Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live

UZINDUZI WA MAADHIMISHO YA SKAUTI WA KIKE (GIRL GUIDE)

$
0
0
Na Mugishagwe Zablon
Ingawa dunia inataja nchi nyingi kusgindwa kufikia malengo ya milenia klushindwa kutimiza bWasichana na wanawake nchini wametakiwa kuchangamkia fursa zinazojitokeza katika taasisi mbalimbali ikiwa ni pamoja na za Chama cha Skauti wa Kike (Girl Guide) ili kupambana na mambo ambayo yanachangia ukatili kwa wanawake. 
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘Msichana anaweza kuzuia ukatili dhidi ya Wanawake’, Mratibu wa kampeni hiyo, Agnes Fivao alisema wasichana kwa nafasi yao wanaweza kudhibiti hali hiyo kwa kuwa viungo baina yao na wanajamii wengine. 
“Wewe Girl Guide au msichana mwingine yeyote, unafanya nini kuwasaidia wenzako wanaokuzunguka ambao hawaendi shule, wanaotumikishwa katika ajira mbaya, una nafasi ya kuwaunganisha, kufikiri mbali zaidi, kuwa na mtazamo wa kudunia katika kile kinachowakabili” alisema. 
Alibainisha kuwa ulimwengu bado unakabiliwa na changamoto kubwa ya tohara kwa wasichana na wanawake, biashara ya binadamu hususan watoto wa kike na wasichana wataweza kupambana nayo kwa kutoa taarifa, kupaza sauti na kuwaelimisha wengine. 
“Mnatakiwa kuwa sauti yao na skauti wa kike ni walinzi wa wanawake wenzao” alisema na kuongeza kuwa wasichana na wanawake wanatakiwa watambue kuwa wanatakiwa kupiga hatua zaidi kimaendeleo kutoka katika kujiongoza hadi kuongoza wengine. Awali aizungumza wakati wa uzinduzi huo ambao uliambatana na maadhimisho ya kila mwaka toka 1926 ya muanzilishi wa skauti ulimwenguni Lord Robert Baden-Powell, Mkufunzi wa Girl Guide mkoa wa Dar es Salaam, Margareth Olumbe alisema watafanya shughuli mbalimbali za kijamii kuanzia sasa hadi siku ya kilele 22 Februari mwaka huu 2016. 
“Tutafanya usafi na shughuli zingine za kijamii, kuanzia ngazi ya Taifa hadi wilaya, kutoa huduma katika vituo vya wasiojiweza, Hospitalini na kwingineko” alisema na kuongeza kuwa kauli mbinu ya mwaka huu ni kuwaunganisha wasichana na wanawake milioni 12 ulimwenguni ifikapo 2020. 
Dunia bado inakabiliwa na changamoto ya kushindwa kufikia lengo namba tatu la milenia kuelekean 2015 linalotaka Usawa wa Kijinsia na kwa Wanawake na kazi ya ziada inahitajika kufanyika ili kupata uwiano huo ikiwa ni pamoja na wasichana na wanawake kujisimamia wenyewe badala ya kusubiri njia zingine.
 Kamishna wa Chama cha Skauti wa Kike (Girl Guide), Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Shaba akizungumza wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya kuanzishwa taasisio hiyo ulimwenguni katika hafla ilioyofanyija jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mkufunzi wa mafunzo, Margreth Olumbe.

 Mwenyekiti wa Chama cha Maskauti wa Kike, Sawi Dath (kushoto) na mkufunzi wa mafunzo wa chama hicho, Margareth Plumbe wakiimba nyimbo za hamasa wakati wa uzinduzi wa maadhimuisho ya chama hicho ya kila mwaka, jijini Dar es Salaam,

 Waasisi na wanachama wa Chama cha Maskauti wa Kike, wakizindua maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwa muasisi wa chama hicho ulimwenguni, Lord Robert Baden-Powell jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Chama cha Maskauti wa Kike, Sawi Dath (kushoto) na mkufunzi wa mafunzo wa chama hicho, Margareth Plumbe wakiimba nyimbo za hamasa wakati wa uzinduzi wa maadhimuisho ya chama hicho ya kila mwaka, jijini Dar es Salaam.


