Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110139 articles
Browse latest View live

GOVERNMENT CHALLENGED TO INVOLVE PRIVATE SECTOR IN DECISION-MAKING

$
0
0
Deputy Head of Development Cooperation, Lars Johansson said yesterday in Dar es Salaam that for Tanzania to attain her targeted economic development she must involve the private sector which contributes about 70 percent of the country’s economic growth.

Johansson made the remarks before presenting certificates of participation and diplomas to 15 Tanzanians after completing a Private Sector Development (PSD) training programme that was introduced early last year.
The training programme, sponsored by the Swedish Government through SIDA, is designed to strengthen public and private sector cooperation in order to facilitate economic development.

The official added that the government alone cannot accelerate economic development by 100 percent without involvement of the private sector.
The sector, he noted, plays an important role in accelerating development, especially in education and health.Hence the programme aims mainly to bring together public servants and private workers to share experiences and to explore on possible ways of solving development challenges.
Deputy Head of Development Cooperation Swedish Embassy, Lars Johansson.
 Permanent Secretary (PS) in the Ministry of Industry, Trade and Investment, Adolf Machemba.
The Swedish Embassy has challenged the government to involve private sector in preparations of development plans to achieve its goal of becoming a middle income country by 2025.
The training programme is offered in Tanzania by the Swedish government for one year and it covers areas of economic cooperation, management as well as entrepreneurship.

Permanent Secretary (PS) in the Ministry of Industry, Trade and Investment, Adolf Machemba said the programme is crucial for the nation as it also supports cooperation of private and public sectors as stipulated in the Public Private Partnership Act 2010.“We applaud the Swedish government for the training programme as it paves the way for the government to be able to meet the goal of becoming a middle income country,” the PS noted.

He said that the programme shall help to create more employment opportunities in the private sector and help to reduce youth unemployment.
 Participant of the training programme, sponsored by the Swedish Government through SIDA.

PS Machemba observed that the programme will also empower public servants with capacity to deliver effectively to the people and facilitate accountability and transparency.The official assured the Swedish government of full support from the Tanzanian government in efforts to enhance cooperation between public and private sectors.

Peter Lanya, Chairman of the programme, said the training has provided the ground for the private sector to be part of the policy making process.

WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI WATUNUKIWA TUZO ZA HESHIMA KUTOKA CHUO KIKUU AFRICAN GRADUATE UNIVERSITY CHA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Profesa Stephano Nzowa akimvika kofia Mwimbaji wa nyimbo za injili, Stella Joel wakati akimtunuku Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Mahusiano katika mahafali hayo. Kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho kutoka nchini Zambia, Profesa Timothy Kazembe.
Hapa Stella Joel akipongezwa na ndugu yake.
Mkuu wa Chuo hicho kutoka nchini Zambia, Profesa Timothy Kazembe akimvika kofia Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Ado Novemba wakati akimtunuku tuzo ya heshima ya udaktari. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania (FCC), Dk.Fredrick Ringo akimkabidhi tuzo hiyo.
Waimbaji wa nyimbo za injili, Stella Joel (kulia) ambaye ametunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Mahusiano na mwenzake Upendo Mbila (kushoto), aliyetunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Umma wakiteta jambo kwenye mahafali hayo ya pili ya Chuo cha African Graduate University yaliyofanyika Dar es Salaam juzi.
Wahitimu wakiwa katika picha ya pamoja.
Paul Mbila (kulia), akimvika taji mama yake Upendo Mbila ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za injili baada ya kutunukiwa tuzo Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Umma.


Na Dotto Mwaibale

Chuo Kikuu cha African Graduate University kimewatunuku tuzo za heshima za stashahada ya uzamili katika ngazi mbalimbali waimbaji wa nyimbo za injili nchini kutokana na mchango wao katika jamii.

Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hizo kwa waimbaji hao katika mahafali ya pili ya chuo hicho yaliyofanyika Dar es Salaam juzi Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Askofu Profesa Stephano Nzowa alisema ni jambo jema kuwakumbuka watu mbalimbali waliolifanyia taifa mambo mazuri.

"Chuo chetu kimeona ni vema kikawapa tuzo za heshima watu mbalimbali wakiwemo wanamuziki wa nyimbo za injili kwani kupitia uimbaji wao wameweza kutoa mafunzo kwa watu na wengine kuacha kutenda dhambi na kuamua kuokoka" alisema Profesa Nzowa.

Baadhi ya waimbaji wa nyimbo za injili waliotunukiwa tuzo hizo ni Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Ado Novemba ambaye alitunukiwa tuzo ya heshima ya udaktari, Stella Joel ambaye ametunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Mahusiano na Upendo Mbila aliyetunukiwa Tuzo ya Heshima ya Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Umma.


