Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110000 articles
Browse latest View live

Wagonjwa 316 wapata huduma za madaktari bingwa mkoani Kigoma

$
0
0
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya wakina Mama,Dk. Mrema (wa pili kutoka kulia) akimsikiliza kwa makini mmoja wa wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo kwa lengo la kupatiwa ushauri na tiba sahihi,wakati Madaktari hao Bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili walipofanya ziara mkoani humo.
Wauguzi katika Hospitali ya Maweni wakitoa namba kwa wagonjwa waliojitokeza kuonana na madaktari bingwa wa Hospitali ya Muhimbili.
Dk. Vence (Katikati) akiwa katika chumba cha upasuaji akitoa huduma kwa mmoja wa watoto ambaye alifanyiwa upasuaji mapema leo (Jumanne).
Wagonjwa wakisubiri kuonana na Daktari Bingwa wa magonjwa ya Kawaida.

BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI

UWF yatoa zawadi kwa mshindi wa nne na watano wa shindano la mwanamakuka 2013

$
0
0
Mshindi wa nne wa shindano la Mwanamakuka 2013 bi Maajabu Rajab akipokea hundi  yake kutoka kwa  Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB),Bi Magreth Chacha kwenye hafla fupi iliofanyika kwenye kiota cha maraha,Escape 2 kilichopo Mbezi Beach,jijini dar.Kulia ni Mwenyekiti wa UWF Bi Ester Wakati  na kushoto ni Meneja Mradi wa Mwanamakuka,Bi.Mariam Shamo.
 Wa pili kutoka kulia ni Mshindi wa tano wa shindano la Mwanamkuka 2013 Bi Agnes Daud akipokea hundi yake
Mtangazaji wa Kipindi cha Leo tena,Kutoka Clouds FM, Dina Marios akipokea cheti cha shukrani kwa kazi yake nzuri ya kumtafuta Mwanamakuka 2013,kutoka kwa Meneja  Mradi wa Mwanamakuka ,Bi.Mariam Shamo.
Wa pili kutoka shoto ni Mshindi wa kwanza wa shindano la mwanamakuka bi Hadija Mbogulume akiwa na picha zake anazochora na kununuliwa hapo hapo zote na akiwa sambamba na baadhi ya Wanachama wa UWF.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Kinana awapongeza vijana wa ifakara kwa uchapaji kazi,awaasa kutobweteka.

$
0
0
Mmoja wa wanachama wa chama cha CHADEMA akikabidhi kadi yake kwa Ndugu Kinana na baadae kukabidhiwa kadi ya chama cha CCM,akiwa ni mwanachama mpya aliyejiunga na chama hicho.
Baadhi ya Wanchi wa eneo la Ifakara Mjini wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurahman Kinana alipozungumza nao eneo la Stendi kuu ya mabasi ya Ifakara mjini,Ndugu Kinana alizungumza mambo mengi ikiwemo  namna ya kufanya utatuzi wa mambo ambayo yamekuwa kero kwao,ikiwemo suala la Umeme,Kilimo na miundo mbinu,sambamba pia kuisaidia miradi mbalimbali inayofanywa na vijana wa mji wa Ifakara ambao unakuwa kwa kasi siku hadi siku.
Ndugu Kinana akikazia jambo wakati alipokuwa akizungumza na baadhi ya Wanchi wa eneo la Ifakara Mjini,eneo la Stendi kuu ya mabasi ya Ifakara mjini,wilayani Kilombero mkoani Morogoro.Ndugu Kinana aliwasifu na kuwapongeza vijana wa mji wa Ifakara kwa kuonyesha uwezo wao mkubwa kujituma kwa kufanya kazi kwa bidii na kujitegemea.Ndugu Kinana yumo mkoani Morogoro kwa ziara ya siku kumi ya kuimarisha chama cha CCM sambamba na kukagua miradii mbalimbali kwa ajili ya maendelo ya wananchi,
Mkuu wa wilaya ya Kilombero,Bwa.Hassan Masalla  akifafanua jambo kuhusiana na tatizo la kukatika katika kwa umeme mbele ya wakazi wa mji wa Ifakara mjini mapema jana,aidha Masalla aliwatoa hofu wananchi wa eneo hilo la Ifakara mjini kuwa tatizo hilo ambalo limekuwa kero kubwa kwa wananchi wa eneo hilo linashughulikiwa kwa nguvu zote na kuhakikisha linatengamaa na kwisha kabisa,kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurahman Kinana akimsikiliza kwa makini.
Ndugu Kinana akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na baadhi ya wanachama wa Ifakara mjini kwenye mkutano wao ndani mapema jana.
Baadhi ya wanachama wakimsikiliza Ndugu Kinana alipozungumza nao kwenye mkutano wao ndani,Ifakara Mjini wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro,ambapo alizungumza mambo mbalimbali ikiwemo na suala zima la kukiimarisha chama hicho.
Ndugu kinana akizindua moja shina la Wakaretwa wa chama cha CCM kati ya mashina manne aliyoyazindua Ifakara mjini.

