Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live

Wakorintho wapili kuzindua Mchepuko sio dili Tamasha la Krismasi

$
0
0
KWAYA ya Wakorintho Wapili ya Wilayani Mafinga mkoani Iringa inatarajia kuzindua albamu yake ya Mchepuko sio dili kwenye tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama albamu hiyo ina nyimbo nane ambazo zinafikisha ujumbe  wa neno la Mungu kwa jamii.Msama alizitaja nyimbo hizo ni pamoja na Tanzania, Mchepuko sio dili, Watenda mabaya, Ee bwana, Yahwe tunakuinua, Tuokoe baba, Dunia hii na Hana.

Aidha Msama alisema maandalizi ya kuelekea katika tamasha hilo yanaendelea vizuri, hivyo Watanzania wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kuelekea tamasha hilo.Aidha Msama alisema Watanzania walichukilie tamasha hilo kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa Mungu baada ya kutupitisha katika kipindi kigumu cha uchaguzi Mkuu ambao ulifanyika kwa amani na utulivu ingawa kulikuwa na viashiria vya uvunjifu wa amani.

Msama alisema waimbaji wa Tanzania watakaosindikiza tamasha hilo ni pamoja na Rose Muhando, Upendo Nkobe, Joshua Mlelwa, Kwaya ya Wakorintho wapili.Wengine watakaopanda jukwaani siku hiyo ni Martha Mwaipaja, Jesca BM,  na Christopher Mwahangila, Sifael Mwabuka sambamba na Kwaya ya Yombo KKKT.


“Tumejipanga vilivyo na tamasha la Krismasi, hivyo tujiandae kupiga goti la kumrudishia Mungu Shukrani baada ya uchaguzi Mkuu ambao ulikuwa na mguso wa aina yake kutoka kwa vijana walioonesha kutaka maendeleo kutoka kwa serikali,” alisema Msama.

MAAFISA MAGEREZA NCHINI WAMETAKIWA KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

$
0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Mbarak Abdulwakil akihutubia kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza uliofanyika leo Desemba 16, 2015 katika Ukumbi wa Bwalo Kuu la Maafisa Magereza,Ukonga jijini Dar es Salaam.
 Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kutoka vituo mbalimbali hapa nchini wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi kama wanavyoonekana.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe. Mbarak Abdulwakil akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza (walisimama). Wa Pili tatu kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(wa tatu kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Deonice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(Picha zote na Lucas mboje wa Jeshi la Magereza).

TPDC yachangia ujenzi wa kisima cha maji Mkuranga

$
0
0
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Marie Msellemu akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi (10,000,000) kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Abdallah Kihato (wa tatu kulia) kwa ajili ya ujenzi wa kisima cha maji katika kijiji cha Njia Nne.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Abdallah Kihato akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhiwa kiasi cha shilingi milioni kumi (10,000,000) kwa ajili ya ujenzi wa kisima cha maji katika kijiji cha Njia Nne.
Wanakijiji wa kijiji cha Njia Nne wa walio hudhuria shughuli ya makabidhiano hayo.

WAZEE TAFF WAMWOMBA WAKIFAMBA AGOMBEE TENA NAFASI YA URAS

$
0
0

Msemaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Ahmed Olotu (mzee Chilo) akisoma waraka wa kupinga uamuzi wa Rais wa Shirikisho hilo Simon Mwakifwamba kwa kutogombea tena nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kushoto ni Mzee Ramadhani Ditopile.
 Mzee wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Hamisi Kagaye (kushoto) akichangia mada wakati wa kupinga uamuzi wa Rais wa Shirikisho hilo Bwana Simon Mwakifwamba wa kutogombea tena nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo. Kulia ni Mzee Ramadhani Ditopile.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia tamko la Wazee wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) lililohusu kupinga uamuzi wa Rais wa Shirikisho hilo Simon Mwakifwamba wa kutogombea tena nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). 
(Picha zote na Benedict Liwenga)

TANZANIA AND U.S. CELEBRATE SIGNIFICANT PROGRESS IN THE FIGHT AGAINST MALARIA AFTER 10 YEARS OF U.S. GOVERNMENT INVESTMENT IN TANZANIA

$
0
0
In order to eliminate malaria carrying mosquitoes, the USAID supported Tanzania Vector Control Scale-Up Project in partnership with the malaria control programs in Tanzania and Zanzibar implemented indoor residual spraying in 28 districts, covering a cumulative 5.9 million households in the Lake Zone and Zanzibar.