Akizungumza baada ya kupata tuzo hiyo Stella Joel alisema anamshukuru mungu kwa kumuwezesha kupata tuzo hiyo na kuwa imemtia nguvu kuendelea kufanya kazi ya mungu kupitia uimbaji.

Kwa upande wake Upendo Mbila alitoa shukurani zake kwa chuo hicho kwa kutambua mchango wa waimbaji wa nyimbo za injili kwa kuwapa tuzo hizo ambazo ni muhimu kwao.

PSPF YAZIDI KUJITANUA, WANAFUNZI WA VYUO VIKUU WAZIDI KUMIMINIKA KWENYE MFUKO HUO KWA KUJIUNGA NA MPANGO WA PSS

$
0
0

 Balozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Msanii wa majigambo, Mrisho Mpoto, akitoa elimu juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSS, na umuhimu wa wanafunzi wa UDSM kujiunga na Mfuko huo kupitia Mpango wa uchangiaji wa hiari, PSS. Warsha hiyo iliyokusanya wanafunzi karibu 3,000 ilifanyika ukumbi wa Nkurumah wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani jijini Dar es Salaam, Februari 6, 2016

NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WANAFUNZI wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, sehemu ya Mlimani na wale wa Chuo Kikuu Cha Tumaini, kampasi ya Dar es Salaam, (TUDACO) wameendelea kuchangamkia “fursa” kwa kujiunga na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia Mpango wa uchangiaji wa Hiari, PSS

Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, UDSM, Kitapenda Ahadi na Makamu wake, Irine Deodatus Ishengoma, waliongoza mamia ya wanafunzi pale mlimani kwa kujaa fomu za kujiunga na Mfuko huo.

Hatua ya kujiunga na Mfuko huo ni baada ya semina iliyotolewa na Maafisa wa Mfuko huo, wakiongozwa na mabalozi wa PSPF, Mwanamitindo wa Kimataifa anayefanya kazi zake Ulaya na Marekani, Flaviana Matata, na Msanii maarufu wa hapa nchini, Mrisho Mpoto almaaruu kama “Mjomba”.

Akizungumzia huduma zitolewazo na Mfuko huo, Afisa wa Matekelezo (compliance), wa PSPF, Albert M.Feruzi na Hadji Jamadary, walisema, kuna uchangiaji wa mpango wa lazima, (mandatory scheme) na ule wa hiari Supplementary Scheme) na kuwataka wanafunzi hao ambao wengi wao ni wa mwaka wa mwisho, kuchangamkia fursa kwa kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari.

Nao mabalozi wa PSPF, waliwaeleza wanafunzi hao kuwa pindi wakijiunga na PSPF, hawatajutia uamuzi wao, kwani kuna watafaidika na mafao mbalimbali kama vile mkopo wa elimu, fao la uzazi, mkopo kwa muajiriwa mpya, mkopo wa nyumba na mkopo wa viwanja.

Chuo Kikuu ChaTumaini, tawi la Dar es Salaam, (TUDACO), ndio waliokuwa wakwanza kujiunga na Mfuko huo ikiwa ni wiki moja tu baada ya wanafunzi wenzao hapo hapo kuchukua uamuzi huo.

Afisa Masoko na Uhusiano wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, Rahma Ngassa, (wakwanza kushoto), mhamasishaji, Anthony Luvanda, (wapili kushoto), Mabalozi wa PSPF, Flaviana Matata, (watatu kushoto) na Mrisho Mpoto, (wane kushoto) na Makamu wa Rais wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Irine Deodatus Ishengoma, wakifurahia jambo wakati wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na uongoz wa DARUSO kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, na kufanyika ukumbi wa Nkuruma wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Mamia ya wanachuo walijiunga na Mfuko huo kupitia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS)

Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, sehemu ya Mlimani, wakijaza fomu za kujiunga na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kupitia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari (PSS), wakati wa semina ya siku moja iliyofanyika Ukumbi wa Nkrumah wa chuo hicho mwishoni mwa wiki.
 Afisa wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Gasper Lyimo, akigawa fomu za kujiunga na uanachama wa Mfuko huo, kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, ambao walijiunga na Mpango wa uchangiaji wa hiari, PSS
 Rais wa Serikali ya Wanafuzni wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, DARUSO,