Baadhi ya wakazi wa Ifakara Mjini eneo la Sokoni,wakimsikiliza Ndugu Kinana alipozungumza nao kwenye eneo la mradi wa chama hicho.

Mipango ya Kutumia Mfumo Wa Kieletroniki Kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 Nchini inatekelezwa

$
0
0



Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Tanzania Bw Damian Lubuva
--
Tume ya uchaguzi ya Tanzania imesema ina mipango ya kutumia mfumo wa kieletroniki kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 inatekelezwa.

Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari nchini Zimbabwe, mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Tanzania Bw Damian Lubuva amesema serikali imetoa uamuzi huo ili kufanya mchakato wa upigaji kura uwe salama na kuongeza imani kuhusu usahihi wa matokeo ya uchaguzi. 

Bw Lubuva amesema kwa sasa serikali ya Tanzania inajiandaa kutoa zabuni ili kupata mfumo huo, lakini gharama zake bado hazijajulikana, lakini wataomba wahisani kugharamia mfumo huo. Bw Lubuva pia amekanusha habari kuwa kuna usiri kwenye mchakato wa kupata mfumo huo. 

Tume ya uchaguzi ya Kenya ilitumia mfumo huo kwenye uchaguzi mkuu uliopita lakini mfumo huo uliachwa kutokana na matatizo ya kiufundi
.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA TFF LEO

$
0
0

AS FAR RABAT YA MOROCCO SASA KUTUA DAR ES SALAAM SAA 7 LEO
TIMU ya AS FAR Rabat ya Morocco itakayoikabili Azam kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho inatua nchini leo (Aprili 17 mwaka huu) saa 7.30 mchana kwa ndege ya Qatar Airways. 
Msafara wa timu hiyo wenye watu 28 kwa ajili ya mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itakayochezwa Jumamosi (Aprili 20 mwaka huu) saa 10 kamili jioni Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utafikia hoteli ya Sapphire iliyoko maeneo ya Kariakoo. 
Wakati Azam imetinga hatua hiyo baada ya kuitoa timu ya Barrack Young Controllers II ya Liberia kwa jumla ya mabao 2-1, AS FAR Rabat imeingia raundi hiyo moja kwa moja kutokana na nchi hiyo kufanya vizuri kwenye michuano ya klabu Afrika. 
Timu nyingine ambazo zimeingia raundi hiyo moja kwa moja katika Kombe la Shirikisho kama ilivyo AS FAR Rabat ni Asec Mimosas ya Ivory Coast, Atletico Petroleos (Angola), C.S.S. (Tunisia), DC Motema Pembe (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), El Ahly Shandy (Sudan), Enppi (Misri), Heartland (Nigeria), Ismaily (Misri), Lobi Stars (Nigeria), U.S.M. Alger ya Algeria na Wydad Casablanca (Morocco). 
Mwamuzi Emile Fred atakayesaidiwa na Steve Maire, Jean Ernesta na Jean Claude Labrossa wote kutoka Shelisheli ndiye atakayechezesha mechi hiyo. Kamishna ni Abbas Sendyowa kutoka Uganda. Waamuzi watawasili nchini kesho (Aprili 18 mwaka huu) jioni.

MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI
Ujumbe wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambao uko nchini kwa ajili ya kushughulikia mchakato wa uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) utakutana na waandishi wa habari leo (Aprili 17 mwaka huu) saa 10 jioni hoteli ya Serena. 
Mkuu wa Idara ya Uanachama ya FIFA, Primo Covarro ndiye aliyeongoza ujumbe huo ambao una siku tatu tangu ulipowasili nchini kushughulikia suala hilo. 
Ujumbe huo jana (Aprili 16 mwaka huu) ulikutana na Sekretarieti ya TFF, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, wagombea ambao walikata rufani FIFA na ambao waliomba marejeo (review) ya rufani zao kwa Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF. 
Leo asubuhi ujumbe huo wa FIFA ulitarajiwa kukutana na Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF inayoongozwa na Idd Mtiginjola.

Article 22

kumbukumbu

$
0
0

MRS ELIZABETH CHISENGA TSERE

Mama yetu mpendwa, Leo tarehe 17 April imetimia miaka 8 tangu uitwe mbele za haki.
Unakumbukwa sana na wanao Patrick,Francis na Assumpta pia wakwe zako Tumaini,Agnes na Chris Chika pamoja na wajukuu zako wote kumi.
Mpendwa mama R.I.P"

introducing Ree K-Farida's 'mpenzi' official video


KUTOA TAARIFA ZA SIRI KATIKA MAWASILIANO YA ELEKTRONIKI NI KOSA LA JINAI - serikali

$
0
0
Serikali imeona kuzuka kwa tabia ya uvunjaji wa kanuni ya utunzaji wa siri za taarifa za mawasiliano binafsi ya watumiaji wa huduma za simu za mkononi. Taarifa hizo zimefikia hatua ya kuchapishwa katika vyombo vya habari kwa kutaja bila idhini yao, namba za simu, wahusika wa namba hizo, maongezi na muda wa mawasiliano Kati yao. Jambo hili ni Kosa la Jinai. 

Serekali inapenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha wenye makampuni ya Simu, Vyombo vya Habari na wananchi kwa ujumla kuwa, kutoa taarifa za mawasiliano binafsi ya simu baina ya watumiaji wa huduma hiyo, ni uvunjaji wa Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta Na. 3 ya mwaka 2010 na Kanuni za Mawasiliano (Kulinda Wateja) za mwaka 2005.

Kifungu cha 98 ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kinasema;

“Mtu yeyote ambaye ni mfanyakazi wa kampuni yenye leseni ya kutoa huduma za mawasiliano, au mwakilishi wake, ana wajibu wa kutunza siri za mawasiliano binafsi na taarifa zozote za siri za wateja kwa mujibu wa sheria hii”. Aidha, “Mtu yeyote haruhusiwi kutoa taarifa binafsi za mteja yeyote alizopokea au kusikia kwa mujibu wa sheria hii isipokuwa tu mtu huyo ameruhusiwa kwa mujibu wa sheria”

Kanuni ya 12 ya Kanuni za Mawasiliano za mwaka 2005 za Tanzania (Kulinda Wateja) inasema:-

“Mtoa huduma za Mawasiliano haruhusiwa kuingilia kati, kusikiliza au kutoa taarifa zozote za mazungumzo ya mteja yeyote yaliyopitia kwenye mtandao wa mtoa huduma, isipokuwa kwa ruhusa kulingana na mahitaji maalumu kwa mujibu wa sheria zilizopo”

Hivyo basi wananchi wanapewa tahadhari kuhusu kutafuta au kutaka kupata taarifa za mawasiliano ya siri kutoka kwa watoa huduma na kuzitumia taarifa hizo binafsi za mawasiliano pasipo kufuata utaratibu ulioruhusiwa kisheria.

