BEI YA MADAFU HII LEO
↧
↧
RATIBA YA KAMPENI ZA MGOMBEA URAIS/MGOMBEA MWENZA KWA VYAMA VYA SIASA (Kama ilivyorekebishwa tarehe 20/10/2015)
↧
MAMA MWANAMWEMA SHEIN AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA UWT WILAYA YA MJINI UNGUJA KUMUOMBEA KURA DK SHEIN NA DK MAGUFULI
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Mkoa wa Mjini Bi Waridi Juma akisoma risala ya Wanawake wa Mkoa wa Mjini wakati wa mkutano na Mke wa Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk Ali Mohamed Shein, Mama Mwanamwema Shein, uliofanyika katika ukumbi wa Afisi Kuu ya Mkoa wa Mjini Amani Zanzibar.
Viongozi wa UWT Mkoa wa Mjini Unguja wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, wakati wa mkutano wake na Viongozi hao uliofanyika Afisi ya CCM Mkoa Amani Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Salama Aboud Talib akizungumza wakati wa mkutano huo na kuwakaribisha Viongozi wa Ujumbe wa Kampeni ya Mama Mwanamwema Shein, kuzungumza na Viongozi wa UWT Mkoa wa Mjini Unguja.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
↧
HOTUBA YA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, MATHIAS CHIKAWE (Mb) ALIYOTOA KATIKA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 21 OKTOBA, 2015 KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA WIZARA
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika leo katika ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Ndugu Waandishi wa Habari, Mabibi na Mabwana,
Kama mnavyojua tarehe 25 ya mwezi huu wa Oktoba mwaka 2015 siku ya Jumapili katika nchi yetu kutafanyika Uchaguzi Mkuu kwa ajili ya kuchagua rais, wabunge na madiwani zoezi ambalo litawashirikisha watanzania wote waliojiandikisha kupiga kura kwa mujibu wa sheria.
Zoezi hili kwa mujibu wa sheria za uchaguzi litasimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi yaani NEC kama ambavyo imekuwa ikifanyika katika chaguzi mbalimbali zilizopita ama kuwahi kufanyika katika nchi yetu.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inalo jukumu kubwa la kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unaimarishwa kabla, wakati na baada ya zoezi hilo la Uchaguzi Mkuu katika maeneo yote ya nchi yetu, ili wananchi waweze kuwa salama na kuendelea na maisha yao ya kila siku.
Ndugu Waandishi wa habari,
Kumekuwepo na taarifa mbalimbali za vitisho zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na hata mitaani na watu wasio na nia njema kwa taifa letu, zikiwataka wananchi wanunue mahitaji yao mbalimbali ikiwemo vyakula na kuvihifadhi kwa ajili ya kuja kuvitumia wakati na baada ya uchaguzi kwa ubashiri wa kuwepo kwa vurugu wakati ama baada ya uchaguzi.
Taarifa hizi zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na mitaani kwa ujumla ni taarifa potofu ambazo zinalenga kuwajengea wananchi hofu na mashaka, wasiwasi na vitisho pasipo sababu zozote zenye tija kwa taifa letu.
Ndugu zangu Waandishi wa habari,
Nitoe rai kwa Raia wote waishio hapa nchini yaani Watanzania na Wageni kupuuza taarifa zote zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na mitaani kwa kuwa taarifa hizo si za kweli, na wala hazilengi kulinda amani iliyopo nchini kwetu.
↧
KIJANA FIKIRIA MARA MBILI KISHA WEKA TIKI KWA MGOMBEA
↧
↧
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO, KATIKA KITUO CHA KUTUNZIA KUMBUKUMBU CHA TAIFA (NATIONAL INTERNET DATA CENTRE) KIJITOMYAMA.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa, kwa pamoja wakifunua kitambaa kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Makame Mbarawa (kushoto) na Mwakilishi wa Ofisi ya Uchumi na Biashara ya Serikali ya China, nchini Tanzania, Lin Zhiyong, kwa pamoja wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kituo cha kutunzia kumbukumbu cha Taifa (National Internet Data Centre) Kijitonyama, leo Okt 21, 2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa hafla ya uzinduzi huo baada ya kuzindua rasmi leo Okt. 21, 2015 Kijitonyama, jijini Dar es Salaam.