WADAU MBALI MBALI WAJIZOLEA ZAWADI ZA WAFANYE WATABASAMU

$
0
0
Marafiki mbalimbali wa Programu ya Wafanye Watabasamu, hivi karibuni wamejitwalia zawadi za michoro ya ukutani iliyochorwa na Mchora vibonzo maarufu ambaye pia ni Mratibu wa programu hiyo, Nathan Mpangala aka Kijasti, baada ya kuposti mara nyingi kwenye mitandao ya kijamii bango lililokuwa likihamasisha watu kujitokeza kwa wingi kwenye onesho la michoro lililoandaliwa na Nafasi Art Space ya jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita. Pichani Mpangala aliyevaa suruali ya rangi ya Wekundu wa Msimbazi, akimkabidhi zawadi Mjasiriamali, Bi. Joyce Athanas huku wakishuhudiwa na marafiki mbalimbali hivi karibuni. Wengine Waliojitwalia zawadi hizo (hawapo pichani) ni Jesca Haule, Kanuni Midundo, Linah Mrimia, Orest Kawau wa Magic Fm na Othman Michuzi wa Michuzi Blog.
Mchoraji nguli nchini, Komredi Lute Mwakisopile (mwenye kifriji), akidakishwa zawadi yake toka kwa Mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala.
Mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala (anayekaribia paa), akimzawadia mchoro wa kupamba ukutani Meneja mafunzo, motisha na mawasiliano wa Vodacom, Bi. Belinda Wera.
Mjasiriamali Bi. Nana Mzobora wa Dar es Salaam akijitwalia yake.
Meneja masoko wa Nafasi Art Space, Kelvin Kyando akidaka ya kwake. 

WIMBO MPYA UNAOZUNGUMZIA MAUAJI YA ALBINO

Rais Dkt. Magufuli atuma Salamu za Rambirambi kwa IGP kufuatia vifo vya askari 3

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Ernest Mangu kufuatia vifo vya askari watatu waliopoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea jana tarehe 06 Februari, 2016 katika kijiji cha Isuna, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida. Askari waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Inspekta Miraji Mwegelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerald Ntondo.

Katika salamu hizo Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa na vifo vya askari hao, ambao wamekutwa na mauti wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kikazi.

"Kupitia kwako Mkuu wa Jeshi la Polisi natoa pole nyingi kwa familia za Askari waliopoteza maisha, Ndugu, Jamaa na Marafiki pamoja na askari wote wa Jeshi la Polisi Tanzania ambao wameguswa kwa namna ya pekee na msiba huu" Amesema Rais Magufuli.

Ameongeza kuwa anaungana na wote walioguswa na vifo hivyo katika kipindi hiki kigumu, na amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi, Amina.

Rais Magufuli pia amewatumia salamu za pole Askari walioumia katika ajali hiyo, akiwemo Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani katika Mkoa wa Singida Mrakibu wa Polisi Peter Magira na kuwaombea wapone haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao ya kila siku.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
07 Februari, 2016

Dr.Mwaka ndani ya kipindi cha THE AVENUE mawazo huru

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAANZA KAZI RASMI - YAPOKEA TAARIFA YA UTENDAJI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akijitambulisha kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kabla ya Kamati hiyo kuipokea taarifa ya Wizara hiyo katika kikao cha kwanza cha Kamati hiyo baada ya kuundwa na Bunge hivi karibuni. Wapili kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu anayefuatia ni Makamu wake, Kanali Masoud Khamis. Kulia kwa Masauni ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Balozi Adadi Mohamed Rajabu akizungumza jambo na Wajumbe wa Kamati yake pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika kikao chao kwanza tangu Kamati hiyo iundwe na Bunge hivi karibuni. Wapili kulia mstari wa mbele ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni, na kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Projest Rwegasira. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Kanali Masoud Khamis. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Injinia Hamad Masauni akitoa taarifa ya Wizara katika kikao cha kwanza cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama. Kikao hicho kilichohudhuriwa na Wajumbe wa Kamati hiyo pamoja na Maafisa wa Wizara, kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Balozi Adadi Mohamed Rajabu.


SIMU TV: Kupotea kwa sarafu ya shilingi 500 kumeonekana kuleta mkanganyiko mkubwa miongoni mwa wananchi na kusema ina vito vya thamani

