Quantcast
Channel: MICHUZI BLOG
Viewing all 110017 articles
Browse latest View live

ngoma azipendazo ankal: Tanzania, Tanzania nakupenda.....

$
0
0
Mrs Bernadette Mathias akiimba Wimbo wa Tanzania Nakupenda kwa Kiswahili

JE MNAHITAJI SACCOS, IJUE NAMNA YA KUANZISHA.

$
0
0
NA  BASHIR   YAKUB.
NILIWAHI  kueleza  namna ya  kuanzisha  kampuni   pamoja  na  usajili  wa  jina  la  biashara. Katika  makala  hayo  pia  nilieleza  tofauti  kati  ya   kusajili  kampuni  na  kusajili  jina  la  biashara.

  Hii  ilikwenda  sambamba  na  maelezo  ya  tofauti  za  kiuchumi   ya  vyote  viwili.  Ifahamike  kuwa  hizi  zote  ni  njia  za  kisasa  za  kujitafutia  kipato.  Makala  ya  leo  yanaeleza  namna   ya  kisheria  ya  kuanzisha   SACCOS.  

Tutaona  utaratibu  mzima  ambao   unaweza  kupitia  katika  kulifanikisha  hili.  Muhimu  ni  kujua  kuwa  SACCOS  nayo  ni  njia  kati  ya  njia  za  kisasa  za  kujipatia  na  kujiongezea kipato.  Aidha utaratibu  mzima  wa kuanzisha  na  kuendesha  SACCOS   unaongozwa  na  Sheria  namba  6  ya  2013  ya  vyama  vya  ushirika  ambayo  ndiyo  msingi  wa  makala  haya.

1.SACCOS  NI  NINI ?                                                                                                      
SACCOS   ni  kifupi  cha  neno  la  kiingereza  lijukanalo  kama  Saving  And Credit  CO-operative  Society.  Kwa  Kiswahili  kizuri  ni  chama  cha  ushirika  cha  akiba  na  mikopo.

  Kwa  faida  tu  ni  kuwa,  kwa  mara  ya  kwanza SACCOS  zilianzishwa  Ujerumani   na  mtu  aitwaye  Fredrick  Taylor.  Sura  ya  SACCOS   aliyoanzisha  Taylor  imekuwa  ikibadilika   kadri  shughuli  za  kijamii  na  kiuchumi  zinavyokua  mpaka  kufikia  aina  ya  SACCOS  zilizopo  sasa.

2.  SACCOS   KIUCHUMI.
Saccos  ni  asasi  ya  kifedha. Ni  muungano  wa  watu  ambao  lengo  lao  ni  kukusanya  fedha  na  kukopeshana  au  kufanya  biashara  moja  kwa  moja  na  kugawana  faida. Taratibu  za  kukopeshana  na  kufanya  biashara  katika  Saccos  hufanywa  na  watu   wenye  msimamo  au  fungamano  linalofanana.
Kusoma zaidi bofya  HAPA AU  HAPA

HAFLA YA MCHAPALO (COCKTAIL PARTY) WA KUSHEREHEHEA KUAPISHWA KWA RAIS DKT MAGUFULI

$
0
0

 Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli
  Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan kifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli
  Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Hadija Mwinyi akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli
  Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake
 Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Mtera Mteule Mhe Livingstone Lusinde "Kibajaji". Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

MAGUFULI AAPISHWA KUWA RAIS WA AWAMU YA TANO WA TANZANIA

$
0
0
JK akiaga wananchi kwa furaha wakati akiingia uwanja wa Uhuru katika sherehe rasmi za kumuapisha mristhi wake Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa awamu ya Tano wa Janhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais Kikwete akipokea saluti kwa mara ya mwisho kama Rais huku wimbo wa Taifa ukipigwa sambamba na mizinga 21.
Rais Kikwete akikagua gwaride la heshima lililojipanga katika muundo wa Omega - yaani mwisho.
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akila kiapo.
"....Hapa ndipo panapokustahili Mheshimiwa...." Rais Mstaafu wa awamu ya nne anamwambia Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akila kiapo.
Rais mstaafu  na Makamu wake Mstaafu wakiaga rasmi.
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride rasmi likiwa katika muundo wa Alpha kuashiria kushika madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akikagua gwaride rasmi likiwa katika muundo wa Alpha kuashiria kushika madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu
Rais wa awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akitembea kikakamavu bada ya kukagua  gwaride rasmi likiwa katika muundo wa Alpha kuashiria kushika madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA



BALOZI MULAMULA AWASINDIKIZA MARAIS WA DRC NA MSUMBJI

$
0
0
Rais Kabila (katikati) akielekea kwenye ndege, kulia ni Balozi Mulamula na kushoto ni Balozi wa Kongo nchini Mhe. Khalifani Mpango
Mhe. Rais Kabila akipita kwenye gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la wananchi Tanzania.
Katibu Mkuu Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akiagana na Rais Joseph Kabila tayari kwa kuanza safari ya kuelekea nchini kwake.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

ENEO LA LEBANON KATIKA SOKO LA KIMATAIFA LA SAMAKI LA FERI JIJINI DAR NI HATARI KWA UCHUMI.

