Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110009 articles
Browse latest View live

BENKI YA CRDB YATOA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU YA BUNGE.

$
0
0
NA MWANDISHI WETU, DODOMA
BENKI ya CRDB imetoa msaada wa vifaa vya michezo kwa wabunge wa Jamhuri la Muungano wa Tanzania.

Vifaa hivyo vilikabidhiwa na Mkurugenzi wa benki ya CRDB Tawi la Dodoma, Rehema Hamis na kupokelewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni jezi seti mbili ikiwamo ya golikipa, viatu, mpira, soksi na suti za michezo ambavyo vimegharimu zaidi ya Sh. Milioni 5.

Awali Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, aliwapongeza wafadhili na wadhamini wanaojitokeza kusaidia sekta ya michezo na kuwataka wengine waige mfano huo, kwani hivi sasa michezo ni uchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi kutoka makao makuu ya CRDB anayeshughulikia Mikakati na Ubunifu, Goodluck Nkini, alisema wameamua kutoa vifaa hivyo kutokana na mapenzi yao kwa wananchi hususan wateja wao, ambao wabunge ndio wawakilishi wao.

“Pia ni katika mpango wa taasisi kuunga mkono katika kazi, kwani michezo mbali ya burudani hujenga afya, hivyo wabunge na wafanyakazi wa CRDB wakiwa na afya njema watatekeleza vema majukumu yao,” alisema Nkini. 

Jioni ulipigwa mchezo wa kirafiki kati ya Bunge FC na CRDB kwenye Uwanja wa Jamhuri na kumalizika sare ya bao 1-1.

Walikuwa ni CRDB walioanza kuzifumania nyavu za Bunge FC dakika ya 49 mfungaji akiwa Faisal Mbuya.

Bunge FC walicharuka na kuwachukua dakika sita tu kuchomoa dakika ya 55 kwa bao la Yusuf Gogo. Hadi mwamuzi Peter Mdachi akipuliza kipenga kuashiria dakika 90 kumalizika, hakuna aliyeibuka mbabe. 
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma, Rehema Hamis akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa vya michezo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (kulia) akipokea msaada wa vifaa vya michezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma, Rehema Hamis kwa ajili ya timu ya soka ya Bunge. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Wa pili kulia ni Naibu Spika Dk. Tulia Akson, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa na kushoto ni Mkurugenzi wa Mikakati na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Goodluck Nkini. 

SERIKALI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA.

$
0
0
Naibu waziri afya Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee Mhe.Hamis Adrea Kigwangalla akijibu maswali kutoka kwa wabunge mbalimbali katika kipindi cha maswali na majibu katika kikao cha Tano cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma. Picha na Raymond Mushumbusi Maelezo

Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
SERIKALI imejipanga kutoa huduma bora za afya kwa wananchi kwa kuwawezesha kila mwananchi kupata Bima ya Afya itakayosaidia kupata huduma bora za afya katika zahanati na hospitali mbalimbali.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe.Faida Mohammed Bakar(CCM) lililouliza kuwa bado kuna ukiukwaji wa huduma za afya, haki za afya na haki za uzazi katika baadhi ya vituo vya kutolea huduma za afya wakati wa maswali na majibu,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee Mhe.Hamis Adrea Kigwangalla amesema katika kuhakikisha kuwa haki hizi zinapatikana, Serikali kwa kupitia mifumo yake, ikiwa ni pamoja na mabaraza ya weledi, kurugenzi ya uhakiki na ubora wa huduma za afya na idara mbalimbali zilizo chini ya Waziri zinatoa mafunzo kwa watoa huduma za afya kuhusiana na haki za wateja.

Mhe. Hamis Adrea Kigwangalla amesema katika kutekeleza hili, vituo vyote vya kutolea huduma za afya vina masanduku ya maoni na ofisi za malalamiko ambazo ni sehemu muhimu ambapo wateja wanaweza kupeleka malalamiko yao ili hatua zaidi zichukuliwe kukomesha na kutokomeza ukiukwaji wowote wa haki za wateja.

“ Tutawachukulia hatua wale wote watakaobainika kukiuka haki za wateja kwa kupitia baraza la wauguzi na wakunga ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazostahili ili kuokoa maisha ya wananchi hasa maisha ya mama na mtoto” Alisema Mhe.Kigwangalla.

Aidha Mhe. Hamis Adrea Kigwangalla amesema Wizara yake imeandaa rasimu ya Sheria ya Bima ya Afya ambayo itamuwezesha kila mwananchi kupata bima ya afya itakayomsaidia kupata huduma bora za afya katika maeneo yao.

Serikali kupitia Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee inatoa mafunzo kwa Wakunga wa Jadi ambao wamekuwa wakitumika sana sehemu ambazo huduma za afya zipo mbali ili kuwezesha wananchi hao kupata huduma bora za afya kutoka kwa wakunga hao hasa katika afya ya mama na mtoto.

