Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR YASAINI MIKATABA MIWILI YA UJENZI NA MAKANDARASI M/S.HUMPHREY CONTRUCTION LIMITED YA ARUSHA NA MINDSET TECHIES (T) YA DAR ES SALAAM.

0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khadija Bakari Juma akitoa ufafanuzi kwa Wadau waliohudhuria hafla ya Utiaji Saini wa Mikataba miwili ya Ujenzi baina ya Wizara yake na Makandarasi kutoka M/S. Hamphrey Construction Limited ya Arusha na Mindset Teches (T) ya Dar es Salaam Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Elimu Zanzibar.
 Wadau mbalimbali waliohudhuria katika sherehe za kutiliana saini mikataba hiyo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Khadija Bakar Juma na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi M/s. Humphrey Construction Limited ya Arusha wakibadilishana Mikataba baada ya kutiliana saini.
PICHA NA ABDALLA OMAR ( HABARI- MAELEZO ZANZIBAR)

SIMU TV: UCHAMBUZI WA HABARI TOKA VITUO MBALIMBALI VYA TELEVISHENI December 30, 2015

0
0
 Kampuni iliyopewa kandarasi ya kusambaza umeme katika mkoa wa Kagera imelalamikiwa kuwa baadhi ya wafanyakazi wake kujihusisha na vitendo vya Rushwa.https://youtu.be/46Yk2_Je9us

Familia 79 za walemavu wa ukoma katika kambi ya Nyabange wilayani Butiama watoa wito kwa taasisi na mashirika mbalimbali kuwasaidia kuboresha huduma za kijamii.https://youtu.be/Haig5So1Fow

Wakazi wa kijiji cha Mwambegwa kilosa Mkoani Morogoro waiomba Wizara ya ardhi kufuta mashamba pori ya wawekezaji ambayo hayajaendelezwa.https://youtu.be/A9Isi7VHu8I

Serikali yapongeza jitihada zinazofanywa na taasisi za dini kwa kuwawezesha wajasiliamali ili kujikwamua kiuchumi: https://youtu.be/SDjOg38IUBo

Wizara ya ardhi yaanza kutumia mfumo mpya wa tehama ili kuboresha huduma zao na kutatua migogoro ya ardhi nchini: https://youtu.be/4j5F8pgIxLI

Waziri Simbachawene aagiza kusimamishwa kazi kwa maafisa biashara wawili wa manispaa ya Dodoma

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. George Simbachawene amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuwasimamisha kazi mara moja Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa ya Dodoma Bw. Elias N. Kamara na Bibi Donatila D. Vedasto (Afisa Biashara) kuanzia leo tarehe 30/12/2015 kwa kosa la kusababisha urasimu katika utoaji wa leseni za biashara.

Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kumuondoa kwenye nafasi yake Kaimu Afisa Biashara wa Manispaa na Msaidizi wake na nafasi zao kukaimishwa kwa watu wengine ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zilizotolewa dhidi yao.

Agizo hili limetolewa na Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wafanyabiashara ambayo yalionyesha kuwepo kwa mazingira ya rushwa.

Katika uchunguzi ambao umefanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imegundulika kuwa kulikuwa na maombi ya leseni 750 ambayo yalikuwa hayajashughulikiwa bila sababu za msingi na hali hiyo ilipelekea kuikosesha Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kiasi cha shilingi Milioni 75.

Aidha, Mhe. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI ameagiza Mamlaka za Serikali kote nchini kuhakikisha wanatoa leseni za biashara bila urasimu wowote na muombaji apate leseni ndani ya siku 2 au 3 anapoomba leseni.

Mhe. Simbachawene ametoa agizo kwa Maafisa biashara wote nchini kuacha urasimu katika kutoa leseni na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Imetolewa na:
Rebecca Kwandu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Rais - TAMISEMI 30 Desemba, 2015

MHE. KAIRUKI AENDELEA NA ZIARA KATIKA TAASISI ZILIZO CHINI YA OFISI YAKE KUHIMIZA UWAJIBIKAJI

0
0
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) (wa pili kulia) akizungumza na watumishi wa Bodi ya Mishahara na Masilahi katika Utumishi wa Umma alipoitembelea ofisi hiyo mapema leo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) (kushoto) akiwahimiza watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma kuwajibika alipoitembelea ofisi hiyo mapema leo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akitazama nyaraka inayoandaliwa kutunzwa katika nakala laini (soft copy) alipoitembelea Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa mapema leo.