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Soko la Samaki la Kimataifa la Feri, Ali Kibwana, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo. Kushoto ni Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.
Mama Lishe wa soko hilo, Taus Barnabas, akichangia neno katika mkutano huo.
Mwonekano wa sehemu ya soko la Samaki la Feri.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Na Dotto Mwaibale
ENEO la Lebanon katika Soko la Kimataifa la Samaki la Feri ambalo lipo jirani na Ikulu jijini Dar es Salaam limedaiwa kuwa ni hatari kwa wafanyabiashara wa soko hilo na kuwa linadhohofisha uchumi kutokana na kukithiri kwa watu wasio rasmi.

Hayo yamebainishwa na Mwezeshaji wa Sheria wa soko hilo, Asha Malenda wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wanaotembelea masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala kuona jinsi gani vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia umepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa mafunzo ya kupinga ukatili katika masoko hayo.

"Tunachangamoto kubwa sana katika soko letu la Feri tunayoipata kutoka eneo la Lebanon lenye mwingiliano wa watu wasio rasmi kutoka nje ya soko ambao ni kama wamejianzishia soko lao na wamekuwa na maamuzi yao lakini viongozi wa soko la Feri wanashindwa kuwachukulia hatua hali ambayo inatudhalilisha sisi wafanyabiashara hasa mama lishe na kuharibu uchumi wa soko letu" alisema Malenda.

Alisema wengi wa watu waliopo katika eneo hilo lisilo rasmi wamekuwa wakifanya biashara kiholela huku wakipika vyakula katika maeneo yanayoweza kuhatarisha afya ya mlaji wakati katika soko hilo kuna eneo maalumu la mama lishe na wengi wa watu hao wakienda kula eneo hilo rasmi wamekuwa hawalipi fedha na wakibanwa kulipa wanadiliki kutoa visu na silaha za jadi kuwatishia wanaodai.

"Eneo hilo la Lebanon ni hatari na kinachoshangaza linatizamana na Ikulu lakini hakuna hatua yoyote ya makusudi inayochukuliwa na viongozi wetu na linapopelekwa kwa viongozi wa kisiasa wanadai waachwe kwani ndio wapiga kura wao" alisema Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Bakari Said.

Said alisema katika soko hilo kuna changoto nyingi za udhalilishaji wanawake kwa kushikwa katika maungo yao lakini kupitia EfG wamejitahidi kupunguza changamoto hizo kwani wasaidizi wa sheria waliopatiwa mafunzo na shirika hilo wanajitahidi kuupenyeza ujuzi waliopata kuifikishia jamii ambayo imeanza kuelewa kuhusu vitendo hivyo.

Aliongeza kuwa uvaaji wa nguo za kubana na kuacha vifua wazi kwa upande wa wanawake pia ulikuwa ukichochea kukithiri kwa vitendo vya udhalilishaji uliokuwa ukifanywa na vijana wasio rasmi katika eneo hilo la Feri ambao hawana makazi na maisha yao yapo Feri lakini baada ya kufikiwa na mafunzo ya EfG hali hiyo imepungua kwa asilimia 80.

Mwezeshaji Fatuma Saijali alisema changamoto kubwa iliyopo hivi sasa katika soko hilo ni kuzuiliwa kupika chakula katika eneo hilo la Feri lakini wakati huo huo kuna kundi la wanawake wamekuwa wakiingiza chakula kutoka majumbano kwao na kukiuza hivyo kuharibu soko lao la chakula.

Mwenyekiti wa Kamati ya Soko hilo, Ali Kibwana alisema mafunzo waliyopata kupitia EfG yamesaidia sana kupunguza vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia katika soko hilo na kila mtu anayebainika kujihusisha na vitendo hivyo amekuwa akiitwa na kukanywa na kama akiendelea kuwa mkaidi anachukuliwa hatua nyingine kwa kufuata kanuni na sheria.

