaam wanaojishughulisha na kutengeneza sabuni, akiwa mwenye furaha baada ya kukabidhiwa na Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (Kulia), msaada wa pikipiki ya magurudumu matatu aina ya Toyo, malighafi na vifaa mbali mbali vya shughuli hiyo, kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’, katika hafla fupi iliyofanyika katika eneo lao la biashara kigamboni jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki hii. Wanaoshuhudia ni wanakikundi wa Akilimali wapatao vijana 12.

· Airtel Fursa imewapatia pikipiki aina ya Guta, vifaa vya kutengenezea sabuni na vitendea kazi kwa vijana hapa nchini

Akili Mali ni kikundi cha vijana wajasiriamali 12 wanaojihusisha na biashara ya kutengeneza sabuni za maji za kufanyia usafi jijini Dar Es Salaam, ambao leo wamepokea vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka Airtel Tanzania kupitia mpango wake wa Airtel FURSA. Kundi hilI limepokea vifaa mbalimbali vikiwemo pikipiki aina ya Guta, vifaa vya kufungia sabuni, vifaa vya uzalishaji na vifaa vya usalama vya kufanyia kazi hiyo.

Meneja wa Airtel huduma kwa jamii bi, Hawa Bayumi aliwapongeza kundi la Akilimali kwa uvumilivu wao na kufanya kazi kwa bidii. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano alisema, "Airtel imeona sifa hizo na juhudi zao na ndio maana leo imewakabidhi vifaa vitakavyowawezesha kufanya kazi kwa haraka na endelevu ili kukuza biashara yao".

"Kikundi cha Akilimali kimeshapata mafunzo ya biashara ya ujasiriamali kupitia Airtel FURSA na wataendelea kupata ushauri na uongozi kutoka kwa washauri wa Airtel FURSA ili kuwawezesha kuimarisha biashara yao " aliongeza Bayumi

Bayumi alielezea kuwa, "mwaka huu Airtel kupitia mpango wake wa Airtel FURSA umepanga kutumia zaidi ya bilioni moja kwa kuwawezesha vijana mbalimbali hapa nchini na kutoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi na kuchangamkia nafasi hii muhimu katika maisha yao.

"Kama kampuni ya simu inayojali jamii yake, tumeahidi kuwawezesha vijana hapa nchini kwa kuwawezesha kwa njia mbalimbali ili waweze kufikia ndoto zao.." alisema Bayumi.

Kwa upande mwingine kundi la Akilimali waliahidi kuweka ujuzi wao wote na kutumia kwa umakini vifaa vilivyotolewa kwao na Airtel kwa matumizi bora na yaliyo sahihi. Kiongozi wa kikundi hicho, Fatuma Rashidi, aliishukuru Airtel kwa msaada na kutoa wito kwa mashirika mengine hapa nchini kuiga mfano wa Airtel.

"Hatukuamini siku moja tutakuwa na uwezo wa kufikia malengo yetu katika biashara hii, tunaahidi kuweka juhudi zaidi na kutumia vifaa hivi na mafunzo tuliyopata kwa umakini zaidi kuhakikisha tunainua zaidi biashara yetu," alisema Fatuma.

Airtel FURSA, inazunguka nchi nzima kukutana na vijana kwa lengo la kuwapa elimu ya ujasiriamali na kisha kutoa uwezeshaji kwa vijana ili kuhakikisha kuwa wanafikia ndoto zao.

HALI YA WAKIMBIZI NCHINI

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Kama inavyofahamika, tangu mwezi Aprili mwaka jana, nchi yetu imekuwa ikipokea raia toka Burundi wanaoingia nchini kuomba hifadhi ya ukimbizi kutokana na hali ya machafuko iliyotokea nchini mwao.

Hadi kufikia tarehe 10 Februari, 2016, kiasi cha wakimbizi 129,210 toka nchini Burundi wamepokelewa nchini.

Kati ya hawa, wakimbizi 79,290 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma. Wengine 45,487 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyoko wilayani Kibondo na 4,543 wanahifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Mtendeli iliyoko wilayani Kakonko mkoani Kigoma.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) na wadau wengine imekuwa ikitoa huduma muhimu kama vile za afya, chakula, maji na ulinzi ili kuhakikisha kuwa wakimbizi hawa wanaishi kwa usalama.

Hata hivyo, ukiacha wakimbizi hawa walioanza kuingia nchini mwezi Aprili 2015, Tanzania bado ina wakimbizi wengine ambao wapo katika Kambi ya Nyarugusu. Katika kambi hiyo kuna Wakongo 61,887, Wasomali 150 na wengine 189 toka nchi mbalimbali. Hii ina maana kuwa hadi kufikia tarehe 10 Februari, 2016 nchi yetu ilikuwa na jumla ya wakimbizi 191,436 ambao wamehifadhiwa katika makambi.

RAIA WA NJE WALIOOMBA HIFADHI NCHINI

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pia imeendelea kushughulikia raia wa nchi za nje ambao baada ya kuingia hapa nchini wameomba kupatiwa hifadhi ya ukimbizi.

Hadi sasa maombi 815 ya waomba hifadhi yameshashughulikiwa na Kamati ya Kitaifa ya Kuwahoji Waomba Hifadhi (NEC).

Kati ya hawa, 735 wametoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, 25 wametoka nchini Burundi, 14 wametoka nchini Rwanda na 15 wametoka nchini Yemen. Wengine 18 wametoka nchini Syria, 3 Iran, 2 Kenya na 3 wametoka nchini Eritrea.

