Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109980 articles
Browse latest View live

RC Makalla afurahishwa na matokeo mazuri ya darasa la saba wilayani Hai

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro, Amos Makalla, akiwa ameshika glasi ya kinywaji kwa ajili ya kufurahia kwa pamoja kwenye hafla ya kuwapongeza walimu wa wilaya ya Hai mkoani humo baada ya kupata matokeo mazuri katika ufaulu wa darasa la saba mwaka huu. Hai imeshika nafasi ya kwanza kiwilaya mkoani humo na nafasi ya nne kitaifa.

Na Mwandishi Wetu, Hai

MKUU wa Mkoa Kilimanjaro, Amos Makalla, amehudhuria halfa ya kuwapongeza walimu wilayani Hai, mkoani humo, kwa kufanikisha ufaulu mzuri wa darasa la saba. Wilaya ya Hai imepata nafasi ya kwanza kiwilaya mkoani Kilimanjaro, huku ikishika ikishika nafasi ya nne kitaifa, jambo lililomkuna Mkuu huyo wa Mkoa Kilimanjaro.
Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Amos Makalla, mwenye suti nyeusi akiingia katika hafla hiyo, wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza katika halfa hiyo akiwa kama mgeni rasmi, RC Makalla, alisema kwamba Hai wanastahili pongezi na wanapaswa kuendelea kufanya bidii ili wazidi kufaulisha kiwilaya na kitaifa. Alisema kuna haja ya sekretarieti ya Mkoa huo na Halmashauri zote kujipanga na kushughulikia kero za walimu, madai ya mishahara, kupandishwa kwa madaraja pamoja na kujibu barua zao kwa wakati ili kuwapa moyo walimu wao hao.

“Mkoa wetu unawapa pongezi kubwa walimu wote wa wilaya ya Hai kwa kufanya kazi kubwa na nzuri ya kuhakikisha kwamba wanafunzi wenu wanafaulu vizuri. “Naomba muendelee kujituma katika ufundishaji wenu, huku nikiahidi ushirikiano mkubwa katika ofisi yangu na kwenu ninyi walimu ili kuleta ushirikiano mkubwa kati yetu,” alisema.

RC Makalla amekuwa akifanya ziara mbalimbali mkoani Kilimanjaro ili kuongeza ufanisi katika majukumu yao ya kila siku, huku wakiitumia vyema falsafa ya Hapa Kazi Tu, inayotumiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli.

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU 7 KWA WAFANYABIASHARA WANAOKWEPA KULIPA KODI

$
0
0
 Rais John Magufuli ametoa siku 7 kwa wafanyabiashara waliokwepa kulipa kodi kwa kutorosha makontena  kuhakikisha wanalipa haraka.

Statement by Ambassador Ramadhan Mwinyi on Culture of Peace

$
0
0
The General Assembly met on  Thursday  to consider a report of the  Secretary - General on  the Culture of Peace. The  following  is  the   statement  delivered by  H.E Ambassador Ramadhan Mwinyi, Deputy Permanent Representative of Tanzania to the United Nations on   the  agenda item.

======  ======  ======

Mr. President,

My delegation welcomes the opportunity to participate in today’s debate on a very important subject of peace – fostering a culture of peace.
We see today’s meeting as an opportunity to reaffirm the purposes and principles of the Charter, which have been immaculately summed up in the resolutions set for adoption.

Like many delegations in this august Chamber, we are deeply concerned about the growing wave of extremism, violence and conflicts that are engulfing many societies, including Africa’s, whose people – have for the past 400 years – endured the horrors of slavery, colonialism, apartheid, resource plunder, chronic poverty and protracted conflicts.

MBUNGE WA JIMBO LA FUONI ZANZIBAR ATIMIZA AHADI ZAKE KWA KITUO CHA AFYA FUONI.