SERIKALI KUJENGA VYUO VYA VETA KILA WILAYA.

$
0
0
Waziri Elimu Wazira wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi Mhe. Mhandisi Stella Manyanya akijibu maswali kutoka kwa wabunge mbalimbali katika kipindi cha maswali na majibu katika kikao cha Tano cha Bunge la 11 linaloendelea Mjini Dodoma Picha na raymond Mushumbusi MAELEZO

Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi inatarajia kujenga Vyuo vya Ufundi (VETA) kwa kila wilaya ili kutoa fursa kwa wananchi wengi hususani vijana kupata mafunzo mbalimbali ya ufundi yatakayowasaidia kujikwamua kiuchumi na kujenga taifa.

Akijibu swali la Mbunge wa Lupa Mhe.Victor Kilasike Mwambalaswa (CCM) kuhusu ujenzi wa vyuo vya VETA kwa kila Wilaya ambapo Wilaya ya Chunya ni moja kati ya Wilaya kumi za mwanzo zilizo katika mpango wa ujenzi wa vyuo hivyo wakati wa maswali na majibu, Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi Mhe. Mhandisi Stella Manyanya amesema Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuwa na Chuo Cha VETA sio kwa wilaya ya Chunya tu bali kwa Wilaya zote nchini, tayari maandalizi ya awali ya ujenzi wa chuo cha VETA ikiwa ni pamoja na kufanya utambuzi wa stadi zinazohitajika katika vyuo hivyo.

“ Natoa wito kwa wabunge katika majimbo yao kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya zote watafute ardhi kwa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivi ili hata mipango ya ujenzi ikikamilka ikute eneo lipo tayari kwa kuanza utekelezaji wake”Alisema Mhe.Manyanya.

Mhe. Mhandisi Stella Manyanya amesema katika mwaka wa fedha wa 2015/2016 Wizara yangu kupitia Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeshateua wataalamu elekezi watakaoshindanishwa kutayarisha andiko la jinsi ya kuifanya kazi ya kubuni majengo na kupata gharama ya kazi hiyo ili kuanza ujenzi mara moja.

Serikali kupitia Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imejipanga kutoa elimu bora ya ufundi yenye kuleta ufanisi katika maendeleo ya ufundi stadi nchini ili kuwawezesha wahitimu kupata ujuzi ulio bora kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

DAWATI LA MSAADA (HELP DESK)

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI YA LUGOBA WAFAIDI UJIO WA MTANDAO WA SIMU ZA MKONONI WA HALOTEL.

$
0
0

Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Lugoba wakiwa Darasani wakijisomea masomo yako wa njia ya Kompyuta.

WANAFUNZI wa shule ya Sekondari ya Lugoba iliyopo Msata-Bagamoyo mkoani Pwani wamefaidika na kompyuta zilizotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Halotel kwaajili ya kusaidia masomo ya TEHAMA shuleni hapo. 

Halotel imetoa msaada wa kompyuta 19 pamoja na kuziwekea mtandao wa intaneti yenye spidi kubwa ya kampuni hiyo bure, kwaajili ya kuwezesha wanafunzi wa shule hiyo kujisomea kwa urahisi. 

Akizungumza na waandishi wa habari Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya Lugoba, Abdala Sakasa ameishukuru kampuni ya Halotel kwa kuiangalia shule hiyo kwa jicho la pekee na kuamua kuisaidia kompyuta hizo. 

‘Wanafunzi wa dunia ya sasa ni muhimu waweze kutumia mtandao kujifunza na kupata maarifa mbalimbali tofauti na vizazi vilivyopita, na hivyo tunaishukuru Halotel kwa kusaidia kuwezesha hali hii’ alisema mwalimu Sakasa. 

Kwa upande wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lugoba, wameushukuru mtandao wa Halotel kwa kuwapa msaada wa kompyuta hizo ambazo zimeweza kuongeza ari na juhudi za kujifunza kupitia kompyuta hizo. 

‘Tunaishukuru kampuni ya Halotel kwa kutujengea darasa la komputa pamoja na kutupa komputa mpya zilizounganishwa na mtandao wa 3G, hali ambayo imeturahisishia kujifunza kwa vitendo masomo ya TEHAMA’ alisema Asha Mohamed, mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo. 

Kampuni ya Halotel yenye kauli mbiu ya Pamoja katika Ubora, inalenga kuhakikisha kila mtanzania anapata huduma ya mtandao kwa kila sehemu ya Tanzania, ambapo mpaka sasa imeshaunganisha mtandao wa simu kwa zaidi ya vijiji 1500 ambavyo vilikuwa havijaunganishwa na huduma ya mtandao wowote wa simu kutoka mwanzo. 