Shule ya St. Jude ya jijini Arusha yapongezwa

$
0
0
Shule ya Sekondari ya St. Jude ya jijini Arusha kwa namna ya pekee wameelewa azma na malengo ya Shule Direct. Hawakuwahi kuwaambia Shule Direct kwa maneno lakini takwimu zinaelezea ukweli huu. 
Ni shule inayoongoza kwa kuwa na wanafunzi wengi wanaojifunza kupitia tovuti ya Shule Direct kuliko Shule nyingine yoyote; na kufuatiwa na Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Azania na ya tatu ni Shule ya Sekondari ya Kibasila. 
Wanafunzi wa shule hizi wametumia muda mwingi zaidi kujifunza kupitia Shule Direct kuliko watumiaji wengine. 
Shule hizi ni mfano wa kuigwa kwa sababu maarifa hayana mipaka, kadri tunavyojenga hulka ya kutafuta na kujifunza kwa kutumia fursa mbali mbali, hivyo ndivyo wanafunzi watakavyokuwa hata pale watakapokuwa wamemaliza shule. 
Kwa namna ya pekee, Shule Direct wanawapongeza na kuwasifu shule ya St. Jude kwa sababu wamekuwa mfano wa kuigwa. 
Shule Direct ni taasisi inayoboresha fursa za mwanafunzi kuweza kusoma, kufanya mazoezi na kujadiliana katika masomo mbalimbali na wanafunzi wenzake pamoja na walimu kwa kutumia Teknolojia. 
Elimu bora ni haki ya kila mtoto na kila mwanafunzi. Ukuaji wa Teknolojia Tanzania na barani Afrika kwa ujumla unapaswa kuwa nyenzo ya kuboresha upatikanaji wa maarifa na elimu ambapo kuna changamoto nyingi zinazowazuia wanafunzi kuipata. 
Shule Direct inaamini kwamba elimu inapaswa kupatikana saa yoyote na mahali popote kwa sababu elimu ni chachu ya kubaini uwezo na vipaji vilivyomo ndani ya mtu.

 Wanafunzi walioongoza kujifunza kupitia Shule Direct kutoka Shule ya St. Jude, (kwa kutumia majina yao ya kujisajili, wala si majina yao kwa kweli), ni iBOY, Brightstar, Nasmar, Mkavi, Chrisspros, Mathew.bob, Muller, Amaur, Shabbb, Jariss.j.jr. Tunawazawadia wanafunzi hawa “digital coins” za Shule Direct zitakazowawezesha kununua vitabu na vifaa mbalimbali kupitia hapo hapo kwenye tovuti.





SIMU TV: baadhi ya matukio yaliyojiri katika michuano ya kombe la Shirikisho hii leo.

$
0
0
Kutoka uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Simon Msuva anaipatia Yanga goli la kuongoza dhidi ya Friends Rangers; https://youtu.be/OdfOIIGrH7g

Kutoka uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Simon Msuva anaipatia Yanga goli la pili;https://youtu.be/GTm57NeJCOM

Kutoka uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Matheo Antony anaipatia Yanga goli la tatu; https://youtu.be/jaGLGX4CXXQ

Kutoka mjini Shinyanga, Jerryson Tegete anaipatia Mwadui FC goli la kuongoza;https://youtu.be/ISvrBBeCrF4

Kutoka uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, Pambano baina ya Yanga na Friends Rangers limemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa goli 3-0;https://youtu.be/gSsMbJfAusE

Kutoka mjini Shinyanga pambano baina ya Mwadui na Stand United yalakamika kwa Mwadui kuibuka na ushindi wa goli 1-0; https://youtu.be/NUVNaUj6Gzs

NAIBU KATIBU MKUU MAMBO YA NDANI YA NCHI AFANYA ZIARA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA)

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizaraya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (katikati), akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Mwaimu (kulia), wakati alipotembelea kituo cha kumbukumbu cha Mamlaka hiyo, mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (kulia), akielezea jambo wakati alipotembelea Kitengo cha kudhibiti ubora wa Vitambulisho vya Taifa, kilichopo kwenye Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA),Katikati ni Mkurugenzi wa Uzalishaji Vitambulisho, Paul Bwathondi na kushoto ni Afisa Usajili anayeshughulikia ubora, Jemima Mulokozi. Naibu Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya kutembelea Mamlaka hiyo mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Uzalishaji Vitambulisho wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Paul Bwathondi (kulia), akitoa ufafanuzi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (watatu kutoka kulia waliosimama), Naibu Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya kutembelea Mamlaka hiyo mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.
 Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), anayeshughulikia ubora, Jemima Mulokozi (kushoto), akimuelezea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (kushoto), jinsi wanavyothibiti ubora wa Kitambulisho cha Utaifa kabla akijachapishwa.Naibu Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya kutembelea Mamlaka hiyo mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), anayeshughulikia ubora, Jemima Mulokozi (kushoto), akimuelezea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya (kushoto), jinsi wanavyothibiti ubora wa Kitambulisho cha Utaifa kabla akijachapishwa.Naibu Katibu Mkuu alikuwa kwenye ziara ya kutembelea Mamlaka hiyo mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam.((Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

