Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live

KINANA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA VYAMA VYA SIASA KUSINI MWA AFRIKA MJINI MAPUTO,MSUMBIJI

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Komredi Abdulrahman Kinana katikati ya wiki iliyopita aliongoza ujumbe wa Tanzania nchini Msumbiji kuhudhuria mkutano wa Vyama vya Siasa Kusini Mwa Afrika. 
Mkutano huo uliohudhuriwa na baadhi ya Wenyeviti na Makatibu Wakuu wa vyama  hivyo, umemalizika mwishoni mwa wiki mjini Maputo kwa mafanikio makubwa.

Mkutano huo ulijadili masuala yaliyolenga kutatua changamoto mbalimbali za mataifa hayo na mipango ya maendeleo kwa ujumla.

Baadhi ya viongozi wa vyama hivyo vya siasa waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa ANC ya Afrika Kusini Rais Jacob Zuma, Mwenyekiti wa FRELIMO ya Msumbiji Rais Filipe Nyusi, Mwenyekiti wa SWAPO ya Namibia Rais Hage Geingob pamoja na Komredi Kinana na ujumbe wake.

Ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Komredi Kinana umewajumuisha Katibu wa NEC anayeshughulikia Siasa na Mambo ya Nje Dkt. Asha-Rose Migiro pamoja na Makatibu Wakuu wa Jumuiya za CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman  Kinana (kulia)akiwa kwenye picha ya pamoja na Zuma Mwenyekiti wa ANC ya Afrika Kusini Rais Jacob  (kushoto) na Mwenyekiti wa FRELIMO ya Msumbiji Rais Philipe Nyusi  (katikati).
 Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Chama cha SWAPO cha Namibia Rais Hage Gengob,  katika mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza kwenye mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa vya Kusini mwa Afrika mjini Maputo, Msumbiji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na Makatibu Wakuu wa vyama vya ANC, FRELIMO, MPLA, SWAPO na ZANU PF mjini Maputo.

MRADI WA VETA, VSO NA LNG TANZANIA WASHINDA TUZO YA BRITISH GAS

$
0
0
Tuzo iliyotolewa kwa Mradi wa EEVT baada ya kupata ushindi katika eneo la Mazingira na Huduma kwa Jamii.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa BG Bw. Helge Lund akizungumza na washiriki wa hafla hiyo ya kutunuku tuzo kwa washindi iliyofanyika Kensington Palace nchini Uingereza hivi karibuni.
 Mkurugenzi wa VETA kanda ya Kusini Mashariki Joseph Kibehele (watatu kutoka kushoto) akiwa ameshikilia tuzo hiyo katika picha ya pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa BG Bw. Helge Lund (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Meneja uwekezaji kwa jamii wa LNG Tanzania Bi. Kate Sullam, Mwakilishi kutoka LNG Tanzania Bi. Patricia Muhondo, Meneja Mradi wa Hali Bora ya Maisha (Livelihood) wa VSO Bi. Rose Tesha na mmoja wa majaji wa shindano hilo.
 Washiriki kutoka nchi mbalimbali walioshiriki katika hafla hiyo katika picha ya pamoja wakati wa chakula cha jioni.



MRADI wa Kuongeza Sifa za Kuajirika kupitia Mafunzo ya Ufundi Stadi (EEVT) unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), shirika la VSO na Kampuni ya Gas LNG nchini Tanzania umepata ushindi kwa mwaka 2015 katika eneo la Mazingira na Huduma kwa Jamii.

EEVT ilitangazwa mshindi miongoni mwa kundi la washiriki wanne bora walioingia fainali kwenye eneo la Mazingira na Huduma kwa Jamii wakati wa halfa ya kutunuku tuzo iliyofanyika Kensington Palace nchini Uingereza tarehe 12 Novemba, 2015 ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Afisa Mtendaji Mkuu wa BG Bw. Helge Lund.

Tuzo za BG hutolewa kila mwaka kwa kubaini, kushirikishana na kusherehekea mwenendo ulio bora miongoni mwa washirika wa BG.