Katika hatua nyingine, kampuni ya Halotel itaweka mkazo wa hali ya juu katika kuboresha mtandao, huduma kwa wateja, huduma kwa jamii hali itakayopelekea mapinduzi katika sekta ya mawasiliano nchini. 

Ikiwa na kilomita 18,000 za fibre optic, pamoja na zaidi ya minara 2500, Halotel ndiyo kampuni yenye mtandao mkubwa zaidi nchini, ambayo pia itatumika kuunganisha serikali za mitaa 150, hospitali 150, vituo vya polisi 150, ofisi za posta 65 na intaneti ya bure kwa shule zaidi ya 450. 

Hadi sasa Halotel imeshawekeza zaidi ya dola bilioni 1 za kimarekani mpaka sasa kwa kutengeneza miundombinu na kuboresha mtandao wa mawasiliano, kampuni ya Halotel imefanikiwa kufikisha huduma za mtandao katika mikoa yote 26 nchini, pamoja na miji na vijiji, ikiwa ni zaidi ya asilimia 95% ya watanzania wote hivyo kuifanya kuwa kampuni yenye mtandao mkubwa zaidi nchini.

Hili hapa tamko la serikali dhidi ya wafugaji wanaoruhusu mifugo yao kuwatia hasara wakulima nchini.

WATUMISHI WA AFYA NCHINI WAMETAKIWA KUACHA KUHUJUMU DAWA ZINAZOPELEKWA KWA AJILI YA WANANCHI

$
0
0
 Baadhi ya wafanyakazi wa bohari ya dawa (msd)kanda ya kaskazini wakimsikiliza naibu waziri wa afya, maendeleo ya jamii,jinsia, wazee na watoto (hayupo pichani).
 Naibu waziri Dkt.Hamisi kigwangwala akiongea na watumishi hao.
Watumishi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya naibu waziri wao
(Habari na picha toka wizara ya afya)

WATUMISHI wa afya nchini wametakiwa kuacha kuhujumu dawa zinazopelekwa kwa ajili ya wananchi na si za biashara kama wanavyofanya.

Onyo hilo yamesemwa mwishoni mwa wiki na naibu waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia,wazee na watoto, Dkt. Hamisi Kigwangwalla wakati akiongea na wafanyakazi wa bohari ya dawa(msd)pamoja na wale wa hospitali ya mkoa ya mount meru.

Dkt. Kigwangwalla alisema serikali ya awamu ya tano yenye kaulimbiu ya "hapa kazi tu"haitawavumilia watumishi wa aina hiyo na kama wapo basi waanze kujipima kabla rungu la dola halijawafikia

Aidha,alisema suala la upatikanaji wa dawa kwa wananchi na kwa bei nafuu ni moja ya mambo yaliyopewa kipaumbele katika serikali ya awamu ya tano
"Wananchi wanatakiwa kupata dawa sahihi, kwa bei nafuu na kwa wakati, ndo maana serikali imeamua kufungua maduka ya dawa ya ndani ya hospitali, hii ni moja ya malengo yaliyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya chama cha Malibu"

Hatahivyo aliongeza kuwa katika kudhibiti upotevu wa draws nchini, serikali imeanza kutekeleza uwekaji nembo ya GoT katika vidonge vyote"na mimi nawapa changamoto ya kuweka mkakati wa kuweka rangi Maalum 'colour code'
Kwa dawa zote zinazokuwa zimenunuliwa na serikali, sambamba na huo mkakati wenu wa nembo.

Licha ya hivyo aliwataka wakuu wa hospitali,vituo vya afya pamoja na zahanati wasipokee dawa bila kuwepo kwa kamati ya afya ambayo ndio wawakilishi wa wananchi wa mahali husika ili kusiwepo na udanganyifu na kwenda kwenye mfumo usio rasmi pamoja na kuzibandika dawa zilizopokelewa kwenye mbao za matangazo.

Aliitaka bohari ya dawa(msd)kukamilisha uwekaji nembo dawa zilizosalia na wawe na utaratibu wa kusimamia na kukagua kama dawa za serikali zimefika hadi sasa vidonge vipatavyo 65 vimekwishawekewa nembo ya GoT.

MAADHIMISHO YA SIKU YA ARDHI OEVU

$
0
0
 Afisa Wanyamapori  kutoka Wizara ya Mali Asili na Utalii Bw.Sadick   Lotha akiwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu maadhimisho ya siku ya ardhi oevu Duniani inayotarajiwa kufanyika februari 2,2016 ambapo siku hiyo itatumika kutoa elimu kwa kuwakumbusha watu kuhusu uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za ardhi oevu. Kulia ni Afisa Habari wa Wizara hiyo Bw. Lusungu Helela, kushoto ni Afisa Wanyamapori Mkuu na Mratibu Kitaifa wa Uhifadhi Ardhi Oevu Bw. Pellage Kauzeni.
 Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Mali Asili  na Utalii Bw. Pellage Kauzeni akitoa wito kwa wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya ardhi oevu kushirikiana na Serikali katika kuyatunza maeneo hayo kushoto ni Afisa Wanyamapori  kutoka Wizara ya Mali Asili na Utalii Bw.Sadick Lotha na kulia ni Afisa Habari wa wizara hiyo Bw. Lusungu Helela.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatlia mkutano wa Wizara ya Mali Asili na Utalii uliolenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maadhimisho ya siku ya ardhioevu ambayo huzuia mmomonyoko wa udongo kwenye fukwe unaoweza kusababishwa na mawimbi ya bahari.( Picha zote na Frank Mvungi )