Kamanda wa Ulinzi na Mazingira wa Soko hilo, Nurdin Hassan amesema hali katika soko hilo ni nzuri kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na EfG ya kufanya semina na matamasha ya uhamasishaji hivyo kuifanyajamii kuelewa kuhusu vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia.

Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa EfG, Shaban Rulimbiye alisema Shirika hilo linaendesha mradi wa miaka mitatu wa Mpe Riziki si Matusi wenye lengo la kutoa elimu ya kupinga ukatili wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na udhalilishaji na nia zaidi mradi huo ni kuusambaza hadi katika maeneo mengine ya nchi.

MTO MSIMBAZI UNAOKATIZA ENEO LA JAGWANI WAANZA KUPIGWA SOP SOP

$
0
0
 Mhandisi wa  Kampuni  ya Chico, David Waruma  akizungumza leo jijini Dar es Salaam juu ya kazi ya kusafisha na kuzibua uchafu katika daraja la Mto Msimbazi eneo la Jangwani, Jijini Dar es salaam kuzuia na kukomesha mafuriko yanayotokea kipindi cha mvua ambayo huleta  athari kwa jamii inayozunguka eneo hilo pamoja na kulinda Kituo cha Mabasi yaendayo Haraka (BRT) cha Jangwani  (Jangwani Depot),  kisiathirike na Mafuriko endapo  yatatokea.
  Vifaa maalum kwa ajili ya  kusafisha Mto Msimbazi, Jangwani jijini Dar es Salaam.
Kazi ikiendelea ya kusafisha eneo la Mto Msimbazi leo jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakitazama  daraja la Mto Msimbazi  jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii

Rais Magufuli akutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria Ramtane Lamamra

$
0
0



Rais Dkt. John Pombe Magufuli akutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria Mhe. Ramantane Lamamra Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
(Picha na Freddy Maro)

NEC YATANGAZA MGAWANYO WA VITI MAALUM BUNGENI

MR TZ - LOADING........

Rais Magufuli akutana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala Cha China Mhe.Zhang Ping

$
0
0
 Rais Dkt.John Pombe Magufuli akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala Cha China Mhe. Zhang Ping ikulu jijini Dar es Salaam leo.Bwana Zhang alimwakilisha Rais wa China katika sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano. Kulia ni Balozi wa China nchini Dr. LU Youqing
 Rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala Cha China Mhe.Zhang Ping ikulu jijini Dar es Salaam leo.Bwana Zhang alimwakilisha Rais wa China katika sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano. Kulia ni Balozi wa China nchini Dr. LU Youqing na kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini China Lt General (rtd) Abdulrahman Shimbo.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli katika mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala Cha China Mhe.Zhang Ping ikulu jijini Dar es Salaam leo.Bwana Zhang alimwakilisha Rais wa China katika sherehe za kuapishwa Rais wa Awamu ya Tano. Picha na Freddy Maro

NEWS ALERT: Serikali yasitisha matumizi ya Picha Rasmi ya Rais Magufuli

$
0
0
Serikali inapenda kuzitaarifu ofisi za umma  na  wananchi  kwa ujumla  kwamba  imesitisha    matumizi  ya  picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  wa Serikali ya Awamu ya Tano, Mhe.Dkt. John  Pombe Josep Magufuli mpaka hapo itakapotangazwa tena.


Awali   majira ya saa 6: 00 mchana leo Novemba 6, mwaka huu Serikali ilitangaza kuhusu kuanza rasmi kwa matumizi ya picha ya Rais.



Aidha,   Serikali  imesema kwamba  itazitangazia  ofisi hizo na umma wa Watanzania  kuhusu kuanza tena  kwa  matumizi ya picha  hiyo hapo baadae.


Imetolewa na
IDARA YA HABARI.
Novemba 6,mwaka 2015

NEWS ALERT: RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE AONDOKA RASMI IKULU NA KUELEKEA KIJIJINI MSOGA LEO

$
0
0
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiagana na watumishi wa Ofisi ya Rais Ikulu wakati wakiondoka rasmi katika jumba hilo waliloishi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita na kurudi kijijini Msoga. kushoto kwake ni Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
  Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete  akiagana na watumishi wa Ofisi ya Rais Ikulu wakati akiondoka rasmi katika jumba hilo waliloishi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita. kushoto kwake ni Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli

  Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimsindikiza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete   na mkewe mama Salma Kikwete wakati wakiondoka rasmi Ikulu alimoishi kama Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita.  
  Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiagana na  Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete   na mkewe mama Salma Kikwete wakati wakiondoka rasmi Ikulu walimoishi kama Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita. 
 Rais wa awamu ya tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Katibu Mkuu Ikulu Mhe Peter Ilomo na watumishi wa Ofisi ya Rais wakiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho kikwete.