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe A bass Ali Hassan Mwinyi, akitembelea Kituo cha Afya cha Fuoni Zanzibar kinachotowa huduma kwa Wananchi wa Jimbo hilo na jirani wakati akitimiza ahadi yake kwa kutuo hicha, akipata maelezo kutokwa kwa mdhamini wa kituo hicho Muuguzi wa Afya ya Jamii Bi Mwaka Pandu Makame akitowa maelezo ya eneo lao la kuchomea taka za kituo hicho.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Adass Mwinyi akitembezwa katika kituo hicho na Madaktari wa Kituo hicho, akiwa katika ziara yake ya kukamilisha ahadi yake juu ya kituo hicha kikifanyia mategenezo sehemu.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi fedha shilingi milioni moja Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar Said Fadhil Abass, kwa ajili ya kutatua makero zinazokikabili kituo hicho cha Afya Fuoni ili kufanya kazi zao kwa kuwahudumia Wananchi kwa ufanisi zaidi.

AIRTEL FURSA YABADILISHA MAISHA YA KIJANA MFUGA KUKU.

$
0
0

Afisa Uhusiano wa Airtel, Dangio Kaniki (kushoto) na Meneja uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (katikati) wakipima uzito wa kuku wa kienyeji wanaofugwa kisasa na kijana Mohamed Kigumi (kulia), anayeishi Kiluvyia jijini Dar Es Salaam baada baada ya kutembelewa nyumbani kwao na kuona maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita iliyopita.
Afisa Uhusiano wa Airtel, Dangio Kaniki (kulia) na Meneja uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (katikati) wakitazama maandalizi ya utunzaji wa kuku wa kienyeji wanaofugwa kisasa na kijana Mohamed Kigumi (kulia), anayeishi Kiluvyia jijini Dar Es Salaam baada baada ya kutembelewa nyumbani kwao na kuona maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita iliyopita.
Kijana Mohamed Kigumi anayeishi Kiluvyia jijini Dar Es Salaam akiwaelekeza meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (katikati) na afisa Uhusiano wa Airtel, jinsi anavyoendesha ufugaji wake wa kuku baada ya kumtembelea nyumbani kwao na kuona maendeleo aliyoyapata baada ya kuwezeshwa na Airtel kupitia mpango wa Airtel ‘Fursa Tunakuwezesha’ miezi sita iliyopita.

VIJANA wengi wana ndoto za kujiletea maendeleo lakini wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na kukosa elimu sahihi na kutokuwa na mitaji ambayo ingewawezesha kujiunga kwenye miradi ya ujasiriamali.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mradi wake wa Airtel FURSA imeiona changamoto hiyo na kuamua kuwafikia vijana mbali mbali hapa nchini akiwemo kijana Mohamed Kigumi ambaye mpaka sasa ameonesha jitihada za kujikwamua na umaskini kwa kuwawezesha kupata mitaji ama vifaa vitakavyotimiza ndoto zao.

Akiongea katika kijiji cha kiluvya, Muhamed Kigumi ambaye anajishuhulisha na ufugaji wa kuku wa kienyeji, amesema licha ya kuanza kazi hiyo kwa muda mrefu lakini sasa ameanza kuona mafanikio makubwa katika kazi yake kutokana na kujengewa mabanda ya kisasa ya kufugia kuku wake na mfuko wa Airtel FURSA tofauti na hapo awali ambapo alikuwa akifugia kukuwake kwenye mazingira magumu.

Amesema mabanda ya kisasa aliyojengewa na mfuko wa Airtel FURSA pamoja na kupatiwa msaada wa kuku, maisha yake yamebadilika kwani sasa ameamua kujiajiri katika kazi hiyo na kumuwezesha kusaidia familia na kuuomba mfuko huo kendelea kuwasaidia vijana wengine hapa nchini.

Akiongea katika mabanda ya kuku ya kijana huyo alipomtembelea hapo jana, meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando amesema kuwa mpango wao wa Airtel FURSA umefurahishwa na jitihada za kijana huyo ambapo wamemtembelea bila kumpa taarifa lakini wamebaini kuwa msaada waliompatia kijana Mohamed umeweza kuyabadilisha maisha yake kutokana na kuwa makini na kazi yake.