WAZIRI MKUU, MAJALIWA ATAKA MAELEZO JUU YA UBADHILIFU WA MALI ZA UMMA HALMASHAURI YA KIGOMA UJIJI

0
0
Na Editha Karlo wa Globu ya Jamii, Kigoma.

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amemtaka Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma Ujiji, Mhandisi na Mhasibu kupeleka taarifa ya maandishi kwa katibu tawala wa mkoa juu ya ubadhirifu waliofanya wa mali za umma.

Hayo ameyasema leo wakati akiongea na watumishi wa Wilaya zote kwenye kikao cha majumuisho ya ziara yake kilichofanyika katika ukumbi wa NSSF .

Alisema kuwa katika halmashauri ya Kigoma Ujijikuna ubadhirifu wa mali za umma umefanyika wa kuuza soko la Kigodeko, Jengo la Baby Come na jengo la MI Boss kwa kiasi cha shilingi milioni mia tatu badala ya milioni 800.
Alisema kuwa anawataka wajieleze kwa katibu tawala wa Mkoa kwa maandishi ni utaratibu upi wametumia kuuza mali za umma na kwavnini walikiuka agizo la mkuu wa Mkoa la kuwataka wasiuze mali hizo.

Mhe. Majaliwa alisema kuwa maelezo yao anayataka Jumamosi January 2, 2016 yawe yamekamilika na kufika ofisini kwakwe ili kama kuna ukweli hatua za kinidhamu ziweze kuchukuliwa kwa waliohusika na ubadhilifu huo.

Akiongea na mtandao huu juu ya tuhuma hizo mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji mhandisi Boniface Nyembele alisema kuwa ni kweli mali hizo wameuza lakini kwa kufuata utaratibu.

"Utaratibu wote tulifuata kuuza malu hizo na vikao halalu vilikaa na kupitisha na mihutasari ya vikao ipi na tenda tulitangaza tika mwaka 2013 tumeuza mwaka huu mwezi wa 6"alisema Mkurugenzi, na kuongeza kuwa  fedha walizopata  zilitumika katika ujenzi wa mahabara na shughuli zingine.

'Kwa kuwa Waziri Mkuu ametutaka tujieleze kwa maandish ikwa katibu tawala tutafanya hivo kwani kila kitu kipo wazi"alisema.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongea na watumishi kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Kigoma juu ya ziara yake ya kikazi Mkoani hapa.
Baadhi ya watumishi na viongozi wa mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majliwa katika Kikao cha Majumuisho ya ziara yake mkoani humo kwenye ukumbi wa NSSF Desemba 30, 2015.