Mchakato wa Tuzo za mwaka 2015 ulihusisha washiriki 147 kutoka nchi mbalimbali na wakiwa katika makundi matano ya Ushirikiano katika Kazi; Mazingira na Huduma kwa Jamii; Uthabiti na Ubora katika Utendaji Kazi; Utendaji kazi kwa Usalama na Uadilifu katika matumizi ya Rasilimali; na Ugunduzi. Washiriki wanne bora kutoka kila kundi walichaguliwa kuingia katika kinyang’anyiro cha mwisho.

KWA HUDUMA BORA FIKA RHG HAIR BEAUTY SALON, KINONDONI JIJINI DAR

VWG watoa msaada kwa yatima wa kituo cha chakuwama jijini dar

$
0
0
 
KIKUNDI cha wakinamama kijulikanacho kwa jina la Victory Women Group (VWG) chenye makao yake makuu jijini Dar es salaam, mwisho mwa wiki, kilijumuika pamoja na kuwapatia msaada wa mahitaji mbali mbali watoto Yatima wanaolelewa kwenye Kituo cha CHAKUWAMA, kilichopo Sinza Mori jijini Dar es salaam.

VWG iliamua kutembelea kituo hicho ikiwa ni sehemu ya maadhimisho yake ya kutimiza mwaka mmoja toka kuanzishwa kwake.

Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika kituoni hapo, Mwenyekiti wa VWG, Bi. Consolata Maimu, alisema kuwa waliamua kufanya hivyo kwa kuwa wao ni kina mama na wanahofu ya Mungu hivyo wakaona ni vyema kujumuika na watoto hao kuliko kwenye kusherehekea wenyewe.

VWG ni kikundi cha wanawake kilichoanzishwa mwezi mei 2014, kikiwa na lengo la kusaidiana wao wenyeke katika kujikwamua na umaskini na pia kusaidia jamii inayowazunguka, huku lengo lingine likiwa ni kuwasomesha watoto wanaolelewa kwenye vituo mbali mbali kwa kuanzaia elimu ya Sekondari mpaka Chuo kikuu.
Mwenyekiti wa Kikundi cha wakinamama kijulikanacho kwa jina la Victory Women Group (VWG), Bi. Consolata Maimu (katikati), akikabidhi kwa Mlezi wa Kituo cha Watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hassan Hamis, sehemu ya sare za shule kwa ajili ya watoto wanaolelewe kwenye kituo hicho, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na kikundi hicho. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kikundi cha VWG, Bi. Sauda Sinare.
Mlezi wa Kituo cha Watoto yatima cha CHAKUWAMA, Hassan Hamis, akizungumza machache mbele ya wageni wake, juu ya hali ya kituo hicho.
Mwenyekiti wa Kikundi cha wakinamama kijulikanacho kwa jina la Victory Women Group (VWG), Bi. Consolata Maimu akizungumza katika hafla hiyo.
Sehemu wa wanachama wa Kikundi cha wakinamama kijulikanacho kwa jina la Victory Women Group (VWG), wakijumuika pamoja na watoto Yatima wa kituo cha CHAKUWAMA kukata keki na kufungua shampein.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Ratiba ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue Hospitali ya Muhimbili

$
0
0
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atafanya ziara katika Hospitali ya Taifa Mhimbili Kesho Jumatatu (23 Novemba, 2015) kuanzia majira ya saa nne asubuhi.

Ziara hiyo ni kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyeagiza fedha zilizochangwa ajili ya hafla ya wabunge zitumike kununulia vitanda vya wagonjwa katika hospitali hiyo.


Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasilino, IKULU


20 Novemba, 2015

TANAPA RECEIVE ANTI-POACHING AIRCRAFT FROM GERMANY

$
0
0
Germany Foreign Minister Hon. Frank –Walter Steinmeier (right) handing over a symbolic key of a light Husky aircraft for anti-poaching operations to Director General of TANAPA Allan Kijazi. Others in the picture from left are Director of Wildlife Herman Keraryo and Acting Director General of Tanzania Wildlife Authority Martin Loibooki.
Germany Foreign Minister Hon. Frank –Walter Steinmeier (second right) posed in a group picture with some of the Germany Members of Parliament who accompanied him during the handing over event of two surveillance aircrafts from Germany to Tanzania yesterday
Germany Ambassador to Tanzania Hon. Egon Kochanke (right) and the Permanent Secretary Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation Ambassador Liberata Mulamula during the event.
Director General of TANAPA Allan Kijazi in a joyous mood when presenting some of the souvenirs of TANAPA to Germany Foreign Minister Hon. Frank –Walter Steinmeier.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
TANZANIA NATIONAL PARKS
PRESS RELEASE