On Tuesday, December 15, 2015, the United States Agency for International Development (USAID), the Government of Tanzania, and RTI International convened at the Hyatt Regency Hotel to celebrate significant reductions in malaria morbidity and mortality in mainland Tanzania and Zanzibar, which have resulted in the protection of up to 8.5 million people annually.

This progress was made possible in large part by the Tanzania Vector Control Scale-up Project, implemented by RTI International with support from USAID through the U.S. President’s Malaria Initiative (PMI). The celebration was attended by representatives of the National Malaria Control Programme (NMCP) and the Zanzibar Malaria Elimination Programme (ZAMEP) as well as others working to control malaria in Tanzania and across sub-Saharan Africa.

The Tanzania Vector Control Scale-up Project, which began in 2006 and will conclude its activities in September 2016, contributed to a substantial decrease in illness and death caused by malaria through a combination of interventions, including indoor residual spraying of households with insecticide (IRS), distribution of insecticide-treated bed nets, and enhanced disease surveillance.

READ MORE HERE

MKUTANO MKUU WA TFF WAAHIRISHWA

$
0
0
Mkutano Mkuu wa kawaida wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) uliokuwa ufanyike Tanga ikiwamo shughuli ya uwekaji jiwe la msingi kwenye kiwanja cha TFF jijini Tanga sasa umeahirishwa kwa muda usiojulikana.

Mwishoni mwa mwezi Novemba 2015, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) mkoa wa wa Ilala ulitoa agizo la kufungwa na kuchukuliwa fedha kutoka kwenye akaunti za Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) ili kulipa fedha zaidi ya shilingi bilioni 1.6, sehemu kubwa ikiwa ni malipo ya kutoka kwenye mishahara (PAYE) ya makoch Jan Poulsen, Kim Poulsen, na Jacob Michelsen na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye mchezo kati ya Tanzania na Brazil mwaka 2010.

Baada ya hatua hiyo TFF iliwasiliana na TRA na kuweka bayana kwamba deni la walimu (makocha) na mchezo dhidi ya Brazil lilistahili kulipwa na serikali na haikuwa sahihi kulielekeza TFF.

Aidha TFF ilieleza athari ambazo zingetokea iwapo amri hiyo (Agent Order) ingetekeleezwa kuwa ni pamoja na kusitishwa kwa ziara ya timu ya vijana chini ya miaka 15 (U15) katika nchi za Rwanda, Uganda na Kenya, kusimama kwa program za vijana na wanawake, Mkutano Mkuu, Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Kombe la Shirikisho.

Baada ya utekelezaji wa amri hiyo kuanza TFF ilifanya kikao na TRA na makubaliano ya kufungua akaunti yakafanikiwa. Hata hivyo akaunti zilifunguliwa zikiwa hazina fedha kwa kuwa zilishapelekewa Benki Kuu (BOT) na zoezi la madai haliwezi kukamilika kwa muda mfupi.

Baada ya hali hiyo kujitokeza, TFF ilifanya kila linalowezekana kuhakikisha Mkutano Mkuu unafanyika ikiwa ni pamoja na kutafuta ufadhili toka kwa wadau wake, lakini zoezi hilo limeshindikana katika muda mfupi uliopo na hivyo Shirikisho limeamua kuahirisha Mkutano Mkuu 2015 mpaka hapo hali itakaporuhusu.

TFDA Yafunga Kiwanda Bubu Kagera

Philips launches new range of patient monitors in Tanzania designed to provide access to high quality care at affordable costs

$
0
0
Royal Philips (NYSE: PHG AEX: PHIA) has announced the launch of its Efficia CM Series patient monitors in Tanzania – these cost effective products are designed to provide clinicians with access to high-quality of care, even in resource-limited facilities. These solutions highlight Philips’ commitment to enhance access and enable quality care across the health continuum – from healthy living and prevention, to diagnosis, treatment, recovery and home care, including in remote areas.

“As we innovate to improve health care, monetary constraints should not be a reason for limiting access to the best care available for improving a patient’s health,” said Roelof Assies, General Manager, Philips East Africa. “The Efficia suite is designed to bring trusted and effective Philips technology and performance at an affordable price to the health care facilities where resource limitations have prevented this access before.”
Making quality care affordable
Effective patient monitoring can help improve diagnosis and provide earlier intervention, which is not only critical for improving patient outcomes, but can also help hospitals improve operational efficiencies. 