Aidha Serikali inapenda kuwatoa wananchi hofu kuwa Mawasiliano yao (maudhui) hayapaswi kuingiliwa kwa kusikilizwa mazungumzo yao au kusomwa meseji zao katika mitandao ya simu. Serikali Kwa kutumia vyombo vyake vya usalama inawahakikishia wananchi kuwa haki zao za faragha katika mawasiliano zinalindwa Kwa Mujibu Wa Sheria Na. 3 ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya mwaka 2010 pamoja Na Kanuni zake.

Kwa taarifa ambazo zimechapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari hivi karibuni, Mamlaka ya Mawasiliano pamoja na taasisi nyingine husika kwa mujibu wa Sheria ya EPOCA pamoja na Kanuni zake, wanaelekezwa kufanya uchunguzi wa uvunjwaji huo wa sheria na Mamlaka husika zichukue hatua za kisheria kwa yeyote atakayebainika kuvunja sheria hiyo. 

Serikali inayakumbusha Makampuni ya simu, Vyombo vya Habari na wananchi kwa ujumla kuhakikisha siri za mazungumzo binafsi ya wateja zinahifadhiwa na hazitolewi kwa yeyote isipokuwa kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na Idara ya Habari Maelezo

kumbukumbu

$
0
0
Marehemu Anthony Njeje.

Ni miaka mitano sasa imepita tangu ulipokwenda kwenye makao ya kudumu Baba yetu Mpendwa tarehe 17.04.2008.  
Baba, hatupo nawe kimwili lakinii kiroho upo nasi daima. Tunakukumbuka sana Baba yetu Mpendwa. Unakumbukwa sana na Mke wako Mpendwa Mama Elizabeth Anthony Njeje, Wanao Aninziye, Luseshelo-Ernest, Fredy na Sarah. Wajukuu zako Anthony Jr, Shikunzi-Alvin, Amarisa na Yasinta, Pia unakumbukwa na wafanyakazi wenzako wote, majirani zako, waumini wenzako, ndugu Jamaa na Marafiki. Sisi Tulikupenda sana lakinin Mungu alikupenda Zaidi. 

Jina la Bwana Lihimidiwe.
Amen

KCMC'S Shine A Light group launch official website

$
0
0
This is a group founded by KCMC (Kilimanjaro Christian Medical University College)students in 3 years ago aimed at helping children who are less fortunate (orphans ,street children etc ) achieve their dreams, have a chance at life and a bright future . If you feel you can participate or support us in any way or means (currently based in Moshi, Tanzania), Contact us: email-sal.kcmc@gmail.com Last thursday 11/4/13 shine a light launched its official website !!!
Shine a Light members and the provost of KCMUCo (kilimanjaro christian medical university college ) Prof .Egbert Kessy pose for a group photo after the official launching of the website
The provost of KCMUCo (kilimanjaro christian medical university college ) Prof .Egbert Kessy registering himself to be the first member to officially register online  through the website .
One of shine a light's member with the official Tshirt at the launch of the website .

-The provost of KCMUCo (kilimanjaro christian medical university college ) Prof .Egbert Kessy having a word with bahati daniel from the msamaria center for street children.Bahati  was given the honour of  officially launching the website at the event  .We found it fitting for her to launch the website as for the last three years a member of shine a light has sponsored her education through our educations sponsoring program.

We hope the launching of the website will not only garner support for shine a light and help children in our communities but it will serve as an inspiration for everyone to help children in need in their communities.

WEBSITE LINK - www.shine-a-light.org  

Miss Dar Indian Ocean 2013 kufanyika April 30

$
0
0
 Warembo wa Kitongoji cha Dar Indian Ocean (Redd's Miss Dar Indian Ocean) wakiwa kwenye picha ya Pamoja wakati wakiwa kwenye maandalizi ya kuingia kwenye kinyang'anyiro chai kitakachofanyika April 30,kwenye Ukumbu wa Makumbusho jijini Dar.Katikati ni Mrembo anaeshikilia taji hilo kwa sasa ambaye ndie Mwalimu wa Warembo hao,Diana Hussein.