 
TANAPA RECEIVE ANTI-POACHING AIRCRAFT FROM GERMANY


Germany Foreign Minister Frank-Walter Steinmeier yesterday handed over symbolic key of two Husky aircrafts to Tanzania National Parks and Tanzania Wildlife Authority respectively. The aircrafts will be used for anti-poaching operations in the protected areas.


Director General of TANAPA Allan Kijazi said that the aircrafts would take the joint approach by the Germany Government through Frankfurt Zoological Society, TANAPA and TAWA to tackle poaching in the protected areas.


The Husky A-1C is an ideal plane for monitoring and anti-poaching surveys as it operates at low heights and slow speeds-similar to that of a helicopter and has proven long-term success rate for its use in finding poacher camps and recording GPS positions for follow-up actions by teams on the grounds.


The Huskies will be used to monitor two of Tanzania’s elephant hotspots, Selous Game Reserve and Serengeti National Park.


Tanzania is home to some of the most elephant and rhino populations on the planet but of recent days it has experienced a severe threat from a massive upsurge in poaching.



Issued by Corporate Communications Department

Tanzania National Parks

23rd November, 2015

T: 027 250 1933


VOTE FOR KARISMA ALEX ON SWAHILI FASHION WEEK 2016

TAARIFA YA MSIBA JIJINI MWANZA

$
0
0
Mwalimu Kulthum R. Mussa (Mwambambale) wa Nyakato National Mwanza anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Mumewe Dr. Hassan Marekero Mdee kilichotokea katika Hospitali ya Bugando Mwanza tarehe 22.11.2015. Msiba upo nyumbani kwake Nyakato National Mahina karibu na kanisa la Roma. Heshima za mwisho zitatolewa siku ya Jumanne kuanzia saa 7 mchana nyumbani kwa Marehemu Mahina. Marehemu atasafirishwa siku ya Jumatano alifajiri kuelekea Moshi Uchira kwa mazishi ambayo yatafanyika siku ya Alhamisi. “Innalilahi Wainnailahi Rajiun”

STANDARD CHARTERED APPOINTS ITS FIRST TANZANIAN CHIEF EXECUTIVE OFFICER, LEVERAGING ON LOCAL TALENT

$
0
0
Tanzania, 23 November, 2015 – Sanjay Rughani becomes Standard Chartered Bank Tanzania’s first local Chief Executive Officer. Sanjay assumed the Bank’s top role earlier in the month succeeding the former CEO, Liz Lloyd, who has taken up the role of Group Company Secretary for the Bank, based in London.
  
Sanjay joined the Bank in Tanzania in 1999 as Manager, Finance and Business Support. Within two years he was promoted to the role of a Regional Finance Manager for Africa, based in London. He then returned to the country in 2002 to become the Bank’s Executive Director for Finance in Tanzania, a role he held until 2006.  

In 2007, Sanjay took up the role of Executive Director, Finance for Ghana in addition to being the area Chief Finance Officer for West Africa covering Ghana, Gambia, Cote d' Ivoire & Sierra Leone, a role he held until May, 2013.

In June, 2013  he became the Head of Finance Operations & Change Management for the Africa region, leading the Bank’s Africa Finance Operation and Finance Shared Services which has coverage of fifteen countries to achieve operational excellence with a strong focus on delivery and alignment to the Bank’s Global model. Sanjay held this role until his current appointment. 

Lamin Manjang, Chief Executive Officer for Kenya and East Africa, Standard Chartered commented, “I am delighted to welcome Sanjay back home to Tanzania and to our team in East Africa, following his successes in his various roles within the Group. Additionally, I am delighted that the country now has its first local CEO, a testimony of the country’s richness in talent and capabilities.  We continue to place our best people in top jobs in Africa as we strive to make the strongest possible social and economic contribution to the countries we operate in.”  

