Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 109570 articles
Browse latest View live

SIMU TV: HABARI KUTOKA TELEVISHENI


KIPINDI CHA Danga chee kipo hewani CHANNEL TEN leo na KILA ALHAMISI SAA NNE USIKU NA MARUDIO JUMAPILI SAA SITA MCHANA: HEWANI LEO NI KING KIKII

UN WAZINDUA MRADI WA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI, CHAMWINO DODOMA

0
0
ALVARO KUPANDA MTI-2
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akipanda mti kama ishara ya uhifadhi mazingira baada ya kuzindua mradi wa kupunguza na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia nishati jadidifu ya jua (Mitigating Climate change in vulnerable communities of Dodoma region, Machali village, Chamwino District), katika Kijiji cha Machali A, wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma katika utekelezaji wa moja kati ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
ALVARO MWAGILIA MAJI-3
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akimwagilia maji kama ishara ya uhifadhi mazingira baada ya kuzindua mradi wa kupunguza na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia nishati jadidifu ya jua (Mitigating Climate change in vulnerable communities of Dodoma region, Machali village, Chamwino District), katika Kijiji cha Machali A, wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma katika utekelezaji wa moja kati ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
ALVARO NA BURUDANI-2
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa UNDP, Awa Dabo (kulia) wakieleka kukagua mradi wa ufugaji wa shirika la Tanzania Environmental Friendly Association (TEFA) huku wakiburudishwa na ngoma ya wenyeji wa kabila wa Kigogo, katika Kijiji cha Machali A, wilaya ya Chamwino mkoa wa Dodoma katika utekelezaji wa moja kati ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).

KUMBUKUMBU MRS BARKE M. UBAYA

0
0

index
MRS BARKE M. UBAYA LEO UMETIMIZA MIAKA MIWILI TANGU UTUTOKE DUNIANI SISI TULIO HAI BADO TUNAKUKUMBUKA KWA UPOLE UCHESHI NA UKARIMU WAKO UNAKUMBUKWA NA MUMEO BW.MWINYI UBAYA WANAO SALAMA NA RAHMA MAMA YAKO FAMILIA YA MAGOHA NA UBAYA JIRANI NA MARAFIKI INSHA'ALLAH M MUNGU AKUSAMEHE MAKOSA YAKO AMIN INNA LILLAH WA INNA LILLAH RAJIUN

UCHAMBUZI WA MAGAZETI LEO

0
0
SIMU.TV:  Mh.Majaliwa asema hakutegemea, aahidi kutumikia wote bila ubaguzi. Dk.Tulia achaguliwa kuwa Naibu Spika Bunge la 11; 
SIMU.TV:  Wazimia baada ya nyumba 25 kuvunjwa Dar,  watoto watatu wauwawa  kikatili. Wazanzibari waandamana London; https://youtu.be/2OWnUdzu-rI     
SIMU.TV:  Vyama vya siasa vyatakiwa kuvunja vikundi vya ulinzi. Profesa Lipumba amsifu Rais Magufuli kwa uteuzi wa Waziri Mkuu; https://youtu.be/Me8XZ1KxDy0

SIMU.TV:  Mkwasa abeba lawama zigo la 7-0. MCameroon atua rasmi Simba, safari ya Miss Tanzania , China yaiva. Pata habari motomoto zilizotawala katika magazeti ya leo; https://youtu.be/1wBDkbbtnak

WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA NCHINI KUTEMBEA WAGENI WA KIMATAIFA MAKUMBUSHO YA TAIFA

0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akiwa kwenye ukumbi wa Sanaa, Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo ya Michoro ya Mapangoni kutokwa kwa Mtaalam wa Makubusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam Bi Agnes Gidna.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo ya Chimbuko la mwanadamu kutokwa kwa Mtaalam wa Makubusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam Dkt Amandus Kweka. Fuvu lilipo kulia kwenye sanduku lililo nakshiwa na dhahabu ni la Zinjanthropus lililo gunduliwa zaidi ya miaka milioni 1.7 iliyo pita huko Ngorongoro Oldvuvai kwenye miaka ya 1959. 

REMEMBRANCE THE LATE DONAT SAMIKE MASHIKU

0
0
Baba, God saw you struggling and no cure in this world was there to make you stay, he then decided to call you that day of 20th November 2013. They were days, weeks, months and now 2 years without you. It is true that you are gone.