JAJI MKUU OTHUMAN CHANDE ATOA SIKU SABA KWA MAHAKIMU 508 WATOE MAELEZO KWANINI WASIFUNGULIWE MASHITAKA KWA KUFANYA KAZI CHINI YA KIWANGO.

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania, Othuman Chande (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani), Dar es Salaam leo mchana , kuhusu utendaji wa mahakimu wa mahakama za hakimu mkazi, mahakama za wilaya na mahakama za mwanzo ambapo alitoa siku saba kwa mahakimu 508 watoe maelezo kwani ni wasifunguliwe mashitaka ya nidhamu na kuwajibishwa kwa kufanya kazi chini ya kiwango. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omari Mallungu na kulia ni Jaji Kiongozi wa Tanzania, Shaban Omari Lila. Jaji Chande alitoa kauli hiyo kwenye maonyesho ya wiki ya Sheria yanayoendelea viwanja vya Mnazi Mmoja.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Othuman Chande, akikaribishwa kutembea mabanda mbalimbali kwenye maonesho hayo.
Mkurugenzi Msaidizi Ukaguzi na Maadili Mahakama ya Tanzania, Warsha Ng'humbu (kushoto), akimuelekeza jambo Balbina Mrosso (kulia), kutoka Babati mkoani Manyara aliyetembelea banda la Idara ya Malalamiko kuomba msaada wa kisheria katika maonyesho hayo.

JAJI Mkuu wa Tanzania Othuman Chande ametoa siku saba kwa mahakimu 508 watoe maelezo ni kwanini wasifunguliwe mashtaka ya nidhamu na kuwajibishwa, baada ya kufanya kazi chini ya kiwango.

Jaji Chande ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Viwanja vya Mnanzi Mmoja jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Wiki ya Sheria.

Alisema kiwango cha kesi kwa kila Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya ni 250, ambapo Mahakimu Wakazi 121 kwenye mahakama hizo wameamua kesi chini ya 100 mwaka jana.

Alibainisha kuwa kiwango cha kwa kila Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ni 260, ambapo mahakimu Wakazi na Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo 387 wameamua kesi chini ya 100 mwaka jana.

"Ukiondoa wale ambao wameajiriwa karibuni, wanaofanya kazi kwenye mahakama za mwanzo zisizokua na mashauri mengi au waliyokwenda masomoni kati kati ya mwaka au likizo za ujauzito hawatahusika katika sakata la kujieleza.

"Majaji Wafawidhi nimewaagiza wachambue na kuanisha mahakimu wote walioshindwa kufikia kiwango cha kesi walizopaswa kuamua kesi 250 na kesi 260 kwa mwaka jana na kuwataka watoe maelezo ndani ya siku saba kwa nini wasichukuliwe hatua," alisema Jaji Chande

Jaji Chande alitoa muda wa kukamilika kwa mchakato huo, ambapo walizitaka idara husika ndani ya siku 21 kila kitu kiwe kimekamilika ili ijulikane ni hatua gani wanachukuliwe.

"Mahakama haikubali hakimu ambaye anabembeleza kesi. Hakimu hatakiwi kufanya hivyo anatakiwa asikilize kesi hizo naazimalize. Haiwezekani katika mahakama moja hakimu mmoja anamaliza kesi 800 mwingine anamalizia chini ya 100 hilo halitakubalika kutokana na kasi ambayo tunayo," alisema

Jaji Chande alisema mahakimu hao watapelekwa katika kamati zao kwa hatua ya kujieleza. Kazi kuu ya kamati hizo ni kupeleleza, kuchunguza na kushughulikia mashtaka yote ya nidhamu ya mahakimu.

"Mahakimu wote walioshindwa kufikia malengo ya mwaka la kesi na kushindwa kutoan sababu za kuridhisha kwa nini wameamua idadi ndogo ya kesi kuliko walivyopaswa, ambapo itashughulikiwa haraka na Kamati za Maadili za Mahyakimu kwa mujibu wa sheria na taratibu za haki," alisema

Hata hivyo, Jaji Chande alitoa pongezi kwa mahakimu ambao wamevuka kiwango, ambapo mahakimu 14 wameamua zaidi ya kesi 700 kwa mwaka jana na mahakimu wengine wamesikiliza kesi 915,789 na 778.