Mikutano ya kipupwe yaanza rasmi mjini Washington DC

$
0
0
Mikutano ya kipupwe imeanza rasmi mjini Washington DC kuanzia tarehe 15/4/2013 na kuhudhuriwa na nchi wanachama zaidi ya 188. Kila kunapokuwa na mikutano ya kipupwe maelfu ya wafanyakazi wa Serikali, waandishi wa habari, mashirika yasiyo ya kiserikali, washiriki waalikwa kutoka sekta za elimu na binafsi, wanakutana mjini Washington DC kwa mikutano hii ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shrika la Fedha la kimataifa pamoja na kamati za kifedha, ambazo zinajadili maendeleo ya kazi za Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Bw. Benno Ndulu akitoa maelekezo kwa wajumbe kutoka Tanzania waliohudhuria mkutano wa Kipupwe. Gavana alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho kwa niaba ya Waziri wa Fedha.
Kikao hicho Kikiendelea.
Wajumbe wakisikiliza kwa makini hoja zilizotolewa na Gavana wa Benki Kuu hayumo pichani, Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Utafiti na Sera za Uchumi wa BOT Dr. Joseph Masawe, Kamishna wa Fedha za Nje Wizara ya Fedha Zanzibar Bi. Bihindi Nassor pamoja na Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango Dr. Philip Mpango.
Kutoka kushoto Mkuu wa Kitengo cha Sheria Bi Susan Mkapa pamoja na Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Said Magonya wa Wizara ya Fedha wakisikiliza kwa makini katika kikao hicho pembeni ni Mchumi mwandamizi wa Wizara ya Fedha Bw. Patric Pima.
Kutoka kushoto Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma, Msaidizi wa Gavana Bw. Msafiri Nampesya pamoja na Afisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Bw. Suleiman Saleh wakisikiliza jambo kwa makini kutoka kwa Afisa Mwambata anayeratibu masuala ya Uchumi, Biashara, na Uwezeshaji ya Benki ya Dunia na IMF Bw. Paul Mwafongo.Picha zote na Bi. Ingiahedi Mduma na Bi. Eva Valerian – Washington DC

Golden bush yakipiga na Moro Star Veterans huko mji kasoro bahari

$
0
0
Kikosi kizima cha Golden bush kilikuwa Morogoro mwishoni mwa wiki kupambana na wazee wenzao Moro Star Veterans wakiongozwa na Nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania Mecky Maxime na wachezaji wengine waliowika kwenye ligi yetu ya Tanzania wakiwemo Ali Moshi, Delta na wengine wengi.

Katika mpambano huo, golden bush veterans waliibuka na ushindi wa goli 3-1. Magoli matatu ya Golden bush yalitiwa wavuni na Athumani Machuppa magoli mawili na Abuu Mtiro goli moja wakati goli la Moro Star veterans likiwekwa wavuni na mshambuliaji wao hatari Ushua.

Wapenzi wa soka wa morogoro na vitongoji vyake walihamisika sana na mechi hii na hasa walivutiwa na kiwango cha wachezaji ambao wengi wao wameacha mpira hivi karibuni.

Golden Bush veterans wametumia game hiyo ya morogoro kama sehemu ya maandalizi yao kabambe ya kupambana na wapinzani wao wa jadi Wahenga Veterans game itakayopigwa siku ya Muungano yaani tarehe 26/04/2013 katika uwanja wa TP Africa Sinza.

Pichi hii ndiyo kikoso kamili cha Golden Bush veterans kilichokuwa mjini morogoro siku ya jumamosi.

Waliosimama kutoka kushoto nyuma kabisa: Shomari Pengo, Macocha Tembele, Ali Chuo, Humphrey Machota, Wisdom Ndlovu, Godfrey Bony, Steve Mkumba, Katina Shijja na Faraji Rashid.

Walioinama mstari wa pili kutoka kushoto: Amani Simba, Sadik Muhimbo, Onesmo Waziri, Noel Katepa, Said Sued, Joseph kisenge, Yahaya Issa, Athumani Machuppa na Steven Marash. Na aliyechuchumaa mbele kabisa ni Abuu Mtiro.