Picha na OMR
↧
UCHAMBUZI WA HABARI TOKA VITUO MBALIMBALI VYA TELEVISHENI OKTOBA 21, 2015.
Huu ni uchambuzi wa Habari toka vituo mbalimbali vya Televisheni
Oktoba 21, 2015.
Chama Cha soka Jijini Mwanza Kwa kushirikiana na wanamichezo wamefanya mazoezi maalumu kwaa lengo la kutoa elimu Juu Ya Amani Na Upigaji Kura. https://youtu.be/Pb-8yIRPV1w
Upungufu Mkubwa wa Damu Katika benki ya Hospitali ya Taifa Muhimbili wachangia mrundikano wa wagonjwa hasa wa upasuaji. https://youtu.be/zhI0gAASoSo
Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi toka Jumuiya Ya Afrika Mashariki EAC imezinduliwa jijini Dar na kuahidi kufanya kazi kwa kufuata misingi ya Sheria za nchi. https://youtu.be/mJv-qJF7p_0
Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wameendelea na uhakiki wa majina yao katika daftari la wapiga kura huku baadhi ya makaratasi kuchanywa. https://youtu.be/dO23f6qH184
Ligi Kuu soka Tanzania Bara Inatarajiwa kuendelea leo ambapo Klabu Ya Yanga itamenyana na Toto Africans Ya Mwanza uwanja wa Taifa Dar. https://youtu.be/Qy6kNPakAKo
Kutana na mabalozi wa amani Christina Shusho pamoja na Mrisho Mpoto wakizungumzia swala zima la amani kuelekea uchaguzi mkuu; https://youtu.be/6WJLNbNd3L8
Je uwepo wa viwanja vipya utasaidia kukuza vipaji katika michezo mbalimbali nchini? Fuatilia mjadala hapa;https://youtu.be/Zb9Xt-C6hWc
Leo hii katika mjadala wachambuzi wanaangaliza habari kuu zilizopewa vipaumbele katika taarifa za habari; https://youtu.be/xKyPA5UdOqo
Je ahadi za wagombea zinazotolewa kwenye majukwaa zinatekelezeka? Fahamu zaidi kupitia mjadala wa leo; https://youtu.be/6WYVHA9qnJc
Fahamu chama cha APPT Maendeleo na mikakati ya chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika jumapili tareh 25 Octoba, https://youtu.be/Iq7qQpu4x70
↧
UMMOJA WA WANANCHI WA KIBADA WAFANYA MATENGENEZO GARI LA JESHI LA ZIMAMOTO
↧
RAIS DK. JAKAYA KIKWETE KUONGOZA KONGAMANO LA KUELEKEA UCHUMI WA KATI IFIKAPO 2025
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano kongamano la kuchochea uzalishaji mali, Prof.Leonard Mwaikambo akizungumza na waandishi wa habari juu ya lengo la kongamano ni kutoa fursa kwa watanzania kwa jumla kuelewa malengo na mwelekeo wa taifa letu kufikia uchumi wa kati .
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano Profesa,Leonard Mwaikambo.
Na Emmanuel Massaka ,Globu ya Jamii
RAIS Dk. Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano la kuchochea uzalishaji mali katika kuinua kipaato cha mtanzania wa kawaida kufikia malengo ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 litakalofanyika kesho katika Ukumbi Diamond Jubilei jijini Dar es Salaam.
Hayo ameyasema leo Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano Prof.Leonard Mwaikambo kongamano hilo litakuwa na watoa maada mbalimbali na wataalam katika sekta ambazo zitafanya kufikia uchumi huo.
Profesa Mwaikambo amesema kuwa wakati huu kutokana na harakati za uchumi kunahitajika wataalam ambao wamebobea kwa kuleta maendeleo hayo ambayo watanzania wanayoyataka kwa kukuza kipato.
Amesema kongamano hilo linagusa nyanja zote katika sera za vyama hivyo ni muda mwafaka wa kujadili masuala ya uchumi ni ya msingi katika ukuza ji kipato kwa wananchi.