Tanzania remains core to the Bank’s regional and East African strategy, given the market has seen sustained, strong growth for over a decade.  The economy is a member of Standard Chartered’s ‘7% Club’ – a list of economies which have growth rates high enough to double the size of the economy in the next 10 years. 

On taking up the new role as the Chief Executive Officer for the Bank in Tanzania, Sanjay Rughani said, “Tanzania holds so many opportunities and I’m excited to be returning home to lead Standard Chartered Bank Tanzania to the next level of growth.  The country is playing an increasingly important role in our East African strategy, given the broad-based nature of its economic growth.  Additionally, Tanzania’s discovery of 15trillion cubic feet of gas reserves off its shores is also expected to drive developments in the near-term.”

Sanjay’s professional credentials and qualifications include being a Chartered Accountant, an ACCA member and a Fellow in Institute of Information Management Africa (Nigeria).  He holds an MBA in Finance and has a Management Post Graduate qualification in Human Resource Development and a Bachelor of Commerce. 

Sanjay has also held important governance representations, key amongst them include being a current Non-Executive Director for Standard Chartered Bank Uganda and member of the Professional Accountants in Business Committee of International Federation of Accountants (IFAC).
Sanjay is married and has two children. 

TANZANIA YACHAGULIWA NA UNESCO KUWA MJUMBE WA KAMATI YA URITHI WA DUNIA

$
0
0
 
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akizungumza na Waandishi wa Habari (hawako pichani) leo tarehe 23/11/2015 katika Ofisi za Wizara hiyo ambapo amesema kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia kwa kipindi cha miaka minne. Uchaguzi huo umefuatia uamuzi wa Mkutano Mkuu wa 20 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaohusu Urithi wa Dunia uliofanyika mjini Paris, Ufaransa tarehe 18-20 Novemba 2015.
 
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru kushoto akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Tanzania kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia. Alieleza kuwa katika Kamati hiyo Tanzania itawakilishwa na Bw. Donatius Makamba ambaye ni Mkurugugenzi Idara ya Mambo ya Kale Wizara ya Maliasili na Utalii akisaidiwa na Dkt. James Wakibara, Mwikolojia Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) na Dkt. Mohammed Juma, Mkurugenzi wa Mipango Miji na Vijiji kutoka Zanzibar.
 Bi. Eliwasa Maro Mkurugenzi Msaidizi Utafiti Mafunzo na Takwimu Wizara ya Maliasili na Utalii akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo katika Mkutano huo na Waandishi wa Habari.
 Sehemu ya washiriki wa Mkutano huo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii wakinukuu baadhi ya mambo muhimu.

(Na Hamza Temba - Wizara ya Maliasili na Utalii)

NDEGE YA UTAFITI YATUA KILIMANJARO

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Dkt. James Mataragio akuzungumza mbele ya waandishi wa habari kuhusu ujio wa ndege ya pili ya utafiti wa awali wa mafuta na gesi asilia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) mwishoni mwa wiki, ndege hiyo inatarajia kuanza utafiti wiki hii katika kitalu cha Eyasi Wembere na Mandawa.
 Mkurugenzi Mtendaji TPDC Dkt. James Mataragio akipatiwa maelekezo ya jinsi ndege hiyo inavyofanya kazi (ndani ya ndege) kutoka kwa Meneja wa Mradi Brett Robinson wa kampuni inayoendesha utafiti huo ya “CGG AVITION LTD”  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), utafiti huo unagharamiwa na TPDC kutoka katika mfuko wa fedha za maendeleo.
 Ndege ya utafiti wa awali wa mafuta na gesi asilia inayotarajia kuanza utafiti katika kitalu cha Eyasi Wembere na Mandawa ikiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Mkoani Kilimanjaro mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Mradi Brett Robinson wa kampuni inayoendesha utafiti huo ya “CGG AVITION LTD” (kushoto) akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari jinsi ndege hiyo itakavyofanya utafiti, Mkurugenzi Mtendaji TPDC Dkt. James Mataragio (kulia).