WAZIRI MKUU AHITIMISHA ZIARA MKOANI KIGOMA,ATEMBELEA KAMBI ZA WAKIMBIZI, AWAONYA KUTOJIHUSISHA NA UHALIFU

0
0

 Sehemu ya Wakimbizi wa Kambi ya Nduta, Wilaya ya Kibondo, mkoani Kigoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa (hayupo pichani)  wakati alipokuwa akizungumza na wakimbizi hao. Majaliwa aliwaonya wakimbizi hiyo kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa usalama katika kambi hiyo.
 Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Kambi ya Nduta, Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wakati alipofanya ziara katika kambi hiyo. Katika hotuba yakekwa wakimbizi wa kambi hiyo, Majaliwa aliwaonya wakimbizi hao kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa usalama katika eneo waliohifadhiwa.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akimwagilia mti wa kumbukumbu alioupanda katika Kambi ya Nduta,  Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma wakati Waziri huyo alipoambatana  na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa katika ziara katika kambi hiyo. Katika hotuba yake, Waziri Mkuu Majaliwa aliwaonya wakimbizi hao kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa usalama katika eneo waliohifadhiwa.
 Mkuu wa Kambi ya Wakimbizi ya Nduta, wilayani Kibondo, Fred Nsijile akitoa taarifa ya kambi yake kwa Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa (kushoto). Katika taarifa hiyo Mkuu wa Kambi alisema kambi yake inakabiliwa na upungufu wa maji kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi wanaoishi kambini humo. Hata hivyo katika hotuba yake, Waziri Mkuu Majaliwa alisema atalifanyia kazi tatizo hilo na pia aliwaonya wakimbizi katika kambi hiyo kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa usalama katika eneo waliohifadhiwa. Wapili kushoto meza kuu ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga. Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Job Masima (watatu kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi, Harrison Mseke.
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa (kulia) akiwafurahia wacheza ngoma  ambao ni wakimbizi kutoka Burundi wakati walipokuwa wanamkaribisha katika Kambi ya Nduta, mkoani Kigoma kuzungumza na wakimbizi hao. Katika hotuba yake, Majaliwa aliwaonya wakimbizi hao kutojihusisha na uhalifu ili waweze kuishi kwa usalama katika eneo waliohifadhiwa. Wapili kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa akimkabidhi mkimbizi Cesiwa Angelani (kushoto) zawadi ya ndoo yenye vifaa vya kumuhudumia mtoto baada ya mzazi huyo kujifungua katika Hopsitali iliyopo katika ya Nyarugusu ambapo Wakimbizi wanahifadhiwa. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga.

TCRA YAZICHUKULIA HATUA ZA KISHERIA KAMPUNI ZA SIMU ZILIZOSHINDWA KUWALINDA WATEJA WAKE KITEKNOLOJIA

0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Ally Simba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na makampuni ya simu  za mkononi ya Tigo, Airtel, Halotel na Zantel na Smart kwa kuto kukidhi vigenzo. Pia amesema kuwa Makampuni hayo yamepigwa faini ya shilingi milioni 25 kwa mamlaka ya mawasiliano Tanzania kabla ya Januari 29 mwakani.
Mwanasheria wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mama Elizabeth Zagi akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Ally Simba jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

JAMHURI YA YA MUUNGANO YA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

HATUA ZA KISHERIA NA KIUDHIBITI KWA MAKAMPUNI YA SIMU YALIYOSHINDWA KULINDA WATEJA WAKE KITEKNOLOJIA NA KISHERIA KUHAKIKISHA USALAMA WA MAWASILIANO YAO

1. Katika shughuili zake za udhibiti wa huduma za mawasiliano nchini, Mamlaka ya Mawasilaino Tanzania imepokea malalamiko kutoka kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano dhidi ya kuwepo mazingira yasiyo salama katika huduma za mawasiliano na hivyo kusababisha kufanyika kwa vitendo vya utapeli unaofanywa kwa kutuma jumbe za udanganyifu na kulaghai, hivyo kusababisha watu kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu. Kwa mfano kupokea ujumbe kutoka namba unayoifahamu ukikuagiza utume fedha au ujumbe wa kashfa au matusi wakati hautoki kwa mhusika mwenye namba. Mamlaka imepokea malalamiko mengi kutoka kwa wateja na malalamiko mengine hupelekwa Polisi. Kwa miezi miwili tu, matukio 42 yameripotiwa Polisi pamoja na TCRA ambayo tukio moja tu linakuwa na ulaghai wa takribani milioni 25 peke yake.

2. Tarehe 16 Oktoba, 2015 Mamlaka iliwakumbusha watoa huduma za simu nchini juu ya wajibu wao kuchukua hatua za kusheria na kitaalamu ili kulinda watumiaji dhidi ya utumaji wa jumbe za kilaghai na kuchukua hatua mara moja kuzuia mitandao yao kutumika kutuma jumbe za udanganyifu na kulaghai. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mamlaka tarehe 16 Desemba, 2015 Mamlaka ilibaini kuwa  kampuni za Benson Informatics Limited (inayojulikana kama Smart), MIC Tanzania Limited (inayojulikana kama Tigo), Airtel Tanzania Limited, Viettel Tanzania Limited (inayojulikana kama Halotel) and Zanzibar Telecom Limited inayojulikana kama Zantel) zimeshindwa, zimepuuzia na zimekataa kufuata maagizo ya Mamlaka kuchukua hatua mara moja kuzuia mitandao yao kutumika kutuma jumbe za kilaghai kinyume na Kanuni Na.8(a) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2011 [the Electronic and Postal Communications (Computer Emergency Response Team) Regulations, 2011].