Aidha amesema wanataaluma hao watatoa mchango wao katika maswala ya kijamii na sekta mtambuka , Utawala Bora ,na Mawasiliano ya kielektroniki kwa ukuzaji wa maendeleo watanzania ,Miundombinu ,Afya ,Maji, Elimu pamoja na ujenzi .
Majadiliano yataongozwa na Waziri Mkuu Mstaaf,Jaji Mstaafu,Joseph Sinde Warioba na neno la shukrani litatolewa na Waziri Mkuu,Mstaafu, John Malecela .
↧
↧
WAANGALIZI WA KIMATAIFA WA UCHAGUZI WAENDELEA KUPATA UFAFANUZI JUU YA MASUALA YANAYOHUSIANA NA VYAMA VYA SIASA NA UCHAGUZI.
Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini . Jaji Francis S. K Mutungi akizungumza na Waangalizi wa uchaguzi Mkuu kutoka Bunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo jana Oktoba 21,2015.
Baadhi ya Waangalizi wa Uchaguzi kutoka Bunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)
kushoto ni Msajili Msaidizi Usajili wa Vyama vya Siasa Bw. Sisty Nyahoza akielezea utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa , kulia ni Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji francis Mutungi.
Picha ya pamoja ya Jaji Francis S.K Mutungi , Waangalizi wa Uchaguzi kutoka Bunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
↧
WATOTO 37 WAFANYIWA UPASUAJI MUHIMBILI
Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na waandishi wa habari leo baada ya taasisi hiyo kufanikiwa kuwafanyia upasuaji watoto 37.
Mkuu wa Kitengo cha Moyo cha Watoto katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Godwin Shirau akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matatizo mbalimbali ya moyo.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini wakimsikiliza Profesa Mohamed Janabi leo katika hospitali hiyo.
HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH) kupitia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (Jakaya Kikwete Cardiac Institute (JKC) imefanikiwa kuokoa zaidi ya Shilingi mIlioni 800 baada ya kuwafanyia upasuaji wa moyo watoto 37 wenye matatizo ya moyo .
Operesheni hiyo imefanyika kuanzia Oktoba 10 hadi 19 mwaka huu kwa kushirikisha timu ya wataalam 18 kutoka nchini Italy na Marekani pamoja na madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka taasisi hiyo.
Kaimu Mkuu wa taasisi hiyo Profesa Mohamed Janabi amewaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kwamba endapo wagonjwa hao wangetibiwa nje, kila mmoja yangegharimu kati ya Dola za Kimarekai 10,000 hadi 15,000, gharama ambazo Watanzania wengi hawawezi kuzimudu.
Kwa mujibu wa Profesa Janabi, changamoto inayowakabili ni upatikanaji wa damu na upungufu wa watalaam.
Alifafanua kwamba hivi sasa kuna orodha ya watu 500 ambao wanasubiri kufanyiwa upasuaji wa moyo, na kwamba desemba mwaka huu, wanatarajia kupokea wagonjwa wenye matatizo ya moyo kutoka nchini Zambia.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Moyo cha Watoto, Dk. Edwin Shiran amesema watoto 17 wamefanyiwa upasuaji wa kufungua kifua na wengine 20 wamewekewa kifaa maalum kwa ajili ya kuziba matundu na kuzibua mishipa ambayo imezibana na kwamba kati ya hao watoto wawili wametokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Tangu Januari mwaka huu tayari wamekwishafanyiwa upasuaji wa moyo watoto 122 na watu wazima 132 .
↧
IJUE NAMNA YA KUKATA RUFAA.
NA BASHIR YAKUB -
Unaposhindwa kesi sio mwisho wa kusaka haki. Hii ni kwasababu kushindwa kesi kunatokana na sababu nyingi . Si kweli kuwa kwakuwa umeshindwa kesi katika mahakama fulani basi maana yake ni kuwa ulikuwa huna haki. Yawezekana kabisa haki ilikuwa yako isipokuwa umeshindwa tu kutokana na sababu nyingine za kiutaratibu na kimbinu (procedures & technicalities). Pia waweza kuwa umeshindwa kutokana na uwezo mdogo wa kujieleza na kushindwa kugusa nukta muhimu ambazo kimsingi ndizo zilizokuwa zinabeba shauri lako.