WANASWA KWA WIZI WA MAJI BUGURUNI

$
0
0
Matukio ya Wizi wa Maji yamekuwa yakikithiri kila kukicha katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam licha ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Mamlaka husika za kisheria pindi mtu au kikundi cha watu kinapobainika kufanya ubadhirifu huo.

 Shirika la majisafi na Majitaka Dar es salaam(DAWASCO), imewakamata raia 2 wa china ambao  wamejiunganishia huduma ya Maji kinyume na taratibu katika eneo la Buguruni Jijini Dar es salaam, katika godauni moja inayomilikiwa na kampuni ya ALLIED TRANSPORT, jengo ambalo wachina hao wamepanga huku wakiendesha shughuli zao za utengenezaji wa mabati.

Kampuni hiyo ya wachina inayojishughulisha na utengenezaji wa mabati imebainika kujiunganishia huduma hiyo na Meneja wa Dawasco Wilaya ya Ilala Mhandisi Ramadhani Mtindasi wakati wa msako mkali ulioanza katika wilaya yake ya kuwabaini wahujumu miundo mbinu ya Maji na wezi wa Maji.

Mhandisi Mtindasi amesema kuwa matukio ya Wizi wa Maji kwa wilaya ya Ilala yamekidhiri sana na yanapelekea adhari kubwa sio tu kwa shirika bali hata kwa watumiaji wa Maji waliopo eneo la Ilala kutokana na Maji mengi kuishia mikononi mwa wachache hivyo kupelekea uhaba na kero ya Maji kwa maeneo yenye stahili ya Maji.


BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

NAPE ASIMIKWA UCHIFU MKOANI MWANZA

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (katikati) akizungumza na Machifu wa kisukuma kwenye kituo cha Utamaduni Bujora, kulia pichani ni Jaji Mstaafu Mark Bomani na kushoto ni Chifu Charles Kafipa wa Bukumbi mkoani Mwanza.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amesimikwa uchifu wa kisukuma mara baada ya kutembelea kituo cha utamaduni wa kisukuma cha Bujora.
Katika tuzo hiyo ya watemi wa kisukuma ambayo risala yake imeandikwa na kusainiwa na Katibu wa Umoja wa Watemi wa Kisukuma Mtemi CM. Dotto Itale, wamemtakia heri na kumuomba mwenyezi mungu amsaidie kufanya kazi zake vizuri na kumtunukia cheo cha Manju Mkuu kiongozi wa ngoma kubwa mwenye kughani umati wote ukaitikia, na kumpa jina la Sangija ambalo linaunganisha Mamanju wote.

WIZARA YA AFYA YAMPONGEZA JK KWA KUTEULIWA KUWA MMOJA KATI YA WENYEVITI JOPO LA USHAURI LANGAZI YA JUU KUHUSU AFYA YA MAMA NA MTOTO DUNIANI

WAZIRI MKUU LESOTHO ATAKIWA KUTANGAZA MATOKEO YA TUME YA SADC

$
0
0
KIKAO maalum cha Wakuu wa Nchi na Serikali na Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Uchumi na Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC Double Troika) kimeiagiza Serikali ya Lesotho iwe imetangaza matokeo ya Tume iliyoundwa kuchunguza matatizo ya kisiasa nchini humo ifikapo Februari Mosi, mwaka huu.

Agizo hilo lililotolewa kwa Waziri Mkuu wa Lesotho, Dk. Pakalitha Mosisili katika kikao cha SADC Double Troika kilichofanyika mapema wiki hii Gaberone, Botswana, chini ya Mwenyekiti wake, Luteni Jenerali Seretse Khama Ian Khama ambaye pia ni Rais wa nchi hiyo.