The Efficia CM Series patient monitors provide the same core physiological measurements and algorithms that are present in other Philips patient monitors, but are designed to be more cost-effective and scalable to the needs of budget-constrained health care facilities. 

The series, including Efficia CM100, Efficia CM120 and Efficia CM150, are solidly built and reliable, able to handle heavy workloads and electrostatic interference, and can be customized for a variety of patient types, acuity levels and clinical settings, and include an intuitive user-interface to ease the burden on busy clinician workflow. 

The Efficia CM patient monitors can be connected to Efficia CMS200 central monitoring system, which provides centralized monitoring and real-time access to patient physiological data and displays waveforms, parameters and alarms for up to 32 patients.

Efficia DFM100 - Providing therapeutic care where it is needed most

To deliver quality care, clinicians need to make quick, informed decisions when responding to an emergency and caring for a patient across the entire course of treatment. The Efficia DFM100 defibrillator/monitor is designed to be easy to use for both basic and advanced life support care providers to meet the demands of patient care in pre-hospital and hospital environments effectively and consistently. 
The Efficia DFM100 provides functionalities needed to enhance patient care, regardless of where they are located. It is also scalable to ensure affordability across all care settings. 

“Clinicians are constantly under pressure to meet clinical demands on a tight budget,” said Dr. Juma A. Mfinanga, Head of Emergency Department at Muhimbili National Hospital. “The Efficia solutions work with the clinicians and the hospital; they are affordable and intuitive, allowing limited staff to focus on care first.”

RAIS WA ZANZIBAR ATEMBELEWA NA RAIS WA KAMPUNI YA KIMATAIFA YA CNOOC KUTOKA CHINA

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya CNOOC kutoka Nchini China Cui Hanyun wakati alipofika Ikulu mjini Zanzibar leo na ujumbe aliofuatana nao.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Ujumbe wa Kampuni ya China National Offshore Oil Company ltd (CNOOC) ulifoka Ikulu Mjini Zanzibar kuonana na Rais, ugeni huo ukiongozwa na Balozi wa China nchini Tanzania Xie Yunliang (wa pili kulia) na Makamo Rais wa Kampuni ya Kimataifa ya (CNOOC) Cui Hanyun (katikati) wengine ni viongozi wa juu wa kampuni hiyo.
[Picha na Ikulu.]

WAZIRI KAIRUKI KUKAA NA WATUMISHI MAOFISINI KUBAINI CHANGAMOTO

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb) amesema atakaa na Watumishi katika ofisi zao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kuzitatua.

Mhe. Kairuki alisema hayo mapema leo wakati alipokutana na Wafanyakazi wa Idara ya Uendelezaji Sera-UTUMISHI  katika  kikao kazi.

“ Watu wasiwe waoga katika kazi, mimi nimekuja kufanya kazi na kila kitu kina utaratibu wake” Mhe. Kairuki alisema na kusisitiza kuzingatia taratibu zilizowekwa ni jambo la  msingi.

Waziri Kairuki alisema kufanya kazi kwa ubunifu na kuwashirikisha Wafanyakazi wengine ili kutoa huduma bora na haraka kwa wananchi katika ulimwengu wa sasa ni muhimu. 

Mhe. Kairuki alielekeza katika mipango ni vizuri kuwa na maeneo maalum ambayo yatatoa huduma zaidi ya moja (Huduma Centre)  ili kupunguza mzunguko usio lazima, na kuokoa muda  kwa wananchi wanaofuata huduma hizo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb) anakutana na kila Idara na Kitengo ndani ya ofisi yake ili kubaini changamoto na kuzitatua.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Idara ya Uendelezaji Sera wakiwa katika kikao kazi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki (Mb), akitoa maelekezo kwa Watumishi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI mapema leo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Anjella Kairuki ( Mb), kushoto, akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Bw. Mathias B. Kabunduguru. Waziri Mhe. Kairuki anatembelea kila Idara na Kitengo katika ofisi yake kubaini changamoto mbalimbali na namna ya kuzitatua.