$
0
0
SIMU.TV:  Timu ya mpira wa miguu Kawawa imeibuka kidedea dhidi ya Jitimaye katika mashindano ya kuadhimisha miaka 39 ya CCM;https://youtu.be/ojTgaWtzl_Y
 SIMU.TV:  Ligi kuu Vodacom yazidi kushika kasi kufuatia timu 3 za juu katika michuano kuweza kushinda katika michezo yao mitatu iliyochezwa; https://youtu.be/z-l_Ar83XWE
SIMU.TV:  Vilabu  vya DARTS Dar es salaam  vyaingia kambini kuanza mazoezi kwajili ya mashindano ya taifa huku wakiomba udhamini kutoka kwa wadau; https://youtu.be/6QFKqv5_C1A 
SIMU.TV:  Kiwanda cha sukari Mahonda Zanzibar huenda kikasitisha uzalishaji wa sukari kufuatia hujuma za kuchomwa kwa mashamba ya miwa; https://youtu.be/tlAHrxg_W5U
SIMU.TV:  CCM Makangira Msasani yazindua ofisi mpya za chama iliyogharimu mil 57 ili kuboresha mazingira ya utendaji wa chama;https://youtu.be/F09e3Uysl88 
SIMU.TV:  Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani Tanga, wametakiwa kutenga bajeti ili kuboresha sekta ya elimu mkoani humo:https://youtu.be/Pd3E8NQjdAM
SIMU.TV:  Kupotea kwa sarafu ya shilingi 500 kumeonekana kuleta mkanganyiko mkubwa miongoni mwa wananchi na kusema ina vito vya thamani: https://youtu.be/KWluNFn805w 
SIMU.TV:  Waziri mkuu Mh.Kassim Majaliwa amesema ataitisha kikao na viongozi wa dini zote nchini ili kuweza kuishauri serikali ya awamu ya tano:https://youtu.be/-ErxBVYaA64
SIMU.TV:  Vikosi vya ulinzi na usalama visiwani Zanzibar watakiwa kuwa mstari wa mbele katika kulinda na kutetea  mapinduzi ya Zanzibar:https://youtu.be/D7uFbznl3e0
 SIMU.TV:  Yajue mambo kadha wa kadha kutoka kwa mchambuzi akikudadavulia kuhusu Tanzania yenye viwanda nini nafasi ya kilimo:https://youtu.be/WxfKD_U_hoA
SIMU.TV:  Fahamu mengi kutoka kwa wadau wa kitengo cha ardhi nchini wakikuelimisha mengi kuhusu masuala faini ya kodi ya ardhi:https://youtu.be/8a1_tchAriU
SIMU.TV:  Jifunze mambo mengi kutoka kwa Mkurugenzi wa vyuo vya amali visiwani Zanzibar  akikujuza mambo mengi kuhusu vyuo hivyo :https://youtu.be/vGaHtI7wMvc

twiga Bancorp yawatengea wajasiramali wa vikundi Bilioni 5 nchi nzima, yaendelea kukopesha Bajaji na Pikipiki

$
0
0
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Twiga Bancorp, Solomon Haule akimkabidhi funguo wa bajaji Mwenyekiti wa kikundi cha Chama cha Madereva wa Bajaji cha Mikocheni kwa Kairuki (Chamabavi) John Roberto baada ya kupewa mkopo huo wa bajaji.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Twiga Bancorp, Solomon Haule akimpongeza Bi Shamsa saidi baada ya kukabidhi mkopo wa pikipiki.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Twiga Bancorp, Solomon Haule akiwasha bajaji huku pembeni yake (aliekaa) ni Mwenyekiti wa kikundi cha Chama cha Madereva wa Bajaji cha Mikocheni kwa Kairuki (Chamabavi) John Roberto baada ya kupewa mkopo huo wa bajaji.

AHADI YA SH.BILIONI 12.3 YA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI YA MAOMBI YA UENDESHAJI WA MAHAKAMA YATIMIA LEO.

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango (Katikati) akiwakabidhi Naibu waziri wa katiba na sheria, Amon Mpanju(kulia) na Mtendaji mkuu wa Mahakama Hussein Kattanga cheki ya shilingi Bilioni 12 na milioni mia tatu ikiwa ni kutimiza ahadi  ya Rais Dkt. John Pombe Josef Magufuli aliyoahidi siku alipokuwa mgeni rasmi siku ya Mahakama hapa nchini ikiwa ni siku tano tuu tangu siku ya kuahidi.
Waziri wa Fedha Mipango, Philip Mpango (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na kutimiza ahadi aliyoiahidi Rais  Dkt. John Pombe Josef Magufuli alipoahidi katika maadhimisho ya siku ya mahakama hapa nchini. Kulia ni Naibu waziri wa katiba na sheria, Amon Mpanju na kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile. 
Mtendaji mkuu wa Mahakama Hussein Kattanga (kushoto)akimshukuru Rais  Dkt. John Pombe Josef Magufuli kwa kutimiza ahadi yake aliyoiahidi siku ya maadhimisho ya siku ya mahakama. kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

 Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 
WIZARA ya Fedha na Mipango imetoa sh.bilioni 12.3 kwa ajili shughuli za mahakama ikiwa ni sehemu ya ahadi ya  Rais Dk. John Pombe Magufuli aliyoiahidi katika kilele cha maadhimisho ya  siku ya mahakama.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango amesema fedha hiyo imetolewa kwa kutimiza ahadi ya Rais ya uendeshaji wa shughuli za mahakama.