SADC Double Troika ni kikao maalum cha Wakuu wa Nchi na Serikali (SADC Summit) na wakuu wa nchi wanaounda Kamati ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics, Defense and Security Cooperation) kilichofanyika kwenye kituo cha mikutano ya kimataifa (GICC), jijini Gaborone, Botswana.

Pamoja na kutaka Lesotho itangaze matokeo ya tume hiyo, SADC Double Troika iliitaka nchi hiyo iandae mchakato wa kueleza njia za utekelezaji wa mageuzi kama yalivyopendekezwa kwenye ripoti ya tume hiyo ifikapo Agosti, mwaka huu.

“Vilevile, nchi ya Lesotho inatakiwa kuandaa mazingira wezeshi yatakayotoa nafasi kwa viongozi wa upinzani na baadhi ya maofisa wa kijeshi wanaoishi uhamishoni ambao walikimbia machafuko, waweze kurejea nyumbani,” ilisema sehemu ya taarifa iliyotolewa na sekretariati ya SADC siku moja baada ya kikao hicho kumalizika.

Mkutano huo wa Botswana ulihudhuriwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye alikuwa akimwakilisha Rais Dk. John Pombe Magufuli; Rais wa Botswana, Luteni Jenerali Khama; Rais wa Afrika Kusini, Bw. Jacob Zuma; Rais wa Msumbiji, Bw. Filipe Jacinto Nyusi; Waziri Mkuu wa Swaziland, Dk. Barnabas Dlamini na Waziri wa Mambo wa Nje wa Zimbabwe, Bw. Simbarashe Mumbengegwi ambaye alimwakilisha Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo.  

SADC Double Troika ni mkutano unaohusisha viongozi wakuu watatu wanaoongoza chombo cha ushirikiano wa siasa, ulinzi na usalama na wengine watatu kutoka kwenye Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa SADC. Hawa wanawakilisha mwenyekiti aliyepo madarakani, mwenyekiti aliyemaliza muda wake na mwenyekiti ajaye ambaye huwa ni makamu mwenyekiti.

Kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Balozi Radhia Msuya, chini ya muundo wa SADC, kuna mambo makuu mawili; la kwanza likiwa ni utangamano wa kikanda ambao unasimamiwa na mkutano wa wakuu wa nchi (SADC Summit) na la pili ni la siasa, ulinzi na usalama ambalo linasimamiwa na chombo maalum (SADC Organ).

Akifafanua zaidi, Balozi Msuya alisema wajumbe wa mkutano wa SADC Organ ni Msumbiji (Mwenyekiti); Afrika Kusini (Mwenyekiti aliyemaliza muda wake) na Tanzania inayotarajia kuchukua uenyekiti wa chombo hiki ifikapo Agosti, 2016. Botswana, Zimbabwe na Swaziland ndizo zinaunda SADC Summit.

Mapema, kikao hicho, kilipokea taarifa ya msuluhishi wa SADC kwenye mgogoro wa Lesotho ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Afrika Kusini, Dk. Cyril Ramaphosa ambayo iliainisha mambo kadhaa yakiwemo ya kikatiba na kiusalama ndani ya nchi hiyo.

Dk. Ramaphosa alitakiwa kuhakikisha kuwa mgogoro huo uliovihusisha vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi ya Lesotho, unatatuliwa kwa njia ya mazungumzo kati ya wadau husika ili kuhakikisha kuwa nchi hiyo inarudi kwenye hali ya amani - kisiasa na kiusalama.

Mgogoro wa Lesotho umehusisha kuuawa kwa aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Lesotho, Luteni. Jenerali Maaparankoe Mahao, mnamo Juni 25, 2015. Pia baadhi ya wananchi wanadaiwa kutiwa vizuizini na wengine kuwekwa ndani.

NAVY KENZO WAPAGAWISHA MASHABIKI WAO KATIKA UZINDUZI WA VIVA NIGHT CLUB JIJINI MBEYA

$
0
0
Kikundi cha Muziki wa Kizazi Kipya cha Navy Kenzo kimetoa Burudani ya nguvu katika uzinduzi wa Viva Night Club iliyopo maeneo ya Forest ya Zamani mkabala na Chuo Kikuu cha Mzumbe Jijini Mbeya..
Kiota Kipya cha Burudani Jijini Mbeya kiendacho kwa Jina la Viva Night Club Pichani kilichopo Eneo la Forest ya Zamani mkabala na Chuo Kikuu cha Mzumbe Jijini Mbeya..
Baadhi ya Wadau wa Burudani wakiwa katika Matanuzi Ndani ya kiota hicho cha Burudani kiendacho kwa Jina la Viva Night Club kilichopo Eneo la Forest ya Zamani mkabala na Chuo kikuu cha Mzumbe Jijini Mbeya..
PICHA ZOTE NA MR.PENGO MBEYA.