Our hearts were hurt but we had no choice, we had to let you go. We miss your smile, your words, and many more that we cannot express .We continue praying for you papa that your heart continue to rest in Eternal Peace. 

There will be a holy mass at University od Dar es Salaam Chepel on 20th November 2015  and on Saturday 21st November 2015 at 1500hrs onward we will gather at your home Mapinga for lunch and remembrance of your great life teachings. 

Our friends and family please join us when commemorating the life of a beloved HUSBAND,DAD,BABU,UNCLE and a BROTHER. 

May your gorgeous soul continue to Rest In eternal Peace. Amen.

WATEJA WA AIRTEL KUANGALIA VIPINDI VYA TELEVISHENI KUPITIA SIMU ZA MKONONI

0
0
 Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akionyesha huduma mpya ya "Airtel TV" inavyofanya kazi wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo
itakayowawezesha wateja wa Airtel kuangalia vipindi katika vituo
mbalimbali vya television kupitia simu zao za mkononi, akishuhudia ni
Meneja huduma za ziada wa Airtel,Prisca Tembo.
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma  mpya ya "Airtel TV" itakayowawezesha wateja wa Airtel kuangalia vipindi katika vituo mbalimbali vya telesheni kupitia simu zao za mkononi.

 *   Kuunganishwa na chanel  8 za ndani na nje
  *   Kujiunga na vifurushi vya kuangalia TV bila kikomo vya siku, wiki na mwezi   Dar es Salaam, Tanzania 19 Novemba 2015, kampuni ya simu za mkononi ya  Airtel leo imezindua huduma ya ziada itakayowawezesha wateja wake nchi nzima kuangalia vipindi vya televisheni katika vituo vya ndani na nje  ya nchi kupitia simu zao za mkononi.

Huduma hii mpya ijulikanayo kama "Airtel TV" imeunganishwa na vituo 8 za televisheni vya ndani na nje ya nchi na kuwawezesha wateja wa Airtel kuangalia vipindi vilivyopita katika tamsilia wanazozipenda,
kuangalia sinema na video wanazohitaji  kupitia simu zao.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa "Airtel TV" Meneja Uhusiano wa Airtel ,
Bw Jackson Mmbando alisema "kwa kawaida mara nyingi watanzania wanaangalia vipindi vya televisheni wakiwa nyumbani  wakati wa jioni baada ya kutoka katika kazi zao. 

Tunazindua huduma yenye gharama nafuu itakayowawezesha wateja wetu kupata taarifa pindi wasipokuwapo 
majumbani mwao.

"Airtel TV" itawapatia uzoefu wa kipekee na
kuwahabarisha wateja wetu wakati wowote  wakiwa katika shughuli zao au kwenye foleni,  bila kikomo kupitia simu zao za mkononi"" huduma hiii imelenga kukidhi mahitaji ya wateja kwa kuwapatia habari  kiurahisi kwa kujiunga na kifurushi cha siku , wiki au mwezi.

Tunaamini huduma hii itapunguza uwiano wa watu wasiokuwa na fursa ya  kuangalia Televishoni na pia kuwawezesha kupata matukio kwa wakati kupitia simu zao mahali popote pale walipo" aliongeza Mmbando
Akiongea kuhusu mahudhui na jinsi ya kujiunga na huduma hiyo, Meneja
huduma za ziada ,Prisca Tembo alieleza zaidi  kuhusu dhamira yao ya
kutoa huduma yenye kiwango cha juu na gharama nafuu. 

"tunayo furaha kuwawezesha watanzania kuangalia vipindi vya televisheni kupitia simu zao kwani tunaenda sambamba na mpango wa serikali wa kidigitali wenye lengo la  kuwa na jamii kupata taarifa za yanayotokea ndani na nje ya nchi kwa wakati na kiwango cha juu.

Tembo aliongeza kwa kusema ili kupata huduma ya  "Airtel TV" mteja
anatakiwa kupakua  au kudownload application kwa kupitia linki  ya
https://goo.gl/iSvaJC kwa simu za Android na   https://goo.gl/IMvzCt
kwa simu za IOS.