Alisema mkakati wao ni kuanza kesi sifuri mwaka unapoanza, kwa sababu kuna baadhi ya mahakama za mwanzo zimekuwa zikimaliza kesi na kuanza mwaka upya.

Jaji Chande alisema Januari 1, 2015 mahakama za mwanzo zilianza na kesi 34,126 na mwaka huu Januari 1 zilianza na kesi 20,431. Kiwango cha kumaliza kesi ukilinganisha na idadi ya kesi zilizosajiliwa 2015 nni zaidi ya asilimia 100. Mahakama ya Mkuranga asilimia 141, Rufiji asilimia 121 na Bukoba Mjini asilimia 224.

RAIS DKT. MAGUFULI AMHAMISHA NAIBU KATIBU MKUU KATIBA NA SHERIA KWENDA UTUMISHI NA UTAWALA BORA

$
0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemhamisha Bi. Suzan Paul Mlawi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, kwenda kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Manejimenti ya utumishi wa umma na Utawala Bora.


Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imeeleza kuwa uhamisho huo umeanzia tarehe 26 Januari, 2016.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa pamoja na shughuli nyingine za Unaibu Katibu Mkuu, Bi. Suzan Paul Mlawi, atashughulikia eneo la Utawala Bora.

Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria iliyoachwa wazi, haitajazwa kwa sasa.


Gerson Msigwa,

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.

Dar es salaam.


01 Februari, 2016.

Walemavu: Msama anajitambua

$
0
0
BAADHI ya walemavu hapa nchini  wametoa wito kwa Watanzania wengine kujitambua kuhusu Mungu na mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika jamii ikiwa ni kuelekea Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Machi 27 jijini Mwanza.

Akizungumza leo kwa niaba ya Esperance Wetewabo ambaye ni mlemavu wa mikono na mguu, mchungaji wa Godfrey Rubanzibwa 'Punda  wa Yesu' alisema jamii inatakiwa kujitambua kuhusu Mungu kama alivyo Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama anavyotekeleza majukumu yake katika muziki huo.

Punda wa Yesu alisema Msama amejitambua ndio maana anashirikisha kada mbalimbali katika jamii kuelekea Tamasha la Pasaka ambalo lina mafunzo mengi kwa jamii.

Punda wa Yesu alisema katika tamasha lake Msama anashirikisha waimbaji chipukizi, walemavu na wengineo ambao wanabeba dhana ya tamasha hilo ambalo dhamira yake ni kumuimbia na kumtukuza Mungu.
"Msama anajitambua waimbaji chipukizi na viongozi wa dini mbalimbali wanaohudhuria tamasha hilo, ivyo wengine nao waige mfano huo," alisema Punda wa Yesu.

Naye Honoratha Michael alitoa wito kwa Watanzania kujiandaa vilivyo na tamasha la Pasaka ambako pia alitoa wito kwa jamii kujitokeza kuwasaidia walemavu kama anavyofanya Msama.

Honoratha aliumia fursa hiyo kuwapa usia Watanzania wote wakiwemo walemavu kuiga mfano wa Msama ambaye anatekeleza majukumu hayo.

Serikali yapanga kufanya matumizi yenye tija

$
0
0
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO

Serikali katika mwaka wa fedha 2016/2017 imejipanga kufanya matumizi yeneye tija kwa kuelekeza bajeti kubwa kwenye mambo muhimu hasa sekta zenye za kutoa huduma na zile zenye kuleta maendeleo ya nchi moja kwa moja.
 
Akiwasilisha mwongozo wa kuandaa mapango na bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017  Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Phillip Mpango amesema mwongozo wa  mpango na bajeti umezingatia mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/2017 pamoja na kuzingatia sera za uchumi na hadi sasa sera za bajeti kwa  mwaka 2016/2017 zinaonesha jumla ya shilling trillion 22.9 zinatarajiwa kukusanywa na kutumika katika kipindi hiki.
 
“ Kati ya mapato hayo,serikali inalenga kukusanya mapato ya kodi ya jumla ya shillingi trillion 14.1 sawa na ongezeko la asilimia 14.1 ikilinganishwa na makadirio ya mwaka 20015/2016, na kwa mapato yasisiyo ya kodi na mapato kutoka vyanzo vya Halmashauri ni shilling trillion 1.1.
 
“ katika mwaka wa fedha 2016/2017,Serikali tunatarajia kukusanya jumla ya shilling trilllioni 14.1 kutoka kwenye vyanzo vya kodi ,sawa na asilimia 13.2 ya pato la taifa hii ni sawa na ongezeko la asilimia 14 ukilinganisha na matarajio ya kukusanya jumla ya shilling trillion 12.3 kwa mwaka wa fedha 2015/2016” Alisema Mhe. Mpango.
 