KUTOKA MAKTABA: TABIA MWANJELWA AKIWA NA MAQUIZ DU ZAIRE - JANE

NGOMA AZIPENDAZO ANKAL

Leo Nimemkumbuka Shakespeare

$
0
0

Na Profesa Joseph Mbele

Leo, bila kutegemea, nimemkumbuka Shakespeare. Nimeona niandike neno juu yake, kama nilivyowahi kufanya. Nimekumbuka tulivyosoma maandishi yake wakati wa ujana wetu katika shule ya sekondari.
Katika kiwango kile, tulisoma tamthilia tulizozimudu, kama The Merchant of Venice naJulius Caesar. "High school," ambayo kwangu ilikuwa Mkwawa, tulisoma tamthilia ngumu zaidi, kama Othello na Hamlet.  Othello ilikuwa katika silabasi ya "Literature."
Nakumbuka sana kuwa hapo hapo Mkwawa High School tuliangalia filamu ya Hamlet, ambamo aliyeigiza kama Hamlet alikuwa Sir Lawrence Olivier. Huyu ni mmoja wa waigizaji maarufu kabisa wa wahusika wakuu wa Shakespeare. Niliguswa na uigizaji wake kiasi cha kujiaminisha kwamba sitaweza kushuhudia tena uigizaji uliotukuka namna ile. Nilipoteza hamu ya kuangalia filamu yoyote baada ya pale, kwa miaka mingi.
Ninavyomkumbuka Shakespeare, ninajikuta nikikumbuka mambo mengi. Kwa mfano, nakumbuka tafsiri murua za Mwalimu Julius Nyerere za tamthilia mbili za Shakespeare: The Merchant of Venice na Julius Caesar. Nakumbuka pia jinsi Shaaban Robert alivyomsifu Shakespeare, kwamba akili yake ilikuwa kama bahari pana ambayo mawimbi yake yalikuwa yanatua kwenye fukwe zote duniani. 
Shaaban Robert alitoboa ukweli; Shakespeare ni mwalimu asiye na mfano. Aliingia katika nafsi za wanadamu akaelezea silika na tabia zao kwa ustadi mkubwa, na alitafakari uhalisi wa maisha yetu akatuonyesha maana na mapungufu yake. Alitukumbusha kwamba dunia ni kama jukwaa la maigizo, ambapo kila mmoja wetu anakuja na kutimiza yanayomhusu na kisha anatoweka. Kusoma zaidi BOFYA HAPA

yale yale.... wadau kuweni macho na utapeli kama huu. ukiletewa delete hapo hapo

$
0
0
Re: CONGRATULATION ON YOUR PAYMENT OF USD1,500,000.00

Attention: Beneficiary,

Be inform that We have been authorized by the United Nations Compensation Commission (UNCC) to release your compensation payment totaling the sum of US$1,500,000.00 through Money Gram transfer.You will be receiving the sum of US$5,000.00 daily until the total sum of US $1,500,000.00 is completely transferred to you.

Besides,we have already sent your first payment of US$5,000.00 today,therefore,you are advice to contact our director of foreign Remittance Department MR.JOHN CHIDOZIE by replying to this email and request him to give you the payment details such as Money Gram reference Numbers and senders name to enable you pick up your first payment of US$5,000.00 at any Money Gram office located around you.Also,you can reach him through the telephone numbers stated below for faster process.

Contact Person: MR.JOHN CHIDOZIE
Phone Number: +229 940 677 68

REMEMBER TO FORWARD HIM YOUR FULL INFORMATION AS REQUIRED BELOW TO ENABLE HIM LOCATE YOUR PAYMENT FILE AND ATTEND TO YOU IMMEDIATELY.

1. Your Full Name:
2. Address:
3. Age:
4. Occupation:
5. Telephone Numbers:
6. Country:

NOTE: that the amount to be paid to you is (USD1.500,000.00 ) we expect your urgent response to this email to enable us monitor the payment effectively.