Baada ya kuzi download mteja ataweza kununua kifurushi cha internet
maalum cha Televisheni  kwa kupiga *148*88#  tozo za kujiunga ni Tshs
499 kwa siku, Tshs 2,999 kwa wiki naTshs 11,999 kwa mwezi. Vituo
vinavyopatikana katika "Airtel TV" ni pamoja na Star TV, TBC, Fight
Box, 360 tune box, Citizen, FilmBox, Channel Ten na Aljazeera. 

HAFLA YA KUAPISHWA KWA WAZIRI MKUU.

0
0
SIMU.TV:  Viongozi Mbalimbali wawasili katika ukumbi wa Ikulu Ya Chamwino Dodoma kushuhudia kiapo cha Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa. 
SIMU.TV:  Mhe. Kassim Majaliwa ni waziri wa 11 tangu Tanzania ipate uhuru wake toka kwa wakoloni.https://youtu.be/w8QL1Xqn-uE
 SIMU.TV:  Makamu wa Rais Mstaafu Mhe. Gharib Bilal awasili kushuhudia kiapo cha Mhe. Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania. https://youtu.be/UDtuYyt5jVI
SIMU.TV:  Hatimaye Waziri mkuu mteule na Rais Magufuli wawasili ndani ya ukumbi wa Ikulu ya Chamwino na wimbo wa Taifa kuibwa. https://youtu.be/AYcNgFIxW00 
SIMU.TV:  Hatimaye Mhe Kassim Majaliwa ala kiapo cha uaminifu na kuahidi kuhifadhi na kulinda katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. https://youtu.be/G_JWuGmfyrw
SIMU.TV:  Viongozi mbalimbali wajongea kutoa Mkono wa pongezi  Waziri mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
SIMU.TV:  Hii ndiyo orodha ya waliowahi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu katika Serikali ya Tanzania;https://youtu.be/K0YdS_RB7yQ

SERIKALI YABORESHA MFUMO WA UKUSANYAJI WA MAPATO

0
0
 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI Bi. Rebecca Kwandu akifurahia jambo na waandishi wa habari (hawapo pichani)leo jijini Dar es Salaam wakati akiwaeleza mafanikio ya mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki katika mamlaka za Serikali za Mitaa (LGRCIS). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Mifumo ya TEHAMA wa ofisi hiyo Bw. Mtani Yangwe na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.
 Mkurugenzi Msaidizi Mifumo ya TEHAMA kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI Bw. Mtani Yangwe akifafanua kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam namna mfumo wa wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki unavyorahisisha ulipaji wa kodi mbalimbali kwa kuhusisha mifumo ya kielektroniki ya malipo na mifumo ya kibenki. Kulia ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa ofisi hiyo Bi. Rebecca Kwandu.

Picha zote na Fatma Salum (MAELEZO).
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Na Georgina Misama.
SERIKALI imeboresha matumizi ya mfumo wa ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kielekitroniki katika mamlaka za serikali za mitaa.

Hayo yamesemwa na msemaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) Bi. Rebecca Kwandu leo jijini Dar es salaam.

Bi Rebecca amesema kuwa TAMISEMI imekuwa ikiendelea kwa nyakati tofauti kufanya maboresho mbalimbali ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa jamii na kuzisaidia mamlaka hizo katika kuongeza mapato ya ndani na kuondokana na uteuzi wa ruzuku kutoka Serikali Kuu.

“Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI iliamua kuanzisha mfuko wa Local Governement Collection Information System (LGRCIS) baada ya kufanya tafiti mbalimbali kwa nyakati tofauti na zilionyesha kuwa hakukuwa na mfumo wowote wa kielektroniki kurahisisha ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Halmashauri” alifafanua Bi. Rebecca.

Mbali na hayo Msemaji huyo alisema kuwa miongoni mwa malengo makuu ya kuanzishwa kwa mfumo wa LGRCIS ni pamoja na kupata taarifa za walipa kodi wa mamlaka za serikali za mitaa na kuhifadhiwa kwa usahihi katika kanzi data ya mfumo.

“ Kupata takwimu sahihi ya vyanzo vya mapato na kufanya usuluhishi kati ya kilichokusanywa na kilichotarajiwa kukusanywa, kuongeza mapato kwa kasi zaidi kwa kuwa na uhakika wa makusanyo katika vyanzo vikuu, kuweka uwazi na uwajibikija katika makusanyo ya mapato,na kuhimarisha ulipaji miamala ya kodi na tozo itakayofanywa na walipakodi” aliongeza Bi Rebecca.