3. Tarehe 18 Disemba, 2015 Mamlaka iliwaamuru watoa huduma za mawasiliano waliotajwa hapo juu kufika mbele ya Mamlaka na kujieleza kwa nini hatua za kisheria zisichukuliwe dhidi yao kwa kuvunja sheria na kanuni ya 8(a) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielectroniki na Postal ya Mwaka 2011 [the Electronic and Postal Communications (Computer Emergency Response Team) Regulations, 2011] kwa kushindwa kuweka mazingira salama kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano.

4. Watoa huduma walifika na kutoa maelezo ya utetezi kati ya tarehe 21 na 23 Desemba, 2015.

5. Baada ya kuwasikiliza na kutilia maanani utetezi wa watoa huduma na kwa mujibu wa uchunguzi na majaribio uliofanywa na Mamlaka, Mamlaka imejiridhisha kuwa mitandao ya watoa huduma waliotajwa hapo juu haikuwa salama na kuwa watoa huduma hao walishindwa kufuata maelekezo ya Mamlaka juu ya kuweka mazingira salama katika huduma wanazotoa. Hivyo Mamlaka imejiridhisha kuwa watoa huduma wamekiuka matakwa ya Kanuni ya 8(a) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielectroniki na Postal ya mwaka 2011 (The Electronic and Postal Communications (Computer Emergency Response Team) Regulations, 2011) inayowataka watoa huduma kuweka mazingira ya mitandao salama kwa kuchukua hatua za kusheria na kitaalamu ili kulinda watumiaji dhidi ya uhalifu ikiwa ni pamoja na utumaji wa jumbe za kilaghai kupitia mitandao yao.

6. Kwa mujibu wa Kifungu cha 17 cha Jedwali la Pili katika Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306 ya Sheria za Nchi, kinachoipa Mamlaka uwezo wa kutoa adhabu kwa Wenye Leseni dhidi ya uvunjifu wa Sheria, Kanuni na Masharti ya Leseni, Mamlaka ya Mawasiliano imetoa:

A. Onyo kali kwa Kampuni za:
(i) Benson Informatics Limited (inayojulikana kama Smart),
(ii)  MIC Tanzania Limited (inayojulikana kama Tigo),
(iii)  Airtel Tanzania Limited,
(iv)  Viettel Tanzania Limited (inayojulikana kama Halotel), na 
(v) Zanzibar Telecom Limited (inayojulikana kama Zantel). 

kwa kushindwa kutimiza matakwa ya Kanuni ya 8(a) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Postal ya mwaka 2011  [the Electronic and Postal Communications (Computer Emergency Response Team) Regulations, 2011] kwa kushindwa kuweza mazingira salama kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano.
B. Imeamuru Kila Kampuni husika:
(i)   Kuhakikisha kuwa, kuanzia siku ya kutolewa kwa amri hii, inaweka mazingira salama katika mtandao wake yatakayozuia utumaji wa jumbe za kilaghai (yaani ‘spoofed messages’) na matishio mengine ya kiusalama;
(ii)   Kulipa faini ya Shilingi za Kitanzania Milioni Ishirini na Tano (Shs 25,000,000.00) kwa Mamlaka ya Mawasiliano kabla ya tarehe 29 Januari, 2016; na
(iii) Endapo Makamuni haya yatashindwa kutimiza amri Na.2 hapo juu, Mamlaka itachukua hatua zaidi za kisheria na kiudhibiti dhidi ya Kampuni ya Simu husika.
7. Aidha, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania inapeda kuchukua fursa hii kuwatahadharisha wananchi kuwa makini na jumbe za kuwataka kutuma fedha bila ya kuwa na uhakika. Inashauriwa kuhakiki ujumbe husika kwa kupiga simu na kuongea na mhusika kabla ya kufanya maamuzi ya kutuma fedha hata kama namba inayotumika unaijua. Vilevile wawe makini wanapopokea jumbe zinazoonesha zinatoka kwa mtu fulani wanayemjua kumbe ni matapeli wanaotumia ulaghai kwa njia hii ya “spoofing”.