Mmbando aliongeza kwa kusema, mpango wa kuwasaidia vijana wenye umri kati ya miaka 18-24 uitwao Airtel FURSA umeanzishwa na mtandao wa simu za mikononi wa Airtel ili kuwasaidia vijana wa Tanzania wenye ndoto zao ili kuweza kuzitimiza ndoto zao kwa kuwawezesha kwa kuwapatia elimu ya biashara na nyenzo za kufanyia kazi.

BEI YA MADAFU LEO

Naibu Katibu Mkuu wa TAMISEMI akagua hali ya mazingira ya soko la Temeke Sterio, jijini Dar

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba (aliyetangulia) akikagua machinjio ya kuku jana katika soko la Temeke Sterio Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo (wa pili kushoto) akimwongoza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu Bw. Zuberi Samataba(katikati) kukagua soko la Temeke Sterio lililopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.Zoezi hilo lilifanyika jana wilayani humo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la usafishaji wa mazingira.
Katapila la Halmashauri la Manispaa ya Temeke likizoa uchafu jana katika soko la Temeke Sterio ikiwa ni utekelezaji agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli la usafishaji wa mazingira.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Droo ya kwanza ya Jaza Mafuta na Ushinde kutoka Gapco yachezeshwa jijini Dar

$
0
0
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya GAPCO Tanzania, Vijay Nair (katikati) akibonyeza kitufe kwenye Kompyuta kuwatafuta washindi wa promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" inayowawezesha wateja wa mafuta katika vituo mbali mbali vya GAPCO jijini Dar es salaam kujipatia mafuta ya bure. Jumla ya Wateja 25 hupata bahati ya kuwekewa mafuta bure. Kushoto ni Mkaguzi wa Michezo ya kubahatisha nchini, Abdallah Hemedy na kulia ni Meneja Mradi wa GAPCO, Mohit Sharma.

MANISPAA YA ILALA WASHIRIKIANA NA FORUMCC KUANZISHA MFUKO WA MAZINGIRA NA MABADILIKO YA TABIANCHI.

$
0
0
MANISPAA  ya Ilala kwa kushirikiana na ForumCC wako katika hatua za mwisho za uanzishaji wa Mfuko wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi ukiwa na lengo la kukusanya pesa za kukabiliana na changamoto za mazingira na mabadiliko ya tabianchi katika eneo hilo

Mkuu wa Idara ya Usafi na Mazingira Manispaa ya Ilala, Abdon Mapunda anasema baada ya kukamilisha zoezi la ukusanyaji wa maoni ya wadau wa mazingira, mfuko huo utaanza mara moja kabla ya mwaka 2015 kumalizika

Wakati Manispaa ya Ilala ikiwa na jukumu la kusimamia uanzishwaji na uendeshaji wa mfuko huo, ForumCC wao wanajukumu la kutoa msaada wa kitaalamu ili kuhakikisha kuwa mfuko huo unafanikiwa na kufikia lengo lililokusudiwa.
Mtaalamu wa Misitu na Mazingira, Kahana Lukumbuzi ambaye alikuwa na jukumu la kutengezeza andiko la uanzishwaji wa mfuko huo, akitoa ufafanuzi wa baadhi ya vipengele vilivyomo kwenye andiko hilo.
Wadau wa mazingira wakifuatilia mkutano huo.
Sehemu ya mapendekezo ya namna Mfuko wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi utakavyokuwa.
Wadau wa mazingira wakifuatilia mkutano huo.
Wadau wa mazingira wakifuatilia mkutano huo.
Picha zote na Tabianchi.

Article 11

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MKUTANO WA TANO WA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA NA CHINA, JIJINI JOHANNESBURG LEO.