Best Regards

SHINDANO LENYE FURSA YA KUKUZA MITAJI KWA VIJANA LA MO MJASIRIAMALI LAZINDULIWA

$
0
0
DSC07284-2
Mwenyekiti wa Taasisi wa MO Dewji, Mohammed Dewji
Na Modewjiblog team
Mwenyekiti wa Taasisi wa MO Dewji, Mohammed Dewji kwa kushirikiana na kampuni ya Darecha Limited leo (jumatatu) wamezindua shindano la Mo Mjasiriamali lenye lengo la kusaidia kukuza ujasiriamali miongoni mwa vijana.
Shindano ya Mo Mjasiriamali litatoa fursa ya ukuzaji wa mitaji, ulezi wa wajasiriamali na mitandao ya biashara kuongeza mwanga, ujasiri na kuzalisha wajasiriamali Tanzania.
“Mimi kama Mjasiriamali kijana na mzaliwa wa Singida vijijini, sikufikiria hata mara moja kama leo ningekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa moja ya makampuni yaliyofanikiwa sana katika nchi yetu na hata barani Afrika.” Inasema taarifa Mkurugenzi Mtendaji huyo wa MeTL kwa vyombo vya habari mwishoni mwa wiki.
Aidha alisema Afrika ni moja ya bara linalokua kwa haraka na lenye ukuaji imara wa uchumi na amini vijana wa Tanzania wana nafasi kubwa ya kutumia fursa hizo ili kujiletea uchumi endelevu.
Lakini pamoja na ukweli huo changamoto kama za ukosefu wa mitaji, ukuzaji ujasiriamali na mitandao ya biashara zimekatisha tamaa vijana wengi kukuza kwa mafanikio makampuni yao hapa Tanzania na hivyo kupunguza kasi ya ukuaji wa uchumi kwa watu wa kipato cha kati.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Benki ya maendeleo ya Afrika (ADB), watu wenye kipato cha kati katika bara la Afrika wataongezeka na kufikia watu bilioni 1.1 ifikapo mwaka 2060.
Watu wa kipato cha kati ndio wanaochagiza ukuaji wa uchumi kutokana na mahitaji yao na pia ari ya ujasirimali.
Pamoja na ukweli huo kunachangamoto nyingi zinawakabili watu hao wa kipato cha kati. Mathalani nchini Tanzania changamoto kubwa kwa vijana wajasirimali ni gharama za kutafuta mtaji kwa kazi hizo.
“Kuna haja kubwa ya kuhakikisha kwamba vijana hawa wanaondolewa tatizo la ujasirimali ili waweze kusukuma mbele uchumi wa Tanzania.” inafafanua taarifa hiyo.
Aidha kwa kuwa Tanzania inaelezwa kuwa ni nchi ya 19 katika bara la Afrika kuhusiana na fursa na ujasirimali ipo haja ya kusaidia ili kuiondoa katika nafasi hiyo. Taarifa ya nafasi ya Tanzania imo katika ripoti yake ya mwaka 2014 ya Africa Prosperity Report.
Taarifa ilifafanua zaidi kwamba kutokana na haja hiyo Taasisi ya Mo Dewji na Darecha Limited wameungana pamoja na kuanzisha shindano la Mo Entrepreneurs ili kutambua na kuuenzi mchango wa wajasirimali chipukizi na kufanikisha ndoto zao.
Ili kufanikisha nia ya kuwa na wajasiriamali wengi, shindano hilo linatarajiwa kuwa daraja kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji, Mohammed Dewji (MeTL Group na Mwenyekiti wa Mo Dewji Foundation) ambapo vijana ambao wanaonekana wana kitu cha kufanya, lakini hawana msaada watashiriki kwa lengo la kupata msaada katika mfumo wa mtaji, mtandao na usimamizi wa ukuaji wa shughuli wanayofanya au kutaka kuifanya ili kuianzisha na kuikuza.
Mambo hayo yatatekelezwa katika mfumo wa shindano litakalogusa wajasiriamali ambao wana ari na nia ya dhati ya kuendeleza shughuli walizofikiria na kuzianzisha kwa lengo la kuinua uchumi wao binafsi na wa taifa.
Washindi watatu watakaotangazwa Aprili mwaka huu watapatiwa mtaji wa kuanzia au kuendeleza, pia watapatiwa maarifa ya kuendeleza shughuli zao na kuanzishwa mtandao wa kibiashara na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa MeTL Group na mwenyekiti wa Mo Dewji Foundation, Mohammed Dewji.
Wakati akipewa tuzo ya Forbes ya mwaka 2015, Mohammed Dewji aliitoa kwa heshima ya vijana akiwatakia kila la heri waking’aa, kuvunja nira ya woga, kukabili changamoto na kuendelea katika ujasiriamali kwa lengo la kufanya dunia yetu mahali bora pa kuishi.