IMETOLEWA NA

Dkt. Ally Y. Simba
MKURUGENZI MKUU
30 Disemba, 2015

ELIMU DHIDI YA KIPINDUPINDU


BBC DIRA YA DUNIA JUMATANO 30.12.2015

NGOMA AFRICA BAND IS WISHING YOU A HAPPY NEW YEAR 2016

0
0
Ngoma Africa band is wishing you all Happy New Year 2016.
And right the way through.
May it bring all the things That are Special to you!
Every Future Happiness
enjoy music at www.ngoma-africa.com

WAZIRI WA AFYA, MHE. UMMY MWALIMU ATEMBELEA MSD, AAHIDI KUWA BALOZI WAO NA KUWATATULIA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI IKIWEPO DENI WANALOIDAI SERIKALI

0
0
ummy-msd 175
Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akitembelea moja ya ghala la kuhifadhia dawa iliyopo makao makuu ya MSD,kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laureane Bwanakunu na watatu kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya MSD Prof.Idris Mtulia.

SIMU TV:HABARI KUTOKA TELEVISHENI

JK,WAZIRI LWENGE WAKAGUA MITAMBO YA MAJI WAMI,CHALINZE

0
0

Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (katikati), akizungumza na Waziri wa Maji, Gerson Lwenge wakielekea kukagua mitambo ya kusafisha na kusafirisha maji Wami, katika Halmashauri ya Mji wa Chalinze, mkoani Pwani leo.
Rais Jakaya Kikwete na Lwenge wakiangalia mitambo ya kusafisha maji

Wakiwa katika picha ya pamoja
Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete , akizungumza na Waziri wa Maji, Gerson Lwenge (kushoto kwake) wakielekea kukagua mitambo ya kusafisha na kusafirisha maji Wami, katika Halmashauri ya Mji wa Chalinze, mkoani Pwani leo.Wa pili kulia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete.
Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete akionesha kitu walipotembelea mitambo ya maji Wami
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akizungumza na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge katika mitambo hiyo.

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI INAKUSUDIA KUVIFUTA VYAMA VYA KIJAMII VIFUATAVYO BAADA YA KUKIUKA TARATIBU ZA USAJILI

Droo ya nne ya promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" ya GAPCO yafanyika jijini Dar es Salaam

0
0
Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania, Caroline Kakwezi (katikati) akibonyeza kitufe kwenye kompyuta kuwatafuta washindi wa droo ya nne ya promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" inayowawezesha wateja wake kujipatia lita 40 za mafuta kwa kila mshindi wa droo hiyo kila wiki. Kulia ni Mkaguzi wa michezo ya kubahatisha nchini, Bakari Maggid, na kushoto ni Meneja wa Fedha wa Kampuni ya mafuta ya GAPCO Tanzania, Michael Chobu.

Wizara ya Mambo ya Ndani yatoa Orodha Ya Vyama Vinavyopewa Kusudio La Kufutwa

Ligi Kuu ya Zanzibar: JKU yaitandika KVZ bao 2-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Amaan

0
0
Wachezaji wa Timu ya JKU wakisalimiana na Wachezaji wa Timu ya KVZ kabla ya kuaza mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar Timu ya JKU imeshinda 2--0.

Mchezo uliochezwa jioni mabao ya JKU yamefungwa katika kipindi cha kwanza na katika dakika ya 8 mshambuliaji wa Timu ya JKU Mbarouk Chande ameipatia bao timu yake katika dakika ya nane ya mchezo huo kipindi cha kwanza na Bao la ushindi la JKU limepatikana katika kipindi hicho cha kwanza katika dakika ya 35 ya mchezo huo lililofungwa na mshambuliaji wake Nassor  Mattar.
Kocha Mkuu wa Timu ya KVZ King akifuatilia mchezo huo wakati timu yake ikiwa nyuma kwa mabao 2--0. 
Beki wa timu ya KVZ Juma Abdalla, akijiandaa kumzuiya mshambuliaji wa Timu ya JKU mwenye mpira Nassorv Mattar, wakati wa mchezo wao wa Ligi Kuu ya Zanzibar uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar. 