Pia alisema kuwa matarajio ya TAMISEMI ni kuwa mfumo wa LGRCIS utaleta mabadiliko makubwa katika Halmashaurina kuachana na utegemezi wa ruzuku kutoka Serikali kuu.

Hata hivyo teknolojia pekee ya matumizi ya TEHAMA haiwezi kuleta mabadiliko pasipo fikra za watumiaji wa mfumo wa walipakodi kubadili mazoea.

SHEREHE ZA KUAPISHWA WAZIRI MKUU WA AWAMU YA TANO VIWANJA VYA IKULU NDOGO CHAMWINO MJINI DODOMA

0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli, akimwapisha Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, kuwa Waziri Mkuu wa awamu ya tano, wakati wa sherehe hizo zilizofanyika leo Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino mjini Dodoma.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli, akimkabidhi nyaraka za Serikali baada ya kumwapisha Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, kuwa Waziri Mkuu wa awamu ya tano, wakati wa sherehe hizo zilizofanyika leo Nov 20, 2015 kwenye Viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimpongeza Waziri Mkuu mpya wa awamu ya Tano, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa baada ya kuapishwa rasmi leo kwenye Viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino mjini Dodoma, leo Nov 20, 2015.
Rais Dkt. John Magufuli (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wake, Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, baada ya kuapishwa Waziri huyo Mkuu kwenye Viwanja vya Ikulu Ndogo Chamwino mjini Dodoma leo.

BOMOA BOMOA YA MANISPAA YAENDELEA MBEZI BEACH (BLOCK K) JIJINI DAR

0
0
  Nyumba nyingine eneo hilo nayo ikisubili kubomolewa na manispaa ya Kinondoni. 
 Ubomoaji ukiendelea.   





 Wazee wa kazi wakiwa katia geti la nyumba inayotakiwa kubomolewa  maeneo ya mtaa wa  Libermann Mbezi Beach jijini Dar es Salaam leo.
 Wakazi wa nyumba nyeupe inayobomolewa wakitoka nje ya nyumba baada ya kuanza kubomolewa na manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam leo
Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.


BASATA YAWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYAMA VYA WASANII

0
0
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (Kulia) akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya wasanii yaliyoandaliwa na Baraza hilo mapema wiki hii. Kulia kwake ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni anayeshughulikia Lugha kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Shani Kitoga
 Msanii mkongwe wa Sanaa za Maonesho Bw. Kassim Mbelemba maarufu kwa jina la Mzee Jangala akipokea cheti chake kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utamaduni anayeshughulikia Lugha kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Shani Kitoga baada ya kumaliza mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya wasanii yaliyoandaliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mapema wiki hii.  
 Mwezeshaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa vyama vya Wasanii katika eneo la Hakimiliki na Hakishiriki Bw. John Kitime akipokea zawadi kutoka kwa mmoja wa viongozi wa vyama vya wasanii baada ya kutoa mafunzo kwa viongozi hao. 
Viongozi wa vyama vya Wasanii walioshiriki mafunzo ya Kujengewa Uwezo wakiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi Bi. Shani Kitoga
IMETOLEWA NA KITENDO CHA HABARI NA MAWASILIANO, BASATA.

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limewapa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika maeneo mbalimbali viongozi wa vyama na taasisi zinazojihusisha na wasanii ili kujenga ufanisi zaidi katika sekta ya Sanaa.

Mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tatu kuanzia Jumanne hadi Alhamisi ya wiki hii yalijikita katika kuwajengea uwezo Wasanii kwenye maeneo ya uandaaji bajeti, uandaaji wa mipango mikakati na sheria ya hakimiliki na hakishiriki na mikataba kwenye kazi za Sanaa. 

MDAU ATOA SHUKRANI KWA MICHANGO YA MATIBABU

0
0
SHUKRANI
Habari Ndugu zetu Watanzania mlio ndani na nje ya nchi nawasalimu.

Natumaini wote mko salama.
Kwa niaba ya Dada yetu Ndugu yetu Mtanzania Mwenzetu AMINA ALLY JUMA na Familia yake yote kwa ujumla, Leo tunarudi kwenu kwa SHUKRANI ZA DHATI kwa Moyo kwa kujitolea kwenu kwa hali na Mali na Sala zenu.