MHAGAMA: AZITAKA HAMASHAURI ZOTE NCHINI KUTEKELEZA MAELEKEZO YA SERIKALI YA KUJIAANDAA NA KUKABILI MAAFA

$
0
0
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akiangalia Sehemu ya mtaro wa maji katika eneo la Tegeta, Basihaya wilayani Kinondoni, Jijini Dar es Salaam leo wakati alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo, kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), akimsikiliza mkazi wa Tegeta, Basihaya Jijini Dar es Salaam, Jumanne Malongo alipokuwa akimueleza jinsi wembamba wa mtaro huo unavyosababisha maji kujaa katika makazi yao, leo wakati alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo, kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda. 
 Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Manisipaa kinondoni, Ando Mwakunga akimueleza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Bibi Jenista Mhagama (Mb), uharibifu wa “kalvati” katika eneo la Boko, Ununio Jijini Dar es Salaam, leo wakati Waziri huyo alipofanya ziara kuangalia jinsi wilaya hiyo ilivyojiandaa kukabili maafa ya Mvua zinazoendelea kunyesha jijini humo. 

TFDA wakamata bidhaa za magendo jijini Mbeya leo

$
0
0
Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi jijini Mbeya, mapema mchana wa leo wamekamata bidhaa zilizoingizwa nchini kimagendo kupitia mpaka wa Tunduma. Bidhaa hizo ni vinywaji aina ya Dragon vilivyokuwa vikisafirishwa na gari aina ya Toyota Hiace. Pichani ni Kamanda wa Polisi Mkoani wa Mbeya, SACP Ahmed Msangi (akiwasiliana kwa njia ya simu) akiwa pamoja na Afisa wa TFDA Kanda ya Nyanda za juu kusini, Peter Namaumbo.


Watanzania wahitimu shahada ya uzamili kutoka taasisi ya kimataifa international institute of social studies ya chuo kikuu cha Erasmus cha nchini uholanzi.

$
0
0
Watanzania wahitimu shahada ya uzamili kutoka  taasisi ya kimataifa International Institute of Social Studies ya chuo kikuu cha Erasmus cha nchini uholanzi.Kutoka kushoto ni Mama  Agnes mtumishi wa ubalozi wa Tanzania nchini uholanzi,   Shamy Chamicha mhitimu shahada ya uzamili ya uchumi, Balozi wa tz nchini uholanzi mh.Irene kasyanjo, Ruth John  mhitimu shahada ya uzamili ya uhakiki wa chakula na mazingira, Jackson Bulili mhitimu shahada ya uzamili Uchumi na Rector wa taasisi hiyo mhe. Inge Hutter. Mahafali yalifanyika tarehe  11 December, 2015 nchini Uholanzi. Wasomi hawa wanamuomba MheRais Dkt. Magufuli awatumie pia ili wachangie maendeleo ya nchi yao kwa kasi kubwa.

DIRA YA DUNIA JUMATANO 16.12.2015

BREAKING NYUZZZZ....RAIS Dkt. John Pombe Joseph MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU Dkt. Hosea


NHIF YARIDHISHWA NA MATUMIZI YA MKOPO WALIOIPATIA HOSPITALI YA MKOANI WA SINGIDA

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Michael Mhando ameelezea kuridhishwa na matumizi ya mkopo uliotolewa na Mfuko huo kwa Hospitali ya mkao wa Singida.

Hospitali hiyo ilichukua mkopo wa Shilingi Milioni Mia Tano kutoka NHIF kwa ajili ya Ununuzi wa vifaa Tiba vya hospitali hiyo.

Akizungumza baada ya kukagua vifaa hivyo, Mhando amesema ameridhiswa na matumizi ya mkopo huo kwani umefanya kazi iliyokusudiwa.

Amesema NHIF itaendelea kushirikiana na uongozi wa mkoa huo ili kuboresha huduma za matibabu kwa wanachama wa NHIF na wananchi kwa ujumla.

Aidha amewahimiza watoa huduma wengine kuendelea kuchukua mikopo ili kuboresha huduma katika vituo vyao vya matibabu.

Hivi sasa Mfuko huo umeanza pia kutoa mikopo ya dawa ili kukabiiliana na uhaba wa dawa ktk vituo vya matibabu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF ), Michael Mhando akikagua baadhi ya vifaa Tiba vilivyopo kwenye Hospitali ya mkao wa Singida, ambavyo ni Ultra sound, incubator, mashine ya dawa za usingizi, vitanda vya kujifungulia na kadhalika vilivyotolewa kwa mkopo na Mfuko huo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF )Bwana Michael Mhando akitoa maelekezo kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Mkao wa Singida Dokta Ernest Mugeta (hayupo pichani) juu ya utumiaji wa vifaa hivyo, katika Mkoa wa Singida.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMTEMBELEA JAJI WARIOBA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati alipokwenda nyumbani kwa mstaafu huyo Oysterbay jijini Dar es salaam kumtembelea, Desemba 16, 2015. 

Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati alipokwenda nyumbani kwa mstaafu huyo Oysterbay jijini Dar es salaam kumtembelea Desemba 16, 2015.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAPITIO YA MAGAZETI LEO

TANZANIA NAMED FINALIST IN BEST TOURIST BOARD AFRICA CATEGORY FOR ANNUAL TRAVVY AWARDS.

$
0
0



By:  Geofrey Tengeneza.

Tourism sector in Tanzania is continuing to perform well at international arena after the country’s responsible organ for marketing Tanzania as a tourist destination Tanzania Tourist Board (TTB), being named one of three finalists in Destination:- Best Tourist Board Africa category for the 2015 Travvy Awards that recognizes the highest standards of excellence in the Industry today and honors travel companies, travel products, travel agencies, travel executives, travel agents and travel destinations. Other two finalist countries under the category are South Africa Tourism and Namibia Tourism Board.

Selection of the finalists is based on votes by travel agents. The final two winners in the respective categories are determined by the award-winning Travel Alliance editorial team.The Annual Travvy Awards will be presented by TravAlliancemedia at a Gala Awards night, New York City, January 6, 2016.

 “Tanzania is honored to be among the finalists for Africa. This is the result of the dedicated and pro-active work in the US market by Tanzania Tourist Board (TTB), together with The Bradford Group, TTB’s USA representative, and the strong support of Tanzania National Parks and Ngorongoro Conservation Area Authority as well as the Tanzania Embassy in Washington and the Tanzania Mission to the UN in New York.“ commented, the Permanent Secretary of the Ministry of Natural Resources and Tourism Dr. Adelhelm Meru 

He further said that In addition to Tanzania having some of the world’s most renown tourism icons, the Serengeti and the Great Animal Migration, Mt. Kilimanjaro, the Ngorongoro Crater as well as the hidden gems of the South, the Selous Game Reserve and Ruaha National Park, visitors from all over the world are also attracted to Tanzania because of its peace and tranquility, stability and prevailing democracy in the country that makes Tanzania a suitable place to stay for visitors.

This new development comes after recent developments where Tanzania mainland and Zanzibar were named by the US Travel and Leisure Magazine among the annual Best Places to Travel in 2016. Tanzania was also named among 52 places to go this year by the ‘New York Times’, the best African Destination to visit by the Fox News Channel, the best safari Country of Africa by SafariBookings.com and Tanzania’s Mt Kilimanjaro and Serengeti National Park being named two of the greatest parks in the World by National Geographic Magazine to mention just a few. Destination Tanzania has also received continuous positive coverage in the major travel publications and broadcast media.





SHIRIKA LA NDEGE LA ETIHAD LAUNGANA NA COGNIZANT KUBORESHA HUDUMA KWA WAGENI WAKE DUNIANI.

$
0
0
SHIRIKA la ndege la Etihad, ndege rasmi ya taifa za Falme za kiarabu na Cognizant (NSADAQ: CTSH), shirika linaloongoza kwa huduma za teknolojia ya habari, ushauri na biashara, leo wametangaza makubaliano ya kimkakati yatakayoendesha mabadiliko ya kidijitali pande zote za shirika hilo pamoja na washirika wake.

Chini ya mpango wao wa miaka mitatu wenye thamani ya mamilioni ya madola, Cognizant watawasaidia Etihad kufafanua mkakati wao wakidigitali na kutengeza dhana mpya ambayo itatumika katika kutoa huduma bora kwa wageni wao watakaosafiri popote na ndege za Etihad.

Kwa kuleta pamoja mikakati ya kidijitali, teknolojia, sekta na uzoefu wa ubunifu, Cognizant watafanya utafiti wa hali ya sasa ya biashara na teknolojia ya shirika la ndege la Etihad na kutumia utafiti huo kutengeneza mazingira ya kidijitali ya kiwango cha hali ya juu, itakachowezesha usambazaji kupitia idhaa nyingi, ugawaji wa wateja kwa kina zaidi na kubinafsisha ujuzi katika masoko.

Kwa kutumia taarifa mbalimbali na ufahamu wa mteja, Cognizant italiwezesha shirika la ndege la Etihad na washirika wake, kuelewa zaidi mahitaji ya wageni wake.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Viewing all 110105 articles
Browse latest View live




Latest Images