NEWS ALERT: NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO ILALA JIJINI DAR LEO

$
0
0
 Sehemu ya waokoaji katika Nyumba iliyoteketea kwa moto, wakiangalia namna ya kuokoa wa baadhi ya mali zilizokuwepo ndani ya nyumba hiyo, moto huo umetokea mchana wa leo katika mtaa wa Tabora, Ilala jijini Dar es salaam. Chanzo cha moto huo hakikuweza kufahamika mara moja.

Shughuli ya uzimaji moto huo ikielekea ukingoni baada ya kikosi cha zima moto kufika eneo la tukio na kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa.
Moto ukiendelea kuteketeza nyumba hiyo leo mtaa wa Tabora Ilala jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Massaka wa  Globul ya Jamii.

SPEA ZA MASHINE ZA MRI NA CT-SCAN ZIMEFIKA NA MATENGENEZO YAMESHAANZA KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI

$
0
0
 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete baada ya kufuatilia agizo la Rais John Pombe Magufuli ambaye awali aliagiza wagonjwa wasilale chini. Rais Magufili aliitembelea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) hivi karibuni na kutoa agizo hilo. Leo Balozi Sefue ameitembelea mashine ya MRI, ST-Scan na Jengo la Taasisi ya Mifupa ya MOI. Akiwa katika ofisi ambako ipo mashine ya MRI na ST-Scan Balozi Sefue amepewa taarifa ya matengenezo ya mashine hizo. 
 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (katikati) akiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ambako amefanya ziara kuangalia utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli kuhusu huduma bora kwa wagonjwa na kutekeleza wagonjwa kutolala chini. Wagonjwa hivi sasa wanalala kwenye vitanda na siyo chini. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi na Jamii, Dk Donan Mmbando na kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Mifupa ya Moi, Othuman Wanin Kiloloma.
 Katibu Mkuu wa Kiongozi (kulia), Balozi Ombeni Sefue akihoji kutokamilika kwa mashine ya MRI kwa wakati baada ya kutembelea chumba ambako mashine hiyo imehifadhiwa. Ofisa anayesimamia utengenezaji wa mashine hiyo, Monica Joseph ameahidi kwamba mashine hiyo itakamilika Alhamisi ijayo. 
 Mmoja wa mafundi wa mshine ya ST-Scan akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Kiongozi (kulia), Balozi Ombeni Sefue kuhusu utengenezaji wa mashine hizo. Fundi huyo ameahidi kwamba mashine hiyo itakamilika Jumatano.
Picha zote kwa hisani Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).


SERIKALI Kuendelea Kuboresha Sekta ya Afya Nchini
Katibu  Mkuu  Kiongozi  Balozi Ombeni  Sefue leo amefanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) pamoja na mambo mengine amesema serikali itaendelea kuboresha sekta ya afya nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.

Akizungumza baada ya kutembelea MNH, Balozi Sefue amesema  amekagua mashine za MRI na CT-SCAN  na kueleza kuwa spea zimeshafika na kazi ya kutengeneza mashine hizo inaendelea. Pia amesema kwamba Serikali ya Tanzania imesaini mkataba mpya na Serikali ya Uholanzi wa kununua vifaa vipya na Hospitali ya Muhimbili itapata CT-SCAN moja wakati Hospitali ya Bugando itapata mashine moja ya MRI.

Pia,  amewataka wahudumu wa afya kuwahudumia vizuri wagonjwa wanaotumia Bima ya Afya ili kuongeza mapato katika hospitali za serikali.
Akizungumzia kuhusu kudhibiti wizi wa dawa za serikali, Balozi Sefue amesema ni vema ukaimarishwa mfumo wa MSD kwa kutumia mifumo ya Tehama  na kuwa na maduka yao ya ndani.
Katika ziara hiyo, Balozi Sefue amepata fursa ya kufanya kikao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dk Donan Mmbando  na  watendaji wa MNH  ili kupata sura ya matatizo yote katika hospitali hiyo.