Hawa wote maombi yao yameshashughulikiwa na matokeo yatatolewa hivi karibuni baada ya uchambuzi yakinifu kukamilika.

Maombi mengine 147 pia yamepokelewa na hivi karibuni Kikao cha NEC kitakaa kujadili maombi yao.

Kati ya hawa raia 24 wametoka nchini Yemen, 13 Syria, 3 Somalia, 6 Rwanda na 18 kutoka DRC. Wengine 2 kutoka Uganda, 1 kutoka Sudan Kusini na 80 kutoka nchini Burundi.

Kundi hili la waomba hifadhi ni wakimbizi ambao waliingia nchini kabla ya mwezi Aprili, 2015.

Pamoja na kuwafahamisha wananchi na wadau wengine kuhusu hali ya wakimbizi nchini, Taarifa hii pia inatolewa ili kuweka sawa habari potofu zilizoandikwa katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la This Day toleo la tarehe 15 Februari, 2016 kuwa Tanzania ina wakimbizi 1,960,000 na kuwa 63,000 kati ya hawa, wengi wao kutoka Syria na Yemen, wameomba hifadhi Tanzania. Taarifa za gazeti hili sio za kweli.

IMETOLEWA NA ISAAC J NANTANGA
MSEMAJI - WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

BASATA YAAGIZA WASANII WOTE KUSAJILIWA NA YAONYA MAPROMOTA

$
0
0
BASATA LAAGIZA WASANII WOTE KUSAJILIWA, LAONYA MAPROMOTA WATAKAOTUMIA WASANII WASIOSAJILIWA

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) linawataka wasanii wote nchini kuhakikisha wamesajiliwa na kuwa na vibali vya Baraza kwani kufanya vinginevyo ni kuvunja sheria ya Bunge namba 23 ya mwaka 1984 iliyolianzisha BASATA ambayo inamtaka mtu yeyote anayejihusisha na shughuli za Sanaa kuwa amesajiliwa na kupewa kibali na BASATA.

Aidha, BASATA linawaagiza Wakuzaji Sanaa wote (Mapromota) wanaoendesha matukio ya Sanaa kama vile matamasha, mashindano, maonyesho na utoaji tuzo nchini kuhakikisha wanafanya kazi na Wasanii waliosajiliwa na wenye vibali vya BASATA na si vinginevyo.

Sambamba na hili, BASATA linawaagiza wamiliki wote wa studio (Production Houses) zinazozalisha kazi za Sanaa kuzisajili mara moja na kuhakikisha zinakuwa na vibali halali vya Baraza la Sanaa la Taifa.

Ieleweke kwamba kwa mujibu wa sheria hii ya BASATA, Baraza limepewa mamlaka ya kutoa vibali na kuratibu matukio yote ya Sanaa nchini hivyo kuanzia sasa Baraza litaanza udhibiti wa matukio haya ya Sanaa hasa katika kuongeza sharti la kuwataka waandaaji wote wa matukio ya Sanaa kuwataka wasanii watakaoshiriki matukio yao kuwa wamesajiliwa na kupewa vibali na BASATA.

BASATA halitavumilia kwa namna yoyote kuona Mkuzaji Sanaa (Promota) akitumia wasanii wasiosajiliwa na kuwa na vibali kutoka BASATA kwani kufanya hivyo ni kuvunja sheria za nchi hasa sheria hiyo namba 23 ya mwaka 1984 inayoelekeza usajili na utoaji vibali kwa wadau wote wa Sanaa.

Itakumbukwa kwamba mnamo Mwaka 2013 Serikali kupitia Sheria ya Ushuru wa Forodha ilitangaza rasmi kuzirasmisha sekta za muziki na filamu. Sheria hii pia inawataka wasanii wote nchini kusajiliwa na kupewa vibali na BASATA na kinyume chake ni uvunjaji wa sheria.

Hata hivyo, toka kuanza kwa mchakato huu wa urasmishaji sekta ya Sanaa ni wasanii wa muziki wa injili pekee ndiyo wamekuwa wakisajiliwa kwa wingi huku wale wa muziki wa kizazi kipya na filamu wakisuasua bila kuwepo kwa sababu za msingi.

BASATA limekuwa likichukua hatua kadhaa kurahisisha mfumo wa usajili wa wasanii ambapo kwa sasa msanii anaweza kupata fomu ya usajili kupitia mtandaoni www.basata.go.tz au kwa maafisa Utamaduni wa Wilaya na baadaye kujaza fomu na kutakiwa kuziwasilisha BASATA zikiwa zimeambatanishwa na wasifu binafsi (CV) wa Msanii husika.

Aidha, gharama za usajili ni kiasi cha Tsh. 75,000/- pekee ambapo fomu hupatikana kwa Tsh. 5, 000/-, Usajili 30,000/- na kibali cha kila mwaka 40,000/- 

Kwa upande wa studio na wakuzaji Sanaa (Mapromota) gharama ni sawa na za msanii isipokuwa tofauti huwa kwenye kibali abapo wao hulipa kiasi cha Tsh. 200.000/- kwa mwaka. 
SANAA NI KAZI TUIKUZE, TUILINDE NA KUITHAMINI.

Godfrey L. Mngereza 
KATIBU MTENDAJI, BASATA

TEASER JOTO LA ASUBUHI JUMANNE FEBRUARY 16, 2016

WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA UJENZI YA CRJE WADAI MIKATABA HALALI

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images