Mpango amesema kuwa ahadi ya Rais ilikuwa ni ya siku tano ambazo zimetimia kwa kutoa hundi ya sh.bilioni 12.3 ambazo zitakwenda kufanya kazi iliyokusudiwa.


Amesema kuwa Wizara ya Fedha na Mipango kutokana na ahadi hiyo imefanya kuweka wazi juu ya fedha hizo kwa waandishi wa habari.


Nae Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju amesema lengo ni kuongeza kasi kwa mashauri yaliyopo kuondoshwa  pamoja na waliokwepa kodi  yashughulilikiwe.


Ahadi ya Rais ilitolewa baada ya maombi ya Jaji Mkuu, Othman Chande katika maadhimisho ya  kuanza kwa mwaka wa mahakama kudai kuwa wana uhaba fedha za maendeleo  katika kuweza kuendesha shughuli za kimahakama.

Airtel Tanzania yapanga upya muundo wa utendaji kuboresha huduma

$
0
0
Dar es Salaam Tanzania Februari 8 2016, Kampuni ya Simu za mkononi nchini Airtel Tanzania, leo imetangaza mkakati wake wa kuboresha muundo katika nafasi zote za utendaji kuwa bora zaidi na kuweka idadi sahihi ili  viwango vya kiutendaji  kuimarika na hatimae dhamira yake ya pkibiashara ya kutoa huduma na bidhaa bora za kimawasiliano nchini Tanzania kufikiwa.

Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano alisema “ Mkakati huu wa kuboresha upya mfumo wa utendaji  wa kampuni yetu ni sambamba kabisa na mfumo wetu wa maboresho uliowekwa na kampuni yetu ambao tunaamini baada ya muda mfupi utakuwa na mafanikio makubwa kwa wadau wote wakiwemo wafanyakazi na wateja wetu tunaowahudumia”

Singano akifafanua alisema “Maboresha haya tunayofanya yatawahusisha takribani wafanyakazi 55  kwa nafasi zao za utendandaji kutokuwepo au kuhamishiwa kwa wadau watakao toa huduma kwa kampuni yetu, mfumo ujulikanao kama “outsource model”,  watoa huduma tutakaowapa jukumu la kusimamia baadhi ya huduma zetu”
Airtel tangu kuanza kwa mkakati huu wa maboresho yake ya kiutendaji kwaajili ya kutimiza malengo ya kibiashara imejizatiti kwa kuweka miundombinu madhubuti kwa kuingia mikataba ya kiutendaji.
“Vilevile kama njia ya kushirikiana na wale watakao guswa na zoezi hili la marekebisho ya mfumo huu kipindi hiki cha  mpito, Airtel tayari imeingia mkataba na kampuni inayohusiana na huduma za rasilimaliwatu ili kutoa mafunzo na ushauri wa kutosha ya jinsi ya kutafuta na kuzipokea nafasi zingine zinazojitokeza, Malipo ya huduma hii kwa wote watakaohitaji yamegaramiwa na Airtel” alimaliza kwa kusema Bi, Singano   .

KAMATI KUU YAFANYA UTEUZI WA WAGOMBEA WATAKAOZIBA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI CCM

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi Mhe. Nape Nnauye akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa NEC, Makao Makuu ya CCM, Ofisi Ndogo Lumumba.

Jana tarehe 07/02/2016 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ilikuwa na kikao maalum cha siku moja mjini Dodoma. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kikao hicho kilikuwa na kazi ya kuteua wagombea wa nafasi mbalimbali zilizo wazi za uongozi ndani ya CCM mikoani na wilayani ambazo uteuzi wake upo kwenye Mamlaka ya Vikao vya Chama Taifa.

Nafasi hizi wazi zimetokana na sababu mbalimbali zikiwemo vifo na baadhi ya viongozi kukihama Chama na kujiunga na vyama vingine. Hivyo, nafasi zilizofanyiwa uteuzi na wagombea wake ni kama ifuatavyo:-

I.     UENYEKITI WA CCM MKOA.
1.      ARUSHA 
(i)      Michael Lekule Laizer
(ii)     Emanuel Makongoro Lusenga
(iii)   John Pallangyo

2.   SHINYANGA
(i)      Hassan Ramadhani Mwendapole
(ii)     Mbala Kashinje Mlolwa
(iii)   Erasto Izengo Kwilasa


3.   SINGIDA
(i)    Hanje Narumba Barnabas
(ii)   Misanga Mohamed Hamis
(iii)  Mlata Martha Moses
(iv)  Kilimba Juma Hassan

NSSF YAZINDUA MPANGO WA AKIBA NA AFYA KWA WANAFUNZI WA VYUO.