Tangu Mwezi uliopita tulikuja kwenu kwa ajili ya kuomba msaada kwa ajili ya Dada yetu AMINA anayesumbuliwa na maradhi ya Saratani ya Damu (ACUTE AMELOID LEUKEMIA) Ambaye kwa sasa yuko nchini India akiendelea na Matibabu.

Napenda Kuwashukuru sana Wadau wote walioweza kuusambaza ujumbe, hasa kwa njia ya mitandao (Social Media) kwani mchango wenu umekuwa mkubwa mno na uliozaa matunda mema. 

Tumefanikiwa kupata kiasi ($7500.00) ambacho kilitakiwa kwaajili ya kutimiza malengo ya dada Yetu AMINA kwa matibabu yake, TUNAWASHUKURU WOTE WALIOJITOLEA KWA HALI MALI NA SALA ZENU MWENYEZI MUNGU AZIDI KUWABARIKI NA TUENDELEE NA USHIRIKIANO HUU.

Pia tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa, MICHUZI BLOG, WANAWAKE LIVE, SMILEY KIDS EVENTS, ZAMARADI MKETEMA, JOKATE MWEGELO, 8020 FASHION BLOG, SARAH RAQEY, DINA MARIOS, ITV na wengine wote kwa njia moja tuliweza kujitoa kwa nia njema katika kuwajibika, TUNASEMA ASANTENI SANA SANA NA MUNGU AWABARIKI.

KUANZIA LEO HII 20/11/2015 TUNASITISHA MICHANGO HII NA TUKIMSHUKURU SANA MUNGU KWA WEMA WAKE WOTE.

Tunawashukuru sana kwa Michango yenu yote, kwa ushirikiano tumetimiza lengo, na sasa tumemkabidhi Mungu mwenyezi muumba wetu atende miujiza yake kwa Dada yetu AMINA na ndugu zetu wote walioadhirika na ugonjwa huu tuzidi Kuombeana Kupendana na Kushirikiana.

PS: KUTAKUWA NA DUA YA SHUKRANI NYUMBANI KWA AMINA MIKOCHENI B’ WARIOBA, TAASISI STREET, SIKU YA IJUMAA 27/11/2015 KWA WALE WATAKAOWEZA KUFIKA KARIBUNI SANA.

ASANTENI SANA KAZI NJEMA NA MUNGU AWABARIKI ……AMEN

NAIBU KAMISHNA MKUU WA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) NA UJUMBE WAKE WATEMBELEA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

0
0
 Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ukiwa katika kikao na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) uliotembelea Wizara hiyo.  Wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo akizungumza na ujumbe wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) (haupo pichani) uliotembelea Wizara hiyo ambapo masuala mbalimbali kuhusiana na wakimbizi yalijadiliwa.  Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazohifadhi wakimbizi, hasa kutoka Ukanda wa Maziwa Makuu.
 Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bi. Kelly Clements akizungumza katika kikao na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (haupo pichani) wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Katikati ni Mkurugenzi wa UNHCR, Kanda ya Afrika na kushoto ni Mtendaji Msaidizi wa Naibu Kamishna Mkuu wa UNHCR, Bi. Geraldine Salducci.
Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke akizungumza katika kikao cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) wakati ujumbe huo ulipotembelea Wizara. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.(Picha zote na Abubakari Akida,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Imeandaliwa na Kitengo Cha  Mawasiliano ya Serikali-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MAHAFALI YA 10 YA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

0
0
 Mkurugenzi wa Elimu ya Ufundi na Ufundi Stadi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Katebalilwe akihutubia kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 10 ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo asubuhi.
   Brass Bendi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ikiongoza maandamano wakati wa mahafali hayo.
 Wahitimu waliofanya vizuri masomo yao wakiwa katika icha ya pamoja na meza kuu.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA

0
0
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA

Mahujaji wengine wane (4) kutoka Tanzania ambao walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa hawaonekani tangu ajali ya kukanyagana kwa mahujaji ilipotokea Makkah nchini Saudi Arabia tarehe 24 Septemba 2015 wametambuliwa kuwa, ni miongoni mwa mahujaji waliofariki  dunia. Kutambuliwa kwa mahujaji hao kunafanya idadi ya mahujaji wa Tanzania waliopoteza maisha katika ajali hiyo kufikia thelathini na mbili (32). 