INTRODUCING NEW HIT SONG zawadi by Option Ft Recho


SIMU TV: MAPITIO YA MAGAZETI LEO

JOCKTAN MALULI, DANIEL MSIRIKALE WAIBUKA WASHINDI KATIKA SHINDANO LA BONGO STYLE

$
0
0
WASHIRIKI wa shindano la Bongo Style linaloratibiwa na asasi isiyo ya kiserikali ya FASDO, Jocktan Cosmas Maluli  (25) na Daniel Msirikale (24) wameibuka kidedea kwa kujinyakulia tuzo za shindano hilo katika fainali iliyofanyika katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar.

Shindano hilo lililoanzishwa mtandaoni mwezi Septemba mwaka 2015, lilijumuisha washiriki wapatao mia tatu wenye vipaji vya upigaji picha na ubunifu wa mitindo huku washiriki kumi pekee wakiingia kwenye fainali baada ya michujo mbalimbali kabla ya washiriki hao wawili wakishinda tuzo hizo.

Washiriki hao walishinda kutokana na kura za majaji waliobobea katika fani hizo ambapo kwa upande wa picha majaji hao walikuwa ni: Sameer Kermalli, Hanif Abdulrasul, Idd John na Angela Kilusungu huku kwenye ubunifu wa mavazi majaji hao wakiwa ni: Martin Kadinda, Rio Paul, Zamda George na Comfort Badaru.

Jocktan Maluli ambaye ameshinda katika kipengele cha Best Fashion Designer 2015 na Daniel Msirikale aliyeshinda katika kipengele cha Best Photographer 2015, wote pamoja wamepokea kitita cha dola 500 kila mmoja huku wakipata nafasi ya kwenda nchini Ubelgiji kwa ajili ya kuonesha ubunifu wao katika maonesho ya Africa Firm Festival Belgium kuonesha kazi zao pamoja na washiriki 18 walioshiriki shindano hilo, yatakayofanyika hivi karibuni nchini humo.

Aidha washindi wa vipengele vingine ni: Shahbaaz  Yusuf aliyeshinda kipengele cha Best Personality of the Year 2015, Winfrida Touwa aliyeshinda katika kipengele cha Peoples Choice Award for Fashion Designers na Rasheed Rasheed aliyeshinda kipengele cha Peoples Choice Awards for Photograph.

Fainali hizo zilizohudhuriwa na wageni waalikwa na wadau mbalimbali wa kazi za sanaa na kupambwa na burudani mbalimbali kama vile nyimbo za asili, muziki na maonesho ya mavazi na kazi za sanaa kutoka kwa washiriki hao.

Mshindi wa Ubunifu mitindo Jocktan Cosmas Maluli A.k.a Makeke(aliyeshika cheti) akiwa katika picha ya pamoja na  waratibu wa shindano hilo kuanzia kushoto ni  Zamda George, Comfort Badaru, Martin Kadinda, Reuben Nabora na Stanley Kamana.
Mshindi wa kipengele cha The Best Photographer, Daniel Msirikale (mwenye miwani) akipokea tuzo yake.

Mlezi wa FASDO, Reuben Nabora akitoa salamu kutoka kwa mwasisi wa FASDO, Lilian Nabora aliyeko Ubelgiji.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI.

CHAMA CHA KARATE MKOANI KILIMANJARO CHAIOMBA SERIKALI KUTUPIA JICHO MCHEZO HUO

$
0
0
Vero Ignatus - Moshi Kilimanjaro.

Chama cha Karate Mkoa wa Kilimanjaro wanaiomba serikali kutupia macho kwenye mchezo huo kwani imekuwa ikiwasahau ukizingatia mchezo huo ni michezo kama ulivyo mingine na kwamba mchezo huo umekuwa ukifundishwa pia katika majeshi mbalimbali hapa nchini. 