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Rais wa China, Xi Jinping, wakati wa Mkutano Mkuu wa Tano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China (China-Africa Forum) uliofanyika leo Dec 4, 2015 jijini Johannesburg. Mhe. Samia amemwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano huo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Shulu Hassan, akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini, Radhia Msuya, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Olver Tambo jijini Johannesburg jana Desemba 3, 2015 kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Tano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China.
Baadhi ya washiriki katika Mkutano huo kutoka nchi mbalimbali za Afrika waliohudhuria ufunguzi wa mkutano huo leo jijini Johannesburg. 
Picha na OMR.

WAFANYAKAZI 35 WASIMAMISHWA KAZI TRA,HUKU KAMPUNI 43 ZIKIBAINIKA KUKWEPA KODI.

$
0
0
Kaimu Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip Mpango akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
 Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano na 
Kaimu Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip                                               Mpango jijini Dar es Salam leo.

Na ChalilaKibuda,Globu ya Jamii

BAADA ya Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa kufanya ziara ya kushitukiza katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kubaini upotevu wa Makontena 329, mapya yaibuka kwa Makampuni 43 kuhusika kukwepa kodi ya Sh.Bilioni 12.6 katika Bandari Kavu inayomilikiwa na Said Salim Bakh ressa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk. Philip Mpango amesema kuwa kampuni hizo 43 zilipitishiwa Kontena katika Bandari Kavu ya Said Salim Bakhressa na kutaka ndani ya siku sita kuanzia leo kampuni zote ziwe zimeshalipia kodi kutokana na idadi ya kontena.

Dk. Mpango amesema katika kampuni ambazo zilizokwepa kodi ambazo zilipitisha Kontena 329 wameshalipa zaidi ya Sh. Bilioni Tano(5) ambapo wanatakiwa kulipa kodi iliyobaki kuweza kumaliza kodi ya Sh.Bilioni 12.6 kwa kipindi alichoweka Rais Dk .John Pombe Magufuli. 

Amesema kuwa hatilafu za kupotea kwa makontena hayo, kazi hiyo walishakuwa wameanza kwa bahati mbaya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa Majaliwa aliwawahi wakati alipofanya ziara katika mamlaka hiyo.

Kampuni zilizokwepa Kodi ya mapato kwa makontena 329 ni Lotai Steel Tanzania LTD yenye makontena 100,Tuff Tyres Centre Company kontena 58 Binslum Tyres Company LTD, Kontena 33, Tifo Global Mart (Tanzania) Company Limited Kontena 30,IPS Roofing Campany Ltd Kontena 20,Rashywheel Tyre Center Com.Ltd Kontena 12, Kiungani Trading Company Ltd 10 Homing International Limited Kontena 9, Red East Building Kontena Saba,Tybat Trading Co Ltd, Kontena Tano,Zing Ent Ltd,Kotena Nne,Juma Kassem Abdul, Kontena Tatu, Salum Continental Co.Kontena Mbili, Zuleha Abbas Ali Kotena Mbili na Snow Leopard Building Kontena mbili na waliobaki walikuwa na kontena moja moja.

Hata hivyo TRA imewasimamisha kazi watu 35 wakiwemo 27 waliokamatwa katika geti namba tano ambao hadi sasa wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano na uchunguzi .

Aidha amewataka wafanyakazi kuwasilisha mali zao ili kuweza kuangalia uwezo wake katika utumishi kama zinaendana na umiliki huo.

WATENDAJI WA SERIKALI WILAYANI KARATU WAMETAKIWA KUTEKELEZA AMRI YA RAIS

$
0
0
Watendaji wa Serikali wilayani Karatu wametakiwa kutekeleza amri ya Rais kwa kusimamia masuala ya usafi katika maeneo yao.