Mhe Philip Mpango amesema mapato yote yatakusanywa na Wizara ya Fedha na Mipango, hivyo basi maafisa,Masuuli,wa Wizara,idara za serikali,Wakala,Taasisi,Sekretarieti za Mikoa, na Mamlaka za Serikali za Mitaa watatakiwa kuwasilisha mapato yote yatakayokusanywa na kuwasilisha kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali na yatagawiwa kulingana na bajeti iliyoidhinishwa.
Aidha amesema Serikali itahakikisha Mashirika ya Umma yaliyoundwa kwa lengo la kujiendesha kibiashara yanajiendesha kwa faida bila ya kutegemea ruzuku ya Serikali, na ameyataja baadhi ya mashirika hayo kuwa ni  Shirika la Umeme(TANESCO),Shirika la Reli ya Tanzania Zambia (TAZARA), Shirika la Reli ya Kati (TRL), Shirika la Ndege (ATCL),Wakala wa Vipimo (WMA), Bodi ya Mazao, na mashirika mengine.
 
Serikali itahakikisha kuwa inahimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuelekeza matumizi kwenye maeneo yenye tija kwa manufaa ya watanzania wote.

BALOZI WA SWEDEN AMTEMBELEA SPIKA OFISINI KWAKE

$
0
0
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiwa katika picha ya pmoja na Balozi wa Sweden Nchini Bi. Katarina Rangnitt na Maafisa wengine wa Ubalozi wa Sweden na wa Bunge
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiaagana na Balozi wa Sweden Nchini Bi. Katarina Rangnitt mara baada ya kuzungumza anye ofisini kwake. Kulia ni Afisa wa Ubalozi wa Sweden Bw. Ludvig Bontell.
Katibu wa Jukwaa la Wahariri Bw Neville Meena akifafanua jambo kwa Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah wakati alipomtembele Ofisini kwake kwa ajili ya mazungumzo. Kuli kwa Spika ni Naibu Katibu wa Bunge-Shughuli za Bunge Bw. John Joel.Wengine katika picha ni Viongozi wa Jukwaa la Wahiri na Maafisa wa Bunge.(Picha na Ofisi ya Bunge)
Balozi wa Sweden Nchini Bi. Katarina Rangnitt akisaini kitabu cha Wageni alipomtembelea leo ofisini kwake tarehe 01 Febuari, 2016 Mjini Dodoma. Kulia kwake ni Afisa wa Ubalozi wa Sweden Bw. Ludvig Bontell.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Bi. Katarina Rangnittaliyemtembelea leo Ofisni kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akifanunua jambo wakati akizungumza na Balozi wa Sweden Nchini Bi. Katarina Rangnitt. Wengine katika picha ni maafisa wa Ubalozi wa Sweden na Wabunge.

RAIS MHE. DKT MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI JAJI DAMIAN LUBUVA

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Ramadhan Kailima.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva Ikulu jijini Dar es Salaam. Picha na IKULU.





MAKALA YA SHERIA: MGAWANYO WA MALI ZA MAREHEMU

$
0
0
Na  Bashir  Yakub. 
Mgawanyo  wa mali  za marehemu   hutegemea   mambo  makubwa  mawili. Kwanza  ni  ikiwa  marehemu  ameacha  wosia  na  pili  ni  ikiwa  hakuacha  wosia.  Ikiwa ameacha  wosia  basi  huwa ni rahisi  sana kwani mali  zake  zitagawanywa  kwa  kufuata  wosia.  Ikiwa  hakuacha  wosia  hapa  huwa  si  kwepesi  sana kwani  mali  zake  hulazimika  kugawanywa  kwa  mujibu  wa  sheria  zilizopo  wakati  sheria  zenyewe  ziko  tatu  tofauti. Wakati  mwingine ni  kazi  kidogo  kuamua  sheria  ipi  itumike  katika  kugawa  mali  za  marehemu. 

1.SHERIA  IPI  ITUMIKE  KATIKA  KUGAWA  MALI  ZA  MAREHEMU.
Ikiwa hakuna  wosia  swali  la  sheria  ipi  itumike  katika  kugawa  mali  za  marehemu  lazima  liibuke.  Kwa  ujumla  kuna  sheria  tatu  zinazotumika  katika  kugawa  mirathi.

( a )  Sheria  ya  kwanza  ni  sheria  ya  urithi  ya  India 1865 .  Hapa  kwetu  sheria  hii hujulikana  kwa  wengi  kama  sheria  ya  mirathi  ya  serikali. 

Sheria  hii  hutumika  kwa marehemu  ambaye hakuishi maisha  ya  kiislam  na hakuishi    maisha  ya  kimila. Zaidi  tunaweza  kusema  kuwa  sheria  hii  hutumika  kwa  wakristo  na  madhehebu  mengine  ambayo  sio   ya  kiislam.Hata  hivyo  hata  muislam  ambaye  itathibitika  kuwa hakuishi  maisha  ya  kiislam  wala  ya  kimila  sheria  hii itatumika  kugawa  mali  zake.