Majina ya Mahujaji hao kutoka kikundi cha Khidmat Islamiya ni:-
1.Abdul Idd Hussein
2.Adam Abdul Adam
3.Rashida Adam Abdul
4.Khadija Abdukhalik Said 

Aidha, hadi sasa mahujaji saba (7) kutoka Tanzania bado hawajulikani walipo na jitihada za kuwatafuta bado zinaendelea. Majina ya Mahujaji hao ni:
1.Burhani Nziru Matata
2.Farida Khatun Abdulghani
3.Juma Jecha Jaku
4.Laila Manunga
5.Nassor Mohammed Hemed
6.Saleh Mussa Said
7.Shabinabanu Ismail Dinmohamed

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, 
Dar es Salaam
20 Novemba, 2015

DIRISHA DOGO LA USAJILI LIGI KUU KUFUNGWA DISEMBA 15

0
0
Kalenda ya dirisha la usajili kwa vilabu vya Ligi Kuu (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) lilofunguliwa Novemba 15, litafungwa Disemba 15 mwaka huu.
Vilabu vinavyoshiriki ligi hizo zilizopo chini ya Shirikisho Mpira wa Miguu (TFF) vinaombwa kufanya usajili katika muda uliopangwa ili kuepukana na kuchelewa, na kufungwa kwa dirisha hilo.
Usajili wa dirisha dogo ni kwa vilabu ambavyo havijajaza idadi ya wachezaji 30 katika usajili uliofanyika wakati wa dirisha kubwa la usajili (Juni – Agosti 2015), usajili huo wa wachezaji unafanyika katika tovuti ya TFF, www.tff.or.tz kisha kwenye link ya Club Registration.

Rais Magufuli aagiza fedha za hafla ya wabunge zipelekwe Muhimbili kununulia vitanda vya wagonjwa

0
0
Baada ya kulihutubia na kulizindua bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFULI amehudhuria hafla fupi iliyoandaliwa kwa ajili ya wabunge katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma na kuagiza fedha zilizochangwa kwa ajili ya kugharamia hafla hiyo zipelekwe Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kununulia vitanda vya wagonjwa.

Mheshimiwa Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa kuwa wadau mbalimbali wamechanga kiasi cha shilingi milioni 225 kwa ajili ya kugharamia hafla ya wabunge katika siku ya uzinduzi wa Bunge.

Dkt Magufuli amesema alipata taarifa za kuwepo kwa michango hiyo ya fedha na kutoa maelekezo kuwa zitumike kwa kiasi kidogo kwa ajili ya hafla hiyo na sehemu kubwa zipelekwe katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili zikatumike kununulia vitanda na hivyo kupunguza tatizo la wagongwa wanaolala chini kutokana na uhaba wa vitanda unaikabili hospitali hiyo.

“Nilipoambiwa kwamba zimechangwa shilingi milioni 225 zimekusanywa kwa ajili ya sherehe, nikasema fedha hizo zipelekwe katika hospitali ya Taifa Muhimbili zikasaidie kununua vitanda” alisema Dkt Magufuli na kusisitiza kuwa “kwa kufanya hivyo tutakua tumejinyima sisi wenyewe lakini tutakua tumewanufaisha wenzetu ambao wanamatatizo makubwa yanayoweza kutatuliwa kwa fedha hizo”.

Awali akitoa taarifa ya michango hiyo Ofisa wa Spika wa Bunge Bwana SAID YAKUBU amesema jumla michango iliyopatikana na shilingi milioni 225 na kwamba fedha zilizotumika katika hafla hiyo ni shilingi milioni 24 tu baada ya kuzingatia maagiza ya Rais Magufuli.

Katika Hafla hiyo Rais Magufuli amekabidhi vyeti vya kutambua mchango wa wadau waliochangia fedha wakiwemo Benki za NMB, CRDB na Benki ya Afrika pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF na PPF.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano IKULU
November 20, 2015

BBC DIRA YA DUNIA NOVEMBA 20,2015

Viewing all 109570 articles
Browse latest View live




Latest Images