$
0
0
 Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde (kushoto) akimkabidhi mfano wa kadi ya uanchama wa NSSF, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Rajabu Mahumba wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mpango wa AKIBA na AFYA 'AAPLUS' kwa wanafunzi wa vyuo hafla hiyo ilifanyika Chuo Kikuu cha Dodoma, mwishoni mwa wiki.
 (Picha na Francis Dande)
 Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mariam Ahmed akimkaribisha Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde kwenye uzinduzi wa Mpango wa Hifadhi ya Jamii kwa Wanafunzi 'AAPLUS', uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde (katikat) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa NSSF pamoja na baadhi ya wanafunzi wa UDOM.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

MKUTANO WA WADAU WA UWEZESHAJI KUFANYIKA KESHO FEBRUARI 9 MWAKA HUU.

$
0
0
BARAZA LA TAIFA LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

 MKUTANO WA WADAU WA UWEZESHAJI UTAKAOFANYIKA TAREHE 9/02/2016.
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilianzishwa mwaka 2005 kwa Sheria ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (Sheria na. 16 ya Mwaka 2004) chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Baraza ni chombo cha juu kitaifa cha kuratibu, kusimamia, kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004.
Katika kutekeleza Sera ya Taifa ya Uwezeshaji, Baraza limeshaandaa Mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Mwongozo wake unaohusisha sekta zote nchini.

 Ili kufanikisha utekelezaji wa mkakati huo, Baraza limeandaa Mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ambao ni muundo rasmi katika kutekeleza Mkakati wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. Mkutano huu ni sehemu ya Uratibu na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji ambao unahusisha wadau mbali mbali ambao ni Wizara, Idara na Taasisi za Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa, mashirika yasiyo ya kiserikali na sekta binafsi.

Mkutano huu wa Wadau wa Uwezeshaji utafunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Majaliwa Kassim Majaliwa (MB), tarehe 9/02/2016 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.

MAJUKUMU YA BARAZA
                     i.        Kuandaa Mpango Mkakati wa Kisekta na kuhamasisha matumizi ya rasilimali kwa shughuli za uwezeshaji wananchi;
                    ii.        Kuhamasisha na kuhimiza uwekaji wa akiba, uwekezaji na ushirikishwaji makini wa wananchi kwenye shughuli za kiuchumi;
                   iii.        Kusimamia, kuongoza na kubaini vyanzo vya fedha kwa ajili ya Mfuko wa udhamini mikopo ya uwezeshaji ;
                   iv.        Kuwezesha na kuratibu mafunzo ya ujasiriamali kwa vikundi mbalimbali vya wananchi kutegemeana na mahitaji na changamoto zinazowakabili;
MALENGO YA MKUTANO WA WADAU WA UWEZESHAJI
  1. Kukutanisha wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kutoka sekta za umma na binafsi hapa nchini,
  2. Kujadili taarifa ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi;
  3. Kutambua  juhudi za wadau wanaotekeleza Sera ya Taifa ya Uwezeshaji;
  4. Kujaidili changamoto na kuibua mbinu bora za utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi;
  5. Kuhamasisha juhudi mbali mbali za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi,
MATARAJIO
Kupitia Mkutano huu wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Baraza lina matarajio yafuatayo;
i.        Kuanza rasmi kwa  Dawati la Uwezeshaji na Ushiriki wa Wananchi kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa, Wizara na Idara katika kufuatilia masuala ya Uwezeshaji, kuandaa taarifa na kuwasilisha katika kamati husika kwa maafikiano na kuwasilisha katika Baraza la Taifa la Uwezeshaji;
ii.        Taasisi za umma na binafsi kuwahudumia wananchi kwa ufanisi bila upendeleo pale wanapohitaji kuwezeshwa kupitia huduma wanazozitoa katika utendaji wao wa kila siku;
iii.        Kuratibu majukumu ya Uwezeshaji kwa kuzingatia uwajibikaji, uadilifu, uaminifu na kujali;
iv.        Kuchochea hamasa na kuhakikisha kuwa wananchi wanapewa upendeleo wa pekee kwa watoa huduma mbalimbali katika zabuni na miradi mikubwa katika maeneo yao pale wanapokidhi vigezo na masharti ya zabuni husika.
v.        Kila kiongozi kuhakisha kuwa rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kiuwezeshaji wananchi kiuchumi zinaelekezwa katika miradi hiyo na kutumika kwa kuzingatia thamani ya pesa na miradi yenyewe;
Baraza linapenda kuwashukuru wadhamini wa Mkutano huu ambao ni (Mradi wa Ushindani wa Sekta Binafsi (Private Sector Competitiveness Project), World Vision Tanzania, Benki ya Maendeleo ya TIB (TIB Development Bank), Benki ya Posta, Benki ya CRDB, UTT Microfinance, Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Umma (PSPF), Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Serikali za Mitaa (LAPF), Mfuko wa Mafao ya Kustaafu (GEPF) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