Lakini pia waweza kuwa umeshindwa kwasababu ya hila na mbinu chafu. Na hii wakati mwingine huwahusisha hata waamuzi yaani mahakimu na majaji. Basi ifahamike kuwa ni sababu hizi zilizopelekea kuwepo utaratibu wa rufaa ili yule anayehisi kutotendewa haki aende mbele ili kuona kama anaweza kupata haki yake huko.
1.RUFAA NININI.
Rufaa ni hatua ya kisheria ya kupeleka malalamiko katika hatua ya mahakama ya juu zaidi baada ya mmoja wa wahusika katika kesi iliyoisha kutoridhishwa na hukumu/maamuzi. Ili ukate rufaa ni lazime uwe ulikuwa mhusika katika kesi iliyoisha na uwe na sababu za kwanini unadhani hukuridhishwa na maamuzi. Sababu yoyote ya msingi inakubalika.
↧
EWE MGOMBEA, WEKEZA KATIKA KUMWENDELEZA MTOTO AKIWA MDOGO
Mpango kwa ajili ya watoto wadogo ipo mstari wa mbele katika vita dhidi ya umasikini. Watoto katika jamii zilizo masikini sana wamo katika hatari kubwa za kupata maradhi na utapiamlo na hawafanyi vizuri shuleni.
Mipango jumuishi ya watoto wadogo inayolenga watoto walio masikini sana huzisaidia familia kuwa na mwanzo mzuri wa watoto wao na husaidia kupunguza pengo kati ya masikini na matajiri. Uwekezaji kwa watoto wadogo una faida mara saba na una thamani kuliko kuwekeza kwenye mipango ya kunusuru maisha ya mtoto hapo baadaye.
Wazazi fukara wapatiwe msaada wanaohitaji ili kuhakikisha kuwa watoto wao wanakuwa na mwanzo mzuri zaidi katika maisha. Msaada kwa ajili ya miradi ya kijamii ya kulea watoto na ya maendeleo na makuzi ya awali ya watoto itasaidia katika kuhakikisha kuwa watoto wanakua wakiwa na afya, wanapata lishe bora na wametayarishwa vizuri kwenda shule.
Maendeleo ya watoto wadogo yaingizwe katika muhtasari wa mafunzo kazini ya walimu. Yaanzishwe mafunzo kazini ya kitaifa kwa wote wanaohudumia watoto wadogo. Wale wanaofanya kazi katika jamii fukara wapewe kipaumbele katika mafunzo haya.
Zianzishwe kamati za kijamii katika ngazi ya wilaya na kata ambazo zitafuatilia upatikanaji wa huduma na kusaidia uboreshaji wa vituo vya kumwendeleza mtoto akiwa mdogo.
#AjendaYaWatoto
↧
↧
Update ya Msiba wa mama/shangazi/bibi yetu TAMALI LEBI MWAKYOMA.
Ndugu Issa BAtenga wa Dar es salaam anapenda kuchua nafasi hii kwa niamba ya familia kutoa tangazo kuwa Mwili wa Marehemu wa mama/shangazi/bibi yetu TAMALI LEBI MWAKYOMA.unawasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam alasiri ya leo Jumatano saa 9 kutoka India na ndege ya Emirates.
Utaratibu ni kwamba Mwili huo utapelekwa moja kwa moja kwenye Hospitali ya Aghakhan kwa ajili ya kuhifadhiwa na Maandalizi..
Taarifa hii ni kutokana na Kuvurugika kidogo kwa Ratiba za ujio wa watoto wa Marehemu waishio Marekani ambao utasababisha kukawia kwao kuwasili Tanzania, kwa kuzingatia haya na pia endapo watawasili siku ambazo hazitaendana na ratiba tulizozipanga hapo awali, ni dhahiri kwamba mwingiliano wa safari ya kwenda Mbeya-Tukuyu, mazishi na safari ya kurudi Dar es Salaam kabla ya Jumapili itakuwa imewakosesha waombolezaji na wafiwa haki zao za msingi za kupiga Kura siku ya Jumapili 25/10/2015.
kwa hivyo na kwa kuzingatia haya, Tumeona ni busara tutoe tamko rasmi kwa kauli moja la kuahirisha Mazishi haya hadi tarehe ya karibu ambayo tutaipanga baada ya Uchaguzi.