MZEE DONATI KEZIRAHABI

$
0
0
This will be 10th anniversary since you left us,
We have lived our lives with you through happiness and joy forgetting that one day you'll be gone from us and all will be gone with you. You were all that, a friend, our love, a husband, a father and grand father.
You were our leader indeed and many followed you. Today we are here thanking your most kind and generous, open and loving heart.You are the reason behind our strengths today.  You are being missed so much and you will always be placed in a cherished part of our hearts. We will forever loving you.
 
On 5/12/2015 this Saturday there's going to be a mass at St Imaculata, Upanga starting at 03:00pm. You arre all invited

May his soul rest in peace Amen.

Mama

Hidaya Kezirahabi

KANUNI MPYA ZA HUDUMA ZA ZIADA ZA MWAKA 2015 ZA SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA YA MWAKA 2010

$
0
0
 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Sayansi na TekinolojiaPriska Olomi (kushoto) , akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam leo, kuhusu kutungwa kwa kanuni za huduma za ziada kwa makampuni ya simu nchini zitakazo walinda watumiaji wa huduma hizo,kulia ni Mkuu wa kitengo cha Sheria wa Wizara hiyo,Veronika Sudayi. 
(Picha na Hassan Silayo).

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KANUNI MPYA ZA HUDUMA ZA ZIADA ZA MWAKA 2015 ZA SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA YA MWAKA 2010 

(THE ELECTRONIC AND POSTAL COMMUNICATION ACT 2010 (VALUE ADDED SERVICES) REGULATIONS 2015) 

Ndugu Waandishi wa Habari 
1. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutupatia uhai na afya njema na kutuwezesha kukutana leo kupeana taarifa kuhusu Kanuni Mpya za Huduma za Ziada za Mwaka 2015 ambazo zinatokana na Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya Mwaka 2010. Napenda pia kuchukua nafasi hii kuwashukuru kwa kukubali mwito kushiriki nasi katika siku hii ya leo. Karibuni sana. 

Ndugu waandishi wa Habari.
2. Sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) imeendelea kukua kwa kasi duniani na hapa nchini kwetu na imeleta mafanikio mengi katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kijamii kwenye ngazi ya kitaifa na kwa mwananchi mmoja mmoja katika maisha ya kila siku kwa waishio mijini na vijijini. Idadi ya watumiaji wa huduma za mawasiliano nchini imeendelea kuongezeka kutoka line za simu za viganjani milioni 2.96 mwaka 2005 hadi kufikia milioni 32.1 mwezi Desemba 2014. Watumiaji wa mfumo wa intaneti nao wameongezeka kutoka milioni 3.56 mwaka 2008 hadi kufikia milioni 11.34 mwaka 2014.

CONGRATULATIONS – EALA TELLS H.E. DR JOHN MAGUFULI AND TANZANIANS

$
0
0
EALA has moved a Resolution congratulating President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr John Pombe Joseph Magufuli following his election as the fifth President of the United Republic of Tanzania. EALA further commends the people of the United Republic of Tanzania on their commitment to peace and democracy during the General elections.

At the same time, EALA wants H.E. Dr John Pombe Joseph Magufuli to address the Assembly at the earliest opportunity.

“Aware of the credible elections held in Tanzania, we would like to seize this great opportunity to extend to His Excellency, President John Pombe Joseph Magufuli our warmest congratulations and to wish him every success at a time of great expectations in Tanzania, the East African Community and Africa in general in terms of national unity, prosperity of the people in maintaining the position as a strong champion for regional integration and democracy in Africa.

We would also like to extend our sincere congratulations to the CCM party for the renewed confidence and trust by the people of the United Republic of Tanzania to spearhead their aspirations for a great future.  We commend the opposition fraternity for a well fought battle, for behaving responsibly after the defeat, keeping in mind the peace and security which are the common interest are above any other individual interest”, a section of the Resolution says.

The Resolution moved by Hon Jeremie Ngendakumana, recognizes and takes pride in the success of the United Republic of Tanzania which it avers has made history in what could be the most competitive Presidential elections ever since multiparty politics commenced.