 Hayo yamesemwa nakapteni wa timu na katibu msaidizi wa chama cha Katrate mkoa wa Kilimanjaro bwana Wembo Hamisi katika viwanja vya mazowezi mkoani hapo na amekusema kuwa wamekuwa wakikwama mara wanapohitajika kwenye mechi za kirafiki,ndani na nje ya nchi kwasababu hawana sapoti kutoka serikalini na wafadhili. 
 Aidha amesema kuwa Karate ni mchezo ambao mtu yeyote anaweza kuucheza na akatengeneza afya ya mwili,na mchezo huo ni wa kawaida kama ilivyo michezo mingine kama mpira wa miguu amewataka watu wote kujitokeza kwa wingi kujiunga katika mchezo huo wa Karate kwa sifa kuu ya karate ni nidhamu. 

Sambamba na hayo bwana Wembo amesema kuwa katika mchezo huo wapo wanawake na ameiomba jamii waondokane na ile dhana potofu kwamba mwanamke akicheza mchezo huo wa Karate hawezi kupata mtoto na kufanya shughuli nyingine za kijamii amesema huo ni upotoshaji kwani mwanamke anao uwezo wa kupata mtoto kama walivyo wengine na anatengeneza afaya nzuri kabisa. 

Aidha amesesema kuwa mchezo huo wa Karate kwa historia umeanzishwa miaka mingi kwa mkoa wa Kilimanjaro chama cha karate kina takribani miaka saba sasa tangia kuanzishwa kwa chama hicho,na baadae wakaunda shirikisho la Karate nchini Tanzania ambapo inajumuisha michezo yote ya karate ,ambapo januari 30 watakuwa na tamasha la Karate la kuwatambulisha wachezaji wa timu litakalofanyika mkoani hapo katika ukumbi wa shule ya msingi Mwenge. 

Katibu huyo ameinisha ratiba yao ndani ya miezi sita ambapo watafanya matamasha mbalimbali ikwemo februari 13/2016 watafanya tamasha wilayani Same katika ukumbi wa kimweli same mjini, machi 24-26, mashindano ya mchezo wa GOJUKAI KARATE ya Afrika Mashariki, Kampala Uganda , aprili 30 mashindano ya GOJUKAI Karate ya wazi ya kuuenzi mlima Kilimanjaro ambapo watashiriki watoto wenye umri wa kati na watu wazima yatafanyika Moshi, Mwisho ni Tamasha la shukrani litakalofanyika mei 16 hapo hapo Moshi Kilimanjaro. Kwa mkoa wa Kilimanjaro mchezo wa karate unaochezwa unajulikana kama Gojukai Stayle, ambayo ilianzishwa kutoka nchini Japan,na chama katika mkoa huo kinaundwa na vilabu mbalimbali ambavyo klabu mama ni Ralway club, Pasua Club, Mwenge Club, Ccp Club,Rau Club,na vilabu vingine vinaundwa na wanafunzi mbalimbali ambapo kila club ina zaidi ya wanafunzi 20-30.hivyo wanawaomba ,Taasisi mbalimbali ,wafanyabiashara,makampuni mbalimbali hata watu binafsi kujitokeza kuudhamini mchezo huo wa Karate.

KATIBU MKUU WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO AWATUNUKU VYETI WAHITIMU WA CHUO CHA BAHARI

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sehemu ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga, akizungumza na wahitimu (hawapo pichani) katika mahafali ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sehemu ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga, akimtunuku cheti mmoja kati ya wanafunzi bora waliofanya vizuri katika masomo yao Chuoni hapo.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sehemu ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga, (wa nne kutoka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa chuo hicho pamoja na baadhi ya wahitimu.

HARUSI YA MTOTO WA MTEMVU, AMINA MTEMVU YAFANA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Bwana Harusi Masoud Masoud akimwekea mkewake Amina Mtemvu mkono kichwani wakati wa harusi yao iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee VIP Holl.(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Bwana Harusi Masoud Masoud
Bi harusi Amina Mtemvu akiwa katika tabasamu baada ya hafla ya harusi yake iliyofanyika katikaUkumbi wa Diamond Jubilee (VIP) Holl, Dar es Salaam  
Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiagana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke wakati wa hafla ya ya harusi ya Amina Mtemvu iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee (VIP) Holl, Dar es Salaam.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Viewing all 109996 articles
Browse latest View live




Latest Images