Kwa ramani, Msiba upo barabara ya Rose Garden Mikocheni. kwa kutumia njia ya kutokea kwa Mwalimu Nyerere ni baada ya uzio wa TPDC/ Njia iendayo Data vision. Kuna kibao.
Na kwa Barabara ya kutokea Maji Machafu/Sayansi, ni kwenye njia mita 100 kandokando ya je go la Tume ya Vyuo Vikuu (Commision of High learning Institutions)
Tunawashukuru kwa uvumilivu na kwa kutufariji kila siku.
Mungu Awabariki na awape nguvu wafiwa.
↧
TAARIFA YA UWONGO NA UPOTOSHAJI KUMHUSU JAJI MKUU
2.0Taarifa hii si ya ukweli na ni ya upotoshaji,Mhe Jaji Mkuu hajawahi kuzungumzia chochote kuhusu sheria hiyo ukitilia maanani kesi hiyo iko Mahakama Kuu shauri Namba 37 ya 2015 iliyofunguliwa na Bi. Amy Kibatala dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Uchaguzi (DE) na itatolewa maamuzi kati ya tarehe 22 au 23 mwezi huu. Hivyo, kwa mujibu wa sheria Mhe.Jaji Mkuu asingeweza kuzungumzia chochote kuhusu sheria hiyo kwa kuwa suala hilo liko MAHAKAMANI.
3.0 Tulimwandikia Mkurugenzi wa Habari MAELEZO nakala East Africa Television na kufuatilia kwenye Baraza la Habari (Media Council) kuomba maelezo ya kina na usahihi wa taarifa hiyo, tarehe 21/10/2015 tumepokea barua Kumb Na EATV/ADMN/096/10/2015 ilyosaniwa na Bi Regina Mengi Mkurugenzi Mtendaji wa East Africa Television akiomba msamaha kuhusu taarifa hiyo potofu na kuwa watatoa maelezo ya ziada kuwa, taarifa hiyo haikutolewa na Mhe.Jaji Mkuu wa Tanzania
Tunashukuru kwa ushirikiano mkubwa tulioupata toka uongozi wa juu kabisa wa East Africa Television kwa kuomba radhi mapema na Tunamini kuwa, vyombo vya Habari na Wananchi kwa ujumla vitasitisha usambazaji wa taarifa hii iliyokuwa si sahihi.
Barua ya kuomba radhi imeambatanishwa:
Imetolewa na:
MTENDAJI MKUU WA MAHAKAMA
MAHAKAMA YA TANZANIA
↧
UCHAMBUZI WA HABARI ZA MAGAZETINI OKTOBA 22,2015
Kesi ya mita 200 moto, Lowasa sasa atishia kushtaki jeshi la polisi ICC. GP Hamdan awaonya waoandaa vurugu. Ni katika magaazeti ya leo Octoba 22.2015;https://youtu.be/TkIYjEUaJyw
Yanga acha kabisa, Chipukizi Simba kutimukia Ubelgiji, Ndemla afunguka. Nyoso atafutiwa mbadala. Kwa habari hizi na nyingezo za michezo utazipata katika udondozi wa magazeti hapa Simu.tv ; https://youtu.be/yL4C4fUOPgo
Rais Kikwete asema wanaimarisha jeshi ili kulinda mipaka ya nchi, NHIF yapania makubwa. Pata habari za kina hapa Simu.tv; https://youtu.be/eE10aUBwMHU
↧
BALOZI MPYA WA MISRI AWASILISHA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mpya wa Misri, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf. KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA. |
↧
↧
TAARIFA KUHUSU WALIOPOTEZA KADI ZAO ZA KUPIGIA KURA
OFISI Usambazaji na Ugavi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Eliud Njaila akiwaonyesha waandishi wa habari vizimba vya kupigia kura siku ya uchaguzi. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema wapiga kura waliopoteza kadi zao za kupigia kura hawataruhusiwa kupiga kura katika uchaguzi utakaofanyika nchini kote siku ya Jumapili.
Akizungumza katika mkutano wa vyama vya siasa na NEC mjini Dodoma leo, Ofisa Mwandamizi wa tume hiyo William Kitebi, amesema watu hao hawataruhusiwa hata kama majina na taarifa zao zipo kwenye Daftari la Wapiga Kura (BVR).