BREAKING NYUZZZZ....: RAIS MAGUFULI ATANGAZA SIKU YA UHURU KUWA SIKU YA KUFANYA KAZI

$
0
0
Kwa mujibu wa  Sheria ya Sikukuu za Kitaifa  (The Public Holidays Act, Cap 35) pamoja na Sheria zingine zinazompa mamlaka Rais kutangaza siku yoyote kuwa sikukuu au mapumziko,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameamua kuwa maadhimisho ya Sherehe za Uhuru na Jamhuri zitakazofanyika tarehe 9 Desemba, 2015, yatumike  kwa kufanya kazi.  

Kwamba maadhimisho ya Uhuru ya mwaka huu  (2015) yatatumika kama kichocheo cha kujenga tabia ya kufanya kazi (Uhuru na Kazi) katika Taifa letu.  Mheshimiwa Rais ameelekeza Watanzania wote siku hiyo waitumie kwa kufanya kazi mbalimbali kama vile, mashambani, maofisini, sokoni, viwandani na usafi wa miji yao katika kutimiza dhana ya Uhuru na Kazi kwa vitendo.

Aidha, kwa kuwa Sherehe za Uhuru na Jamhuri huendana na Maandalizi mbalimbali ambayo yanatumia fedha, kwa kuzingatia kuwa siku hiyo itaadhimishwa kwa kufanya kazi,  fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hiyo sasa zitumike kwa shughuli zingine za kijamii ikiwa ni pamoja na kupambana na maradhi hasa kipindupindu, kununulia dawa za hospitali, vitanda vya hospitali n.k. kadri kamati za maandalizi zitakavyoamua.

Ieleweke kuwa sherehe za Uhuru na Jamhuri ni muhimu katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa nchi yetu. Hivyo,   sherehe hizi zitaendelea kuadhimishwa kila mwaka kama kawaida kuanzia mwaka 2016.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

wananchi watahadharishwa dhidi ya bidhaa feki za IVORI

$
0
0
Kampuni ya IVORI-IRINGA Inawataadharisha Wateja wake  Hususani Wasambazaji na Wauzaji wa Maduka ya Jumla na Reja reja kuwa, kumekuwepo na matapeli katika baadhi ya mikoa Nchini, Wakiuza bidhaa Feki kwa kutumia jina la pipi za Ivori kwa madai ya muonekano mpya wa bidhaa zetu.

Kampuni ya Ivori Iringa haijaubadilisha muonekano wa pipi zake wala Nembo yake,Hakikisha kila pipi unayonunua  ina nembo halisi ya Ivori kutoka Iringa.

kwa yeyote atakaenunua na Kutumia bidhaa  zinazofananishwa na Pipi za Ivori Iringa na kudhurika kiafya, basi kampuni ya ivori iringa haitahusika na malalamiko yoyote.


Ewe Mteja USIDANGANYIKE,
Nunua Pipi orijino ya Ivori Iringa kwa usalama wa Afya yako .

Imetolewa na

Mkurugenzi Mkuu


I.F.B (LTD)


UTT-PID yashiriki mkutano wa mwaka wa Wanahisa wa UTT-AMIS jijini Dar es Salaam

$
0
0
1 (1)
Maafisa masoko wa UTT-PID, Laurence Nzuki (kushoto) na Martin Mchanjila (katikati) wakitoa maelezo kwa baadhi ya watu waliotembelea kwenye banda hilo la UTT-PID wakati wa mkutano huo wa mwaka wa Wanahisa wa UTT-AMIS uliofanyika mwishoni mwa wiki, Novemba 21-22.2015, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam.

Na Andrew Chale, Modewjiblog
Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyochini ya Wizara ya Fedha (UTT-PID) inafanya miradi mbalimbali ikiwemo huduma za uuzwaji wa viwanja katika maeneo tofauti nchini ikiwemo vile vya mradi wa katika miji ya Chalinze na Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani. Pia mradi wa viwanja vya Bunju, Tundwi songani-Kigamboni ambayo ipo Jijini Dar es Salaam. Mingine ni Kingorwila, Madaganya, Mkoani Morogoro. Lindi, Bukoba, Sengerema na kwingine kwingi hapa nchini.
UTT -PID ni miongoni mwa taasisi zinazofanya vizuri na utendaji wa kasi katika utoaji huduma za ushahuri katika maeneo ya upembuzi yakinifu wa miradi mbalimbali, Uratibu wa fedha na huduma zinazohusiana katika maandalizi ya mapendekezo ya miradi kwa benki au taasisi za fedha, uteuzi wa watoa huduma kuhusiana na maandalizi ya zabuni na usimamizi wa majengo na mali ambao ni utoaji wa huduma fanisi za usimamizi wa majengo yaliyochini ya uangalizi thabiti wa taasisi.
AsfOxbUQv7XGaXHM7H-QB4HDmtD0NoXc-5OrHiTpRdSOPicha ya juu na chini Afisa masoko wa UTT-PID, Mary Lugusi akielimisha wananchi juu ya miradi inayoendeshwa na taasisi hiyo kwa wananchi hao waliotembelea banda hilo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI 