KIDOGO CHA UCHANGIAJI DAMU CHA MBAGALA RANGI TATU JIJINI DAR CHAZINDULIWA LEO.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadic akizungumza leo katika uzinduzi wa Kituo cha Damu salama kilichopo Mbagara Rangitatu jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadic akikata utepe kuzindua kituo cha uchangiaji Damu salama cha Mbagala langitatu jijini Dar es Salaam leo.
Wananchi wakijitolea damu katika kituo cha Rangi tatu jijini Dar es Salaam leo.
MPANGO wa Taifa wa damu salama nchini ulio chini ya wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto  leo wamezindua kituo kidogo cha uchangiaji damu kilichopo Mbagala Rangi tatu. Uzinduzi huu unaambatana na uzinduzi wa vituo vingine vya afya vilivyopo wilaya zote za mkoa wa Dar es salaam kama vile Amana, Mwananyama, Sinza, Vijibweni na Mbweni.

Viituo hivi vimejengwa kwa ushirikiano wa wadau mbalimbali ambao ni Hospitali ya CCBRT, Hospital ya Mbweni Mission MDH, Umoja wa wamiliki hospital binafsi (APHTA) NA Halmashauri za temeke Ilala na Kindondoni.  Vilevile  Mpango wa Taifa wa Damu salama unawapongeza wachangia damu kwa hiari ambao  wamekuwa wakichangia damu mara kwa mara ili kuokoa maisha ya wahitaji tangu kampeni hii ilipoa nza rasmi tarehe 3 februari 2016.

Maisha ya watu wengi yanaokolewa kila mwaka nchini kwa kuongezewa damu . Nchini Tanzania kinamama wengi na watoto hupoteza maisha kwa kukosa damu. Takwimu za hivi karibuni zinaonyesha  kuwa nchini Tanzania takriban wanawake 432 kati ya vizazi hai 100,000 hufa kila mwaka kutokana na uzazi na asilimia 80 ya hivyo vifo husababishwa na ukosefu wa damu. Hivyo ufunguzi wa vituo hivi utasaidia kuondoa tatizo la uhaba wa damu na hatimaye kutokomeza tatizo la vifo vinavyotokana na kukosa damu.

Katika mkoa wa Dare s Salaam mahitaji ya damu ni makubwa , kwa mwezi tunahitaji chupa 4000 lakini zinazopatikana ni chupa 2000 tu ambayo ni nusu ya mahitaji. Kuna wakati mahitaji haya yanakuwa makubwa zaidi na hivyo upungufu huongezeka kufikia asilimia 70, hali ambayo ni hatari kwa maisha ya binadamu.

Damu ni uhai na haipatikani kwa njia yeyote ile isipokuwa  kwa kuchangiwa na binadamu wenzetu . Uchangiaji damu ni zoezi endelevu na la kudumu kwakuwa damu huhifadhiwa kwa muda wa siku 35 tu tangu inatolewa . Kutokana na uhifadhi wa damu kuwa ni wa muda mfupi ndio maana inasisitizwa umuhimu wa watu kuchangia damu walau mara mbili kwa mwaka.

WAZIRI MBARAWA AWATAKA AIR TANZANIA KUANZA KUFANYA KAZI.

$
0
0
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa,akisisitiza jambo kwa Menejimenti ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), alipokutana nao kabla ya kuongea na Wafanyakazi.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (mwenye koti la kaki), akisisitiza jambo kwa Wafanyakazi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL),alipokutana nao jijini Dar es Salaam.
 Rubani Lilla Borri wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa Wafanyakazi wa Shirika hilo na Waziri Prof. Mbarawa, uliofanyika  katika ofisi za Shirika hilo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akiagana na Wafanyakazi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), mara baada ya kuongea nao Ofisini Hapo.

SERIKALI imezungumzia umuhimu wa kulifufua upya Shirika la Ndege nchini Air Tanzania (ATC) kwa kulinunulia ndege mpya na kulipa mtaji ili lifanye kazi kibiashara na kutengeneza faida kama ilivyokusudiwa awali.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (Pichani)ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na menejimenti na wafanyakazi wa Shirika hilo alipolitembelea jijini Dar es Salaam leo.


“Tutawekeza kwenye Air Tanzania ili kuongeza fursa za kiuchumi na kuvutia wasafiri wengi kufika nchini moja kwa moja na kuvutia sekta ya utalii”, amesema Waziri Prof. Mbarawa.