“Hakuna jinsi ya kuwasaidia watu waliopoteza kadi zao za kupigia kura ,”amesema Kitebi
Hata hivyo, Kitebi amesema kutokana na kasoro zilizojitokeza kwenye BVR kuna baadhi ya mambo NEC wameyawekea utaratibu ili watu waweze kupiga kura.
Amesema watu ambao namba za kadi zinatofautiana na zile zilizopo kwenye BVR lakini taarifa nyingine ni sahihi wataruhusiwa kupiga kura.
“Kuna wale ambao picha zao hazionekani kwenye daftari lakini kadi za kupiga kura wanazo, hawa wataruhusiwa kupiga kura,”amesema.
Kuhusu wale wapiga kura walioathiriwa na mipaka ya utawala, Kitebi amesema maamuzi ya tume kuwa watu hao watapiga kura kwenye kata walizopo.
“Kuna maeneo kulikuwa na mabadiliko ya mipaka ya kiutawala baada ya zoezi la uandikishaji kama Kishapu (Shinyanga) na Kaliuwa (Tabora), wao wataruhusiwa kupiga kura kwenye maeneo yao mapya,”amesema.
Kwa upande wa wapiga kura ambao wanakadi za kupigia kura lakini hawaonekani kwenye BVR, Kitebi amesema hao wamewekewa utaratibu utakaowawezesha kupiga kura.
“Kama kule Mbarali (Mkoa wa Mbeya), kuna watu kama 6,000 ambao hawaonekani katika daftari lakini wanakadi na fomu zao zimejazwa na kuwasilishwa tume hawa wanaruhusiwa kupiga kura,”amesema.
↧
MAKAMU WA RAIS DKT. AGANA NA WATUMISHI WA OFISI YAKE DAR
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Saz Salula, akizungumza kutoa shukurani wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa ajili ya Mhe. Makamu wa Rais kuagana na Watumishi wa Ofisi yake. Hafla hiyo ilifanyika juzi Okt 20, 2015 kwenye Makazi ya Dkt. Bilal
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi kutoka kwa Katibu Mkuu wa Ofisi yake, Saz Salula, wakati wa hafla fupi ya kuagana na watumishi wa ofisi yake, iliyofanyika Oysterbay jijini Dar es Salaam, juzi Okt 20, 2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib BIlal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Ofisi yake baada ya hafla hiyo.
Picha na OMR
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amewashukuru watumishi wa ofisi yake kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote cha miaka mitano kiasi cha kuweza kutekeleza majukumu ya msingi ya ofisi hiyo ya kudumisha Muungano na uhifadhi wa mazingira kwa ufanisi mkubwa.
Akizungumuza katika hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika jana jijini Dar es salaam Dkt. Bilal alisema kuwa, anayo furaha kufikia kipindi hiki na kwamba alifanya majukumu yake vema kutokana na kuwa na wasaidizi mahiri na waliojitoa kufanya kazi zao kwa weledi na uvumilivu mkubwa muda wote.
“Natumia nafasi hii kuwashukuru Watanzania wote. Walinisaidia sana katika kipindi nikifanya kazi ya kuitumikia nchi yangu. Niwashukuru ninyi wafanyakazi wa ofisi yangu, mlifanya kazi kwa kujituma sana na majukumu yetu kwa mujibu wa taratibu tuliyatekeleza kwa ufanisi,” alisema
Mheshimiwa Makamu wa Rais na kuongeza:
“Nakutakieni kila la kheri katika utendaji wenu. Jitahidini kufanya kama mlivyofanya kwangu kwa yule atakayekuja baada yangu. Nakushukuruni kwa zawadi hasa ya vitabu maana mimi ni muumini wa kusoma, nitavisoma”.
Dkt. Bilal aliwaambia watumishi hao kuwa ushirikiano waliompa katika utendaji wa kazi umewezesha kuzipatia ufumbuzi hoja mbali mbali za muungano na kusema hoja zilizobaki zinafanyiwa kazi na zitapatiwa ufumbuzi katika serikali ijayo.