( b ) Pili  ni  sheria  ya kiislam.  Sheria  hii  hutumiwa  na waumini  wa  dini  ya  kiislamu. Lakini  haitoshi  kusema inatumiki  kwa  waislam  isipokuwa  inatosha  kusema itatumika kwa waliokuwa wakiishi  maisha  ya  kiislam. Sheria  hii  hufuata  misingi  ya  Quran  tukufu  na  Sunnah.

( c ) Tatu  ni  sheria  za  kimila. Sheria  hizi  hutumika  iwapo  marehemu  aliishi  maisha  ya  kimila. Mfano  wake  ni  kama  tunavyoona  kwa wamasai, wahadzabe,  na  makabila  mengine  hasa  vijijini  ambao huishi  maisha  yao  yote pasi  na  kufuata  dini  yoyote  isipokuwa  mila  tu. Sheria  hii  imo  katika  kanuni   za urithi,  tangazo  la  serikali  namba  436  la  mwaka  1963.

Kwa ujumla  swali  la   sheria  ipi  itumike   kugawa mali  za  marehemu  pale  ambapo  hakuacha  wosia,  hujibiwa  kwa   kuangalia  aina  ya  maisha  aliyoishi  marehemu. 


TAMKO LA SERIKALI KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI

Mkuu wa Wilaya ya Iringa aongoza Matembezi ya Ufunguzi wa Wiki ya Mahakama

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela amezindua wiki ya mahakama kwa matembezi mjini Iringa yaliyoongozwa na brass band ya Jeshi la Magereza. Akihutubia majaji pamoja na wananchi amesisitiza uharaka wa kutoa HAKI. kesi nyingi zinachelewa kuisha na wananchi wengi wamedulumiwa haki yao na huu ni uvunjwaji katiba.

Pia amesisitiza wakimama wasimamiwe haki zao. Kasesela pia alisisitiza polisi na ofisi ya mwanasheria mkuu wakae pamoja kubaini kwa nini kesi nyingi ushahidi unakuwa haujakamilika? Wakamilishe ushahidi kabla ya kufungua kesi. Bila haki nchi haiwezi kuendelea hata kidogo.

Akitoa salamu zake Jaji Mfawidhi kanda ya Iringa Mh Mary Shangali aliahidi kuharakisha kesi pia kutembelea magereza yote ili kubaini waliocheleweshewa haki zao.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akiongoza matembezi ya wiki ya Mahakama.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akihutubia wakati wa ufunguzi wa wiki ya Mahakama, uliofanyika jana Mkoani humo.
Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesela akiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu mkoa wa Iringa.

SIMBA SPORT CLUB WAZINDUA DUKA LA VIFAA VYA MICHEZO DAR FREE MARKET JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Rais wa Simba Sport Club Evans Aveva Akikata Utepe wakati wa Uzinduzi wa Duka la Vifaa vya Michezo Dar Free Market Mtaa wa Ali Hassan Mwinyi (jirani na Ubalozi wa Kenya na DSTV) jijini Dar es salaam akiwa Ameambatana na Afisa Mtendaji Mkuuwa EAG Group Ndugu Iman Kajula Pamoja na Wadau wengine wa Club Hiyo.
 Katika kukuza wigo wake wa mapato pamoja na upatikanaji wa vifaa, klabu ya Simba leo imezindua duka lake rasmi kwa ajili ya kuuza vifaa vya michezo vyenye chapa ya Simba.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Rais wa Simba Evans Aveva alisema “kama  mtakumbuka moja ya malengo ambayo uongozi wangu huu uliopo madarakani ulijiwekea ni pamoja na kuongeza wigo wa mapato kupitia vyanzo vyake vilivyopo lakini pia kuja na mkakati kabambe kwa ajili ya kuongeza na leo wote tunakuwa mashuhuda katika kuzindua duka letu la vifaa vya michezo. Duka ambalo litakuwa likiuza kila bidhaa ambayo inachapa Simba hivyo wanachama na wapenzi wa Simba kuweza kujua ni wapi mahala pa kupata vitu halisi vya Simba na kwa bei nafuu zaidi”

 Duka hili si tu litasaidia katika kuongeza mapato kwa klabu lakini pia litaziba mianya yote ya wale watu wote wasio itakia mema klabu yetu na kuamua kutengeneza vitu feki vyenye chapa ya Simba, kwakuwa sasa mtu ukikutwa na bidhaa feki basi mkono wa sheria utakuwa juu yako. Nipende kuwa sisistiza wanachama, wapenzi na wadau wote wa Simba na soka la Tanzania kwa ujumla kuwa kwanza tupende vyetu vya nyumani lakini pia tupende kutumia vitu halisi na kuachana na utamaduni wa mazoea ya kutojali ni kipi halisi na kipi ni feki” aliongeza Rais Aveva.