Waziri Prof. Mbarawa amewataka wafanyakazi wa Shirika hilo ambao sio waadilifu na wavivu kuondoka mara moja ili kupisha wafanyakazi wabunifu na wenye mawazo ya kibiashara kuendesha shirika hilo kwa faida.


“Tunataka watu watakaolitoa shirika hili kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa kuliwezesha kiuchumi na kujitegemea ili kushindana na mashirika mengine ya ndege katika biashara“, amesisitiza Prof. Mbarawa.


Prof. Mbarawa amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli yuko tayari kununua ndege mpya ili kulifufua shirika hili hivyo amewataka wafanyakazi hao kuwa na mtazamo chanya wa kufanya biashara ili kuiletea taifa tija.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ATC Bw. Johnson Mfinanga amemwambia Waziri Prof. Mbarawa kuwa kwa sasa shirika hilo lipo katika hali mbaya kiuchumi na hivyo kuhitaji nguvu ya Serikali kulikwamua ili litoe huduma inayoshahili.


Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amesisitiza kuwa Serikali itaangalia upya taratibu za ajira katika shirika hilo na watakaobainika kuajiriwa kinyume cha taratibu watafukuzwa kazi mara moja.


“Tutanataka watu waadilifu, wabunifu na wenye sifa stahiki ili wafanye kazi kwa maslahi ya shirika na taifa kwa ujumla”, amefafanua Waziri Mbarawa.


Shirika la Ndege nchini ATC toka mwaka 2009 limekuwa likijiendesha kwa hasara na Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kulifufua shirika hilo ili lifanye kazi kwa faida na kuboresha usafiri wa anga ndani na nje ya nchi na hivyo kuvutia wasafiri wengi kuja nchini moja kwa moja.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

MATUMIZI YA BIDHAA YA VYAKULA YAMEPUNGUA -NBS

$
0
0
 Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephrahim Kwesigabo akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira Bi. Ruth Minja.
Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Ruth Minja akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei mapema hii leo jjijjini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephrahim Kwesigabo.


Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 
MATUMIZI ya kaya kwenye bidhaa za vyakula imepungua hadi asilimia 38.5 mwaka 2011/2012 kutoka asilimia 47.8 ya mwaka 2007. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa Takwimu za jamii na Sensa ya Watu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephraim Kwesigabo amesema kuwa kutokana na hali hiyo kunaashiria kupungua kwa umasikini wa kipato kwenye kaya kwa kuelekeza matumizi mengine bidhaa zisizo za vyakula kama usafiri, mawasiliano, makazi, maji pamoja na nishati. 

Amesema matokeo yanaonyesha kwamba mizania ya matumizi ya kaya kwenye bidhaa za vyakula imepungua hadi asilimia 38.5 mwaka 2011/2012 kutoka asilimia 47.8 mwaka 2007.

Amesema kumekuwa na ongezeko la zaidi ya mara mbili ya matumizi ya kaya kwenye kundi la Mawasiliano asilimia 5.6 ikilinganishwa na asilimia 2.1 ya mwaka 2007. 

Nae Meneja wa Takwimu za Bei na Ajira kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ruth Minja amesema baadhi ya vigezo muhimu vinavyotumika kupata Fahirisi za bei zinzoonyesha uhalisia wa matumizi ya kaya binafsi kuwa ni pamoja na mizania katika bidhaa za huduma muhimu ikiwemo Vyakula, afya, Usafiri, Maji na Nishati.

DKT MAHIGA AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KUWAANDALIA MABALOZI MCHAPALO WA MWAKA MPYA (SHERRY PARTY) IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akihutubia wakati akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika Mchapalo wa Mwaka Mpya kwa Mabalozi na Wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Kimtaifa maarufu kama "Sherry Party" Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu February 8, 2016
Mabalozi na Wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Kimtaifa wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akihutubia wakati akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika Mchapalo wa Mwaka Mpya maarufu kama "Sherry Party" Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumatatu February 8, 2016 
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika picha ya pamoja Mabalozi na Wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Kimtaifa jijini Dar es Salaam leo.

MKE WA RAIS MAMA JANETH MAGUFULI AMTEMBELEA MUFTI MKUU WA TANZANIA SHEIKH ABUBAKAR ZUBEIRY HOSPITALI MUHIMBILI.

$
0
0
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimjulia hali Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry aliyelazwa kwa matibabu katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Mhe Ummy Mwalimu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe George Masaju pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi leo Jumatatu February 8, 2016.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisindikizwa wakati wa kuondoka baada ya kumjulia hali Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry aliyelazwa kwa matibabu katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Pamoja naye ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Mhe Ummy Mwalimu na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi 
leo Jumatatu February 8, 2016.
Viewing all 110139 articles
Browse latest View live




Latest Images