Hoja ambazo zipo katika hatua mbalimbali za kutafutiwa ufumbuzi ni pamoja na Hisa za SMZ zilizokuwa katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki na Mgawanyo wa Mapato yatokanayo na Faida ya Benki Kuu; Usajili wa vyombo vya moto, Uchimbaji na Utafutaji wa Mafuta na Gesi Asili na Mapendekezo ya Tume ya Pamoja ya fedha.
Kwa upande wa mazingira alisema katika kipindi chake Tanzania ilipata nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Masuala ya Mazingira kwa viongozi wa Bara la Afrika jambo ambalo limewezesha nchi kutoa mchango mkubwa katika suala zima la uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika Bara la Afrika.
Hata hivyo, Dkt. Bilal alionyesha wasiwasi wake katika eneo la usafi wa mazingira na kuwataka watumishi wa ofisi hiyo kushirikiana na taasisi nyingine katika kuhakikisha usafi wa mazingira unapewa kipaumbele katika maeneo yote nchini.
Mapema, akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula alimshukuru Makamu wa Rais kwa uongozi wake ambao umekuwa mwongozo kwa watumishi katika utendaji wao wa kazi na kumtakia kila la heri katika kipindi cha kustaafu kwake.
Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam.
↧
UCHAMBUZI WA HABARI TOKA VITUO MBALIMBALI VYA TELEVISHENI OKTOBA 22, 2015.
Huu ni uchambuzi wa Habari toka vituo mbalimbali vya Televisheni Asubuhi Hii October 22, 2015.
SIMUtv: Fuatilia mwenendo na uchambuzi wa kampeni za vyama mbalimbali za lala salama baada ya kusalia masaa 48 kuelekea uchaguzi Mkuu mwaka huu
SIMUtv: Katibu wa chama cha madereva TADU, Rashid saleh akizungumzia vitendo vya wamiliki wa vyombo vya usafirishaji kuwaadhibu madereva: https://youtu.be/ne2li6v5HN8
SIMUtv: Tambua namna ambayo Nchi imejiandaa kulinda amani siku ya uchaguzi zikiwa zimesalia takribani masaa 48 kuifikia siku hiyo maalumu: https://youtu.be/dK2fdWR1jS0
SIMUtv: Fuatalia mazungumzo na viongozi wa dini wakihamasisha amani katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu ikiwa zimesalia siku 2: https://youtu.be/-JyP0slzlIc
SIMUtv: Fuatilia vipaumbele vinavyotiliwa mkazo zaidi na mgombea udiwani kata ya Mwananyamala jijini Dar es salaam kupitia chama cha ACT https://youtu.be/61OyRSbdgEI
SIMUtv: Mamlaka ya Chakula Na Dawa TFDA imezindua mfumo mpya wa utoaji na usajili wa vibali kwa njia ya kieletroniki. https://youtu.be/EKpX7i9iUpg
SIMUtv: Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kesho itatoa maelekezo maalumu juu ya Madai Ya Upinzani kukaa Mita 200 kusubiri matokeo. https://youtu.be/NniBsA0A4uA
SIMUtv: Mgombea Uraisi CCM Bi. Samia Suluhu awaahidi wananchi wenye ulemavu kushirikiana na serikali katika shughuli za kimaendeleo. https://youtu.be/YpieDVjInjo
SIMUtv: Serikali imesema itaimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao kabla, wakati na baada ya uchaguzi utakaofanyika oktoba 25. https://youtu.be/MIxU_FaGfQs
SIMUtv: Mgombea Uraisi CHADEMA Mhe. Edward Lowassa aahidi kurudia upya mchakato uliotumika kubadili matumizi ya Fedha kwa ajili ya kuboresha bandari ya Tanga. https://youtu.be/pN50aOZzqr8
SIMUtv: Mgombea Uraisi CCM Dkt. Magufuli amewaahidi wananchi wa Dar es Salaam kushughulikia mradi mkubwa wa maji na kuondoa kero hiyo. https://youtu.be/-Zb1ocoEOjo
SIMUtv: Siku 3 zimesalia kabla ya uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani kufanyika lakini kasi ya wananchi yaelekezwa katika Wagombea Uraisi pekee https://youtu.be/AGUCEprc9pc
↧
More Pages to Explore .....