Imetolewa na

Onesmo Waziri
Msemaji wa timu na mchezaji mwandamizi.

Mstahiki Meya Jerry Silaa azindua kambi ya Starkey itakayotoa huduma Bure na vifaa kwa wananchi wenye matatizo ya kusikia

$
0
0
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akilakiwa na uongozi wa Starkey alipowasili katika shule ya Buguruni Viziwi kuzindua kambi ya Starkey itakayokuwa inatoa huduma ya uchunguzi, vifaa na matibabu bure kwa wananchi wenye matatizo ya kusikia.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akipewa maelezo na mmoja wa wauguzi katika kambi hiyo mara baada ya kuwasili.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akifanyiwa uchunguzi wa tatizo la kutosikia wakati kuzindua kambi ya Starkey itakayosaidia kutoa huduma na matibabu bure kwa wananchi wenye matatizo ya kusikia iliyopo kwenye shule ya watoto wenye ulemavu wa kusikia (Buguruni viziwi) jijini Dar.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Mh.Jerry Silaa jana tarehe 16 April 2013 amezindua kambi ya Starkey ya kusaidiawananchi wenye matatizo ya kusikia iliyofanyika katika shule ya watoto wenye ulemavu wa kusikia (Buguruni viziwi), ambapo wenye magonjwa watatibiwa na wenye kuhitaji vifaa vya kuongezea usikivu watatengenezewa kulingana na size zao na watapewa bureee.
Mstahiki Meya amepima na kwa kuwa ameonekana kutokuwa na tatizo amepata fursa ya kutengenezewa "custom made earphones" wote wenye matatizo mnakaribishwa. Huduma hii ni bureee...
Mstahiki Meya Jerry Silaa akivishwa "Custom made earphones" na mmoja wa madaktari bingwa katika kambi hiyo mara baada ya kuzindua huduma hiyo atakayokuwa ikitolewa bure kwa wananchi wenye matatizo ya kusikia.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akimsalimia mmoja wa watoto waliofika kambini hapo kupatiwa huduma baada ya kuizindua.

Wajela jela Original

Article 11

BREAKING NYUZZZZ...........: BI KIDUDE AFARIKI DUNIA

$
0
0
TAARIFA YA UHAKIKA KABISA ILIYOIFIKIA GLOBU YA JAMII HIVI PUNDE,INAELEZA KUWA MKONGWE WA MUZIKI WA MWAMBAO HAPA NCHINI,KIDUDE BINT BARAKA MAARUU KAMA BI. KIDUDE,AMEFARIKI DUNIA MUDA MFUPI ULIOPITA.

BI. KIDUDE AMEFIKWA NA MATUTI HAYO LEO KUTOKANA NA MARADHI YALIYOKUWA YAKIMSUMBUA KWA MUDA MREFU.

HABARI KAMILI YA MSIBA HUO ITAWAJIA BAADAE KIDOGO.

Rais Mstaafu,Alhaj Ali Hassan Mwinyi akutana na Waandishi wa Habari Jijini Dar leo na kuzungumzia swala lenye utata wa Kuchinja hapa nchini

$
0
0
 Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Alhaj Ali Hassan Mwinyi akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) aliowaita leo nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam,wakati alipozungumzia swala uhalali wa kuchinja ambalo limekuwa ni gumzo sana hapa nchini kwa kipindi cha hivi karibuni.Mzee Mwinyi ametoa rai kuwa Swala hilo ambalo limekuwa na utata mkubwa na kupelekea kuzua vurugu kwa baadhi ya maeneo hapa nchini,kuwa liachiwe watu wenye dharula kama linavyoelekeza kwenye Moja ya Vitabu vya dini.
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wamsikiliza kwa Makini Rais Mstaafu,Alhaj Ali Hassan Mwinyi.
 Rais Mstaafu,Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiwa kwenye picha ya pamoja na Baadhi ya waandishi wa Habari waliofika nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam leo.

TAARIFA KAMILI ITAWAJIA BAADAE KIDOGO.

Article 8

Viewing all 110000 articles
Browse latest View live




Latest Images