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Waraghbishi wilayani kahama wapania Kumkomboa Mwanamke

0
0
Na Krantz Mwantepele .Kahama

Wanawake ni nguzo muhimu sana katika uchumi wa watanzania wengi. Mwanamke ana ushawishi mkubwa na hasa pale anapoamua kuwa chachu ya maendeleo. Na hasa anapowezeshwa kufanya hivyo.


Katika kufanikisha hili waraghbishi wameamua kutoa mafunzo ya uraghbishi kwa makundi mengine ya jamii. Mojawapo ya kundi hilo ni la wanawake. Waraghbishi wapya toka katika kijiji cha Nyandekwa, kati ya hao wapo 9 ambao ni wanawake.

Mmoja wao ni Anna Alphonce, Mwenyekiti wa kitongoji cha Busolo, katika kijiji cha Nyandekwa. Akielezea jinsi alivyoanza uraghbishi alisema:

“Mi niliona kuna kikundi wanakaaga humu karibu kila jioni. Na kila nilipokuwa napita jirani na hapa naona watu wamejaa, basi nikapenda namimi nijiunge nao na hasa baada ya kujua nini wanafanya. Na hapo ndipo nilipoanza uraghbishi,”
Anna Alphonce (katikati) ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busolo akifafanua jambo wakati akielezea uraghbishi anaofanya .

Akiwa kama mwenyekiti mwanamke wa kitongoji aliweza kutumia nafasi yake kufanya uraghbishi kwa anaowaongoza. Kwa kuwa kilikuwa ni kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu, aliitisha mikutano kwenye kitongoji chake kwa lengo la kutoa hamasa ya wananchi kujitokeza kwa wingi. Kwa nafasi yake aliweza kuyafikia makundi ya wazee, vijana na wanawake. Ingawa kati ya hawa wanawake ndio walikuwa washiriki wazuri.

SIMU TV: MAPITIO YA MAGAZETI LEO

Benki ya Exim yafunga mauzo ya dhamana yake kwa mafanikio makubwa.

0
0
Benki ya Exim Tanzania imetangaza kufunga mauzo ya dhamana yake ya muda mrefu (hati fungani) huku ikibainisha kuwa kiasi kilichopatikana kutokana na mauzo ya hati hizo kimezidi mara dufu (asilimia 195) ya malengo ya awali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo jijini Dar es Salaam jana, uuzwaji wa dhamana hizo ulifungwa rasmi Disemba 18 mwaka huu huku benki hiyo ikifanikiwa kukusanya kiasi cha sh bilioni 19.7 kutokana na mauzo ya dhamana hiyo tofauti na makadilio ya sh. bilioni 10 iliyokuwa imejipangia kukusanya hapo awali.
“Awali lengo letu lilikuwa ni kukusanya takribani kiasi cha bilioni 10 hadi bilioni 15. Tunashukuru kuona kwamba tulichokusanya ni karibu asilimia 200 ya malengo yetu ya awali na kiasi kilichopatakina kimetoka kwa wawekezaji mbalimbali kutoka kila kona ya nchi,’’ alibainisha, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki hiyo, Bw. Selemani Ponda.
Kupitia dhamana hiyo wawekezaji wanapatiwa uhakika wa kupata riba ya 14% kwa mwaka isiyokuwa na makato ya kodi,itakayolipwa kila baada ya miezi 6 kwa kipindi cha miaka 6 huku  ikiruhusu wawekezaji wenye kiasi cha kuanzia shilingi milioni moja.
Akizungumzia zaidi mafanikio hayo Bw Ponda alisema yametoa fursa kwa watanzania kuwa sehemu ya ukuaji wa benki hiyo huku akiongeza;“Mafanikio haya yanaonyesha imani kubwa waliyonayo watanzania kwa benki ya Exim na zaidi wanavutiwa na ubunifu wa benki hii katika huduma za kifedha.,’’

Bw Ponda alitumia fursa hiyo kuwashukuru baadhi ya wadau ikiwemo Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana nchini (CMSA), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Wakala wa mauzo ya dhamana hiyo, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) pamoja na wawekezaji wote kwa kufanikisha mchakato mzima wa mauzo ya dhamana hiyo.
Viewing all 109593 articles
Browse latest View live




Latest Images