INTRODUCING FURAHA BY AMINI

TEASER JOTO LA ASUBUHI LA 93.7 EFM JUMANNE NOVEMBER 24

HATIMA YA MWILI WA MAREHEMU MAWAZO KUAGWA JIJINI MWANZA KUAMULIWA KESHO NA MAHAKAMA

$
0
0

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akitoa taarifa kwa wananchi baada ya Chadema Kufungua Kesi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga kuzuiliwa kwa mwili wa Marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza.

Na George Binagi - GB Pazzo wa Binagi Media Group

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema leo kimefungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, ili kuiomba Mahakama hiyo kutengua zuio la kuuaga mwili wa aliekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Geita Marehemu Alphonce Mawazo, lililotolewa na Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kutokana na hofu ya kiusalama pamoja na uwepo wa ugonjwa wa Kipindupindu.

Katika kesi hiyo, Chadema inawakilishwa na Mawakili watatu ambao ni James Millya, John Mallya pamoja na Paul Kipeja ambapo mlalamikaji ni Charles Lugiko ambae ni baba mdogo wa Marehemu Mawazo.

Mahamaka hiyo chini ya Jaji Lameck Mlacha, imesikiliza malalamiko ya upande wa washtaki na kuahirisha kesi hiyo hadi kesho ambapo imeamuru mlalamikiwa ambae ni Mkuu wa Polisi Mkoa wa Mwanza pamoja na mwanasheria Mkuu wa Serikali kupelekewa nyaraka za kesi hiyo kabla ya kusikiliza utetezi wao hapo kesho.

Mapema kabla ya kesi hiyo kusikilizwa, wafuasi wa Chadema waliokuwa wamekusanyika nje ya viunga vya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, walilalamikia hatua ya jeshi la polisi kuwazuia kuingia Mahakamani hapo ili kujua hatima ya kesi hiyo, ambapo wamesema kitendo hicho kinaondoa dhana ya Rais John Pombe Magufuli, kuwa yeye ni rais wa wananchi wote wakati wao kama Chadema wananyimwa haki zao.

Licha ya Malalamiko hayo pamoja na ulinzi mkali wa polisi uliokuwa umetanda Mahakamani hapo, bado wafuasi wa Chadema hawakuondoka katika viunga vya Mahakama hiyo hadi pale Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Freeman Mbowe alipowasihi kurejea majumbani mwao hadi kesho kesi hiyo itakaposikilizwa tena.

Ni zaidi ya siku nane sasa tangu marehemu Alphonce Mawazo auawe kikatili Mkoani Geita na watu wasiojulikana kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni chuki za kisiasa ambapo mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando.
Mmoja wa Mawakili wa Chadema John Mallya akitoa taarifa ya kesi baada ya Chadema Kufungua Kesi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kupinga kuzuiliwa kwa mwili wa Marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza.

TANZANIA PUBLIC SERVICE PENSIONS FUND RECEIVES THE GOLDEN AWARD FOR QUALITY AND BUSINESS PRESTIGE IN GENEVA, SWITZERLAND

$
0
0
The PSPF has received the Golden award for Quality and Business Prestige from the Association Otherways Management and Consulting based in Paris, France in recognition of her achievements in areas of Innovation, Quality Commitment and Excellence.
The award was received on behalf of PSPF by Ambassador Modest J. Mero, Permanent Representative of Tanzania to UN, at the ceremony held at Hotel Intercontinental in Geneva on 23 November 2015.
Viewing all 110130 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>