The Assembly further appreciates the brilliance and tone of campaigns demonstrated which exemplifies maturity and vitality of democracy in Tanzania.

Prof. Ole Gabriel mgeni rasmi maadhimisho ya siku ya kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aliyevaa suti akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya vijana wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kujitolea wakati wa maadhimisho ya siku ya kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni Prof. Elisante Ole Gabriel wa pili kutoka kulia akiongea na wanahabari katika maadhimisho ya siku ya kujitolea duniani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo,wa kwanza kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika lisilo la Kiserikali la Volountary Overseas (VSO) Dkt. Philip Goodwin.

Serikali yaweka kanuni za utoaji wa huduma za ziada

A Video You Will NEVER FORGET!!! - TB JOSHUA

NEWS ALERT: WATUMISHI NANE WA TRA WAPANDISHWA KIZIMBANI LEO

$
0
0
Mshitakiwa namba moja katika kesi ya kuhujumu uchumi, Tiagi Masamaki (katikati) na washitakiwa wenzake wakitoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo mchana baada ya kusomewa mashitaka yao.

MAOFISA wanane wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), akiwemo Kamishna wa Forodha wa mamlaka hiyo Tiagi Masamaki (56) wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutoa makontena 329 bandarini bila ya kulipiwa kodi na kuisababishia Serikali hasara ya sh. bilioni 12.7 za kitanzania.

Ukimuondoa Masamaki maofisa wengine waliopandishwa kortini ni Habibu Mponezya (45) Meneja wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja,Bulton Mponezya (51) 

Wakili wa Serikali Mwandamizi Christopher Msigwa akisaidiana na Peter Vitalis ameadi leo mchana mbele ya Hakimu Mkazi Huruma Shahidi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa watuhumiwa hao wanatuhumiwa kwa makosa mawili.

Alidai makosa mawili ya uhujumu uchumi ni kula njama ya kuidanganya Serikali na kuisababishia Serikali hasara. Kesi hiyo ni namba 35/2015 ya uhujumu uchumi. 

Ilidaiwa katika shtaka la kwanza katika tarehe tofauti kati ya Juni 1 na Novemba 17 mwaka huu, sehemu isiyojulikana ndani ya Jiji la Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama ya kuidanganya Serikali kuwa sh. bilioni 12.7 zimetolewa kwa kutoa makontena 329 katika Bandari Kavu ya Azam, baada ya kodi zote kutolewa.

Katika shtaka la pili, washtakiwa wanatuhumiwa katika ya Juni Mosi na Novemba 17 mwaka huu ndani ya Jiji la Dar es Salaam walishindwa kutimiza majukumu yao kwa namna inavyotakiwa na kusababisha Serikali kupata hasara ya sh. bilioni 12.7.

Baada ya washtakiwa hao kusomewa makosa yao, Hakimu Shahidi aliwaeleza kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, kwa hiyo hawatakiwi kujibu chochote kama kweli au si kweli.

Aliongeza kuwa Mahakama Kuu ndiyo inamamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, kwa hiyo kama wanataka dhamana wapeleke maombi ya dhamana katika mahakama hiyo.

"Kama mnataka dhamana pelekeni maombi Mahakama Kuu kwa sababu mahakama hii hawezi kutoa dhamana," alisema Hakimu Shahidi 

Hata hivyo, upande wa utetezi ulidai kuwa kesi hiyo ifikishwa mahakamani hapo bila kibali na pia waliomba mshtakiwa namba nne Mrema anamtoto mchanga kwa hiyo wanaiomba mahakama imfikirie.




Wakili Msigwa alidai upelelezi bado unaendelea, wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Kesi hiyo itatajwa Desemba 17 mwaka huu kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika
Watuhumiwa hao wakisindikizwa na maofisa wa polisi kuingia chumba cha Mahabusu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Hapa Masamaki na wenzake wakiingia ndani ya gari kuelekea gereza la Segerea.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Viewing all 109980 articles
Browse latest View live




Latest Images