Akizungumza kwenye ufunguzi huo Mkurugenzi wa kampuni ya EAG Group Ltd ambao ni washauri na watekelezaji wa masuala ya biashara na masko kwa klabu ya Simba Bw. Imani Kajula alisema “nadhani sasa wanasimba tunaweza kufurahia vya kwetu kwani kwa sasa tunajua ni wapi vinapatikana na ni wapi ukienda huwezi kukutana na kitu feki chenye chapa ya Simba na hapo si pengine bali ni Simba Sports Shop lililopo katika jingo la DarFree Market. Pamoja na kuwepo kwa duka hili lakini pia vifaa vyote vitakavyokuwa vikipatikana hapa ndani ya siku za hivi karibuni vitakuwa vikipatikana kwenye duka mtandao (Online Shops) na hivyo kuweza kuwafikia watu wote popote walipo nchini Tanzania”. 

 Unapotaka vifaa vyenye ubora wa hali ya juu hakuna sehemu nyingine zaidi ya Simba Sports Shop. NUNUA HALISI ICHANGIE TIMU YAKO. Alimalizia Mkurugenzi wa EAG Group Ltd Imani Kajula

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa duka hilo msimamizi wa Duka la vifaa vya michezo venye chapa ya Simba mkurugenzi wa kampuni ya Insight Media Bw. Tahir Othman ambao ni waamiliki wa Dukakwa kuhamasisha wapenzi wote wa Soka Tanzania kuweza kuunga mkono juhudi zinazofanywa na klabu ya Simba ili kuweza kukuza mapato kwa klabu yetu lakini pia kuweza kupata bidhaa bora na halisi za chapa ya Simba. 

VIDEO: GODAUNI LA MAFUTA LATEKETEA KWA MOTO JIJINI MBEYA

MPANGO WA KUSAIDIA KAYA MASIKINI WANUFAISHA KAYA MILIONI 1.1 NCHINI

$
0
0

Mpango wa Kijamii wa Uzalishaji Salama ili kusaidia kaya masikini kupambana na umasikini (PSSN) umefanikiwa kuwa na matokeo mazuri kwa kusaidia kaya Milioni 1.1 nchini na kusaidia juhudi za serikali kupambana na umasikini.

Hayo yamefahamika wakati washirika wa maendeleo ambao ni Umoja wa Mataifa, Benki Kuu ya Dunia, Serikali ya Uingereza kupitia kitengo cha Maendeleo ya Kimataifa, Irish Aid, USAID, Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Sweden (SIDA) walipotembelea miradi ya maendeleo katika wilaya za Unguja, Chamwino, Babati, Sumbawanga (Manispaa na Wilaya), Singida na Hanang kwa kipindi cha siku tatu kuanzia Januari, 19 hadi 22.
Bi. Kazijya Kila ambaye ni mmoja wa wanufaikaji wa fedha akitoa ushuhuda kuhusu mradi wake wa chakula ulivyowezeshwa na TASAF ambapo hadi hivi sasa anatengeneza faida ya Shilingi 7000 kwa siku na kabla ya kuwezeshwa alikuwa akikaa nyumbani na mama yake bila kuingiza kipato chochote.

Katika Mpango huo ambao utekelezwaji wake unasimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) unafanyika Tanzania Bara na Tanzania visiwani ukiwa na lengo la kuzisaidia kaya masikini pesa za matumizi ili kukidhi mahitaji ya kupata chakula pamoja na kuwawezesha kusaidia watoto wao kupata elimu jambo ambalo linaonekana kuzaa matunda kwa maeneo mengi ikiwepo Tanzania visiwani.

Serikali ya Tanzania imekuwa ikisaidia na washirika wa maendeleo ili kupunguza umaskini uliokithiri kwa wananchi wake na mwaka 2013 iliweka mpango wa kusaidia kaya masikini 275,000 kwa kipindi cha miaka mitano na tangu ianzishe mpango huo ilifanikiwa kusaidia kaya 275,000 kwa mwaka 2013 pekee katika wilaya nane nchini.
Mtaalamu Mwandamizi wa Masuala ya Jamii kutoka Benki ya Dunia, Bw. Muderis Abdulahi Mohamed (kushoto) na Msimamizi wa mpango wa PSSN, Bw. Ramadhani Madari wakifuatilia kipindi cha maswali na majibu kwa wanufaikaji wa fedha hizo.

Na mpaka kufikia sasa mpango huo umeshatoa malipo mara 12 na jumla ya kaya masikini milioni 1.1 zimeshafaidika na mpango huo ikiwa ni kwa wilaya 161 na vijiji 9789 nchini.

Viewing all 110009 articles
Browse latest View live




Latest Images