Tamko la Waziri wa Mambo ya Nje John Kerry kuhusu Uchaguzi wa Tanzania

$
0
0

Ubalozi wa Marekani

 Dar es Salaam

TANZANIA

5 Novemba, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Kwa niaba ya Rais Obama na watu wa Marekani, nawapongeza watu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uchaguzi wa rais na wabunge ulioendelea kuthibitisha rekodi nzuri ya Tanzania katika kujenga demokrasia imara.
Wakati Rais John Pombe Joseph Magufuli na serikali yake wakichukua majukumu yao, tunatarajia kuendelea na ubia wetu wa karibu na kuimarisha zaidi ushirikiano baina ya nchi zetu mbili tunapofanya kazi pamoja ya kusaidia ujenzi wa demokrasia, kukuza usalama wa kikanda na kuendelea kuchochea maendeleo ya kiuchumi.
Aidha, napenda kumshukuru Rais aliyemaliza muda wake Jakaya Kikwete kwa jitihada zake za kujenga uhusiano imara na wa kudumu kati ya Marekani na Tanzania.
Hata hivyo, Marekani inaendelea kustushwa sana na tamko la mamlaka visiwani Zanzibar la kusudio la kufuta matokeo ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar wa Oktoba 25.

Kwa dhati kabisa, tunatoa wito kwa serikali mpya kuhakikisha kuwa maamuzi ya watu wa Zanzibar yanajidhihirisha  katika ukamilishwaji wa haraka, wa haki na wa amani wa mchakato wa uchaguzi visiwani Zanzibar.




Rais Magufuli akiwa Ofisini Kwake Siku ya Kwanza

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifanyakazi ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni siku yake ya kwanza ofisini kwake tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano.
(Picha na Freddy Maro)

Rais Magufuli afanya Ziara ya Kushtukiza Hazina

$
0
0
Rais Dkt.John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha wageni muda mfupi baada ya kuwasili katika makao makuu ya Wizara ya Fedha(HAZINA) kwa ziara ya kushtukiza leo mchana.Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt.Servacius Likwelile.Rais Magufuli alitembelea na kukagua ofisi zote wizarani hapo na kisha kuongea na viongozi waandamizi.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli akiwa na wafanyakazi wawili wa Wizara ya Fedha ambao ni walemavu Bwana Fundi Maruma na Frank Mkyama wakati Rais alipofanya ziara ya kushtukiza wizarani hapo leo.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha wakati alipofanya ziara ya kushtukiza Wizarani hapo ambapo alitoa maagizo ya kuziba mianya ya wakwepa kodi.(picha na Freddy Maro)

KIONGOZI MKUU WA CHINA ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA JIJINI DAR

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala cha Nchini China Mh ZHANG PING akiwa kwenye ukumbi wa Historia wa Makumbusho na Nyumba ya Utamani Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala cha Nchini China Mh ZHANG PING katikati akiwa kwenye ukumbi wa Sanaa wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala cha Nchini China Mh ZHANG PING watatu kushoto akiwa kwenye chumba mahususi akipewa maelezo na Dr Amandus Kweka ya fuvu la Zinjanthropus lililopo Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam.

UZINDUZI WA KANISA HOUSTON

JUMAMOSI 7 NOV 2015 ! NGOMA AFRICA BAND JUKWAANI MJINI BREMEN.UJERUMANI

$
0
0
 Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa Band aka FFU-ughaibuni yenye makao nchini Ujerumani ,itatumbuiza mjini Bremen,Ujerumani
Leo  jumamosi 7 November 2015,katika ukumbi wa Weserterrasse, uliopo
mtaa wa Osterdeich 70b, D- 28205 Bremen kuanzia saa usiku, onyesho hilo limeandaliwa na Pan-African Org tawi la Bremen ambalo linasherekea miaka 10 ya kuanziswa kwake. bendi ya Ngoma Africa band kwa sasa wanatamba na CD yao mpya La Mgambo na pia song lao jipya waliloliachia juzi tu "Mapenzi ya Pesa" nyimbo zote hizo zinapasua anga ya kimataifa
unaweza pia kusikiliza at www.ngoma-africa.com

Rais Magufuli alipofanya ziara ya ghafla Wizara ya Fedha

Viewing all 110017 articles
Browse latest View live




Latest Images